NATAMANI KUFANYA BIASHARA BAADA YA KUACHA UALIMU NA KUSOMEA UGAVI (PROCUREMENT) | JIFUNZE UJASIRIAMALI

NATAMANI KUFANYA BIASHARA BAADA YA KUACHA UALIMU NA KUSOMEA UGAVI (PROCUREMENT)

Nipo njia panda, chuo au biashara

Mimi nilisomea ualimu na mpaka sasa hivi bado ni muajiriwa shule ya serikali lakini kwakweli kazi ninayoipenda kutoka moyoni ni kazi ya ununuzi na ugavi (Supply and Procurement). Hivyo wakati nikiendelea na ualimu nilichukua uamuzi wa kwenda kusomea course ya ununuzi na ugavi chuoni na tayari nimekwisha fanya mipango yote ya kujiunga na chuo. 

Hata hivyo wakati nikijiandaa na chuo kuna mawazo mengine yameibuka kichwani mwangu na kunifanya niwe katika wakati mgumu sana wa kuamua. Kuna biashara nikiwa bado mwalimu naendelea kuifanya ambayo pia nilichukua mkopo mahali kwa ajili yake na tayari mkopo huo karibu namaliza kuurejesha.

Sasa kinachonitatiza ni kwamba, nikaendelee na masomo ya ugavi chuoni miaka 3 au niamue kuzama moja kwa moja kwenye biashara na kuachana kabisa na ndoto za kuajiriwa serikalini?

Ingawa ninao uhakika nikimaliza chuo bado naweza kuajiriwa na serikali kwani sasa hivi pia nimeajiriwa nayo kwa kazi hii ya ualimu ila tatizo nahisi miaka 3 na 1 wa kusubiri ajira naona kama ni muda mrefu mno, nitakuwa nimechelewa sana.

Hiyo ni changamoto anayopitia msomaji wangu mmoja kutokea kule Mkoani Kigoma akiomba ushauri ili aweze kuondokana na mtanziko unaomkabili juu ya kuchagua aendelee na chuo au biashara.

MAJIBU:

Katika changamoto yako nimegundua kwanza kuna mambo makubwa matatu yanayokufanya ushindwe kuamua ni lipi sahihi unalopaswa kushika na kuachana na mengine, lakwanza ni ualimu ambao unasema ulisomea lakini moyo wako haukuwa kwenye ualimu, jambo la pili ni kusomea course ya manunuzi na ugavi (Procurement and Supply) ambayo unasema ndiyo moyo wako ulipo hasa lakini kuna jambo la tatu ambalo umesema ni biashara uliyoanzisha tangu ukiwa mwalimu na bado unaendelea kuifanya.

Sasa unataka ama uendelee na chuo au uamue kuzama moja kwa moja kwenye biashara yako na kuachana kabisa na mambo ya kuja kuajiriwa serikalini iwe ni ualimu au kwenye manunuzi na ugavi

Ushauri wangu kwako

Ushauri wangu ni kwamba, usiachane na hiyo ndoto yako ya kuendelea na chuo kwa ajili ya masomo ya procurement and supply kisa biashara uliyoanzisha hata kama unaona inalipa kiasi gani.

Jambo la busara ambalo unaweza kulifanya ni kuendelea kufanya mambo yote mawili kwa wakati mmoja kama ulivyokuwa ukifanya kwenye ualimu kwani inawezekana kabisa ukizingatia kazi ya ualimu ni lazima serikali itakuruhusu usimame kwanza kupisha hayo masomo yako mapya chuoni.

Kwanini nakushauri hivyo?

Fursa yeyote ile ya masomo kwa binadamu  kwa kawaida ni ya muda mfupi sana ukilinganisha na muda atakaokuja kuishi mtaani akifanya biashara au kwenye ajira. Watu wengi waliozichezea fursa za kukaa shuleni au chuoni kwa namna moja ama nyingine kuna nyakati katika maisha yao walikuja kuzijutia.

Kwani ukimalizia digrii (shahada) yako hiyo miaka 3 tu na kisha ukaja kuendelea na biashara zako ukiwa umeshahitimu course kuna tatizo gani?

Watu wengi sana siku hizi huponzwa na dhana iliyoenea dunia nzima kwamba, matajiri wengi hasahasa baadhi ya mabilionea wa Kimarekani na hata nchi nyinginezo mfano Uchina na Uingereza ni “drop outs” nikiwa namaanisha walikatisha masomo yao katika vyuo na vyuo vikuu na kwenda kuanzisha biashara ambazo hatimaye ziliwafanya wawe matajiri wa kutupa

Usahihi wa dhana hii ni mdogo sana ukizingatia hali halisi. Kwanza hii ni bahati na sibu zaidi kuliko uhallisia wenyewe, usidhani kila anayeacha shule/chuo basi moja kwa moja atakwenda kutoboa kwenye biashara, si rahsi kihivyo.

