BIASHARA & UWEKEZAJI MWANAFUZI ANAWEZA KUANZA AKIWA CHUO, KIDATO CHA 5, 1, DARASA LA 1 HATA CHEKECHEA | JIFUNZE UJASIRIAMALI

BIASHARA & UWEKEZAJI MWANAFUZI ANAWEZA KUANZA AKIWA CHUO, KIDATO CHA 5, 1, DARASA LA 1 HATA CHEKECHEA

Biashara mwanafunzi angali bado akisoma

Nimewahi mara nyingi kuulizwa swali hili na Wanafunzi hasa wale wa vyuo na sekondari wakati mwingine wakiomba ushauri ni biashara zipi wanaweza wakazifanya wangali wakiwa bado wanasoma. Kwa kweli hili swali nimelijibu mara nyingi katika post na makala zangu ndani ya blogu hii mtu yeyote anaweza akazifuatilia humo. 

Kimsingi katika majibu yangu hayo sijawahi kuwashauri wanafunzi kufanya biashara wakiwa wanasoma bali kujitengenezea mazingira fulani mazuri ya kiujasiriamali yatakayokuja kuwasaidia katika biashara na miradi yao hapo baadae pindi watakapohitimu masomo au course zao.

SOMA: Biashara nzuri 4 mwanachuo anaweza kufanya na mtaji wa laki 2 huku akisoma

Lakini pia kuna mazingira mwanafunzi anaweza akalazimika kufanya biashara angali chuoni au shuleni na ikiwa ni lazima basi mwanafunzi afanye biashara, inawezekana lakini ni lazima mwanafunzi huyo azingatie vigezo na masharti fulani fulani niliyoyaainisha kwenye hizo makala ili kuhakikisha hapotezi malengo yake ya kielimu ambayo ndiyo msingi na  focus yake kwa sasa.

Leo nitazungumzia jinsi ya kutengeneza au kumtengenezea mwanafunzi/mtoto wako mazingira mazuri  ya kiuwekezaji na biashara au kwa maneno mengine unaweza ukasema roho ya kijasiriamali tangu pale anapoanza masomo yeke iwe ni chekechea, darasa la kwanza, kidato cha kwanza, cha tano, chuo na hata chuo kikuu. Hujachelewa unaweza kuanzia darasa lolote lile kwani wengine huanza hata pale mtoto anapozaliwa siku ya kwanza.

Ingawa siku hizi karibu kila mtoto anayezaliwa hupata fursa ya kusoma shule, siyo watoto wote hufanikiwa kupata bahati ya kuajiriwa iwe serikalini ama hata sekta binafsi. Kwanza ieleweke wazi kwamba watoto wengi huishia ngazi za chini za elimu, mfano kidato cha nne, sita na hata vyuo vya kati vya elimu, ni wachache wanaohitimu shahada zenye soko zuri katika vyuo vikuu na kupata uhakika wa ajira.

Kusema ule ukweli ni vigumu mtu kukosa kabisa ajira endapo atasoma kikamilifu na kuhitimu course yenye soko inayohitajika mno katika jamii, tena isitoshe watu kila siku wanazeeka na kustaafu hivyo ajira zitaendelea kuwepo tu siku zote lakini kwa wachache waliosoma na kuhitimu vizuri kozi zenye uhitaji.

SOMA: Kuanzisha biashara nikiwa chuoni nasoma nipe ushauri nina wakati mgumu

Hebu tuachane kwanza na ajira, mimi nitajikita zaidi kwenye kundi lile la wengi wanaoishia ngazi za chini au hata elimu ya juu lakini hawajabahatika kusoma course zilizokuwa na soko la haraka. Ukiwa katika kundi hili bila shaka utakubaliana nami kwamba, ni lazima ujiingize kwenye ujasiriamali na hata ikiwa kama umefanikiwa kuajiriwa kipato chako kinaweza kisikidhi mahitaji ukashindwa kubadilisha maisha yako. Ujasiriamali utaweza kukupa kila kitu unachohitaji kiuchumi ukiufanya inavyotakiwa.

Jinsi ya Kutengeneza Roho ya Ujasiriamali

Mwanafunzi hata yule anayekwenda kuanza darasa la kwanza au shule ya vidudu Januari anapaswa kuanza kufanyiwa maandalizi ya kujengewa uwezo wa kijasiriamali na kiuwekezaji katika umri wake huo mdogo. Mlezi au mzazi ikiwa unataka mwanao umjengee msingi imara anzia hapa hapa na kuna vitu vingi tu unaweza ukavifanya kama nitakavyoeleza huko mbele kwenye hii makala.

