SEHEMU YA 2: MAELEZO YA BIDHAA & TATHMINI YA SOKO | JIFUNZE UJASIRIAMALI

SEHEMU YA 2: MAELEZO YA BIDHAA & TATHMINI YA SOKO

Mafunzo ya kuandika mchanganuo wa usagishaji sembe na dona sehemu ya 2
Sehemu ya 2 tutaandika hatua kwa hatua Sura au vipengele vikubwa viwili ambavyo ni; “Maelezo ya Bidhaa”  na “Tathmini ya Soko”

Lakini kabla ya kuanza sehemu hii naomba turudi sehemu ya kwanza kuna vitu au mambo matatu (3) hautukuyaelezea vyakutosha ambayo ni muhimu kabla ya kusonga mbele zaidi, mambo hayo ni;

                          1)      Orodha ya vipengele vyote vinavyounda mpango wa biashara

                          2)      Vipengele vidogo muhimu 4 , Dhamira kuu, Maono, Malengo na Siri za mafanikio

                          3)      Jedwali la Mahitaji na chanzo cha fedha za mahitaji

Vyote hivi ni vitu tulipaswa kuvijadili kwa kina kwenye sehemu yetu ile ya kwanza

Wakati tunaanza nilisema kwamba baada tu ya kazi ya kufanya utafiti kukamilika sasa unaanza kuandika vipengele vya mchanganuo wako kimoja baada ya kingine kisha nikasema tuanze na kipengele kikubwa cha kwanza ambacho ni Muhtasari ambao tutauandika mwishoni

1. Sasa nataka kabla ya kuanza kuchanganua vipengele niweke hapa chini mlolongo wa vipengele vyote vinavyounda mchanganuo mzima kisha mtu unafahamu kabisa ni kipengele kipi tunaanza nacho na kipi kitafuata kulingana na jinsi nilivyoandika.

Na huu ndio mlolongo wetu wa vipengele vyote 9. Kwanini 9 na siyo 8? Hamna fomula maalumu, kwa mfano mimi hapa nimeweka na kipengele cha UENDESHAJI ambacho mara nyingi watu hukiacha kama biashara haihusishi uendeshaji. Ni biashara chache zenye shghuli za uendeshaji mfano kiwanda au makampuni makubwa.

1.0 MUHTASARI TENDAJI 

 

2.0 MAELEZO YA KAMPUNI / BIASHARA

2.1 Malengo

2.2 Dhamira kuu

2.3 Siri za mafanikio

2.4 Umiliki wa Biashara

2.5 Kianzio (kwa biashara mpya au historia kwa kampuni iliyokwishaanza)

2.6 Eneo la biashara na vitu vilivyopo 

 

3.0 BIDHAA au HUDUMA

3.1 Maelezo ya bidhaa/huduma

3.2 Utofauti wa bidhaa/huduma na za washindani

3.3 Vyanzo vya malighafi/bidhaa

3.4 Kopi za matangazo

3.5 Teknolojia

3.6 Bidhaa au Huduma za baadae 

 

4.0 TATHMINI YA SOKO

4.1 Mgawanyo wa soko

4.2 Soko lengwa 

4.2.1 Mahitaji ya soko

4.2.2 Mwelekeo wa soko

4.2.3 Ukuaji wa soko

4.3 Tathmini ya sekta

4.3.1 Washiriki katika sekta

4.3.2 Usambazaji 4.3.3 Ushindani

4.3.4 Washindani wako wakubwa 

 

5.0 MIKAKATI NA UTEKELEZAJI

5.1 Nguvu za kiushindani

5.2 Mkakati wa soko

5.2.1Kauli ya kujipanga katika soko

5.2.2 Mkakati wa bei

5.2.3 Mkakati wa matangazo/promosheni

5.2.4 Programu za masoko

5.3 Mkakati wa mauzo

5.3.1 Makisio ya mauzo

5.3.2 Programu za mauzo

5.4 Mkakati wa ushirikiano

5.5 Vitendo na utekelezaji

 

6.0 UENDESHAJI

 

7.0 MAELEZO YA UONGOZI NA WAFANYAKAZI

6.1 Mfumo wa uongozi

6.2 Timu ya uongozi na wafanyakazi

6.3 Mpango wa mishahara  

 