Utakuta katika watu labda 1000 ni asilimia % ndogo sana wanaoweza kufanikisha jambo hilo na hao ndio hawa kina Bill Gates, Mark Zuckerberg,  Steve Jobs, Larry Ellison, Richard Branson, Jay-Z na wengineo

Kwanza ni lazima ujiulize, Je mazingira ya watu hao kiuchumi na hata kijamii yanalingana na yale unayoishi wewe? Kwa mfano wengi wa hao mabilionea tunaosema wa Kimarekani kwanza walikuwa ni watu waliokuwa na asili ya utajiri tayari, wazazi wao aidha walikuwa na uwezo mkubwa kifedha au kielimu na hivyo kuwafanya maamuzi yeyote yale ambayo wangeliyafanya yasiweze kuwa na adhari hasi kwenye maisha yao.

Mtu kama Bill Gates tayari alikuwa na ‘exposure’ kubwa sana kwenye kompyuta shauri wazee wake walikuwa wataalamu waliobobea kwenye fani hiyo, hivyo aliachana na chuo kikuu pale Havard akiwa na uhakika kabisa kwamba alikuwa anakwenda kutoboa kwenye fani ya uinjinia wa programu za kompyuta.

Kwa bahati mbaya sana Dunia haina mazoea ya kutangaza sana hadithi za wale wanaofeli kimaisha, vinginevyo watu tungelistaajabishwa mno na idadi kubwa ya wale waliowahi kuanguka kimaisha baada ya kuacha masomo na kwenda kukimbilia kuanzisha ujasiriamali wakidhani watatoboa kirahisi

Ulimwengu wa biashara umejaa vihatarishi vingi mtu unapaswa kukabiliana navyo kabla hujatoboa rasmi na ikiwa hukujiandaa vyema au hauna uvumilivu ni bora usijaribu kujikita huko na kuachana na fursa ya masomo uliyokwisha itia mkononi kama yakwako.

Acha ajaribu mtu asiyekuwa na fursa hiyo ama yule mwenye maandalizi ya kutosha na mazingira yake yanampendelea kama walivyokuwa kina Bill Gates, Mark Zuckerberg,  Steve Jobs, Larry Ellison na Richard Branson.

Unaweza sema leo unaachana na chuo na ajira ya serikali ukafanye biashara zako kwa kuwa tu unao uhakika wa kuishi kwa mshahara uliokuwa ukiupata kwenye ualimu, lakini kumbuka utakapoacha na mshahara wa ualimu utakoma hivyo itakubidi uanze kutegemea faida ya biashara kwa matumizi yako binafsi ya kila siku, je, umeshajiandaa na hilo?

Na umesema kwamba una mkopo wa biashara unamalizia, sasa ikiwa hata biashara ilikuwa inategemea mkopo, huna mtaji toshelevu utakapoanza kutumia faida kwa matumizi ya kila siku biashara itaweza kuhimili hilo?. Mwaswali haya na mengine itakubidi ujiulize kwanza kabla hujafanya maamuzi ya mwisho.Kifupi fanya upembuzi yakinifu wa maana kwanza

Siyo nia yangu kukutisha usiingie mazima kwenye biashara ila ninachotaka tu kukuambia hapa ni kwamba, chuo kikuu siyo kama O Level au A level, unaweza kuwa ‘flexible’ ukaendelea na course yako huku ukifanya biashara mdogomdogo. Siku hizi fursa za biashara zisizomgharimu mtu muda mwingi ziko tele kutokana na maendeleo makubwa ya teknolojia ya habari na mawasiliano hasa kompyuta na mitandao ya kijamii.

Ukiwa Kigoma unaweza ukaagiza mzigo Dar es salaa bila ya kuufuata mwenyewe, ukaletewa na kuuza pasipo kuzunguka nao mtaani wala kuwa na fremu ya duka mahali kwa kutumia tu simu au kompyuta yako mpakato (laptop), tena katika muda wako wa ziada wa mapumziko au ukiwa nje ya kazi za darasani.

Ninachotaka kukueleza hapa ni kwamba, jaribu kuwa mbunifu kidogo usikubali kirahisirahisi tu kuachia fursa hii adhimu ya kupata ujuzi wa Manunuzi na ugavi utakaoishi na wewe milele.

