Kuna aina nyingi za uandishi
wa mpango wa biashara kutegemeana na lengo lako la kuandika. Ijapokuwa faida za
kuandika mpango wa biashara ni nyingi na muhimu zaidi ikiwa ni kusaidia katika
uendeshaji wa biashara yenyewe kwa ufanisi, lakini watu wengi sana na siyo hapa
Tanzania tu peke yake wamezoea kuandika mpango wa biashara au kutafuta
wataalamu wa kuandika andiko hili pale tu wanapokabiliwa na jukumu la kuomba
mkopo benki, kutafuta mwekezaji au wanapotakiwa popote pale kuwasilisha mpango
wa biashara kwa madhumuni yeyote mengine.
Leo nimelenga zaidi
kuzungumzia namna ya kuandika mpango wa biashara kwa madhumuni ya kuomba mkopo
wa benki au taasisi nyingine za kifedha. Wajasiriamali wengi huona ni jambo
gumu sana kuandaa mchanganuo wa biashara hasa pale unapokuta mjasiriamali
hajawahi kulifanya zoezi hili siku nyingine, huwa wanajiuliza maswali mengi
kama vile; naanza anzaje kuandika mpango
wa biashara? Nitakokotoa vipi mahesabu
ya mpango wangu wa biashara? Nitajuaje
ikiwa kila kitu nimeandika kwa usahihi? nk.
Ikiwa na wewe ni
miongoni mwa hao walio na mashaka kama hayo
basi nikukumbushe tu kwamba haupo peke yako, hata na mimi kuna wakati
nilikuwa kama wewe na isitoshe leo wasiwasi wako wooote utakwenda kuyeyuka kama
bonge la barafu…….Na ikiwa mpango huo unauhitaji kwa ajili ya kouombea mkopo
mahali basi fuatana nami mpaka mwisho wa makala hii.
Kwa kawaida mpango wa
biashara umegawanyika katika vipengele mbalimbali na vilevile unaweza
kuvigawanya vipengele hivyo katika sehemu kadhaa. Kwahiyo kabla ya kuanza
chochote ili kurahisisha kazi ya kuandika mpango wowote ule wa biashara ni
lazima kwanza ugawe vipengele au sehemu hizo na uanze kuandika ukilenga
kipengele kimoja baada ya kingine na hatimaye sehemu moja baada ya nyingine.
Hapa chini nitakwenda
kukuangazia hatua kwa hatua mchakato mzima jinsi unavyoweza kuanza mpaka
unamaliza kuandika mpango wa biashara wenye sifa ya kushawishi benki, wafadhili
au wawekezaji katika biashara au kampuni yako.
Ingawa Mpango wa
biashara hauna idadi maalumu ya vipengele lakini mara nyingi una vipengele 8 au 9 kulingana na
vile utakavyoamua, kwani kuna watu wengine huamua kuunganisha vipengele viwili
kuwa kimoja na wengine huhesabu jalada la nje(cover page) kama moja ya
kipengele. Mimi nitatumia vipengele vinane (8) ambavyo ni hivi vifuatavyo;-
1. Muhtasari
Tendaji(Executive summary)
2. Maelezo
ya Kampuni(Business Summary)
3. Maelezo
ya Bidhaa/Huduma(Product/Service Description)
4. Maelezo
ya Soko(Market analysis summary)
5. Mikakati
na utekelezaji(Strategy & Implementation Summary)
6. Maelezo
ya Utawala(Management Summary)
7. Mpango
wa Fedha(Financial Plans)
8. Viambatanisho/Vielelezo(Appendix)
Kama nilivyotangulia kusema, ili kufanya kazi iwe rahisi vipengele hivi 8 nitavigawa katika sehemu ama unaweza ukasema hatua 4. Hatua hizo nne zitawezesha kazi ya kuandika mpango wa biashara kwa ajili ya kushawishi benki, taasisi za fedha au wawekezaji kuwa rahisi kwani nitajua ni kitu gani ninachotakiwa kukifanya kwa wakati gani, kifupi nitaweza kuwa na malengo(focus)
1.
