Kwenye kipengele chetu cha Ushauri ama Uliza ujibiwe leo
tuna swali kutoka kwa msomaji wetu mmoja kutokea kule Babati Mkoani Arusha
aliyetaka kufahamishwa ni kiasi gani cha mtaji kinachotosha kuanzisha duka la
vinywaji mchanganyiko la jumla, soda, maji, bia, wine na pombekali.
Nimeliweka swali lake kama alivyouliza hapo chini bila
kuongeza wala kupunguza kitu chochote pamoja na majibu niliyompatia:
Kumbuka kuuliza maswali mafupumafupi ni bure kabisa, hatumtozi
mtu malipo yeyote yale wala kuweka jina kamili la muulizaji swali pasipo ridhaa
yake mwenyewe.
SWALI:
Habari
kwema?
Nipo
babati Nataka nifungue duka la jumla la vinywaji. ,,,,bia, soda, maji na pombe
kali nianze na mtaji wa sh,ngapi?
Tafadhali
naomba ushauri
MAJIBU:
Kwema kabisa ndugu yangu za huko Babati;
Biashara zote ikiwemo pia biashara ya kuuza vinywaji vya
jumla baridi/laini na pombe kali kanuni ya kutambua kiasi cha mtaji
unaohitajika kuanza ni moja tu na pia ni rahisi sana.
Kanuni hiyo huwa inatumika mara nyingi wakati mtu
unapokuwa ukiandaa mchanganuo wa biashara/business plan sura ile ya maelezo ya
biashara kipengele kidogo cha mahitaji ya kuanzia. Ukisoma katika kitabu changu
cha, MICHANGANUO YA BIASHARA NA UJASIRIAMALI kimefafanua vizuri sana ukurasa
ule wa 61 – 67 lakini hata hivyo hapa nitakuelekeza kwa kadri niwezavyo kwa
maneno machache kusudi uweze kufahamu.
Kwanza fahamu ya kuwa biashara moja haina kiasi mahususi
kimoja cha mtaji kila anayeanzisha biashara kama hiyo atalazimika kuanza nacho.Wewe
duka lalo la vinywaji vya jumla unaweza kuamua uanze na mtaji wa shilingi
milioni tatu (3) lakini mtu mwingine mahali pengine yeye akaamua biashara kama
hiyohiyo ya vinywaji vya jumla akaianzisha kwa mtaji wa shilingi milioni 100.
Tofauti hii hutokana na tofauti pia ya kimazingira baina
ya watu hao wawili nikimaanisha tofauti ya vitu kama soko, Uwezo wa rasilimali
alizonazo mtu, washindani, eneo, nk. Sekta ya vinywaji kwa ujumla imejaa washiriki
mbalimbali na kila mmoja hutofautiana na mwingine.
Ingawa wauzaji wa vinywaji vikali na laini vya jumla
wengi ni watu walio na mitaji mikubwa hata hivyo mtu unaamua kiasi cha mtaji
kulingana na mahitaji utakayoyaweka wewe kama mmiliki wa biashara husika.
Kwa mfano ikiwa unataka biashara yako iwe kubwa na uiweke
eneo zuri let's say labda Kinondoni
kama upo Dar es salaam utahitaji kuwa na mtaji mkubwa na ukitaka mfano kufungua
biashara ndogo tu ya vinywaji vya jumla labda eneo la Chanika mtaji wako unaweza
ukawa kidogo kutokana tofati za mizunguko ya watu katika maeneo hayo mawili tofauti,
vipato nk.
Vilevile duka la vinywaji vya jumla Dar es salaam na duka
kama hilo tuseme labda hapo Babati au Manyara utakuta kiasi cha mtaji hakiwezi
kulingana. Siyo jiografia tu peke yake inayoweza kusababisha tofauti ya mitaji bali
kuna vigezo vingine vingi kikiwemo uwezo wa yule mtu anayetaka kufungua biashara
husika. Unaweza kuwa upo kijijini lakini kutokana na sababu kwamba upo vizuri kimtaji
ukafungua bonge la duka la vinywaji vikali na vya kawaida kumzidi mtu mwingine aliyeko
katikati ya mji lakini yeye uwezo wake kimtaji ni mdogo.
Sasa
kanuni ni hii hapa;
Orodhesha katika daftari mahitaji yako yote kuanzia fedha
kwa ajili ya kusajili biashara yako, vifaa mbalimbali mfano mizani, mashelfu,
usafiri ikiwa utahitaji kuwa nao, gharama zozote zile utakazoingia iwe ni kumlipa
fundi wa kukukarabatia chumba chako cha biashara (fremu), dalali wa kukutafutia
fremu yennyewe na bidhaa zote unazotarajia kuuza kiasi na thamani yake.
Orodhesha bia ni kreti ngapi utataka kuanza nazo, maji
katoni ngapi, soda za pepsi & cocacola creti ngapi, soda nyinginezo za chupa
ya plastiki utanunua carton ngapi au chupa ngapi na pombe kali zikiwemo vodka, gin,
brandy na whisky ni kiasi gani kila moja bila kusahau na mvinyo (wine) za aina mbalimbali.
Kiasi cha kila aina ya bidhaa, vinywaji na pombe kali weka
makisio ya idadi ya chini kusudi mtaji usijekuwa mkubwa kupita kiasi vinginevyo
labda iwe unao mtaji mkubwa usiokuwa wa mashaka.
