KWANINI WAZO ZURI LA BIASHARA NDIO LENYE USHINDANI MKALI & MBINU ZA KUFANYA LIWEZE KUKUPA FAIDA KULIKO WASHINDANI WAKO | JIFUNZE UJASIRIAMALI

KWANINI WAZO ZURI LA BIASHARA NDIO LENYE USHINDANI MKALI & MBINU ZA KUFANYA LIWEZE KUKUPA FAIDA KULIKO WASHINDANI WAKO

Kiwanda cha sabuni
Duniani kuna mawazo mengi sana ya biashara yanayovutia, Watu wengi hasa katika mitandao hii ya kijamii huhamasika sana pale wanapokutana na Makala au video kuhusiana na biashara zenye kulipa kiasi kikubwa cha faida, biashara zinazolipa haraka na hata zile biashara ndogondogo zinazoweza kufanywakwa mtaji mdogo ama hata bila ya mtaji kabisa. Lakini ukweli wa mambo upo hivi, hakuna biashara yeyote isiyolipa, katika kila biashara unayoiona au kuisikia inalipa kutegemeana na mahitaji yake katika jamii yapoje na isitoshe, wewe mwenyewe unaweza ukayatengeneza mahitaji hayo hata ikiwa hayapo au wateja hawayaoni, hili nitalielezea vizuri karibu na mwisho wa Makala hii.

Ikiwa jamii(Wateja) wana uhitaji na bidhaa ama huduma fulani basi ujue wazi hapo kuna biashara na unaweza ukatengeneza wazo lako zuri la biashara inayolipa faida. Pamoja na ukweli huu bado kuna mawazo ya biashara yanayovutia watu zaidi au kuonekana kuwa ni yenye kuleta faida chapchap kushinda mengine ila cha kusikitisha ni kwamba wajasiriamali wengi kila wanaposema “ngoja nikamate wazo hili bora la biashara nipate pesa”, njiani wanakuja kubaini kumbe wazo hilo lina ushindani mkali kupindukia na haiwezekani kirahisi mtu akapata faida aliyotarajia angeliipata haraka.


Miongoni mwa mawazo bora kabisa ya biashara yanayowavutia watu wengi mara kwa mara kuanzisha yapo mengi lakini katika Makala haya nitataja mawazo mawili tu kama mifano ya kuwakilisha yale mengine, nayo ni hii ifuatayo;

1. Miradi au Biashara za ufugaji wa kuku.
Hii ni miradi maarufu sana kote duniani na kila mjasiriamali mdogo anapoisikia tu ikitajwa mahali moyo hulipuka akifikiria namna biashara hii ya ufugaji wa kuku inavyoweza kumtajirisha au kumtoa kimaisha haraka. Kwa mara ya kwanza mimi binafsi kusoma katika vyombo mbalimbali vya habari ukiwemo mtandao wa intaneti na majarida jinsi biashara ya ufugaji wa kuku inavyolipa upesi, mara moja nilikumbuka enzi zile nasoma shule ya msingi kijijini nilpokuwa nafuga kuku wachache wa kienyeji.

Nilipojaribu kuvuta picha ni lini niliwahi hata kujilipia ada kwa faida ya wale kuku nikakuta hakuna hata siku moja zaidi ya pesa za wazazi wangu. Sasa nikajiuliza tena ikiwa kuku wana uwezo wa kulipa kimaajabu namna ile ni vipi sikuweza hata kujilipia ada kutokana na faida niliyokuwa nikiipata?


Nakumbuka changamoto yangu kubwa ilikuwa ni uwekezaji mdogo kwenye mradi ule kwani kuku walikuwa wachache na hivyo kupata faida kubwa ya kutosha halikuwa jambo rahisi ukitegemea majirani walionizunguka nao walikuwa wakifuga kuku huku bei ya kuku na mayai ikibakia kuwa ni ileile huwezi kupandisha kirahisi kuwazidi hao washindani. Nilihitaji uwekezaji(Mtaji) mkubwa zaidi kuniwezesha kupata faida au mafanikio makubwa na ya haraka jambo ambalo halikuwa rahisi kwangu kipindi hicho.