HATUA / SEHEMU YA KWANZA KABISA:
i)
ONYESHA
FURSA ILIYOPO (THE OPPORTUNITY)
Hiki ndicho kiini
hasa cha mpango wa biashara yako na inatakiwa impe afisa wako wa mkopo uelewa
bayana wa mambo yafuatayo;
· Tatizo
hasa biashara yako inalotatua
· Jinsi
bidhaa au huduma zako zinavyoendana na soko lililokuwepo
· Kile
kitu hasa kinachoitofautisha biashara yako na za washindani waliokuzunguka.
Katika Sehemu/Hatua
hii kuna vitu muhimu vitatu kama ifuatavyo;
ii) Tatizo na Suluhisho lake
Hapa utaelezea tatizo
hasa unalotatua kwa ajili ya wateja wako, ni kwa jinsi gani maisha yao yatakuwa
bora zaidi baada ya kuwapatia hilo suluhisho (pain point solution). Ni vyema kwanza kabla haujaanza ukawa umefanya utafiti
wa soko kwa kuwahoji wale unaotarajia watakuwa wateja wako(target customers) ili uweze kujiridhisha kwa uhakika kwamba ni
kweli wanalo hilo tatizo unalotaka kulitatua.
Katika kitabu chetu cha MICHANGANUO YA BIASHARA NA UJASIRIAMALI
tumeweka sura nzima inayoelezea jinsi ya kufanya utafiti wa soko (Feasibility study) kabla hujaandaa
mpango wako wa biashara.
Hakikisha pia
umelielezea tatizo lako kwa ufasaha. Kwa mfano tuseme tatizo lako unalotaka
kusuluhisha ni la watu katika mtaa mmoja
kule Sinza kuhangaika sana nyakati za mchana kwa kukosa mahali muafaka pa
kupata lunch mpaka wengine kulazimika kufungasha viporo kuja navyo kazini
ijapokuwa wana pesa zao na wangeliweza kuzitumia kama wangelipata mahali pazuri
na pasafi pa kupata mlo. Suluhisho lako laweza likawa ni kufungua mgahawa safi
na wa kisasa katika mtaa huo utakaowahudumia vyakula na vinywaji masaa ya
mchana.
iii) Soko Lengwa
Kitu cha pili kwenye
hii hatua ni Soko unalolilenga, Ni kina nani hasa utakaowauzia? Na pia unaweza
kukisia idadi yao wako wangapi?, siyo lazima kupata idadi kamili. Taarifa hizi
zina umuhimu mkubwa na zitaamua ikiwa biashara yako itafanikiwa ama itafeli
huko mbeleni.
Kamwe usifanye kosa
la kudhania tu eti “kila mtu atakuwa
mteja wangu bwana” Kwa mfano ni rahisi sana mmiliki wa mgahawa kumlenga
kila mpita njia midhali yupo njia panda, lakini ni vizuri zaidi akahakikisha
anawalenga kundi la wateja fulani maalumu ili aweze kuufikia uwezo kamili wa
mauzo ya biashara yake. Hapa anaweza badala yake akawalenga wafanyakazi wa
maofisini na wenye biashara tu ambao mchana ni lazima watafute chakula na wana
uhakika wa kula kwani kipato wanacho cha uhakika pia.
iv) Ushindani.
Washindani wako wa
moja kwa moja ni kina nani? Hawa ni wafanyabiashara kama ya kwako iwe ni watu
binafsi au makampuni wanaofanya biashara
yenye suluhisho la kutatua matatizo ya wateja kama lakwako. Kisha elezea
sifa zako za kiushindani(competitive advantage). Maana yake
unaeleza ni kwanini wateja wako watarajiwa(soko
lengwa) wachague kununua kutoka kwako na wala siyo kwa washindani wako?