Biashara ipo kila siku lakini kuja kupata ujuzi baadae umeshapiga teke fursa uliyoipata ni jambo gumu sana, kumbuka binadamu kadri miaka inavyosonga mbele na majukumu nayo huongezeka, leo una mtoto mmoja lakini mwaka kesho na keshokutwa utaweza kuwa na watoto 3, 4 na kuendelea.

Familia haitakuruhusu kirahisi ukafanye digrii yako ikiwa pengine kiuchumi hauko vizuri. Wakati huo pia sidhani kama fursa ya udhamini wa serikali itakuwa bado ikikusubiri, watakuwa wameshaidaka vijana wengine wapya kutoka form six nk.Hivyo ndugu yangu kabla hujafanya maamuzi yako juu ya jambo hili, pima mara mbilimbili matokeo ya uamuzi wako.

Mwisho

 ..........................................................


Tunatoa ushauri mfupimfupi kama huu kwa yeyote mwenye changamoto kwenye maeneo yanayogusa hasa biashara, ujasiramali na uwekezaji. Tuma changamoto yako kupitia;

Whatsapp/sms/call: 0765553030 / 0761002125

 

HUDUMA ZETU MBALIMBALI, VITABU & MICHANGANUO

 

(a) HUDUMA:

1. Kuandikiwa Mpango wa Biashara yeyote ile

-Gharama zetu ni rafiki kuanzia chini ya asilimia 0.5% ya mtaji wa biashara husika

2. Kuandikiwa Company Profile

-Gharama za huduma hii ni kuanzia Tsh. 50,000/=

3. Program ya Make Yourself Great Again 2025

-Ni group la whatsap na channel ya Telegram kwa ajili ya kujifunza jinsi ya kuandika michanganuo ya biashara, Ubunifu kwenye biashara, masomo ya fedha, mauzo na uwekezaji, Jiunge group la MAPOKEZI HAPA kupata masomo ya bure kwanza. VIP ni Tsh. 10,000/=

4. Usomaji wa Kitabu cha Think and Grow Rich kwa Kiswahili na kiingereza

-Ni Group maalumu na Washiriki ni wale wote waliowahi kununua kitabu cha Fikiri & Utajirike (Think & Grow Rich-swahili edition) cha karatasi (hardcopy) au nakala laini (softcopy)

 

(b) VITABU & MICHANGANUO:

1. Think & Grow Rich Swahili Edition:

Hardcopy ukiwa Dar es salaa ni Tsh. 25,000/= unaletewa mpaka ulipo, Mikoa mingine kwa basi ni Tsh. 32,000/= Kwa upande wa softcopy ni Tsh. 10,000/= nunua katika App hii ya GETVALUE kupitia kiungo hicho (bofya kununua)

2. Mafanikio ya Biashara ya Duka la Rejareja:

Nakala ngumu Tsh. 20,000/= Dar es salaa unaletewa ulipo, Mikoa mingine kwa basi ni sh. 30,000/= Kwa nakala laini (softcopy) ni sh. 10,000/= tunatuma kwenye simu au kompyuta yako unapolipia kwa namba, 0761002125 au unaweza kununua katika duka letu la mtandaoni la Selar.com kwa kubofya kiungo hicho

3. Michanganuo ya Biashara na Ujasiriamali:

-Hardcopy ni Tsh. 25,000/= Dar es salaa, Mikoa mingine kwa mabasi ni Tsh. 35,000/= Kwa upande wa softcopy lipia kupitia namba 0761002125 na tutakutumia kwenye simu au kompyuta yako bila kuchelewa popote pale ulipo duniani au nunua online moja kwa moja kwa kubofya hapa>>>Selar.com

4. Kwa Vitabu zaidi na Michanganuo ya Biashara kamili (Ready made Business Plans)

-Ingia kwenye duka letu la mtandaoni kwa kubofya kiungo hiki kifuatacho>>>SELF HELP BOOKS TZ

 

 

 

SOMA NA HIZI HAPA;

1.   Biashara & uwekezaji mwanafuzi anaweza kuanza akiwa chuo, kidato cha 5, 1, darasa la 1 hata chekechea

2.   Biashara nzuri 4 mwanachuo anaweza kufanya na mtaji wa laki 2 huku akisoma

3.   Kuanzisha biashara nikiwa chuoni nasoma nipeni ushauri nina wakati mgumu

4.   Maajabu ya kufikiri mambo makubwa na kwanini uweke malengo makubwa maishani

5.   Biashara ya laini na miamala ya simu kwa mwanafunzi wa chuo kikuu, mtaji laki 3 –ushauri

 

0 Response to "NATAMANI KUFANYA BIASHARA BAADA YA KUACHA UALIMU NA KUSOMEA UGAVI (PROCUREMENT)"

Post a Comment