Unaweza kushangaa ni kwanini nimetaja changamoto za
nyanya kidogo msimu wa masika wakati inafahamika wazi kwamba kipindi hicho
kilimo cha nyanya ndiyo wakulima wengi huacha kulima kutokana na changamoto
lukuki za magonjwa hasa yale ya ukungu na bacteria pia kudondoka kwa maua na
kupasuka kwa matunda ya nyanya kunakosababisha hasara kubwa
Lakini pamoja na changamoto hizo za kilimo cha
nyanya msimu wa masika bado kulima nyanya na kupata mavuno mazuri ni jambo
linalowezekana na ndiyo maana utakuta kipindi hicho sokoni nyanya zipo lakini
bei yake ni ya juu sana nyanya mmoja rejareja mpaka sh. 300. Hebu jiulize kwani hao wanaovuna nyanya kipindi cha
masika nyanya zao hulima Sayari nyingine?
Ikiwa jibu ni hapana wanalima hapahapa sayari yetu ya
Dunia, basi jiulize tena swali la pili, kwani wao hutumia mbinu gani wakulima
wengine wengi wanashindwa kuzitumia na kubwaga “manyanga”?
Kwanini
sasa mimi niseme hizo changamoto ni kidogo kuliko faida zake?
Katika biashara yeyote ile duniani mjasiriamali
anachopaswa kuangalia kwanza kabla ya vitu vyote ni SOKO. Ikiwa soko lipo la
uhakika kwa bidhaa ama huduma fulani ni juu yako wewe mjasiriamali kuhakikisha
unatumia kila njia inayowezekana kulisambazia bidhaa/huduma hiyo, wala haijalishi
ni changamoto kiasi gani utakazokumbana nazo
Kitu kikubwa kinachohitajika hapa ni ubunifu wa
kukabiliana na changamoto hizo na siyo kuogopa na kurudi nyuma. Ikiwa kuna
wateja wa kutosha na faida nono mimi hapo sioni changamoto bali naiona fursa
kubwa ya kuingiza fedha nyingi kwani kila ugunduzi wa jambo duniani ulianza
kwanza baada ya watu wachache kuona changamoto zilizokuwa zikiwatesa binadamu
kwenye maisha yao ya kila siku ndipo wakaamua kubuni suluhisho la tatizo huku
wengine wengi wakiona tatizo lile kamwe isingeliwezekana kulitatua
Hebu fikiria Mtu akiyefariki mwaka 1995 leo hii ingeliwezekana
akafufuka ukamwambia unachati ‘live’
whatsapp na mtu alieko Songea wewe ukiwa Kagera tena muda huohuo unamtumia na
pesa kwa simu hawezi kukuelewa kabisa kwani kipindi hicho alihitaji wiki nzima
kutuma barua na Money Order iliyochukua pia wiki nzima kumfikia, hata hivyo
watu wachache waliliona lile tatizo ndio maana leo hii tuna ‘enjoy’ teknolojia hizi mpya za
mawasiliano, kompyuta na intaneti
Vivyo hivyo na ugumu wa kulima nyanya za masika nao ni
changamoto kwa watu wengi lakini watu wachache wabunifu haziwezi kuwazuia
kulima nyanya
Sasa nisikupotezee muda wako mwingi twende tukazione hizo
pande mbili za sarafu, faida na changamoto za nyanya kipindi cha mvua nyingi za
masika au hata elnino ukipenda kwani
mwaka huu pia mamlaka za hali ya hewa duniani zimetabiri uwepo wa mvua nyingi
za El nino (2026–2027)
FAIDA ZA KILIMO CHA NYANYA WAKATI WA MVUA NYINGI (MASIKA)
1.
Bei Kubwa na Faida Nono Sokoni (Super Profits): Huu ndio mkosi na baraka ya msimu
huu. Wakulima wengi wanaogopa kulima masika kwa sababu ya magonjwa, hivyo
nyanya inakuwa adimu sana sokoni. Ukifanikiwa kuvuna nyanya zako vizuri, utauza
kwa bei ya juu mara mbili au tatu ya bei ya kawaida ya kiangazi
2.
Soko la Uhakika na Haraka: Hauhitaji kutafuta wateja; wao ndio watakaokusaka hadi
shambani kwako. Nyanya inagombaniwa kwa sababu ugavi/supply unakuwa mdogo wakati
mahitaji/demand yanakuwa vilevile au kuongezeka
3.
Kupungua kwa Gharama za Umwagiliaji (Zero Irrigation Cost): Hutatumia gharama yeyote ya mafuta
ya pampu, umeme, au nguvu kazi kwa ajili ya kumwagilia shamba. Mvua inafanya
kazi hiyo bure, jambo linalookoa muda na pesa nyingi za uendeshaji. Ule muda,
nguvu na rasilimali za kumwagilia shamba wewe unazielekeza kwenye huduma
nyingine kwa ajili ya nyanya zako
4.