Kwa upande wa mwanafunzi mwenyewe ikiwa tayari amekwishajielewa pengine ndiyo anakwenda kuanza kidato cha kwanza, kidato cha tano au chuo, kuna mambo kadha wa kadha anayoweza akayafanya katika kujenga mustakabali wake mwema kiuchumi hata ikiwa kama hatafanya biashara moja kwa moja au uwekezaji mkubwa. Hebu sasa tukaone ni mbinu zipi mzazi/mlezi au hata mwanafunzi mwenyewe anaweza akazitumia ili kujenga msingi bora wa ujasiriamali hapo baadae akimaliza masomo yake.

SOMA: Maana halisi ya ujasiriamali, ulikotoka, ulipo na unakoelekea duniani

Watu wazima waliokwishapita umri wa kawaida wa shule, wengi leo hii wanajutia sana ni kwanini hawakuzijua mbinu kama hizi au wazazi wao hawakujishughulisha kuwaandaa mapema kwani wasingelikuwa na hali za kiuchumi walizokuwa nazo sasa.

Kwa Mzazi/Mlezi 

Hata ikiwa mwanao unamwanzisha chekechea/ day-care , hakikisha unamfanyia kitu cha kuja kumsaidia huko mbele maishani mwake. Kumbuka kumpatia mtoto elimu tu peke yake hakutoshi, mjengee kitegauchumi/akiba itakayoweza kuja kuwa kama nyenzo kwake (backup) endapo lolote litaweza kuja kutokea hasa ikiwa kama huna uwezo mkubwa kiuchumi unaoweza kuja kuwahakikishia wanao ulinzi wa kutosha kiuchumi. Hatuombei mabaya lakini leo mzazi upo, na kesho inawezekana ukawa haupo tena duniani,  itamsaidia sana.

Mfungulie mtoto akaunti ya akiba benki kama zawadi ya kuanza masomo yake au bima ambapo zipo za aina mbalimbali kulingana na utakavyopenda mwenyewe. Hivi vitu ni vidogovidogo na unafanya polepole sana lakini vinaweza kuja kuwa na athari chanya  kubwa kwa maisha ya mtoto siku za mbeleni.  Au unaweza kuamua kuanzisha uwekezaji wowote ule wa muda mrefu kwa niaba yake ambao mapato yake utahakikisha yanawekwa mahali salama na huyagusi.

SOMA: Elimu ya fedha na umuhimu wake 2024 njoo tuunganishe nguvu tuhamishe milima!

Kwa wazazi wanaoishi vijijini au pembezoni mwa miji kidogo wanaweza wakaamua kuanzisha miradi mfano shamba dogo la miti kwa ajili ya mtoto, huu ni uwekezaji rahisi utakaochukua muda mrefu lakini una uhakika utakuja kumnufaisha mtoto moja kwa moja kiuchumi baadae.

Miradi si lazima iwe ya maelfu ya shilingi hapana, unaweza kwa mfano kuamua mwanao umuanzishie miradi midogomidogo mfano wa ile nitakayokwenda kuelezea hapo chini kwenye kipengele kinachomhusu mtoto/mwanafunzi mwenyewe.

Jambo jingine la msingi sana unaloweza kulifanya kwa mwanao ni kumfundisha stadi mbalimbali za ujasiriamali kama vile kujiwekea akiba hata kile kidogo sana anachokipata, kutumia muda vizuri, uaminifu, uvumilivu, msimamo na kuwa na kiasi mara zote. Mfundishe pia mtoto kwa vitendo kazi za kuingiza kipato unazozifanya wewe mwenyewe kipindi awapo likizo . Usisahau pia kumpa usaidizi na mentorship katika usimamizi wa miradi yake midogomidogo atakayoanzisha akiwa anasoma kama tutakavyoona hapo chini, mtie moyo.

Kwa Mwanafunzi / Mtoto mwenyewe

Hasahasa hapa inawahusu wale wa vyuo, kidato cha tano na sita, kidato cha kwanza –cha nne na hata waliomaliza darasa la 7 kwakuwa wameshaanza kujitambua tayari. Huwa siwahamasishi kabisa wanafunzi kufanya biashara yeyote ile labda mara chache kwa wale wa vyuo na vyuo vikuu kwenye baadhi tu ya biashara tena kwa mahesabu makubwa wasije wakajikuta wanahujumu muda wao wa course au masomo darasani.

