JE, ULIKOSA SEMINA KUBWA YA UANDISHI WA MICHANGANUO YA BIASHARA 2022? | JIFUNZE UJASIRIAMALI

JE, ULIKOSA SEMINA KUBWA YA UANDISHI WA MICHANGANUO YA BIASHARA 2022?

SEMINA YA UANDISHI WA MICHANGANUO 2022

Habari ndugu mdau wa blogu hii, 

Tafadhali kabla hujasoma makala yangu ya leo kwanza nikupe salamu fupi toka kwa ‘mentor’ wangu Mkuu Napoleon Hill, unaweza pia na wewe leo ukaamua kumfanya kuwa mentor wako kwa kujiunga na Group letu la Kushauriana- MICHANGANUO-ONLINE MASTERMIND GROUP. Group ambalo members wake wanaishi hata baada ya kufa kimwili hapa duniani………...

Unaendeleaje lakini  na mapambano yako dhidi ya umasikini? Bila shaka nitafarijika ukiniambia bado yanaendelea na moto ni uleule haujapoa. Aisee tutafute pesa maanake matatizo mengi duniani yanatokana na umasikini, ikiwa kina Bakhresa, Mo na Bill Gate moto haujapoa sembuse mimi na wewe?

Tutafute pesa kwa njia zozote kasoro tu zile haramu na njia moja kubwa zaidi ya zote ni biashara au uwekezaji tu na si nyinginezo kama alivyonena Napoleon Hill katika kitabu chake maarufu Think & Grow Rich miaka zaidi ya 80 iliyopita, ujumbe huu umebeba maana ileile utafikiria umetoka jana.

Asante na karibu kwa makala yetu ya leo.

Semina ya masomo 11 ya msingi ya jinsi ya kuandika mchanganuo wa biashara yeyote ile ya mwaka 2022 ilifanyika ndani ya group la watsap la Michanganuo-online na tayari semina hiyo imeshamalizika huku washiriki kila mmoja akijipatia nakala ya kitabu cha semina hiyo nzima.

SOMA: Kwanini kundi la kushauriana(Mastermind Group) ni muhimu kwa kila anayetafuta mafanikio?

Ikiwa kwa sababu yeyote ile hukuweza kushiriki semina hii lakini ulikuwa na shauku ya kushiriki, leo ninayo habari njema kwako. Bado unaweza ukaipata semina hiyo kama ilivyo katika mfumo wa kitabu-nakala tete(softcopy. Kitabu hiki cha kurasa 50 kimerahisisha kwa kiasi kikubwa mno kazi ya kujifunza namna ya kuandaa mpango wa biashara ya aina yeyote ile iwe kubwa au ndogo.

Habari njema zaidi ni kwamba kitabu hiki kimeambatana na OFFA ya kipekee sana ambayo sijawahi hata siku moja kutoa offa yenye kufanana nayo kwa thamani. Ni kifurushi kamili cha course ya uandishi wa Michanganuo kinachojumuisha kila kitu mtu anachohitaji kuandika mpango wa biashara yake mwenyewe pasipo kuhitaji mwalimu au mtaalamu. (A complete course on Business Planning including books, templates and B.plan Samples) Nimekuandalia materials zote zinazohusiana na kuandaa mchanganuo wa biashara kwa kiswahili na kiingereza sehemu moja.

Katika ile OFFA iliyopita ya vitu 20 pameongezeka vitu vingine 2 ambavyo ni kitabu hiki cha Masomo 11 ya msingi ya jinsi ya kuandaa Michanganuo pamoja na kitabu kingine cha Semina ya Hesabu za Mpango wa Biashara kwa kina( Advanced Business Plan Financials) ambacho bei yake halisi ni Tsh. 20,000/= Vitabu hivi viwili ni kama Mapacha kwa jinsi vinavyotegemeana.

SOMA: Jinsi mpango wa biashara unavyoweza kuongeza mafanikio ya biashara yako

Ukipata Kifurushi/Package hii hakuna mchanganuo wowote ule wa biashara utakaokushinda kuandika, wala hauhitaji mtu wa kukuelekeza, na hata kama utahitaji bado utakuwa upo ndani ya Mastermind group la Michanganuo-online mwaka mzima ambapo utaweza kushea changamoto zako zozote pamoja na members wengine nikiwemo pia mimi mwenyewe mwandishi wa vitabu na michanganuo yote iliyopo kwenye hii package.