Kutoweka kwa Wadudu Wanaopenda Ukame: Wadudu hatari kama Utitiri Mwekundu (Red Spider Mites), Nzi weupe(White flies), Vidukari
/ Wadudu mafuta (Aphids) na Chawa wa
Mimea (Thrips) ambao husumbua sana kiangazi na kukausha nyanya,
wanapotea kabisa masika kwa sababu hawapendi unyevu na wanaoshwa na mvua
5.
Ukuaji wa Haraka wa Mimea: Udongo ukiwa na unyevu wa kutosha na kukiwa na joto la
wastani, nyanya hukua kwa kasi kubwa, kutoa matawi mengi, na kuwa na majani
yenye afya na rangi ya kijani iliyokolea haraka kuliko kiangazi
CHANGAMOTO ZA KILIMO CHA NYANYA WAKATI WA MVUA NYINGI
Gharama kubwa za kemikali (Dawa za kuzuia ukungu): Utalazimika kununua dawa nyingi za ukungu za kimfumo (Systemic Fungicides) kama Ridomil, Master kutu au Amistar, ambazo ni za bei ghali. Pia unalazimika kupiga dawa mara kwa mara jambo linaloongeza gharama ya uzalishaji
1. Mlipuko wa Magonjwa Hatari ya Fangasi na Bakteria mfano:
· Bakajani Tangulia (Early
Blight):Unasababishwa na fangasi Alternaria solani.
Huweka madoa ya mviringo kwenye majani ya chini na mashina. Majani hugeuka
manjano na kudondoka
· Baka Jani Chelewa (Late Blight): Ugonjwa huu unaweza kuangamiza shamba zima ndani ya muda
mfupi tu kukiwa na baridi na mvua
· Mnyauko wa Bakteria (Bacterial Wilt): Bakteria walio kwenye udongo hushambulia mizizi na
kukausha mmea ukiwa kijani na hauna tiba
2.
Kupukutika kwa Maua (Flower Drop): Vishindo vya matone ya mvua yanapiga na kukatisha maua
machanga. Pia unyevu unagandisha chavua, na kuzuia uchavushaji, hivyo mmea
unatoa maua lakini hayatoi matunda
3.
Matunda Kupasuka (Fruit Cracking): Nyanya inapofyonza maji mengi ghafla kutoka kwenye udongo
uliolowa, nyama ya ndani inatanuka kwa kasi kuliko ngozi ya nje, na kusababisha
nyanya kupasuka zikiwa mbichi na kuanza kuoza
4.
Kuoza kwa Mizizi na Kukwama kwa Lishe (Waterlogging): Udongo ukijaa maji mfululizo unakosa
hewa. Mizizi inalegea (suffocate), inaoza, na mmea unashindwa kufyonza mbolea
uliyoweka chini, hivyo unaanza kugeuka njano na kudumaa
5.
Uharibifu wa Miundombinu na Mazao: Mvua kubwa za masika au El-nino zinaweza kusababisha
mafuriko yanayosomba miche au mmomonoko wa udongo unaosafisha mbolea na
virutubisho vyote vya juu vya udongo
HITIMISHO:
Kilimo cha
masika ni "High Risk, High Return" (Hatari ni kubwa, lakini
Faida ni kubwa mno). Wakulima wanaofeli ni wale waoga ama wanaolima kienyeji
bila ya kutumia ubunifu wowote wala teknolojia zinazoweza kupunguza au kuondoa
kabisa changamoto zilizopo
Kama
mjasiriamali mbunifu una nafasi kubwa sana ya kuwa mmoja wa washindi
watakaomiliki soko msimu huu ujao wa masika !
Nimeandaa
darasa la vitendo kwa ajili ya nyanya za masika hususani mwaka huu wenye mvua
za El nino kwani tunatarajia masika kuwa ndefu kidogo, badala ya kuona majanga
sisi tunaona fursa kubwa! Ni wakati wa wasio na mitaji kupata mitaji kirahisi
kupitia kilimo cha nyanya. Kama mtaji wako ni kidogo mno hama mjini kwa muda,
hamia kijijini au pembezoni mwa mji ukipata mtaji wa uhakika utarudi mjini upya
Mkakati wangu
siyo wa kawaida hivyo darasa langu hili halitafanana kabisa na darasa jingine
lolote lile ulilowahi kuliona. Natambua madarasa ya nyanya yapo mengi
mitandaoni, kwenye magroup ya watsap, facebook, telegram, Google meet,
community mbalimbali nk. lakini hili tofauti yake kubwa ni VITENDO
Toka nimeanza
utafiti wa zao hili kikamilifu nina mwaka sasa kijijini namimi nilihama mjini
kwa muda , nimeotesha nyanya za majaribio huu ni masimu wa tatu na masika
utakuwa msimu wa nne. Kila nikivuna nyanya nasia nyanya, zote kwa ajili tu ya
majaribio ili niweze kupata fomula nzuri kwa wanafunzi wangu ya kuotesha nyanya
kwa ajili ya kupata faida kubwa na sio tu kuuza kujikimu kimaisha
Mimi mkakati
wangu mkubwa siyo kufundisha “jinsi ya
kulima nyanya” bali nafundisha JINSI
MJASIRIAMALI MWENYE MTAJI KIDOGO AU ASIYE NA MTAJI KABISA ANAVYOWEZA KUPATA
MTAJI KUPITIA KILIMO CHA NYANYA ZA MASIKA
Maana kama ni
kujifunza jinsi ya kufanya kilimo cha
nyanya watu wengi wameanza kujifunza tangia wakiwa shule za msingi /
sekondari na sasa kwenye mitandao na vitabu mbalimbali, sasa mimi nitakuja na
jipya gani?