Mwisho jumlisha kupata jumla ya vitu vyote tokea pale mwanzoni
na huo ndio utakaokuwa mtaji wa kuanzishia biashara yako ya duka la vivywaji mchanganyiko,
vikali na vya kawaida.
Jinsi ya kufahamu bei na idadi ya bidhaa mbalimbali
itakubidi ufanye utafiti kupitia kwenda katika maduka kama unalotaka kufungua na
kuulizia taarifa mbalimbali kama bei nk. Angalia usiende moja kwa moja kwenye maduka
na biashara za washindani zilizokuwa karibu na mahali utakapoweka duka lako la vinywaji
kwani wakijua wanaweza wasikupe taarifa zozote muhimu au kukupa taarifa za kukupotosha.
Ikiwa utaenda basi chunga wasitambue kama unalenga kuwa mshindani wao. Maduka ya
mbali hawana shida na wewe ukiwaeleza unatokea mbali.
.........................................................................
HUDUMA NA VITABU VYETU:
1. HUDUMA: Tunaandika mchanganuo wa biashara yeyote ile kwa gharama rafiki sana Cheki hapa baadhi wa wateja wetu tuliofanya nao kazi. Ukihitaji tuwasiliane kwa namba 0712202244 au 0765553030
2. VITABU & MICHANGANUO YA BISHARA:
Kwa vitabu na Michanganuo zaidi tembelea, SMARTBOOKSTZ
3. DARASA (MASTERMIND GROUP MICHANGANUO-ONLINE):
Masomo ya fedha kila siku na semina za michanganuo bunifu ya biashara zinazolipa mara kwa mara. Kiingilio kwa mwaka ni sh. 10,000/= Unapata na offa ya vitu 12 vikiwemo vitabu na michanganuo ya biashara mbalimbali kama ifuatavyo;
1.
COURSE/SEMINA: (compiled
complete course) ya Jinsi ya
kuandika Mchanganuo wa biashara –(Ukishindwa
kuandika mchanganuo wako mwenyewe utarudishiwa pesa zako) - kwa kiswahili
2.
KITABU: Michanganuo ya Biashara na Ujasiriamali chenye course zote muhimu
za BIASHARA, jinsi ya kuandaa
michanganuo ya biashara na sample za michanganuo mbalimbali 10 iliyokamilika
kila kitu. – kwa kiswahili
3.
KITABU: Mifereji 7 ya Pesa na Siri
Matajiri wasiyopenda kuitoa -kiswahili
4.
KITABU: Siri za upishi wa chapati
laini-UPENDO CAFE pamoja na Mchanganuo wake kamili.-kwa kiswahili
5.
KITABU: Njia rahisi ya kuandika mpango wa biashara-dakika 30 - kwa kiswahili
6.
KITABU: HOW TO WRITE A BUSINESS PLAN ni maarufu sana duniani na ndio
hutumika vyuo vikuu vingi.-kwa kiingereza
7.
MCHANGANUO: Kuku wa nyama -Tumaini
Broilers - kwa
kiswahili
8.
MCHANGANUO: Kuku wa nyama –kwa kiingereza
9.
MCHANGANUO: Ufyatuaji tofali za
saruji- kwa
kiswahili
10. MCHANGANUO: Mgahawa wa chakula-Jane Restaurant –kwa Kiswahili
11. MCHANGANUO: Mgahawa wa chakula-Jane Restaurant –kwa kiingereza
12. MCHANGANUO: Kiwanda cha usagishaji Dona (Usado milling) - kwa Kiswahili
13. Kuunganishwa Group la
masomo ya kila siku ya fedha na michanganuo mwaka mzima ukitaka. (Mentorship group) (Ni hiyari yako lakini, usipotaka
hatukuunganishi)
Lipia offa yako kupitia
namba zetu, 0712202244 au 0765553030
jina, Peter Augustino Tarimo, kisha ujumbe watsap au sms usemao;
“NATAKA OFFA MPYA YA VITU 12”
Ukihitaji kuunganishwa na
group, kwenye ujumbe ongeza maneno; “NATAKA OFFA MPYA YA VITU 12 & GROUP”
Na utapata OFFA zako ndani ya dk. 3 tu
Thamani halisi ya offa hii
ni Tsh. 90,000/= lakini lipa Tsh. elfu 10 tu uokoe sh. 80,000/= !
Ukitaka kuthibitisha
uaminifu wetu bonyeza hapo chini kuona baadhi ya wadau wengine waliowahi
kuchangamkia offa na vitabu vyetu siku za nyuma bofya hapa>>>TESTIMONIALS
SOMA
NA HIZI HAPA:
1. Biashara ya vinywaji jumla, mtaji milioni moja (1) naomba
ushauri
2.
Biashara ndogondogo zenye faida ya haraka tanzania ni hizi
hapa, zipo nne(4)
3.
Mtaji wa biashara ya duka la rejareja: nianze na shilingi ngapi
ili nifanikiwe?
4.
Biashara ya soda maji juisi na sigara: tumia siri hii kuongeza
mauzo × 2
5.
Biashara ya kutembeza bidhaa za jumla madukani, mbinu 7
0 Response to "MTAJI WA BIASHARA YA VINYWAJI VIKALI & LAINI JUMLA NI KIASI GANI MFANO SODA, MAJI, BIA NA POMBE KALI? "
Post a Comment