Ikiwa kama unadhania
huna mshindani, jaribu kufikiria tena mara mbili, wateja wakati mwingine
wanaweza kutafuta suluhisho la matatizo yao hata kutoka kwa wale washindani
wako wasiokuwa wa moja kwa moja wanaotumia njia tofauti kutatua tatizo
lilelile. Kwa mfano watu wa mtaa nilioutaja kule Sinza wanaweza kuamua kwenda
kula mihogo ya kukaanga au hata mahindi ya kuchoma kukidhi njaa yao ikiwa
mgahawa wako hautakidhi shida inayowasumbua.
Tumemaliza hatua au
sehemu ya kwanza ya kuelezea fursa iliyopo kwenye biashara unayoandikia
mchanganuo wako. Sasa hapa umegundua nini?
Bila
shaka kama wewe ni mdadisi utakuwa umegundua kwamba katika vile vipengele vyetu
8 vya mpango mzima wa biashara, FURSA
inajikita zaidi katika vipengele vya, Biashara,
Bidhaa na Soko.
2.
HATUA / SEHEMU YA PILI
ONYESHA
NI JINSI GANI UTAKAVYOTEKELEZA MPANGO WAKO.(EXECUTION)
Hapa ndipo vitendo
halisi hutokea! Utaingia kwa undani kuonyesha ni kwa namna gani utaitumia
kikamilifu fursa uliyoionyesha katka hatua ya kwanza. Sehemu hii unaionyesha
benki au taasisi ya fedha kwamba unao mpango thabiti wa kuyafikia mafanikio.
Vitu muhimu vitatu(3) katika sehemu hii ni hivi vifuatavyo;-
i)
Mikakati
ya Masoko na Mauzo
Masoko na mauzo ni
somo pana, na kwenye mpango wa biashara
urefu wa kipengele hiki utategemea aina ya biashara na ukubwa wake. Lakini kitu
cha muhimu zaidi hapa unatakiwa kuelezea ni jinsi gani umepanga kulifikia soko
lako lengwa na jinsi utakavyowageuza watu katika soko hilo kuwa wateja wako.
Baadhi ya vitu muhimu vinavyopaswa kuwekwa katika kipengele hiki ni kama
ifuatavyo;.
Mkakati
wa kujipanga sokoni (Positioning strategy) – hiki ndiyo kitu
kinachoifanya biashara yako kuwa ya kipekee na inayowavutia zaidi wateja wako
walengwa.
Mtangazo (promotion). Utatangaza biashara yako kwa njia ipi? Mabango, redio,
TV, Mitandao ya kijamii au vipeperushi?
Bei: Kile utakachotoza kwa ajili ya bidhaa/huduma zako ni lazima kiakisi mahitaji ya wateja wako. Kuna njia kuu 2 za kupanga bei, ya 1) Kwa kuzingatia gharama ulizotumia(cost plus pricing) na ya 2) Kwa kuzingatia thamani ya bidhaa/huduma (Value pricing)
ii) Uendeshaji (Operations)
Katika
hatua ya pili ya utekelezaji, uendeshaji ndiyo jambo la msingi kuliko
vyote
Ni muhimu hasa hasa katika biashara zile zinazofanyikia kwenye eneo maalumu (Brick & Mortar Business) zilizo na ofisi, fremu au stoo na maghala ya kuhifadhia malighafi na bidhaa mfano kiwanda nk. Unaweza kuelezea hapa ni kwanini eneo lako ni muhimu kwa hiyo biashara husika au ni eneo lenye ukubwa kiasi gani. Katika kipengele hiki pia unaweza kueleza ikiwa biashara yako itafanyikia nyumbani au ni mahali gani, ukubwa wa eneo la ofisi pamoja na vitu vingine mbalimbali vinavyopatikana katika eneo la biashara kama vile mitambo, vifaa na hata programu za kompyuta zinazotumika.