Nakusihi ikiwa
umevutiwa na darasa hili basi usikose hata siku moja kujipatia elimu hii ya
bure kabisa hapa kwenye blogu yako hii ya jifunzeujasiriamali pamoja na
mitandao yetu mingine ya kijamii kama facebook, Insta, Whatsapp group na You
tube
Na ikiwa upo serious zaidi unaweza ukachangia darasa
letu maalumu la VIP ambalo utapata nyenzo muhimu kwa ajili ya kilimo cha nyanya
za Masika/El nino kama vile Michanganuo kamili na halisi ya kilimo cha nyanya
za masika katika eneo la wazi na katika Green house ya gharama nafuu, pia
Muongozo kamili wa kutengeneza Greenhouse ya gharama nafuu na ya kipekee kwa
wenye mitaji kidogo (Haijafika bado
Tanzania, ni China, Israel, Pakistan na Marekani tu mpaka sasa zinatumika)
HUDUMA ZA MALIPO
(1)
Gharama ya VIP class ni TZS
10,000/= msimu mzima mpaka masika na El-nino zinamalizika, Utapewa na mchanganuo
wa Kilimo cha nyanya za masika Eneo la wazi (Open space) bure
(2)
Mchanganuo wa kilimo cha nyanya ndani ya Greenhouse ya gharama nafuu
pamoja VIP Class ni TZS 10,000/=,
Unapata bure Muongozo wa kutengeneza Greenhouse ya bei nafuu hatua kwa hatua na
darasa live la jinsi ya kutengeneza greenhouse hiyo kupitia video
(3)
Ukitaka huduma zote mbili (2) utapata offa ya kulipia sh. 15,000/= badala ya sh. 20,000/=
Mwisho wa
kupokea wanafunzi ni muda wa kuhamisha miche ya nyanya tutakazosia hivi punde
utakapofika, andaa mbolea iliyopoa kidogo ya kuku, ngombe au samadi kwa ajili
ya kitalu nitafundisha karibuni namna ya kuandaa kitalu cha nyanya kwa vitendo
Namba ya
Malipo ni; 0761002125 Jina: Peter
Augustino Tarimo
(4)
Ikiwa bado upo mjini hujaamua
kuhama kwa muda na unahangaika kupata mtaji wa biashara ya ndoto yako bila
mafanikio, pakua kitabu hiki hapa cha>>> MAFANIKIO YA BIASHARA YA DUKA LA REJAREJA NEW TECH EDITION ujue siri
nilizotumia mimi mwenyewe Kariakoo kumiliki duka lenye wasaidizi 2 ndani ya
mwaka 1 tu nikianza na bidhaa chache ‘kibarazani’ nje ya duka la mtu
SOMA NA HIZI HAPA;
1.
Maana kamili ya ujasiriamali:
ulikotoka, ulipo na unakoelekea duniani
2.
Biashara 7 nzuri mwaka 2019: chagua 1 uingize faida na kipato
cha ziada kwa urahisi
3. Ujasiriamali: ubunifu ndiyo msingi wake mkuu na injini ya uchumi katika soko huria
4.
Biashara yenye mtaji mdogo
isiyojulikana na watu wengi bado-1
5.
Kuku wa nyama broilers: kwanini faida na gharama za ufugaji
zinavunja moyo?
6.
Mafunzo matano (5) ya jinsi ya kuanzisha biashara toka mwanzo
mpaka mafanikio
7.
Changamkia fursa hii mpya ya mazao ya tikiti mahindi, maharage
nyanya na mbogamboga
8.
Mchanganuo wa biashara ya genge la kisasa la matunda,
mbogamboga na vyakula
10. Siri ya kupata mtaji wa biashara kirahisi kwa mjasiriamali
mdogo asiye na dhamana mjini na kijijini


0 Response to "KWANINI ULIME NYANYA MSIMU WA MVUA ZA MASIKA? ZIJUE FAIDA ZAKE NYINGI NA CHANGAMOTO KIDOGO"
Post a Comment