MUHAMMAD, MTUME MKUBWA WA MWISHO DUNIANI | JIFUNZE UJASIRIAMALI

MUHAMMAD, MTUME MKUBWA WA MWISHO DUNIANI

Msikiti wa Makka

Najua unaweza kuwa unashangaa ni vipi blogu ya ujasiriamali inaandika tena makala zenye maudhui ya kidini na kujiuliza, “Vipi jamaa wamegeuka kuwa wahubiri nini?” 

Mimi kama mwandishi habari napenda sana kuandika ‘facts’ mambo yaliyotokea kweli au kutokana na vyanzo vya kuaminika na wala siyo riwaya.

UKWELI hauhitaji mtazamo binafsi wala maoni na ndio maana makala hii juu ya Muhammad (S.A.W.W.),  Mtume Mkubwa wa mwisho Duniani naiandika kwa kuzingatia muktadha wa kitabu cha Mwandishi Napoleon Hill kiitwacho Think & Grow Rich (Fikiri & Utajirike) nikiwasilisha ujumbe kama mwandishi mwenyewe alivyokusudia

Ninapomtaja Mtume Muhammad kuwa Mtume Mkubwa wa Mwisho sina maana kwamba leo hii hakuna watu wanaojiita Mitume na Manabii hapana, lakini ni ukweli usiopingika kwamba tokea kuja kwa Mtume Muhammad (s.a.w.w.), Dunia haijashuhudia tena Mtume mwingine aliyeacha alama kubwa na ya kudumu sawa na yeye, na isitoshe nimenukuu maneno sawa na ilivyoandikwa kwenye kitabu hicho cha Think and Grow Rich

Lengo kuu la Napoleon Hill la kukiandika kitabu cha Think & Grow Rich lilikuwa ni kufanya utafiti na kugundua kanuni za mafanikio ambazo hufanya kazi kwa kila mwanadamu aliyewahi kupata mafanikio makubwa hapa Duniani na hivyo kanuni hizo kuwa msingi wa wengine wote hata wale watakao taka kuja kufanikiwa siku zijazo

Bilionea  Andrew Carnegie mtu aliyemuagiza Napoleon Hill kutimiza jukumu hili zito la miaka 20 aliamini katika fikra zake kwamba, ni lazima zitakuwepo kanuni maalumu ambazo watu wote wanaofikia mafanikio makubwa maishani huzitumia kwa kujua au hata pasipo wenyewe kujua ikiwa wanazitumia.

Hatimaye Kanuni 13 zilizomo ndani ya Kitabu cha Think & Grow Rich siyo kwa ajili ya kumpatia mtu utajiri wa kifedha tu peke yake hapana, bali kanuni hizi pia mtu anaweza akazitumia katika kujipatia mafanikio kwenye nyanja nyingine zozote zile za kimaisha mfamo kiroho, kiimani, kifamilia, kiuongozi nk.

Kwahiyo Bwana Napoleon Hill katika kuwachunguza mamia ya watu mashuhuri waliofanikiwa, hakuishia tu kwa matajiri wa mali na fedha peke yake, bali pia aliwachunguza viongozi wakubwa wa kisiasa Duniani kama kina Mahatma Gandhi na Bismark, viongozi na waanzilishi wa Imani na dini mbalimbali kama vile akina Mtume Muhammad, Budha, Yesu Kristo, Confucius na wengineo.

Leo hapa nimeanza na Mtume Muhammad kiongozi na mwanzilishi wa Imani ya Kiislamu Duniani aliyeweza kupata mafanikio makubwa baada ya kupitia vikwazo vingi vya kutisha.

Usiniulize kwanini Uislamu kwenye kitabu hiki kwani dini nyingine zote kuu pia zimezungumziwa ndani ya kitabu na mwandishi, na ninaahidi katika kila imani iliyozungumziwa humo bila ubaguzi wowote ule nitaandaa makala yake maalumu siku zijazo Inshaalah!

Kama nilivyotangulia kusema, kitabu hiki siyo cha Dini isipokuwa tu mwandishi alitumia dini na imani mbalimbali katika kuelezea kanuni za mafanikio alizokuwa akizitafiti.

