Tulianza
hivi....................
Habari za muda huu wapendwa katika group letu hili
maalumu kabisa kwa ajili ya semina za biashara bunifu mbalimbali. Katika
mfululizo huu, leo tunaanza na mchanganuo wa biashara ya ufugaji wa kuku
chotara aina ya Kuroiler kwa ajili ya nyama na itatuchukua siku 5 kumaliza
tukilenga (focus) hasa ubunifu
unaoweza kuifanya biashara hii kuwa yenye faida kubwa tofauti na ufugaji wa
kawaida tu uliozoeleka na kila mtu.
Kwa siku ya leo, yale tutakayojifunza ni haya yafuatayo;
1. Maana
ya Mchanganuo/Mpango wa Biashara
2. Maandalizi
ya kuandika Mchanganuo wa biashara ya ufugaji wa kuku chotara kuroiler
3. Jinsi
ya kufanya Utafiti wa soko lako la kuku chotara kuroiler au sasso
4. Njia 6 za kuandika mchanganuo wa biashara
1.
MCHANGANUO/MPANGO WA BIASHARA MAANA YAKE NI NINI?
Ni
andiko linaloelezea jinsi biashara yako itakavyoendeshwa. Ni ufupisho wa muundo
wa biashara yako, malengo, mikakati na mpango wa fedha.
Ni
muongozo unaokusaidia wewe na wadau wengine katika kuelewa jinsi biashara yako
itakavyofanikiwa.
Malengo
ya Mpango wa biashara
Lengo la msingi kabisa la mpango wa biashara ni
kukusaidia kufahamu muelekeo wa biashara yako na hatua utakazochukua ili
kufikia malengo. Unakuongezea kujiamini hata kama kutatokea mdororo wa kiuchumi
mbele ya safari.
Kazi nyingine za mpango wa biashara ni kama vile;
· Kuombea
mkopo toka taasisi za kifedha na benki
· Kujaribu
wazo la biashara ikiwa kama linawezekana ama la
· Kupima
malengo ya biashara uliyojiwekea na
· Kusaidia
katika kazi ya kuiendesha biashara yako vyema
2.
MAANDALIZI YA KUANDIKA MCHANGANUO WA BIASHARA YA UFUGAJI WA KUKU KUROILER
KUROILER
ni kuku wa aina gani?
Kroiler au Kuroiler ni aina ya kuku chotara wenye sifa
zote mbili za kuku wa mayai na kuku wa nyama. Hukua haraka na kutaga mayai
mengi kuliko kuku wa kienyeji huku wakiwa na uwezo mkubwa wa kubadilisha
chakula chochote kile wanachokula kuwa nyama, hivyo wanakula kilekile chakula cha kuku wa
kienyeji anachokula na kukua muda uleule lakini akiwa na uzito mkubwa zaidi yaw
a kienyeji. Hivyo wanakuwa na nyama nyingi kwa kipindi kifupi sana.
Kuku
chotara maana yake ni mchanganyiko wa aina mbili tofauti za kuku
walio na sifa tofauti kwa ajili ya kupata uzao wa kuku waliokuwa na sifa bora
zaidi ya wazazi wao.
Katika ufugaji wa kuku wa kisasa ufugaji wa kuku chotara
mtu anaweza akachagua mbegu tofauti apendayo kwa mfano mbali na aina hii ya
kuroiler kuna kuku chotara wengine waitwao Sasso, hawa nao wana sifa
zinazokaribiana sana na kroiler na asili ya kuku saso ni huko nchini Ufaransa
miaka ya 50.
Kuroiler
asili yao ni huko nchini India na ni mchanganyiko wa aina ya kuku wa nyama
majogoo (broilers) na matetea aina ya Rhode Island Red
au, Majogoo aina ya White Leghorn na
matetea aina ya Rhode Island Reds.
Baada ya kuamua kichwani
mwako sasa unataka kulifanyia kazi wazo la biashara ya ufugaji wa kuku aina ya
Kuroiler wa nyama, kitu muhimu kinachofuata ni maandalizi kwa ajili ya kuandaa
mpango wa biashara yako. Na si kwa biashara hii tu peke yake bali pia na kwa
biashara nyingine zote ni hivyohivyo.
Kwenye maandalizi ya mpango
wa biashara ni lazima mtu ufanye kitu kinachoitwa UTAFITI au upembuzi yakinifu,
maana yake unafikiria njia tofautitofauti zitakazokuwezesha kulitekeleza
wazo lako hili la biashara. Utaanza kutafuta majibu ya maswali mbalimbali juu
ya ufugaji wa kuku wa kuroiler kusudi baadae uweze kuchagua yale sahihi katika
kuandika mchanganuo wako.
Mfano unaweza kuchunguza mifumo mbalimbali ya ufugaji wa
kuku ukabaini ipo 3, Huria, Nusu huria na mfumo wa ndani. Sasa ukishafahamu
faida za kila mfumo unachagua utumie mfumo gani mmoja kwenye mpango wa biashara
yako, hiyo ndio maana ya kufanya utafiti kupata majibu utakayotumia.
3. NJIA
ZA KUFANYA UTAFITI WA BIASHARA YAKO YA KUKU KROILER
Kuna njia kuu mbili za kufanya utafiti wa soko au
biashara yako
1. Utafiti wa msingi
2. Utafiti wa Dawati
1. Katika utafiti wa msingi unazungumza na wadau
mbalimbali wanaohusiana na biashara ya ufugaji wa kuku chotara kama vile
wanaofuga kuku kama wewe, wafanyabiashara ya kuku chotara na mazao yake, wateja
wa kawaida mtaani, maduka ya chakula na vifaa vya kuku na wataalamu wa
mifugo.