Kabla sijaendelea kwanza kumbuka kwamba kinachowakwamisha sana vijana wengi katika kuanzisha shughuli za ujasiriamali pindi wanapokuwa wamehitimu masomo yao ni suala zima la mitaji na rasilimali za kuanzisha miradi/biashara hizo. Somo hili nalenga hasa kuchochea wazazi, walezi na wanafunzi wenyewe kutengeneza mbinu zitakazomsaidia mtoto kuja kuwa na uwezo wa kuanzisha biashara ikitokea hakupata ajira na mzazi /mlezi wakati huo pengine hana uwezo wa kumpatia hizo rasilimali.

Ikiwa bado hujapata ajira ni lazima ujiajiri na kujiajiri kunahitaji nyenzo (mtaji). Mtaji hata kama ni kidogo namna gani hauwezi kuupata kirahisi kama huko nyuma hukujiwekea akiba au kufanya matayarisho yeyote yale ya maana. Hakikisha kwa namna yeyote ile kile kidogo unachokipata unaweka sehemu ndogo kama akiba, akiba haijali kama wewe ni mwanafunzi au ni nani bali kanuni inasema tenga sehemu fulani ya kile upatacho iwe ni zawadi, ruzuku, kipato au hata pocket money unayopewa na mzazi/mlezi

SOMA: Kuanzisha biashara bila mtaji, hivi inawezekana au ni kutiana moyo tu?

Kumbuka sasa hivi wewe bado upo chini ya uangalizi wa wazazi/walezi au hata serikali inakupatia mkopo wa masomo, tumia fursa hiyohiyo kujiwekea akiba kidogokidogo.

Kama ni lazima ufanye biashara basi wekeza katika miradi midogomidogo isiyohitaji muda au uwepo wako wala kuingilia ratiba zako za masomo. Katika miradi hiyo, epuka miradi yenye hatari kubwa na pia usilenge kupata faida kubwa bali lenga zaidi kutunza fedha zako au na faida kidogo sana kwani huhitaji kuishi kwa kuitegemea hiyo biashara.

Unaweza ukaanza kununua hisa kidogokidogo kwa fedha za ziada unazozipata au biashara nyingine yeyote ile inayoendana na vigezo nilivyovitaja hapo juu kulingana na mazingira uliyopo baada ya kufanya utafiti wa kutosha. Ikiwa unaishi kijijini au nje kidogo ya mji unaweza kuanzisha ufugaji wa kuku wa kienyeji, nunua  kuku wachache hata 3 tu.  Mradi kama huu ni rahisi kuendesha kwani gharama ni banda la kulalia kuku usiku tu na kutagia pia chanjo mara chache hasa mdondo na dawa ya minyoo .

Chakula waache wajitafutie wenyewe na mtu yeyote ndani ya familia asichinje kuku wala kula mayai kiholela pasipo kulipa. Mapato yote yatokanayo na mradi huo yaweke katika akaunti maalumu ya benki kama akiba pasipo kuzitumia kwa jambo jingine lolote lile.

Mradi mwingine rahisi sana ni ufugaji wa ndege aina ya njiwa. Unaweza ukafuga njiwa wa kawaida kwa ajili ya nyama au njiwa wa mapambo. Uzuri wa njiwa ni kwamba hawahitaji gharama kubwa wala muda mwingi wa kuwaangalia.

SOMA: Utajuaje kama biashara yako ya kuku itakupa faida?

Ukishawazoesha njiwa kwenye banda lao dogo wataingia humo kila siku jioni na kutoka asubuhi huku wakizaliana kwa kipindi kifupi sana. Soko lao lipo kwani watoto wengine wengi mtaani watahitaji kuja kununua na kwenda kufuga pia. Mapato fanya kama nilivyoeleza kwenye kuku hapo juu.

Kuku na njiwa wa kienyeji hawana gharama za chakula kabisa labda tu mabaki ya vyakula na kazi kubwa ni kufunga na kuwafungulia mlango asubuhi na jioni, kazi ambayo mwanafamilia yeyote anaweza akaifanya pamoja na usafi wa banda mara chache kwa wiki. Ikiwa upo boarding waachie wazazi/walezi wakuangalizie mradi wako mpaka muda wa likizo utakaporudi nyumbani. Mlezi mwenye mapenzi mema hawezi kuacha mradi ufe kizembe ilihali na wewe mtoto unaonyesha tabia njema, utii na shauku ya mafanikio.

