KWANINI MIKOPO YA RIBA MITAANI, MICHEZO YA UPATU NA BAADHI YA VICOBA SI SALAMA KUJIUNGA? | JIFUNZE UJASIRIAMALI

KWANINI MIKOPO YA RIBA MITAANI, MICHEZO YA UPATU NA BAADHI YA VICOBA SI SALAMA KUJIUNGA?

Mikopo ya riba kubwa mitaani (Kaushadamu)

Biashara ya kukopesha pesa ni moja kati ya biashara kongwe kabisa duniani, miaka kwa miaka binadamu wamekuwa wakiazimana pesa kwa malengo mbalimbali tofauti. Hata kabla ya fedha kuvumbuliwa watu walikuwa wakikopeshana vitu au bidhaa mbalimbali wengine wakichaji riba (chajuu) na wengine walikopeshana tu hivyohivyo pasipo kudai chochote toka kwa mkopaji, mkopaji alitakiwa kurejesha kiasi kilekile alichokopa.

Ni miaka ya hivi karibuni tu au tuseme karne chache zilizopita biashara hii ilikuja kuchukuliwa rasmi na mabenki lakini hata pamoja na hivyo bado watu mmojammoja na vikundi kama vile vya upatu, saccos na viccoba wanaendelea na biashara hii. Uzuri wa biashara hii ni kwamba mtu unaweza ukaingiza kipato pasipo kufanya kazi kubwa sana endapo utaisimamia vizuri. Biashara za kukopeshana pesa zipo za aina mbili;

·      Mikopo isiyokuwa na riba

·      Mikopo yenye riba

1. Mikopo isiyokuwa na riba

Katika aina ya kwanza ya mikopo ndiyo iliyokuwa kongwe zaidi na ipo ya aina nyingi mojawapo ni ile ambayoi hufanyika zaidi baina ya watu mitaani katika vikundi visivyokuwa rasmi maarufu kama MCHEZO, michezo ya upatu sifa yake kubwa ni kutokuwa na riba isipokuwa mingine huwa na faini pale mkopaji anapochelewesha kulipa kwa wakati.

Lengo kubwa la mtu kucheza mchezo ni ili kuweza kupata mtaji au fedha kwa ajili ya kutimiza lengo fulani na kisha fedha hizo kuja kuzirejesha taratibu, lakini pia mchezo unamsaidia mtu kujijengea nidhamu ya utunzaji wa pesa kwani anapokuwa akiwachangia wenzake ni sawa na kuweka akiba kwa ajili ya matumizi yake ya baadae.

Kwahiyo kimsingi kabisa upatu lengo lake ni zuri sana na wala halina shaka yeyote isipokuwa madhara yake ambayo ndiyo tutakayokwenda kuyajadili na kuyafahamu kinagaubaga.

2. Mikopo yenye riba

Hii ni biashara kama zilivyokuwa biashara nyingine zozote zile, ila tu bidhaa inayouzwa ni pesa ili ikatumike kutengeneza fedha zaidi. Biashara ya kukopesha fedha kwa riba hufanywa na makundi yafuatayo;

1) Watu binafsi maarufu kama, MIKOPO YA RIBA MITAANI

2) Vikundi vilivyosajiliwa kama vile SACCOS, VICCOBA nk.

3) Mabenki na taasisi nyinginezo kubwakubwa za kifedha zikiwemo na hata Mataifa kwa Mataifa au nchi na nchi kukopeshana

Kabla hatujakwenda rasmi kuona NI KWANINI MIKOPO YA RIBA MITAANI, MICHEZO YA UPATU NA BAADHI YA SACCOS NI HATARI MTU KUJIUNGA, hebu kwanza tuone mikopo inavyofanya kazi;...............

 

........................................................

 

Ndugu msomaji wangu, somo hili kamili unaweza kulipata unapojiunga na mastermind group letu la masomo ya kila siku ya fedha (MICHANGANUO-ONLINE). Tuna mfululizo wa masomo yenye maudhui ya fedha zaidi ya mia moja (100+) usiyoweza kuyapata mahali kwingine kokote nje na ndani ya mtandao.

Unapojiunga tu hivi, unapata pia OFFA ya vitu 12 ambavyo ni vitabu na michanganuo ya biashara. Ndani ya group mbali na masomo hayo ya pesa lakini pia tuna vitu spesho kama vile semina za kuandika michanganuo bunifu ya biashara zinazolipa haraka Tanzania, mwanachama anayo fursa ya kuuliza swali lolote lile kuhusiana na biashara & ujasiriamali akapatiwa majibu ya kina na wanachama wengine akiwemo admin wenyewe wa group.

Group hili linaibua na kuchochea uwezo mkubwa wajasiriamali waliokuwa nao, ujasiri wa kutenda na kutekeleza majukumu mbalimbali ya kiujasiriamali ili kuleta matokeo chanya yaliyokusudiwa kwa wakati muafaka.

Kujiunga lipia kiingilio chako sh. 10,000/= kwa namba 0712202244 au 0765553030 Jina Peter Augustino Tarimo, kisha tuma ujumbe usemao;

“NATAKA OFFA YA VITU 12 NA KUUNGWA MASTERMIND GROUP”




SOMA NA HIZI HAPA;

1.  Ukisoma hapa hutahangaika kuwalamu mabenki na taasisi za fedha.

2.  Njia za kupata mtaji wa biashara unayoipenda.

3.  Mikopo midogomidogo ya biashara: kabla hujakimbilia kufuga ng’ombe anza angalao na kuku au bata kwanza

4.  Ni biashara ndogo yenye mtaji mdogo faida ndogo lakini inayokua upesi


0 Response to "KWANINI MIKOPO YA RIBA MITAANI, MICHEZO YA UPATU NA BAADHI YA VICOBA SI SALAMA KUJIUNGA?"

Post a Comment