BIASHARA YA LAINI NA MIAMALA YA SIMU KWA MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU, MTAJI LAKI 3 –USHAURI | JIFUNZE UJASIRIAMALI

BIASHARA YA LAINI NA MIAMALA YA SIMU KWA MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU, MTAJI LAKI 3 –USHAURI

Swali la mwanachuo

Wanafunzi wengi hasa wa vyuo wanatamani sana kufanya biashara wakiwa wangali hawajamaliza course zao mfano biashara ya uwakala wa m,itandao ya simu, na hili mara nyingi linatokana na sababu mbalimbali zikiwemo mwamko wa vijana wengi siku hizi wa kuwa na roho ya ujasiriamali hivyo wanaona kama vile wanachelewa kuanza ujasiriamali.

Lakini sababu nyingine kubwa ni mahitaji ya wanafunzi wengi kutokana na fedha kidogo wanazopewa na wazazi ama walezi wao ama mkopo kwa wanachuo kutokutosheleza mahitaji yao jambo linalosababisha maisha ya wanachuo hao kuwa magumu na kuamua kujitafutia fedha kupitia biashara mbalimbali halali.

Nimekuwa nikipokea maombi mengi ya ushauri toka kwa wanachuo mbalimbali na jinsi ya kufanya biashara, mfano ni kijana mmoja kutoka Chuo Kikuu cha TIA mwaka wa pili liyetaka kushauriwa biashara ya kufanya kwa mtaji wa laki 3 (300,000/=)

Hapa chini nimeweka mawasiliano yangu na yeye whatsap kama yalivyo bila ya kupunguza wala kuongeza kitu isipokuwa utambulisho wake kamili tu;

SWALI:

MWANACHUO: Habari za asubuh naitwa Imma..... Niko chuo kikuu TIA second year. Nina mtaji wa laki 3 tatu naomba msaada nifanye biashara gani ili niweze kuzalisha pesa naomba msaada wenu.. ushauri


MAJIBU: 

JIFUNZEUJASIRIAMALI: Nzuri Imma  na karibu,

Biashara utakayoifanya Ni lazima iendane na mazingira yako ya chuo isije ikaingiliana na muda wako wa masomo wala kukufanya ushindwe kwa namna yeyote ile kutimiza majukumu yako ya chuo.

Fanya utafiti kujua Ni kipi utaweza kufanya ukilenga wateja ambao wengi itabidi wawe ni wanachuo wenzako. Uzuri wa biashara hizi ndogondogo za uwakala au uuzaji bidhaa wala huhitaji leseni ya biashara  

Chunguza Wanachuo wana mahitaji gani makubwa ya vitu unavyoweza kwenda kununua na kuja kuwauzia mfano simu, mavazi nk. Unaweza kuwa wakala wa mitandao ya simu na kupata kamisheni. Cha msingi ni kujua jinsi ya kuwa wakala na kumiliki laini za uwakala wa hayo makampuni

Lenga biashara/bidhaa zisizoharibika upesi zisijekukupa presha ya kuuza haraka kwa bei ya chini.

Majibu

Unaweza kuchagua bidhaa hata 2 tu (pc 2) zenye ubora na za kipekee sana ukazifanyia marketing ya uhakika taratibu ukilenga kupata kila bidhaa faida hata ya sh. Elfu 10 mpaka15 tu hivi. Mtaji wa shilingi laki tatu 3 unatosha kuendesha biashara ya bidhaa chache ikiwa hutegemei pesa yeyote ya matumizi kutokana na hiyo biashara.

Zikiuzika unafuata nyingine hivyohivyo. Unaweza ukaamua kudili labda na viatu, suruali, simu, mikanda mikali ya kiunoni au chochote unachojua kuna wanafunzi wenye uwezo wa kuvilipia

Ni lazima hizi bidhaa ziwe za kipekee (unique) na siyo bidhaa mtu anaweza kwenda kutafuta kirahisirahisi tu. Tafuta sababu kubwa itakayomsukuma mteja wako kununua. Siku hizi kuna mpaka uwezekano wa kuagiza bidhaa toka nje mfano China nk. kupitia mtandao wa intaneti.

Mwisho kumbuka ukiwa chuoni kipaumbele/focus yako ni kukamilisha course yako zaidi ya kitu kingine chochote, mwaka wa chuo ni mmoja lakini utakuwa na miaka kibao huko mbeleni kufanya biashara zozote upendazo baada ya kuhitimu, hivyo biashara chuoni ifanye bila kuiwekea mategemeo makubwa kupitiliza usijekujikuta baadae unavunjika moyo vibaya endapo haitafanya vile unavyotaka ifanye.