Si lazima ujiunge na group baada ya kulipia package yako, wengine huwa tu hawapendi kuwa ndani ya magroup haya ya watsap, hivyo ikiwa hupendi nijulishe nisikuunganishe nikutumie tu ‘items’ zako huku ukiendelea kuwa na mawasiliano ya karibu kabisa na mimi kwa usaidizi wowote utakaohitaji mbele ya safari.

SOMA: Nguvu ya Ushirika, Umoja ni nguvu

Lakini pia habari moja ambayo si ya kuvutia sana ni kwamba OFFA hii ni kwa watu wachache tu watakaowahi kulipia shilingi elfu 10. Idadi maalumu hata baada ya masaa mawili na OFFA itafungwa rasmi. Pia muda wa mwisho wa hii OFFA tulipanga uwe ni tarehe 15 June 2022, lakini imebidi tuongeze muda baada ya maombi mengi toka kwa wadau wetu wa masomo kwa njia ya email waliosema muda ni mfupi mno.

Muda umeongezwa mpaka pale tutakapotoa taarifa nyingine hivyo ni fursa kwa wale wote ambao walichelewa muda wa awali kulipia. OFFA ikimalizika ina maana huwezi tena kupata vitabu na michanganuo iliyotajwa pale chini mwishoni mwa hii makala kwa gharama ya shilingi elfu 10, utalazimika kulipa kiasi kikubwa zaidi cha fedha au kuikosa kabisa offa yenyewe.

Hivyo nakusihi sana hasa wewe mdau wangu wa nguvu katika blogu hii na masomo kwa e-mail, ikiwa ulikuwa na shauku ya kujiunga na Mastermind group langu au kupata a complete course on business planning in kiswahili & english, basi changamka sasa hivi uidake hii offa kabla wajanja wengine kama wewe hawajakuzidi kete uje kulipa gharama kubwa bure kupata vitu ambavyo ungeweza kuvipata kwa buku 10 tu.

SOMA: Tabia 9 zitakazobadilisha maisha yako kifedha

Kukuibia tu siri za group ni kwamba, katika nusu ya pili ya mwaka huu wa 2022 tayari tumeongeza vipindi vya masomo, kwanza tunakwenda kuwa na programu ya kusoma vitabu na bila shaka yeyote tutaanza na kitabu PENDWA cha pesa na mafanikio duniani kisichochuja kamwe cha THINK & GROW RICH (FIKIRI & UTAJIRIKE) tafsiri kwa kiswahili ya kitabu halisi cha mwaka 1938 kama kilivyoandikwa na NAPOLEON HILL na nilichokitafsiri mimi mwenyewe Peter Augustino Tarimo mwaka 2021. Kama ulikuwa hujui, kitabu hiki katika top ten ya vitabu bora zaidi duniani vya uchumi, fedha na mafanikio miaka yote(of all time) kimekuwa kikiongoza kushika nambari 1

Tutakuwa tukikisoma katika lugha zote mbili kiswahili na kiingereza kulingana na matakwa ya mtu mwenyewe atakavyojisikia huku mjadala ukifanyika pia kwa mseto wa lugha zote mbili.

SOMA: Je, ipo kanuni ya mafanikio ya kifedha?: Mtazamo wa kisaikolojia

Pili tutaweka pia msisitizo katika Michanganuo mifupi na rahisi ya biashara zile zilizokuwa na fursa kubwa ya kulipa haraka kwa madhumuni makubwa ya kuwawezesha wajasiriamali wadogo, wale wanaostruggle (wanaotaabika kupata mitaji ya biashara zao) kutengeneza mitaji yao wenyewe kwa njia rahisi sana pasipo kumtegemea mtu au taasisi yeyote ile.

Wajasirimali hawa kwanza hawana sifa ya kukopesheka kabisa, na hiki ndiyo kikwazo chao kikubwa kabisa(their biggest obstacle), pili hata wakikopeshwa mahali hawawezi wakapewa kiasi kinachoweza kutosheleza mitaji ya biashara zao kwani wakopeshaji wengi wakiwemo hata na ndugu,marafiki na jamaa zao wenyewe wanawatazama kwa jicho la wasiwasi mkubwa wakihofia watakwenda kupoteza pesa hizo kwani hawana dhamana yeyote ile ya uhakika waliyoiweka.