iii) Utekelezaji vitendo na Vipimo
Wakopeshaji na
Wawekezaji hutaka kujiridhisha kwamba unafahamu jinsi ya kutekeleza mpango wako
kupata mafanikio kibiashara. Haya ni malengo yanayowekwa ambayo hukusaidia
biashara yako kupiga hatua. Kwa mfano tuseme unafungua kiwanda chako, moja kati
ya malengo yanaweza yakawa ni, ukamilishaji wa bidhaa za mfano, ufunguzi rasmi,
kufikisha bidhaa sokoni nk. Vipimo huonyesha namna utakavyopima mafanikio ya
biashara yako, je ungependa kuzalisha kiasi fulani cha bidhaa? au kuhakikisha
gharama hazizidi kiwango fulani? Fikiria ni kipimo kipi muhimu zaidi ya vingine
kisha ueleze jinsi utakavyopima kwa ajili ya ukuaji wa biashara yako.
Katika
hatua hii ya pili ya Utekelezaji (execution) utagundua kwamba inahusisha
vipengele vya, Mikakati na Utekelezaji pamoja
na kile cha Utawala.
3.
HATUA YA TATU
MPANGO
WA FEDHA KWA UNDANI (FINANCIAL PLAN
DETAILS)
Hii ndiyo sehemu
muhimu zaidi ya mpango wa biashara kwa ajili ya kuombea mkopo benki au
wawekezaji na ndiyo sehemu watu wengi huona ni ngumu zaidi kuandaa, Wakopeshaji
wengi na wawekezaji ndiyo sehemu wanayoitazama kwa umakini zaidi ili kutambua
uwezekano wa biashara yako kufanikiwa au kuanguka.
Lakini sehemu hii
haipaswi kuwa ngumu ikiwa mtu utaigawa katika sehemu ndogondogo na zifuatazo ni
sehemu ndogondogo 3 ambazo ni lazima mpango wako uwe nazo;
i)
Mahitaji
na vyanzo vya fedha
Unaonyesha ni kwa
namna gani utatumia fedha zitakazowekezwa kwenye biashara iwe ni fedha za
mmiliki, mkopo au fedha kutoka chanzo chochote kile kingine. Matumizi yanaweza
yakawa ni ya kununulia vifaa, kununulia malihafi/bidhaa au kulipia gharama
mbalimbali za biashara.
ii) Makisio(Forecast)
Haya ni makadirio ya
fedha kwenye biashara yako. Yanakupa wewe na benki wazo la ni faida kiasi gani
biashara inaweza kutengeneza baada ya kipindi fulani kupita. Hapa kuna vitu
vitatu vinavyotakiwa kuwepo;
Mapato.
Unaorodhesha bidhaa zote au huduma biashara yako inazotarajia kuuza ili
kuingiza pesa.
Gharama
za moja kwa moja (Direct costs) Kwa maneno mengine ni zile
gharama za kutengeneza kile unachouza
Expenses;
Hizi ni gharama za kudumu za uendeshaji kama vile mishahara, pango, umeme na
maji, gharama za masoko nk.
iii) Taarifa za kifedha
Watu wa Benki hapa
ndipo hutupia jicho zaidi na ni vitu vifuatavyo utahitaji kuweka;
Taarifa
Faida na Hasara (Profit and Loss) – Taarifa hii huchukua namba
kutoka kwenye makisio yako ya mauzo na maeneo mengine madogomadogo kama gharama
za mauzo kuonyesha kama unapata faida au hasara.
Makisio
ya Mali na Madeni (Projected Balance Sheet) Ni kitu cha kwanza kabsa afisa wa
mkopo atakiangalia. Inaonyesha madeni ya biashara, mtaji na
rasilimali za biashara(assets) inaangazia uimara wa biashara yako kifedha.
Makisio
ya Mtiririko wa Fedha taslimu. Ni taarifa inayopima kiasi
cha fedha taslimu biashara ilizokuwa nazo mkononi au benki katika muda fulani.