Hata baada ya kipindi hicho kupita(sasa hivi) bado nimeendelea kuwa mfugaji mzuri wa kuku na siku moja nikaamua kukaa chini na kufanya tathmini ya kina juu ya miradi hii ya ufugaji wa kuku aina zote kujua kama nilikuwa nakosea wapi muda wote huo nisiwe milionea. Nilifanya utafiti wa kina na kuandaa michanganuo mitatu ya biashara za ufugaji wa kuku, kuku wa mayai, kuku wa nyama na kuku wa kienyeji(MKOMBOZI CHICKS PLAN 3PACKS).


Katika michanganuo hii 3 kitu kikubwa nilichogundua ni kwamba, ni kweli kabisa biashara ya ufugaji wa kuku iwe ni wa mayai, nyama au wale wa kienyeji yote ina faida lakini ni faida ya kawaida ambayo huwa inaweza ikapatikana katika kipindi kifupi mfano wiki tano tu hadi 8 kwa kuku wa nyama. Miradi hii haina tofauti kubwa na miradi mingine ya kibiashara na ikiwa basi mtu atapenda kupata mafanikio makubwa upesi basi hana budi kufuata kanuni zote za biashara sawa tu na mmiliki wa biashara ya nguo au duka la rejareja afanyavyo.

Kitakachokufanya ufaulu kwenye biashara ya ufugaji wa kuku ni kuwa na mtaji wa kutosha pamoja na utekelezaji mzuri wa mipango na mikakati yako ya kimasoko utakayojiwekea na wala siyo wazo lenyewe tu kama watu wengi tulivyokuwa tukifkiria hapo kabla. Na haijalishi kama mtaji wa kutosha unao tayari au utafuga kuku wawili na kusubiria mpaka wafike mia, elfu nk., mafanikio makubwa utayaona tu pale kuku wako watakapofikia idadi kubwa hata kama itakuchukua miaka 10 kufikisha idadi hiyo, vinginevyo utaishia tu kufuga kuku wawili, watatu kwa ajili ya mayai ya kunywea chai asubuhi na kitoweo siku moja moja.


2. Biashara ya Viwanda vidogovidogo
Wazo la kumiliki kiwanda kidogo pia linawavutia watu wengi sana kutokana na ukweli kwamba wapo matajiri wengi leo hii hapa Tanzania na Duniani walioanzia kwenye biashara hizi. Kiwanda ni biashara ya uhakika sana kushinda biashara nyingine za kawaida endapo tu kitatimiza vizuri na kwa ufanisi mahitaji fulani ya kundi fulani la wateja na siyo kila kiwanda tu ilimradi kinaitwa kiwanda kinaweza kumletea faida haraka mmiliki wake. Katika mfano huu wa kiwanda na nimeutoa kwa makusudi kabisa kutokana na maswali mengi ya wajasiriamali ninayokutana nayo wakitaka taarifa mbalimbali jinsi kiwanda kinavyoweza kuwatoa kimaisha, ndio nitajibu swali la ni mbinu zipi utumie katika kiwanda chako kupata faida licha ya ushindani mkali uliopo.

Kama ilivyokuwa kwa biashara nyingine zote kiwanda chako kinatakiwa lazima kizalishe bidhaa itakayotatua tatizo la aina fulani la wateja kwenye jamii. Haiwezekani watu wote wakawa na hilo tatizo ingawa pia wakati mwingine kuna bidhaa zinazoweza kuwa zinahitajika na kila mtu lakini kwa nyakati tofauti. Lakini bado tu hata ikiwa mahitaji yapo ushindani mkali hauepukiki kirahisi, hii ni sababu kubwa inayozifanya biashara zinazovutia sana  mwishowe watu wengi wazione ni ngumu kwao kuzifanya na haziwezi kuwaletea mafanikio ya haraka.


SASA BASI UTUMIE MBINU ZIPI KUSUDI BIASHARA YAKO YENYE USHINDANI MKALI  IWEZE KUPATA WATEJA WENGI NA WA KUDUMU?
Biashara ya kuuza chakula kwa mfano ni wazo jingine zuri la biashara inayopendwa na watu wengi lakini ubaya wake mmoja tu ni kwamba lina ushindani mkubwa sana kutokana na watu wengi kutamani kuifanya kwa kuwa wanafahamu fika watu kila siku wanahitaji kula, iwe masika au kiangazi, kuwe na vita au amani, kuwe na janga la Corona au kusiwe nalo nk. Halikadhalika pia na biashara ya utengenezaji na uuzaji wa sabuni aina zote