SOMA: Je, Mtanzania unakopesheka na taasisi za fedha au benki?

Mchanganuo unaweza ukaonyesha wazi kabisa ili biashara fulani itoboe inahitaji laki 6 au 7, lakini cha ajabu mkopeshaji(ndugu, jamaa, rafiki, Sacoss au Vikoba anampa laki mbili akimsisitizia eti akomae nazo na kubana matumizi tu atatoboa. Mjasiriamali hawezi kukataa pesa kwani yeye shida yake kubwa ni mtaji-pesa, huzipokea kwa shingo upande na kwenda kuwekeza kwenye biashara yake liwalo na liwe.

Lakini ‘masikini’, hauwezi kupita muda mrefu kabla mtaji huo haujakata kutokana na mzunguko mdogo wa pesa katika biashara ambayo mjasiriamali anaitegemea kwa kila kitu, hana njia nyingine na hawezi kufa njaa au ugonjwa na pesa anaziona.

Dawa hapo ilikuwa ni apate tu kiasi cha fedha zinazotosheleza mahitaji ya kuanza hiyo biashara na mambo wala yasingeenda mrama kutokana na biashara nayo kuwa ingelizalisha faida ya kutosha. Biashara nyingi hufa kutokana na ufinyu wa mitaji-pesa

Basi tunakwenda kujadili exactly namna baadhi ya biashara zinavyoweza kuzalisha faida kubwa kwa muda mfupi hata ikiwa mtaji ni mdogo kiasi gani. Mtaji utakua  harakaharaka na kumpa mjasiriamali nguvu ya kwenda taasisi kubwakubwa za kifedha kuchukua mikopo ya maana itakayompeleka viwango vingine, na hapa ndipo utasikia, ooo, fulani kaingia sijui freemason, sijui madudu gani, ilimradi tu wampake matope mtu aonekane siyo pesa zake halali.

SOMA: Biashara ya mtaji mdogo yenye faida kuwa zaidi Tanzania ilivyoshangaza darasa la Michanganuo

Hapa naomba nieleweke vizuri, hatuendi kujadili biashara mpya kutoka mwezini au sayari nyingine hapana, biashara ni zilezile tulizozizoea lakini tofauti moja tu ni kwamba tutaonyesha ni UBUNIFU gani mtu anaweza akautumia zikalipa haraka na pasipokuwa na mtaji mkubwa.

Kulipia offa hii spesho nikutumie kila kitu sasa hivi bila kuchelewa tumia namba zangu hizi, 0712202244 jina Peter Augustino Tarimo, kisha ujumbe wa watsap au sms usemao, “NITUMIE OFFA YA VITU 22” na kama unapenda nikuunge pia na group ongeza hapo maneno, “NA MASTERMIND GROUP”

Kwa mwaka huu wa 2022 hii ndiyo itakayokuwa OFFA yangu kubwa ya mwisho, si kama hakutakuwa na offa nyingine ndogondogo hapana, ila hii ndiyo offa ya kipekee na kubwa zaidi kuliko nyingine zote kwa mwaka huu na pengine miaka mingine yote. Kumbuka offa ina ukomo wake wakitimia idadi fulani tu ya watu. Hivyo kama unaihitaji huna sababu za kutokulipia sasa hivi.

Njoo jiunge sasa kwani hii ni fursa ya kipekee kabisa ya kujifunza kwa kina na kuziishi falsafa za kitajiri ndani ya kitabu mashuhuri zaidi cha fedha na mafanikio duniani, FIKIRI & UTAJIRIKE au hata wengine wamediriki kukiita “MSAHAFU WA MAFANIKIO”

Ni mimi,

Peter Augustino Tarimo

Mtaalamu wa Michanganuo ya biashara na Mfasiri wa kitabu cha Think & Grow Rich(Fikiri & Utajirike) katika lugha adhimu ya Kiswahili. 

0 Response to "JE, ULIKOSA SEMINA KUBWA YA UANDISHI WA MICHANGANUO YA BIASHARA 2022?"

Post a Comment