Nimechagua miradi hiyo 2 ya kuku na njiwa wa kienyeji makusudi ili kuonyesha umuhimu wa mwanafunzi kuchagua miradi isiyoweza kuingiliana na muda wake wa masomo wala kumpa stress za kupata hasara kwa urahisi, na hata ikitokea hasara uwekezaji wake ni mdogo mno kiasi cha kumpa mwanafunzi msongo wa mawazo ashindwe kuzingatia vizuri masomo yake.  Unaweza kubuni miradi mingine rahisi kulingana na mazingira yako uliyopo.

Kitu kingine mwanafunzi anachoweza kukifanya angali shuleni ni kutengeneza mtandao wa mawasiliano mazuri (networking) na watu mbalimbali wanaoweza kuwa msaada kwake siku za baadae. Nasema mawasiliano mazuri kwani kuna mawasiliano au mahusiano mengine ni haramu kwa mwanafunzi na yanayoweza kumtumbukiza kwenye majanga mfano mapenzi nk.

SOMA: Ushauri kwa mwanafunzi aliyehitimu chuo/masomo anayetaka kuanza maisha

Mfano nakumbuka tulipokuwa sekondari kuna rafiki yangu mmoja alikuwa anapenda sana kuandikiana barua na marafiki wa nje ya nchi (ughaibuni) wengine walimtumia zawadi mbalimbali mpaka wakati mwingine fedha za malipo ya ada. Mwishowe alipata rafiki wa kike nchini Sweden ambaye kwao walikuwa matajiri sana akamtumia mwaliko wa kwenda kuishi na kusoma hukohuko elimu yake ya chuo Kikuu. Alihama UDSM na kwenda Sweden ambako mpaka hivi leo anafanya kazi hukohuko na walikuja kuoana na yule msichana.

Simaanishi wanafunzi watafute wachumba mitandaoni hapana, bali wajenge mahusiano mazuri yenye malengo ya kuongeza zaidi uelewa wao kwa mambo mbalimbali yanayoendelea duniani ikiwa ni pamoja na fursa za kiuchumi wanazoweza kuja kuzifanyia kazi hapo baadae wakimaliza kusoma. Uzuri siku hizi mtandao wa Intaneti na akili bandia vimerahisisha mno watu kuwasiliana na kupata taarifa nyingi kwa muda mfupi

.............................................mwisho.....................................

 

 

OFFA MPYA KWA MWAKA 2024 (VITU 14)

Kifurushi cha Offa iliyopita kilikuwa na vitu 12 tu lakini hiki kina vitu 14, vitu vinaweza vikapunguzwa au offa kuondolewa muda wowote ule hivyo kwa watakaowahi itakuwa bora zaidi kwao. Huu ni mchanganyiko wa vitabu na michanganuo ya biashara mbalimbali iliyokamilika.

MALENGO YAKE:

1.   Kifurushi hiki kinalenga kumfanya anayekichukua kujifunza michanganuo ya biashara kwa kina kabisa ikiwa ni pamoja na kujiandalia mwenyewe mpango wa biashara yake bila kuhitaji usaidizi wowote.

2.   Unapojua kuchanganua biashara maana yake umejifunza biashara kwa ujumla wake kwani mchanganuo kamili wa biashara ni jumla ya vipengele vyote vinavyoihusu biashara kuanzia bidhaa/huduma mpaka soko na mpango mzima wa fedha.

3.   Kinalenga pia mtu yeyote mwenye ndoto ya kuwa mtaalamu aliyebobea katika uandaaji wa michanganuo ya biashara kwa wafanyabiashara wengine kama ilivyokuwa mimi mwenyewe, tazama hapa >KAZI ZETU , baadhi ya michanganuo niliyokwishawaandikia makampuni na biashara binafsi za watu mbalimbali

VIGEZO NA MASHARTI YA KUKIPATA KIFURUSHI HIKI:

·      Unalipia shilingi elfu 10 tu badala ya shilingi elfu 90 ukinunua kimoja kimoja na utatumiwa papo hapo kila kitu katika simu au kompyuta yako