Kulijibu swali hili kwa ufasaha kabisa, nimelazimika kuandika Mchanganuo/Mpango wa biashara ya kiwanda kidogo cha Unga wa Dona(USADO MILLING). Niliona kwa maneno matupu tu kama ilivyozoeleka wengi hawatanielewa. Kumbuka mchanganuo au mpango wa biashara maana yake ni maelezo ya kila kitu utakachokifanya katika biashara uliyokusudia kuifanya, ni hatua zote bila kujali hayo uliyoyaandika au kuyawaza utayatekeleza kama yalivyo au tofauti.


Wapo watu wengine hupotosha kwa makusudi kwamba mpango wa biashara si muhimu na kuuandaa ni kupoteza tu muda. Hii si kweli hata kidogo kwasababu kila anayeanzisha biashara ni maono kwanza huanzia kichwani mwake na maono hayo ndiyo mpango wenyewe wa biashara. Ikiwa kama hautatabiri biashara inaweza kukulipa utaingiaje tu kichwakichwa kuifanya?

Hivyo ni kusema kwamba kila mjasirimali awe mdogo au mkubwa huanza na mpango wa biashara kwanza kichwani mwake kabla hata ya kufanya kitu chochote kile. Na sasa utakapoamua uuandike mpango huo kwenye karatasi hilo ni jambo jingine lakini mpango ni mpango tu, iwe umeuandika mahali ama umeufikiria na kuuacha kichwani mwako.

Tukirudi kwenye mbinu zenyewe maanake sasa naona nimezama mno kwenye business plan, mbinu hizo ni hizi hapa chini; Katika kuhakikisha kiwanda hiki cha USADO unga wake unapata wateja wa uhakika na wakudumu licha ya ushindani mkali uliopo, mambo kadhaa yalifanyika;

Kuamua kuwa tofauti
Kwanza kabisa wamiliki wake ambao ni madada wawili(kina mama) baada ya kuunganisha nguvu zao kimtaji walikaa chini na kutengeneza mkakati wao wa masoko utakaowawezesha kuwa tofauti kabisa na wazalishaji wengine wa unga wa DONA sokoni. Mkakati huo naweza kuuita, MKAKATI WA KUFA MTU(The Killer Marketing Plan) Je, unajua ni mikakati gani hiyo waliyokuja nayo? Soma mpango huo mzima.


Bidhaa za kipekee
Unga wa dona umezoeleka sana na hamna mtu asiyeujua, ukienda dukani na kusema nipe dona utachotewa kwenye kiroba na kupimiwa mara moja bila maswali zaidi kutoka kwa muuzaji. Sasa ni mbinu zipi walizozitumia ili kuhakikisha ‘dona lao’ linakuwa tofauti kabisa na Dona wanayozalisha watu wengine wote katika soko wanalolilenga? Mchanganuo huu unajibu kila kitu katika Sura yake ya Mkakati maalumu kabisa wa Masoko wa USADO MILLING. Na kumbuka mkakati wa soko hauhusishi matangazo ya biashara tu peke yake bali ni vitu vingi kuanzia ubora wa bidhaa yenyewe, jinsi unavyoifungasha, bei, wateja, washindani nk.

Kujiposition vizuri katika soko/Kujipanga katika soko/Kujibrandi
Hizi ni kaulimbiu, alama au maandishi mbalimbali watakayoyatumia kwenye matangazo yao mbalimbali katika kujitofautisha kabisa na washindani wao sokoni, ni jinsi wanavyotaka wateja wao wawaone au kuwafikiria. Siyo kila kauli mbiu tu itawahamasisha wateja wazipende bidhaa zako, ni lazima uchague kauli yenye maneno yatakayogusa hisia za watu mpaka muda wote wakiziona bidhaa hizo mahali wazikumbuke hisia hizo. USADO MILLING wameibuka na kauli mbiu ya kipekee sana ambayo wateja wao watarajiwa wataipenda na moja kwa moja kuupenda unga wao kwa kuwa inawagusa mioyoni moja kwa moja.