Weka hatari kidogo kwenye hiyo biashara au risk tu kitu unachoweza kukubaliana na matokeo yake kwa urahisi yawe mazuri au mabaya.

IMMA:  Nashukuru, hapo kiukwer nipe wazo nianze na lipi japo wengi wanajikita kwenye laini na miamala unanisaidiaje kupitia biashara yoyote nipe plan mkuu

JIFUNZEUJASIRIAMALI: Uamuzi Ni wakwako kulingana na mazingira ulipo hata ukiona miamala ya simu, vocha na laini inafaa pia siyo mbaya kwani si vitu vya kuharibika na unaweza kuicontrol kwa urahisi. Vilevile ni bidhaa wanachuo hununua kila siku kwa wingi.

Kama nilivyotangulia kusema biashara yeyote simple inayokuhitaji wewe na begi lako tu chuoni inawezekana kufanya, kikubwa ni kujenga jina na wanachuo wajue bidhaa ama huduma fulani inapatikana kwako tu. Vifaa vya kielectroniki hasahasa vile kwa ajili ya mawasilianao ndiyo habari ya mjini nyakati tulizokuwana nazo sasa kwahiyo hutakuwa umefanya uamuzi mbaya kuchagua miamala ya simu na vifaa vyake kwa ujumla.

Nakumbuka kabla ya kuja simu za mkononi zamani mashuleni na vyuoni wanafunzi walifanya sana biashara ya upigaji wa picha za mnato kwa kutumia kamera aina ya YASHIKA, binafsi ninayo yakwangu mpaka hivi leo ingawa zimepitwa na wakati hazitumiki tena. Vitu ama vifaa vinavyotrendi / kwenda na wakati ni moja ya biashara nzuri sana ikiwa soko lako ni wanafunzi maana wanapenda kwenda na wakati.

Asante Imma Nikutakie mafanikio katika shughuli zako zote chuoni.


...................................................

Huduma za ushauri mfupimfupi kama huu huwa tunatoa Bure kwa mtu yeyote mwenye changamoto au maswali yeyote kuhusiana na Biashara au Ujasiriamali.

 

HUDUMA ZETU NYINGINE

1. UANDISHI WA MIPANGO/MICHANGANUO YA BIASHARA

Tunaandika Michanganuo ya Biashara kwa aina zote za Biashara kubwa na ndogo, huduma au bidhaa na gharama zetu ni rafiki. Walengwa ni mtu yeyote anayeomba nkopo kutoka katika Taasisi za fedha, kutafuta wabia na wawekezaji, kusajili kampuni au biashara au mtu yeyote anayehitaji mpango wa biashara yake kwa ajili ya uendeshaji mzuri wenye tija.

2. MAFUNZO YA JINSI YA KUANDIKA MPANGO WA BIASHARA

Tuna kifurushi cha masomo, vitabu na Michanganuo jumla vitu 14. Kifurushi hili ukikisoma unaweza kuandaa mpango wa biashara yeyote bila usaidizi wa mtu mwingine yeyote. Bei yake ya OFFA ni shilingi elfu 10 tu na unapata nafasi ya kujiunga na group la watsap la masomo na mentorship kwa mwaka mzima.

1. 3. VITABU VYA BIASHARA NA UJASIRIAMALI

Tunavyo vitabu mbalimbali kama ifuatavyo

1.   Michanganuo ya Biashara & Ujasiriamali = 10,000/=

2.   Mafanikio ya biashara Duka la rejareja  = 6,000/=

3.   Mifereji 7 ya fedha na siri Matajiri wasiyopenda kuitoa = 3,000/=

4.   Think & Grow Rich Swahili edition = 10,000/= kwenye app ya GETVALUE

5.   Sayansi & Sanaa ya Upishi wa chapatti laini = 5,000/=

Kupata Huduma yeyote hapo juu wasiliana na sisi kwa namba zifuatazo kupitia Simu, Whatsapp au Ujumbe;

0712202244 au 0765553030

Peter Augustino Tarimo

 

 

 

SOMA NA HIZI HAPA:

1. Biashara nzuri 4 mwanachuo anaweza kufanya na mtaji wa laki 2 huku anasoma

2. Ushauri kwa mwanafunzi aliyehitimu chuo/masomo anayetaka kuanza maisha

3. Kuanzisha biashara nikiwa chuoni nasoma nipe ushauri nina wakati mgumu

4.  Biashara ndogondogo zenye faida ya haraka tanzania ni hizi hapa, zipo nne(4)

0 Response to "BIASHARA YA LAINI NA MIAMALA YA SIMU KWA MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU, MTAJI LAKI 3 –USHAURI"

Post a Comment