Maafisa mikopo wanapendelea waone mtiririko halisi wa fedha katika miezi yote
12 ya mwaka wa kwanza wa biashara.
4.
HATUA YA NNE
MUHTASARI
TENDAJI (EXECUTIVE SUMMARY)
Ingawa hii ndiyo
sehemu inayoonekana ya kwanza katika mpango wowote ule wa biashara lakini
kimlolongo ndiyo huandikwa mwishoni kabisa baada ya kumaliza sehemu nyingine
zote. Kimsingi hii ndiyo huitambulisha biashara yako ukifupisha pointi zile
muhimu kutoka katika kila sura zinazounda mpango wako mzima. Mara nyingi huwa
na urefu wa ukurasa mmoja au miwili tu, jaribu kuandika kwa kifupi na kwa uwazi
kadiri iwezekanavyo ukizingatia kwamba hii ndiyo sehemu ya kwanza kabisa
itakayomfanya mkopeshaji wako au mwekezaji kuhamasishwa na biashara yako hivyo
kukubali kutoa pesa.
HITIMISHO
Huhitaji kuwa na
elimu kubwa sana ili uweze kuandika mpango wa biashara yako mwenyewe. Ikiwa
unao uwezo wa kufanya biashara na ukapata faida basi na ujue pia unaweza
kuandika mpango wa biashara hiyo. Kinachotakiwa tu ni kufahamu namna ya
kupangilia mawazo yako kwani ukishakuwa na wazo la biashara kichwani au kuanza
kuifanya basi tayari na mpango unao kichwani mwako.
MAOMBI YA MKOPO (FUNDING REQUEST)
Kipengele hiki katika makala hii sijakiweka popote kwa makusudi kwani
mara nyingi huandikwa tu pale mtu unapoandika mpango wa biashara kwa ajili ya
kuombea mkopo.
Maelezo yake kwa kina nimeyatoa katika darasa letu watsap, ni
kakipengele muhimu sana na mara nyingi watu hawafahamu umuhimu wake. Kina uwezo
mkubwa wa kuamua upate mkopo au ukose.
Nitakufundisha kwa kina ni wapi kiwekwe, kiandikwe nini na mambo mengine
mengi kukihusu yatakayosaidia kumshawishi mkopeshaji wako au mwekezaji hata akakupatia fedha unazohitaji – Tukutane
darasani!
UNAHITAJI
MPANGO WA BIASHARA?
Kuna njia mbili
unaweza kupata mpango wa biashara yako
1. Kutafuta mtaalamu kama sisi akuandikie: Njia hii utatakiwa kulipia kiasi fulani cha fedha na utashiriki kuandika kwa kujibu maswali machache utakayoulizwa na mtaalamu huyo kama vile jina la biashara, malengo, makisio ya mauzo,soko lako nk.
2. Kuandika mwenyewe:
Hii ndiyo njia yenye faida zaidi kwako kwani inakufanya ufikirie kila hatua
utakayopitia kwenye biashara yako, ni kama vile unafanya mazoezi kwa ajili ya
mechi utakayoicheza baadae ili muda ukifika uweze kupata ushindi kwa wepesi
zaidi. Unaweza kujua kuandika mchanganuo kwa kujifunza kupitia chuoni, katika
vitabu mbalimbali au kupitia kozi mbalimbali mitandaoni.
Sisi tunatoa huduma
zote mbili hapo juu kwa anayehitaji, kufundisha lakini kumuandikia mtu
anayehitaji huduma hiyo.
Sasa hivi tunalo darasa
mtandaoni katika Group letu la Whatsapp liitwalo MICHANGANUO-ONLINE. Ambalo tunafundisha kwa kina jinsi ya kuandaa
mipango ya biashara mbalimbali hasa zile zilizokuwa na ubunifu wa kipekee.
Unapojiunga na group
hili unapata kwanza kozi kamili ya kuandika mpango wa biashara halafu
michanganuo mbalimbali bunifu ya biashara zinazolipa inafuata. Unapata vitabu
papo hapo na sample za michanganuo zaidi ya 10 kwa kiingereza na kiswahili.