8.0 MPANGO WA FEDHA

7.1 Dhana/makisio muhimu

7.2 Tathmini ya mauzo ya kurudisha gharama (Break Even Analysis)

7.3 Makisio ya faida na hasara

7.4 Makisio ya mtiririko wa fedha

7.5 Makisio ya mali na madeni (mizania ya biashara)

7.6 Sehemu muhimu za biashara

 

9.0 VIELELEZO/VIAMBATANISHO

• Taarifa za mahesabu ya fedha kwa undani

• Mahesabu yako ya nyuma

• Leseni, vibali ripoti za kodi, hatimiliki na alama za   

  biashara

• Mikataba mbalimbali

• Orodha ya mali na vifaa mbalimbali(Dhamana)

• CV za viongozi na wafanyakazi muhimu

• Kopi za matangazo ya biashara. 

 

*Kumbuka utakapokuwa ukiandika mpango wa biashara yeyote ile ni vizuri sana ukawa na hii listi ya vipengele mezani kwako.

 

2. Kitu cha pili nilichosema hatukukielezea ni vipengele vidogo 3 vya mwanzo vya sura ya Kampuni/Biashara unavyoona kwenye orodha yetu ambavyo ni; Malengo, Dhamira kuu, Maono na Siri za mafanikio

Haya maneno 3 ya msingi kuna watu wengine huyaweka punde tu chini ya Muhtasari na wengine huyajumuisha kwenye Sura ya Maelezo ya kampuni kama uonavyo hapo juu

Katika mchanganuo wetu huu wa Chamazi milling niliviweka chini ya Muhtasari na siyo kwenye maelezo ya Biashara. Lakini haijalishi popote pale unapoviweka ni sawa tu kati ya hizo sehemu mbili.

Nitaanza kueleza nilivyoandika hivi vipengele vidogo 3 kama ifuatavyo;

Dhamira kuu au wengine huita Dhima, kwa kimombo Mission Statement:  Maana yake ni unaandika lile lengo hasa biashara yako inataka kulitimiza katika mtazamo mpana.

Mara nyingi watu huelezea kile kitu biashara inachokifanya lakini Mission yako pia itategemea biashara inalenga soko gani au ni faida zipi inatoa kwa mteja.

Kwa mfano hata dhamira nyingine hueleza malengo ya ndani mfano kuwajali wafanyakazi nk.

Dhamira yako unapoelezea ni biashara gani unafanya jaribu kutoa maelezo yanayojitosheleza usiminye baadhi ya shughuli zako mfano badala ya kusema ‘dhamira yetu ni kuuza simu za mkononi’, sema dhamira yetu ni ‘kutoa huduma bora za mawasiliano’ , maana utakuwa unaondoa uwezekano wa kufanya mambo mengine yahusuyo simu za mkononi mfano kuuza vocha, vifurushi na accessories nyingine za simu za mkononi.

Pia usiseme dhamira yetu ni kutoa huduma ya usafiri wa daladala, sema ni kutoa huduma za usafirishaji maana hujui ni lini utakuja kununua na malori kwa ajili ya kwenda mikoani.

Kwenye Dhamira kuu ya Chamazi maize milling nilizingatia zaidi fursa kubwa ya soko lililopo katika kata tunazozilenga kwa hiyo hii ikawa ndiyo mission yetu kubwa itakayopelekea hatimaye kutimiza malengo yetu mengine madogomadogo mfano kupata faida, kukua kwa biashara yetu, kuongeza biashara nk.

Niliandika hivi dhamira yetu kuu;

........................................................................................................................................................................................................................................

Maono/ Vision:

Unaeleza kile unachoota biashara yako kuwa baada ya muda fulani kupita huko mbele, unatamani biashara yako ije iwe vipi miaka 2, 3, 5 na kuendelea?

Sisi kwenye Chamazi Milling tuliandika hivi;-

...............................................................................................................................................

Malengo / Objectives

Haya ni malengo au vitu biashara imepanga kufikia au kukamilisha, ni lazima yawe halisi yapimike, na yawe na muda maalumu wa utekelezaji. Mfano yanaweza kuwa kiwango cha mauzo, faida, ukuaji wa soko nk. Malengo yetu Chamazi kwa miaka 3 ni haya yafatayo;

·      Ku...................................................................................................................................................................