Na bila shaka Napoleon Hill alijitahidi sana kutokuonyesha upendeleo wa imani au dini yeyote ile (Biasness) na ndio maana hata utagundua kwenye kitabu hiki ikiwa utakisoma, alikwepa kabisa kutumia majina dini mbalimbali zinayomaanisha “MUNGU” mfano Allah, Mungu nk. na badala yake alitumia tu jina la, “NGUVU KUU ISIYOKUWA NA MIPAKA” (INFINITE INTELLIGENCE)  

Kwa ufupi kabisa nataka utambue ni kanuni zipi ndani ya kitabu hiki alizotumia Mtume Muhammad kutimiza kazi yake ya Utume aliyoagizwa kuifanya na Mwenyezi Mungu. Kumbuka kwamba MUNGU (Nguvu Kuu Isiyokuwa na Mipaka kama anavyoita mwandishi) hufanya kazi na binadamu kupitia njia zinazotambulika wazi na ambazo zimetajwa bayana kwenye kitabu hiki.

Njia hizo kitu cha kustaajabisha ni kwamba zilifanya kazi pia kwa Mitume na Manabii wengine wote wakubwa waliokuwa wamemtangulia Muhammad.

Mwenyezi Mungu anapotaka kuwasilina na mtu huwa hatumii njia nyingine tofauti na hizo zilizoelezwa humo kwenye hicho kitabu ukisoma vizuri.

Na wala si kwamba njia hizo zimegunduliwa na Napoleon Hill hapana, Napoleo Hill yeye alichogundua tu ni kwamba Mitume wote na Manabii wakubwa Duniani walizitumia kanuni na njia zilezile zinazofanana pasipo hata wao wenyewe kutambua ikiwa walikuwa wakizitumia.

Nitadokeza japo kidogo baadhi ya kanuni alizotumia Mtume Muhammad kwa mujibu wa mwandishi lakini kumbuka kitabu kina kanuni 13. Mojawapo ni ile kanuni ya 8, MSIMAMO, ambayo inapatikana Sura ya 9.

Ukisoma vizuri wasifu  wa Mtume Muhammad utabaini alikuwa ni mtu mwenye msimamo thabiti usioweza kuyumbishwa kirahisi, mfano ni pale alipokataliwa na jamii yake akaamua kwenda kuishi Jangwani kwa muda pasipo kusitisha dhamira yake ya kuendelea kuhubiri ujumbe aliokuwa ameagizwa na Mwenyezi Mungu. MSIMAMO wake ulikuwa ni mmoja tu, watu wote Duniani wamuamini Mungu mmoja.

Kanuni nyingine ni ile ya 13, MLANGOFAHAMU WA SITA inayopatikana Sura ya 14. Hii hasa ndiyo kanuni hutumiwa zaidi na Mitume na Manabii kutokana na uwezo wake wa kutenda Miujiza.

Waarabu ni watu wagumu sana kuamini miujiza lakini kitendo cha Mtume Muhammad ambaye wala hakuwa anajua kusoma na kuandika kuwa na uwezo wa kuelezea aya za Quran Tukufu kwa ufasaha na zilizokuwa na maneno yaliyogusa mno mioyo yao, ulikuwa ni muujiza mkubwa sana kwao usio na kifani.

Ingawa Mtume mwenyewe anakiri kuwa yeye si mtu wa miujiza, hakuna njia nyingine unayoweza kuelezea kitendo hiki cha Mtume Muhammad cha kushushiwa Aya za Quran Tukufu akiwa mapangoni kwenye Jangwa zaidi ya Muujiza ambao ndio mawasiliano ya Akili ya ndani ya mtu na Nguvu Kuu isiyokuwa na mipaka (MUNGU/ALLAH), mawasiliano yaliyoelezewa ndani ya kitabu cha Think & Grow Rich

Mtu yeyote yule anaweza akaitumia kanuni hii ya Mlangofahamu wa sita kufanya mambo makubwa mno maishani ikiwa ataamua, unaweza usiweze kufanya mambo makubwa sawa na alivyofanya Mtume Muhammad lakini angalao unaweza kufanya tofauti sana na watu wa kawaida tu wasiozingatia kanuni hii.

Sura hii ya 14 na zile zilizotangulia zinaeleza kwa kina utaratibu mtu unaoweza kuutumia kanuni hii ikakufanyia mambo ya kushangaza mfano hata kugundua hatari mbalimbali kabla hazijakupata nk.