·      Unapata fursa ya kuunganishwa Mastermind group la whatsap kwa ajili ya mentorship na masomo yenye maudhui ya fedha yasiyopatikana mahali pengine popote. Tuna masomo zaidi ya 100 na mwanachama utahakikisha unayapata yote 100 kabla ya muda wa group kuisha (miezi 12). Masomo haya humpa mtu uelewa mpana wa suala la fedha na saikolojia nzima inayolizunguka katika kuondoa na kuvunja imani potofu zinazomfanya mtu kutokusonga mbele

·      Ndani ya group kutakuwa na semina za kuandika michanganuo mifupi ya biashara zenye ubunifu wa hali ya juu kwa ajili ya kutengeneza na kukuza mitaji haraka kwa wajasiriamali wale wasiokuwa na sifa za kukopesheka na taasisi kubwa za kifedha.

·      Kaulimbiu yetu kwa mwaka huu wa 2024 ni; UBUNIFU NA AKILI BANDIA, VITUMIE KUBOOST BIASHARA YAKO VIWANGO VINGINE. Kwahiyo ukiwa ndani ya kundi hili utakuwa ukishiriki moja kwa moja katika kuhakikisha kauli hii unaitimiza kwa vitendo ili kuondoa kabisa vikwazo vinavyokudumaza siku zote usipige hatua ikiwemo suala zima la mtaji na rasilimali nyingine muhimu za kufanikisha biashara Dunia ya leo.

Haiwezekani kuanzisha biashara yeyote bila ya kuwa na mpango wa biashara hiyo kichwani au kwenye makaratasi, njoo ujifunze mbinu za kuweka mpango wa biashara yako yeyote ile na si lazima uandike makumi ya kurasa, unaweza kuuweka mpango wako huo kichwani tu na ikatosha kuendesha biashara yako kwa ufanisi mkubwa.

KUFANYA MALIPO KWA OFFA HII TUMIA MOJA KATI YA NAMBA ZETU 2 HAPA CHINI;

0712202244 AU 0765553030

Jina ni;

PETER AUGUSTINO TARIMO

 

VITU 14 VYA OFFA NI HIVI HAPA CHINI:

                           1.       KITABU: Michanganuo ya Biashara na Ujasiriamali chenye course zote muhimu za BIASHARA, jinsi ya kuandaa michanganuo ya biashara na sample za michanganuo mbalimbali 10 iliyokamilika kila kitu.kwa Kiswahili

                           2.       KITABU: Njia rahisi ya kuandika mpango wa biashara-dakika 30 tu - kwa kiswahili

                           3.      KITABU: Mifereji 7 ya Pesa na Siri Matajiri wasiyopenda kuitoa -kiswahili

                           4.       KITABU: HOW TO WRITE A BUSINESS PLAN  ni maarufu sana duniani, hutumika vyuo vikuu vingi.-kwa kiingereza

                           5.      KITABU: Siri za upishi wa chapati laini-UPENDO CAFE pamoja na Mchanganuo wake kamili.-kwa kiswahili

                           6.       COMPILLATION: Masomo 30 ya fedha usiyoweza kuyapata popote, mengine 70 utayapata kwenye group kila siku - kwa Kiswahili

                           7.      MCHANGANUO: Kiwanda cha usagishaji Dona (Usado milling) - kwa Kiswahili

                           8.      MCHANGANUO: Mgahawa wa chakula-Jane Restaurant –kwa kiingereza

                           9.      MCHANGANUO: Mgahawa wa chakula-Jane Restaurant –kwa Kiswahili

                        10.    MCHANGANUO: Ufyatuaji tofali za saruji- kwa kiswahili

                        11.    MCHANGANUO: Kuku wa nyama -Tumaini Broilerskwa kiingereza

                        12.    MCHANGANUO: Kuku wa nyama -Tumaini Broilerskwa kiswahili

                        13.    MCHANGANUO: Kiwanda cha mvinyo na juisi ya Rosella –Choya Investment – kwa kiswahili

                        14.    MCHANGANUO: Kilimo cha Tikiti maji:- Kibada Watermelon Fruits – kwa kiswahili

 

 

Simu/Whatsap:

0712202244 AU 0765553030

0 Response to "BIASHARA & UWEKEZAJI MWANAFUZI ANAWEZA KUANZA AKIWA CHUO, KIDATO CHA 5, 1, DARASA LA 1 HATA CHEKECHEA "

Post a Comment