·      Ku................................................................................

·      Kufikisha ....................................................................

·      Kuunga ..........................................................................

Siri za Mafanikio

Unataja mambo ambayo ni kipaumbele kwa kampuni katika kutimiza malengo yake

Hata hivyo kwenye mchanganuo wetu huu hatukuwa na siri za mafanikio. Lakini tungeliweza kutaja kwa mfano hata eneo la kimkakati linalokua kwa kasi, Uzoefu wa muda mrefu wa wamiliki kwenye sekta ya mazao ya nafaka nk.

3. Kitu cha tatu nimesema tutarudia kukielezea ni lile jedwali la namba za kuanzia kwenye kipengele kidogo cha “Kianzio”

Kimsingi jedwali la kwanza lina mahitaji ya aina tatu ambayo ni;

·      Gharama za awali

·      Rasilimali za muda mfupi

·      Rasilimali za kudumu

Gharama za awali (Start up expenses), niliorodhesha zile gharama ambazo........................................................................ ...........................................................................................................................................................................................................

Rasilimali za muda mfupi (Short term assets) ni .........................................................................................................................................................................................................

Rasilimali za kudumu (long term assets) Ni vifaa na mashine zote za kudumu mwaka mmoja na zaidi unazonunua.....................................................................................................................................................................................

Jumla ya vitu vyote 3 ukijumlisha unapata mahitaji yote kwa ajili ya kuanzisha biashara hii ambayo ni sh. milioni 29 lakini tunahesabu zile gharama za awali sh. milioni 4 hupotea na hivyo jumla ya Rasilimali au assets zitabakia kuwa sh. milioni 25 tu

Jedwali la Chanzo cha fedha za mahitaji nalo lina vipengele 2, juu kuna Deni au mikopo na chini kuna Mtaji wa wawekezaji.

Jumla ya deni na Mtaji wa wawekezaji (0 +29,000,000 -4,000,000) = hulingana na jumla ya Rasilimali tulizopata kwenye jedwali la mahitaji ya kuanzia( 11,000,000 + 14,000,000) sawa na 25,000,000

Na jumla ya mahitaji yote (4,000,000 + 11,000,000 +14,000,000 ) ni lazima yalingane na jumla ya vyanzo vyote vya fedha(29,000,000 + 0) sawa na milioni 29

NB:Zingatia kanuni ZifuataZo;-

Mahitaji  = Gharama za awali + Rasilimali za muda mfupi + Rasilimali ma mda mrefu

Vyanzo vya fedha = Mtaji wa wawekezaji + Deni(mikopo)

Mtaji jumla = Mtaji uliowekezwa – Gharama za awali zilizopotea

Baada ya kukamilisha vipengele vyote vidogo vinavyounda sura yetu ya kwanza ya Maelezo ya Kampuni /Biashara, sasa tunachagua sentensi muhimu kuunda muhtasari mdogo wa sura hii ambao huwekwa mwanzoni mwa sura yenyewe na kisha kuja kuunganishwa na mihutasari mingine kuunda Muhtasari Tendaji wa mchanganuo mzima.

Mpaka kufikia hapo tumemaliza “Kiporo chetu” cha Sehemu ya kwanza ya mafunzo haya labda ikiwa kama kuna swali lolote unaweza ukauliza nitakujibu. Sasa tuingie rasmi sehemu ya pili.

 

 

SEHEMU YA 2

·      MAELEZO YA BIDHAA

·      TATHMINI YA SOKO

 

3.0 MAELEZO YA BIDHAA

Katika mlolongo wetu wa vipengele/sura zinazounda mpango wa biashara hii ni sura ya tatu na inaundwa pia na vipengele vidogo vifuatavyo .........................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................

Maelezo haya nakuwa nimeyafahamu kupitia utafiti nilioufanya kabla ya kuandika mchanganuo huu kwani kila kitu nilikuwa nimeshachunguza na hapa ilibaki kuandika tu. Kwa mfano....................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................