Uliwahi nyakati fulani kumsikia mtu au wewe mwenyewe kuahirisha safari na kisha baadae ukaja kusikia gari uliyoghairi kupanda ilienda kupata bonge la ajali na watu wakapoteza maisha?

Kuna sauti fulani usiyoijua ilikuja na kukudokeza usisafiri (wakati mwingine watu huiita hali hii, ‘MACHALE’), unaweza kusikia mtu akisema machale yalimcheza akaghairisha safari.

Kwahiyo haya machale si kitu kingine bali mawasiliano ya Akili yako ya ndani na Nguvu kuu isiyo na mipaka. Ni watu wachache huwa na hali hii kwa kuzaliwa nayo lakini unaweza pia kuipalilia na kuwa nayo ukitaka.

Napoleon Hill anasema kwamba tofauti na zilivyo kanuni nyingine 12, mtu huwezi kukuza mlango fahamu wako wa sita ambayo ndiyo kanuni ya mwisho ya 13 pasipo kwanza kujifunza kanuni nyingine zote 12 zilizotangulia, kuna baadhi ya mafundisho ya kanuni hii yanapatikana pia kwenye hizo kanuni nyinginezo mfano kanuni ya 1, SHAUKU. ya 2, IMANI na ya 4, KUJISHAURI BINAFSI

Kwa maelezo zaidi kuhusiana na tabia za kipekee za Muhammad Mtume Mkubwa wa Mwisho usiache kusoma kitabu hiki cha Think & Grow Rich (Fikiri & Utajirike), wasifu wa Mtume Muhammad kama ulivyoandikwa na Mwandishi Essad Bey kwenye kitabu chake cha Wasifu wa Mtume Muhammad.

Uchambuzi huu mfupi wa hicho kitabu alioutumia Napoleon Hill ndani ya Think & Grow Rich uliandikwa na Thomas Sugrue katika Jarida la Herald Tribune

Ukitumia nakala ya kiingereza ni Sura ya 9, PERSISTENCE ukurasa wa 151 “THE LAST GREAT PROPHET

Na ikiwa unasoma nakala ya Kiswahili kilichotafsiriwa na Peter A. Tarimo ni Sura ya 9, MSIMAMO, ukurasa wa 260 “MTUME MKUBWA WA MWISHO

.................................

 

FIKIRI & UTAJIRIKE

Maoni yangu mimi Binafsi kama Peter:

Kitabu cha Think and Grow Rich nimewahi kukisoma na kukirudia mara nyingi. Kusema ukweli, binafsi kimenipa faida nyingi mno na hasa kwenye upande wa kujitambua Binafsi hasahasa kwenye masuala yanayogusa hisia (kufikiri) na Imani.

Masuala ya kiimani na kihisia dunia ya leo yamekuwa ni vitu vinavyowahangaisha watu wengi sana hata wakati mwingine kusababisha maradhi mbalimbali, mitafaruku ya kijamii na hata umasikini wa kutisha

Ukisoma kitabu hiki utagundua kwamba maamuzi mengi tunayofanya hutokana na imani zilizojichimbia ndani ya akili zetu, hivyo kuna hatari kubwa sana mtu unapokuwa na imani fulani potofu kwenye akili yako.

Kwa mfano ikiwa utaamini baba/mama yako mzazi anakuloga uugue itakuwa hivyo kweli hata kama ikiwa wazazi wako hao hawana uchawi wowote ule

Utaugua magojwa ambayo ni matokeo ya imani uliyokuwa nayo juu ya hao wazazi wako na mwishowe unaweza hata kuchukua hatua ya kuondoa uhai wao.

Ukisoma hiki kitabu ukakielewa vizuri hautakaa uyumbishwe kabisa na masuala yahusuyo Imani kamwe, utabaini kuwa Imani zote Duniani zina pande kuu 2, UWONGO na UKWELI. Imani yeyote ni ya kweli kwako ikiwa unaiamini lakini ikiwa huiamini basi imani inakuwa ni ya uwongo kwako

Ukweli huu utakufanya kutokugombana na jirani yako wa imani tofauti hata siku moja na utadumu na Imani yako huku ukiheshimu imani za wengine bila chuki yeyote hata kama unaona imani zao ni za uwongo sawasawa tu na wao pia wanavyoona imani yako ni ya uwongo

Utabaini pia kwamba katika kila Imani, kila dini mtu unaweza ukafanya miujiza ilimradi tu umezingatia kanuni maalumu ambazo siyo za siri na zimethibitishwa kisayansi kwamba zinaweza kufanya miujiza.