Tunatoa pia offa ya Tafsiri kwa kswahili ya kitabu cha THINK AND GROW RICH kwa watu wachache wanaowahi offa hii. Offa
inamalizika tarehe 30 August 2021 baada ya hapo haitakuwepo tena.
Kujiunga na group
upate offa zote na masomo mengine yote yaliyowahi kutolewa katika group siku za
nyuma lipia kiingilio chako sh. Elfu 10 kwa namba, 0765553030
au 0712202244 kisha nitakutumia
coupon ya kununulia kitabu cha Think and Grow Rich-swahili kwa sh. Elfu moja
katika mtandao huu wa GETVALUE(Bonyeza kukiona). Hivyo offa nzima
utakuwa umelipa shilingi elfu 11 tu. Na utakuwa kwenye group ukijifunza kwa
miezi 12 (mwaka mzima toka tarehe uliyojiunga)
Mafunzo ya jinsi ya kuandaa michanganuo ya biashara katika group yanatolewa na Wataalamu walio na uzoefu wa kutosha katika fani hiyo. Tumeshaandika michanganuo halisi mingi kwa ajili ya biashara mbalimbali za watu na makampuni kwa ajili ya kuombea fedha bank na taasisi mbalimbali za kifedha. Baadhi ya michanganuo ya biashara na makampuni hayo tumeiweka hapa kama mfano lakini hatujaweka wazi utambulisho wao. BAADHI YA KAZI ZETU NI HIZI (Bonyeza kuzisoma)
Tunafundisha
kile tunachokifanya!
Nakukaribisha sana
kwenye group letu, na hata ikiwa hupendi kuwa katika magroup ya mitandaoni, basi jipatie tu hii offa kwa ajili ya kupata
vitabu na michanganuo ujifunze mwenyewe taratibu. Fungua kiungo kifuatacho
kusoma idadi ya vitu vilivyoko kwenye OFFA kubwa ya vitabu na michanganuo ya
biashara kikiwemo kitabu Thing & Grow Rich-swahili edition-2021 kwa sh. Elfu
11 tu
Mafunzo ya kuandika
mpango wa biashara ikiwa wewe ni mjasiriamali tu wa kawaida, yatakuwezesha wewe
kufahamu biashara vizuri zaidi na kwa kina kwani mpango wa biashara unagusa
kila hatua inayopigwa katika safari nzima ya kibiashara.
Na ikiwa pengine wewe
ni mwanataaluma mwenye nia siku moja uje uwe mtaalamu (business plan expert) kama sisi kwa ajili ya kuwaandikia watu
wengine michanganuo ya biashara zao wakulipe pesa, basi mafunzo haya hupaswi
kabisa kuyakosa.
Siku ya Leo tarehe 25/08/2021 kwenye group tulikuwa na somo la Matayarisho na kesho tarehe 26 semina yetu ya Jinsi ya kuandika mpango wa Biashara inaanza rasmi.
FUATILA ZAIDI HAPA
Prepared by;
Peter Tarimo
Entrepreneur & Business Plan Expert
SOMA PIA;
1. Jinsi Mpango wa Biashara unavyoweza kuongeza mafanikio ya biashara yako.
2. Sababu kuu (5) kwanini uandike mpango wa biashara yako kwanza kabla hujaanzisha biashara yenyewe.
3. Je, huna muda wa kutosha kuandika mpango wa biashara? Tumia njia hizi 3 rahisi
4. Sababu nne kwanini kipengele cha fedha ni moyo wa mpango wa biashara (The heart of a business plan)
5. Ni lini biashara yako itarudisha gharama zote ulizotumia?(Break Even Point)
0 Response to "JINSI YA KUANDIKA MPANGO WA BIASHARA UTAKAOSHAWISHI BENKI NA WAFADHILI KUKUPATIA FEDHA"
Post a Comment