Unaweza kusoma sura yako nzima kwenye mchanganuo kamili wa Biashara hii niliokupatia na mifano mingine kwenye michanganuo mbalimbali pia niliyokupa.

 

4. TATHMINI YA SOKO

Katika sehemu hii ya pili tunajifunza pia jinsi nilivyoandika Kipengele/Sura ya 4 ya mchanganuo huu wa Chamazi White Maize Milling

Sura hii ni kubwa hivyo lazima ianze na muhtasari mdogo ambao lakini huandikwa mwisho. Kumbuka pia Tathmini ya soko ndio kipengele kinachotumia zaidi taarifa za utafiti tuliofanya kuliko vingine vyote. ..............................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................

4.1 Mgawanyo wa soko

Baada ya kuacha nafasi ya kuja kuandika muhtasari mfupi wa sura nilianza moja kwa moja kipengele hiki kidogo kwa kueleza eneo la soko letu lengwa kuwa ni............................................. ................................................................................................................................................................................................................, unaweza kuzisoma kwenye mchanganuo wako.

Kisha nikaonyesha jinsi nilivyogawanya soko hilo katika makundi makuu mawili nikitumia kigezo cha ..........................................................................................................................................................................................................

4.2 Soko lengwa 

Katika hayo makundi mawili nikachagua soko muhimu zaidi kwetu kuwa ni ..............................................................................................................................................................................................................................................................................................................

4.2.1 Mahitaji ya soko

Kwa kutumia Takwimu mbalimbali nilizopata kwenye utafiti nilioufanya nilionyesha mahitaji ya soko la unga wa mahindi kuwa yapo na hivyo biashara hii inaweza kuleta faida.

Nilionyesha idadi ya watu ipo ya kutosha na namna watu wengi wanavyotumia unga wa mahindi (sembe na dona). Soma takwimu hizo kwenye mchanganuo wako na jinsi nilivyoeleza

4.2.2 Mwelekeo wa soko

Hapa nilieleza muelekeo wa soko la unga wa mahindi nikizingatia mazingira mbalimbali kama vile mazingira ya kisiasa, hali ya hewa na ulaji wa watu

4.2.3 Ukuaji wa soko

Hapa pia kwa kutumia takwimu mbalimbali za utafiti nilionyesha soko la unga wa mahindi Temeke na Tanzania kwa ujumla linakua namnagani

4.3 Tathmini ya sekta

Hapa nilianza na muhtasari mfupi wa kipengele hiki kidogo kwa kuelezea sekta biashara hii ilipo ya usagishaji nafaka kwani ni kipengele kidogo kinajitegemea mbali na soko lenyewe. Nilieleza historia yake kwa ufupi tangia Uhuru pamoja na mabadiliko makubwa yaliyoikuta kipindi hicho chote

4.3.3 Ushindani

Kisha niliingia moja kwa moja kueleza ushindani ulivyo kwenye hii sekta, halafu chini yake nikataja washindani wetu wakubwa wawili na sifa zao, nguvu na udhaifu waliokuwa nao nikilinganisha na sisi Chamazi White Maize Milling.

Fuatilia vizuri mchanganuo wako maelezo yanajitosheleza hayana ugumu wowote ule kueleweka

Baada ya kumaliza vipengele vyote vidogo vya Sura hii ya Soko sasa................................................................................... ....................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................

Tumehitimisha Sehemu ya pili ya Mafunzo yetu haya ya kuandika kwa vitendo Mchanganuo wa Biashara ya Usagishaji nafaka ambapo tuliandika sura 2, ya maelezo ya Bidhaa na Tathmini ya Soko.Tukutane sehemu ya tatu.

 

Semina hii hapa katika blogu ya jifunzeujasiriamali tumeweka dondoo chache tu, ukihitaji semina nzima iliyokamilika jiunge na mafunzo haya pamoja na kupata mchanganuo wako kamili wa Chamazi white maize milling, pia zawadi ya vitabu na michanganuo mingine mbalimbali. Mawasiliano yetu ni; 0765553030 au 0761002125


SEHEMU YA 1                                             SEHEMU YA 3

0 Response to "SEHEMU YA 2: MAELEZO YA BIDHAA & TATHMINI YA SOKO"

Post a Comment