Kutatua matatizo ya wateja.
Unga kazi yake kbwa ni kupikia ugali kwa ajili ya kumpatia mtu shibe ili kutatua tatizo la njaa, hili hamna asiyelifahamu hata mtoto wa chekechea analijua. Sasa unaweza ukaniuliza hivi, “Bwana pita ni tatizo gani la kipekee hapa USADO MILLING watalitatua ili kuwashawishi watu waachane na unga wa dona unaouzwa madukani bei chee?” Sasa hapa ndio penye kazi pevu, pale mwanzoni niliahidi kuja kuelezea dhana ya kutengeneza mahitaji ya bidhaa hata kama wateja wenyewe hawayaoni. Usipoweza kubaini matatizo mengine ya kipekee bidhaa yako inayoweza kuyatatua utaishia kulia kiwanda chako hakilipi.

Hapa sasa ni lazima ufanye kitu kinachoitwa Mchanganyiko wa mbinu za kimasoko(Market Mix) ili uweze kuchuja na kupata kundi fulani tu la wateja wako miongoni mwa wateja wote wanaohitaji zile bidhaa, kundi ambalo limesahaulika na washindani wako bado hawajalishitukia. Watakapokuja kushtuka watakuta wewe upo mbali sana, hukamatiki tena, ni kama unavyowaona kina Moo na Bakhresa sasa, unaweza kuanza biashara ukashindana nao kirahisi sasa hivi? USADO MILLING kwa kutumia unga wao wa Dona wanatatua matatizo mengine tofauti kabisa na yale yaliyozoeleka kila siku. Ni yapi hayo?


Kuacha Wateja wenyewe ndio wakutangazie bidhaa zako.
Mbinu hii ni nzuri na haikugharimu pesa nyingi kwa ajili ya kuzitangaza bidhaa zako, wateja wenyewe ndio watakaochukua jukumu la kukutangaza popote pale kwa wateja wengine watarajiwa. Kazi yako inakuwa ni ndogo tu, kuanzisha mjadala mithili ya vile uwashapo jiko la mkaa kwa tutumia vipande viwili tu vya mkaa wa moto na baada ya muda mchache jiko zima kukolea moto.

Hizo ni baadhi tu ya mbinu za kimasoko unazoweza ukazitumia katika kuhakikisha bidhaa za kiwanda chako zinapata wateja miongoni mwa viwanda vingine vingi vinavyozalisha bidhaa sawa na za kwako na wala siyo sayansi ya kuunda rocketi au kwenda mwezini inayotumika ili kiwanda chako kiweze kuuza kama ‘njugu’ Kujibrandi ni lazima kuoane kweli na uzuri na ubora wa bidhaa zako na siyo kwenye matangazo unadai unga wako ni bora kumbe mtu akiupika anakutana na mabuje au wadudu kibao, hiyo itakufukuzia wateja na kuanza kumtafuta mchawi bure.


Katka mchanganuo huu kuna vitu wamiliki wa USADO MILLING watavitekeleza katika kuhakikisha kweli unga wao unakuwa na ubora brandi au jina lao linaoupigia debe na siyo blaa blaa tu. Kuna mikakati mahsusi itakayotekelezwa kwa lengo la kuwathibitishia wateja kuwa ni kweli ubora huo upo na wala siyo matangazo matupu ya biashara. Yote haya yameainishwa katika mkakati huo wa ‘kufa mtu’ ndani ya Mpango wa biashara ya USADO MILLING.

Nimekudondolea kiasi kidogo sana kuhusiana na Mkakati wa masoko wa biashara hii ya kiwanda cha USADO MILLING, mengi zaidi unaweza kuyapata tu kwa kuusoma mpango huo mwenyewe ukiwa umetulia. Si lazima uandike wa kwako ili uweze kufungua biashara ya kiwanda kama hicho au kinachoshabihiana nacho, bali kwa kuusoma tu unapata madini ambayo yatakuwezesha na wewe kuweka mikakati yako hata ikiwa unaiweka kichwani tu kama watu wengi wanavyofanya kabla ya kuanzisha miradi yao.


Ikiwa utapenda kuupata mpango huu kabambe wa biashara ya USADO MILLING na kuusoma kwa kituo, karibu sana siku ya Alhamisi ya tarehe 2 mwezi wa 4, 2020 katika mafunzo ya siku 3. Pamoja na kupata mpango huo kamili katika lugha ya Kiswahili lakini tutajifunza hatua kwa hatua jinsi mchanganuo huo ulivyotengenezwa tangu Muhtasari wake mpaka Makisio ya ripoti za fedha zote kama faida na hasara nk. pamoja na vielelezo mbalimbali. Mafunzo yatafanyika kwenye magroup ya whatsap ya MICHANGANUO-ONLINE sambamba na Channel yetu mpya ya Telegramu maalumu kwa ajili hiyo.