2. Njia ya pili ya utafiti wa dawati ni kwa kusoma
taarifa mbalimbali zinazohusiana na ufugaji wa kuku chotara kwenye vitabu,
majarida, mitandao na vyombo vingine vya habari.
Vipengele muhimu zaidi kwenye biashara ambavyo hufanyiwa
utafiti ni vile ambavyo taarifa zake mara nyingi haziwezi zikapatikana ndani ya
biashara/kampuni na mfano wake ni kama vipengele vifuatavyo;
1.
SOKO
2.
BIDHAA
3.
USIMAMIZI
na
4.
FEDHA
1. soko
Kwa kuwa soko ndio kitu muhimu pengine kushinda vyote ili
biashara ifanikiwe ni lazima tufanye uchunguzi iwapo kama wateja watapatikana
kweli au la.
Kwenye soko taarifa tutakazochunguza zinalenga katika
kufahamu ukubwa wa soko la kuku wa nyama wa Kuroiler, aina ya wateja
watakaonunua kuku, bei, ubora wa bidhaa zilizopo, ushindani na kiasi
unachotarajia kuzalisha.
2. Bidhaa
(kuku)
Tutachunguza mchakato mzima namna kuku wa Kuroiler
wanavyozalishwa kuanzia uandaaji wa banda, vifaranga wa siku moja mpaka kuku
wanapouzwa wote. Teknolojia pamoja na mikakati mbalimbali itakayotumika katika
kuhakikisha wateja wanapata kuku bora wenye uzito na ladha inayostahili.
Katika kutafiti jinsi kuku wa nyama Kuroiler wanavyokuzwa
unapaswa kuzunguka katika maduka ya vifaa vya ufugaji kuku, kwa wafugaji
unaowajua na kwa maofisa mifugo kuulizia bei za vifaranga wa kuroiler, vifaa
mbalimbali kama madawa, chanjo, vitamini na chakula kwa ajili ya kulishia kuku
hao. Linganisha ufugaji wa kuku wa kienyeji na ufugaji wa kuku wa kisasa kama
vile ufugaji wa kuku wa mayai na hata ufugaji wa kuku wa nyama kibiashara.
3. Usimamizi
Chunguza pia ni kina nani watakaoweza kuuhudumia mradi
wako, Je utakuwa ni wewe mwenyewe? Familia au utaamua kumuajiri mfanyakazi?
Jibu ndilo tutakaloandika kwenye mchanganuo wako.
4. Fedha
Kwenye fedha kitu cha kwanza tunachunguza mahitaji yote yanayotakiwa
gharama zake ni kiasi gani na tutaweza kupata wapi fedha za kugharamia. Kitu
cha pili ni kulinganisha mahitaji ya mradi na kiasi cha fedha mmiliki/wamiliki
walizokuwa nazo, Ikiwa kiasi hakitoshi au umegundua kiasi hicho kitaishia
njiani basi utatathmini uwezekano wa aidha kurekebisha mahitaji au kutafuta
vyanzo vingine zaidi vya mtaji.
4.
NJIA 3 ZA KUANDIKA MCHANGANUO WA BIASHARA
Unaweza kuandika mpango wa biashara yako kwa kutumia moja
kati ya njia hizi 3 zifuatazo;
1. Kwa
kufuatisha vipengele/sura zinazounda mpango wa biashara(Outlines)
2. Kwa
kutumia Vielezo/Templates
3. Kwa
kutumia Programu/Software maalumu za michanganuo ya biashara
Hapa kwenye semina hii tutatumia njia ya 1 ya kufuata
mfululizo wa vipengele vinavyounda mpango wa biashara. Mlolongo wa vipengele
hivyo ni huu ufuatao;
1.MUHTASARI
2.MAELEZO YA KAMPUNI /
BIASHARA
3.BIDHAA au HUDUMA
4.TATHMINI YA SOKO
5.MIKAKATI NA UTEKELEZAJI
6.UENDESHAJI
7.MAELEZO YA UONGOZI NA
WAFANYAKAZI
8.MPANGO WA FEDHA
9.VIELELEZO / VIAMBATANISHO
Vipengele hivyo kwa undani tutaona hapo baadae.
Kwa
siku ya Leo tunaishia hapa na tutaendelea na sehemu inayofuata siku ya kesho.
Hakikisha unapitia kabisa mapema mchanganuo wako wa kuku wa nyama wa Kroiler
niliokupatia kusudi wakati tukiandika hatua kwa hatua uwe unafuatilia kipengele
kwa kipengele kufahamu namna mpangilio wa kila kipengele unavyotakiwa kuwa.
Pia
FOCUS yetu ambayo ni UBUNIFU katika biashara hii bado tutaiona kwenye vipengele
vinavyofuata huko mbele, hivyo fuatilia semina hii mpaka mwisho wake.
Asante
Peter
SOMA PIA NA HIZHI HAPA;
1. Banda la kuku 100 wa kienyeji: vipimo, ramani, picha na jinsi
ya kulijenga kwa ubora
2. Muongozo kamili wa jinsi ya kufuga kuku wa nyama (broilers) kitaalamu- semina siku-3
3. Ujasiriamali: ubunifu ndiyo msingi wake mkuu na injini ya uchumi katika soko huria.
4. Kama una biashara ndogo ya mtaji mdogo, hizi hapa njia 11 za kuibusti
5. Biashara 7 nzuri za kufanya zitakazokuingizia pesa hata kama umelala.
0 Response to "SEMINA: MCHANGANUO WA UFUGAJI WA KUKU CHOTARA WA NYAMA KIUBUNIFU, SIKU-1(MAANDALIZI)"
Post a Comment