Kanuni kwa mfano ile ya Kujishauri binafsi (Autosuggestion) mtu unaweza ukaitumia ukichanganya na baadhi ya nyingine mfano Mlango fahamu wa 6 na Imani zikakufanyia maajabu makubwa!

Zaidi ya yote kitabu hiki kwa anayetaka kutajirika kifedha pia matumizi ya kanuni zilizoko ndani yake kwa usahihi zinaweza kukupatia kiasi chochote kile cha utajiri uutakao wewe, sawa na wale utakaosoma mifano yao ndani ya kitabu.

 

Kundi la Usomaji wa Kitabu cha Think & Grow Rich

Nimeanzisha Kundi maalumu la usomaji wa kitabu cha Think & Grow Rich ambapo tutasoma kitabu hiki kuanzia mwanzo mpaka mwisho katika Lugha zote mbili Kiswahili na Kiingereza

Sifa za mshiriki ni kuwa na nakala ya Kiswahili au ya Kiingereza ya kitabu hicho kutoka kwangu mwenyewe. Nikikupatia nakala ya kitabu haijalishi ni ya Kiswahili au ya kiingereza, moja kwa moja unaweza kujiunga na kundi


Nakala ya kiingereza ni Bure

Nakala ya Kiswahili inapatikana kwa malipo kwa utaratibu ufuatao;

NAKALA NGUMU(HARDCOPY) ukiwa Dar es salaa ni Tsh. 25,000/= unaletewa mpaka ulipo. Na Mikoa mingine ni Tsh. 35,000/= Tunatuma kwa basi au Boti

NAKALA LAINI (SOFTCOPY) ukiwa popote pale Duniani ni Tsh. 10,000/= na kinapatikana kupitia App ya GETVALUE bonyeza kiungo hicho kununua sasa hivi.

 

NAFASI 10 TU ZA OFFA!

Kwa watakakubaliwa kuingia kundi hili na kitabu cha Kiingereza ni watu 10 tu wa mwanzo watakaolipia programu ya 2025 MAKEYOURSELF GREAT AGAIN Tsh. 10,000/= siku ya kesho Jumamosi na keshokutwa Jumapili. Baada ya hapo Ofa itafungwa

PROGRAMU YA 2025 MAKEYOURSELF GREAT AGAIN ni kundi jingine linaloendelea ambalo washiriki hujifunza kila siku jinsi ya kuandaa mipango ya biashara, fedha, masoko nje na ndani ya mtandao, mauzo, uwekezaji, ubunifu kwenye biashara ndogondogo ili kukuza mtaji haraka, Biashara za rejareja na michanganuo ya biashara zinazolipa upesi.

Kiingilio ni Tsh. 10,000/= na unapatiwa Vitabu na Michanganuo ya Biashara jumla vitu 10 kwa ajili ya Rejea kikiwemo Kitabu cha kurasa 430 cha MICHANGANUO YA BIASHARA NA UJASIRIAMALI.

Unapata pia mafunzo kamili ya siku 7 ya uandishi wa mpango wa biashara kwa vitendo

Unaweza kujiunga kwanza group la MAPOKEZI HAPA ambalo pia unapata bure kabisa Basic course on Business planning (masomo 12 ya msingi ya jinsi ya kuandika mpango wa biashara yeyote ile) wakati ukisubiri kujiunga na VIP CLASS

 

Offa ya kesho na keshokutwa kwa Think & Grow Rich ikiisha, kujiunga na magroup yote mawili lile la usomaji wa Think & Grow Rich na la MAKEYOURSEL GREAT AGAIN itakuwa jumla ni Tsh. 20,000/= kwa anayenunua nakala laini na Tsh. 35,000/= kwa 45,000/= kwa wale wa nakala Ngumu

0 Response to "MUHAMMAD, MTUME MKUBWA WA MWISHO DUNIANI"

Post a Comment