Kwa ambaye hatumii Whatsap wala Telegramu hamna shida kwani tunatuma pia kila kitu kupitia Baruapepe(E-mail)

Kila mshiriki mara tu atakapomaliza kulipia kiingilio chake sh. Elfu 10 atapata papo hapo OFFA ya vitu vingine 5 vifuatavyo na offa hii ni ya muda mfupi sana, haitakaa tena muda mrefu kama ile ya mwaka jana ya vitu 15. Vitu hivyo ni Kitabu chetu cha MICHANGANUO YA BIASHARA NA UJASIRIAMALI pamoja na michanganuo mbalimbali kama ifuatavyo;

1.  Kitabu cha MICHANGANUO YA BIASHARA NA UJASIRIAMALI -kwa kiswahili

2.  Kitabu mashuhuri zaidi duniani, HOW TO WRITTE A BUSINESS PLAN kwa lugha ya kiingereza, ndio kinachotumika vyuo vikuu vingi duniani.-kwa kiingereza

3.  Kifurushi maarufu cha michanganuo 3 ya ufugaji wa kuku(MKOMBOZI CHICKS PLAN 3PACKS)-kwa kiswahili

4.  Mchanganuo kamili wa kilimo cha Matikiti maji(KIBADA WATERMELON BUSINESS PLAN) -kwa kiswahili

5.  Mchanganuo wa biashara ya mgahawa(JANE RESTAURANT BUSINESS PLAN) -kwa Kiswahili & kiingereza

Pia kwa wale watakaopenda kubakia kwenye group hili baada ya mafunzo hayo ya siku 3 (Kwani kuna wasiopenda kuwa ktk magroup) wataruhusiwa kubaki mpaka mwaka huu wa 2020 utakapomalizika. Katika magroup ya MICHANGANUO-ONLINE huwa tunajifunza kila siku masomo yenye maudhui ya pesa(Financial Literacy) pamoja na kufanya michanganuo rahisi ya biashara ndogondogo zinazolipa. Kutakuwa pia na michanganuo kamili(Mirefu) mfano wa huu wa USADO MILLING au ile iliyotajwa kwenye OFFA katika vipindi maalumu.

NAOMBA NIRUDIE TENA KWA HERUFI KUBWA KABISA KWAMBA, ADA YA MWAKA MZIMA NI SH. ELFU 10 TU ZA KITANZANIA NA HATUNA MALIPO YALIYOJIFICHA MBELE YA SAFARI. UTA ENJOY MASOMO NA VITU MBALIMBALI KWA ELFU 10 HIYOHIYO BILA KUTIMULIWA KWENYE GROUP AU CHANELI YETU KISA ADA.

Lipia sasa hivi kupitia namba zetu hizi hapa; 0765553030  au  0712202244 kunufaika na OFFA hiyo ya vile vitu 6 papo hapo  huku ukisubiria Mkakati wa masoko wa kufa mtu(The killer Marketing Plan of USADO Milling Plant) siku ya Alhamisi tarehe 2 Aprili.

Jina M-pesa au Tigo-pesa litakuja, Peter Augustino Tarimo
Baada ya kulipa shilingi 10,000/= yako kama ada ya mwaka huu wote, tuma ujumbe kupitia watsap 0765553030 au SMS ya kawaida usemao;

NITUMIE OFFA YA VITU 6 NA KUNIUNGANISHA NA GROUP LA MASOMO YA MICHANGANUO 2020

Si lazima uwe na Watsap au Telegramu, E-mail pia inatosha. Ingawa ukiwa navyo ni vizuri tu.

ASANTE SANA NA UNAKARIBISHWA

PETER A. TARIMO
Writer and Tanzanian Industrialist 2020
I am playing my part, how about you?

0 Response to "KWANINI WAZO ZURI LA BIASHARA NDIO LENYE USHINDANI MKALI & MBINU ZA KUFANYA LIWEZE KUKUPA FAIDA KULIKO WASHINDANI WAKO"

Post a Comment