Swali hili ameniuliza mdau wangu mmoja kupitia watsap na
aliuliza hivi;
Ok,
Peter, mimi bawana ni mdau nataka kuanza kufuga kuku wa kienyeji, nahitaji
muongozo wa kujenge banda na mengineyo yanayohusiana na ufugaji kuku kienyeji.
Nami
nikamjibu kama ifuatavyo;
Habari kiongozi,
Unajua bwana, suala la mabanda kwenye biashara ya ufugaji
wa kuku siyo ishu kubwa sana ni suala tu la kuwa na mtaji wa kutosha, kuku
hawahitaji mabanda spesho sana bali wanachohitaji wao ni mahali watakuwa salama,
pa kuwakinga na hatari zote kama vile hali mbaya ya hewa- jua, mvua na upepo,
lakini wanyama hatari walao kuku kama vicheche, paka, kunguru, fisi, mbwa,
nyoka nk. bila kusahau binadamu wezi.
Kwa kuzingatia mahitaji hayo niliyoyataja mtu unaweza
kumtafuta fundi yeyote yule mzoefu ukamlipa akakutengenezea banda zuri
litakalokidhi mahitaji hayo na wala siyo kuhangaika sijui eti ukatafute ramani
za mabanda ya ghorofa, mabanda yenye hadi siting room, dining room na makorokoro
kibao kama hayo, kuku hawahitaji vitu hivyo, wawekee mabembea, vyombo vizuri
vya maji na chakula, viota na nafasi iwe ya kutosha mita moja ya mraba wasizidi
kuku wakubwa 6 -10, basi umemaliza
Ukitaka uone mafanikio ya faida kifedha kwenye mradi wa
kufuga kuku wa aina yeyote ile iwe ni kuku wa kienyeji, kuku wa kisasa, chotara
au kuku wa aina nyingine yeyote ile, zingatia sana mambo haya 3 nitakayokueleza
hapa
(1) Zingatia sana kitu kinachochangia gharama kubwa
kwenye hii miradi ya ufugaji wa kuku ambacho si kingine bali ni gharama za
CHAKULA.
Gharama za chakula ni zaidi ya asilimia 70% ya gharama
zote za mradi wowote ule wa kuku so, unapaswa ili kuona faida basi uhakikishe
unapata vyakula vya kuku kwa gharama nafuu kadiri iwezekanavyo, jifunze jinsi
ya kupunguza gharama za chakula kwa mradi wako wa kuku na hiki ndicho kitu
kikubwa kitakachoweza kuleta tofauti kubwa kwenye mradi wako na siyo mabanda
ingawa nayo ni muhimu pia.
(2) Kitu cha pili cha kuzingatia ikiwa kama kweli
umedhamiria kutajirika na mradi wa kufuga kuku ni CHANJO. Ikiwa ufugaji wako
siyo kwa ajili ya kitoweo cha siku za sikukuu kama Iddi, Krismasi, Pasaka na
Mwakampya ambapo huna umuhimu mkubwa nao, basi ni lazima uzingatie chanjo zote muhimu
pasipokujali ikiwa unafuga kuku wa aina gani kienyeji au kisasa
Dawa nyinginezo za magojwa ni muhimu pia mfano za minyoo
na kuharisha.
Achana kabisa na kasumba ya kusema eti, “Kuwalisha kuku dawa au chanjo kuna madhara
kwa afya ya binadamu” wewe unafuga kibiashara na tena isitoshe binadamu
tukiumwa tunachoma hizihizi chanjo na madawa antibiotics, sasa kuku kwani siyo viumbe hai kwahiyo hawastahili
dawa?
(3) Jambo la tatu ni UFUGAJI
WA KIWANGO KIKUBWA (Mass production). Kutokana na gharama hasa za chakula na virutubisho nilivyosema
hapo juu, faida kwenye ufugaji wa kuku wachache siyo kubwa sana ikiwa utaamua
kuwahudumia ipasavyo ingawa pia ni ya uhakika kama umezingatia hayo yote. Sasa
kwa kuwa ni kidogo na ya uhakika, basi ili iweze kuwa kubwa na kukujengea
utajiri inakupasa ufanye ufugaji wa kiwango kikubwa na siyo kuku waiwili watatu
wa kitoweo nyumbani
Tatizo la wafugaji wengi wadogowadogo ni kwamba kwakuwa
wanaogopa gharama basi hujikuwa wakipata hasara au kutokuona faida kwenye idadi
ndogo ya kuku wanaofuga na hivyo kuogopa moja kwa moja kufuga idadi kubwa ya
kuku. Hufikiria changamoto walizopata ikiwa wataingiza pesa nyingi itakuwaje?
Lakini changamoto hizo dawa yake ni kuzingatia tu hayo mambo 3
Mtaji wa kufuga kuku pia haupaswi kuwa wa ‘mawazo’
hakikisha unazo pesa za kutosha kulipia gharama za mradi mzima mkononi au benki
kabla hujaanza na siyo kuja kuanza kutafuta pesa wakati vifaranga wameanza
kuota manyoya au matetea wanakaribia kutaga, utawaua na njaa bure
Fanyia mazoezi kwanza mradi wa kuku wachache ukishapata
uzoefu na kuona idadi hiyo kuku wote wamepona na umepata faida kidogo, basi
ongeza mradi wako (scale it up) na utumie mbinu zilezile ulizotumia
kwenye mradi wa idadi ndogo ya kuku halafu utaona matokeo yake yatakavyokuwa
makubwana ya kushangaza.
Imagine kwa mfano umefuga kuku 100 tu ukapata faida ya
shilingi elfu 50, sasa ukifuga kuku 2000 piga hesabu una faida kiasi gani hapo?
Tena ni kwa muda uleule uliofuga kuku 100
Kila la kheri
Peter Tarimo
0765553030 / 0761002125
Kwa
mahitaji ya michanganuo ya kuku aina zote, kienyeji kisasa na chotara kwa bei
rafiki, tuwasiliane.
Mchanganuo
unakuwezesha kujua gharama, faida, changamoto na mahitaji yote kabla hujaanza
kufuga au kufanya mradi mwingine mkubwa zaidi.
SOMA
NA HIZI HAPA;
1. Banda la kuku 100 wa kienyeji:
vipimo, ramani, picha na jinsi ya kulijenga kwa ubora
2. Muongozo kamili wa jinsi ya kufuga kuku wa nyama (broilers) kitaalamu- semina siku-3
3.
Ufugaji wa kuku wa kisasa wa mayai
vs kuku wa nyama ni biashara ipi inayolipa faida zaidi?
4.
Semina: mchanganuo wa
kuomba mkopo biashara ya ufugaji wa kuku 200 wa nyama
5. Kilichokuwa nyuma ya pazia, ufugaji kuku wa kienyeji(kuku
wa asili).
6. Kuku wa nyama broilers: kwanini faida na gharama za
ufugaji zinavunja moyo?
0 Response to "KUFANIKIWA BIASHARA YA UFUGAJI WA KUKU UZINGATIE KITU GANI KATI YA MABANDA, CHAKULA, CHANJO NA DAWA?"
Post a Comment