JINSI YA KUWEKA AKIBA KILA MWEZI UKITUMIA VYANZO VYA PESA USIYOTARAJIA KABISA KUIPATA | JIFUNZE UJASIRIAMALI

JINSI YA KUWEKA AKIBA KILA MWEZI UKITUMIA VYANZO VYA PESA USIYOTARAJIA KABISA KUIPATA

Uwekaji akiba

Katika siri kubwa za kufanikiwa kiuchumi/kifedha au kibiashara kwa ujumla, suala la kuweka akiba ndiyo kitu kinachochukua nafasi ya juu kabisa tofauti na jinsi watu wengi wanavyodhania. Watu wengi tunakimbilia kufikiri labda kitu cha msingi zaidi ni kupata kiasi kikubwa sana cha fedha mkononi ndipo tuweze kutimiza malengo yetu ya kiuchumi na ya kifedha.

Somo letu hili ijapokuwa limeangazia suala zima la uwekaji wa akiba lakini kipekee hasa pale mwishoni mwa somo nimeonyesha njia au jinsi ya kuweka akiba kila mwezi kwa kutumia vyanzo usivyovitarajia kabisa kama unaweza kuvitumia kama chanzo cha fedha za kuweka akiba. Njia hizo zinatatua kile kitendawili cha kwanini ni vigumu sana kwa mtu kuokoa pesa kwa ajili ya kuweka akiba?

Kuweka akiba ni tabia mtu yeyote anayoweza kujifunza na kujizowesha maishani. Binadamu tunatakiwa katika kila kipato tunachopata tujiwekee asilimia fulani ya kipato hicho kama akiba. Wataalamu wengi wamewahi kupendekeza kiasi cha asilimia mtu anayopaswa kuweka kama akiba. Ingawa unaweza ukatenga kiasi chochote kile kama akiba lakini wataalamu wengi hupendekeza kuwa asilimi 10% au zaidi ya hapo.

Hata wanyama na wadudu wakishakula chakula walichopata kuna wakati hukumbuka kuweka akiba mahali kwa ajili ya matumizi yao ya baadae mfano Chui, mbwa, paka na hata nyuki. Tazama mfano mzuri myama Chui amkamatapo swala akishakula na wanawe utamuona akikazana kupandisha mabaki ya mzoga huo kwenye mapango ya mti kusudi akauhifadhi kama akiba kwa ajili ya kitoweo cha siku zinazofuata.

Kwani Kuna Umuhimu Gani WA kuweka Akiba?

Umuhimu mkubwa wa kujiwekea akiba kwanza kabisa upo kwenye uwekezaji, hautaweza kabisa kuwekeza katika kitegauchumi chochote pale fursa zitakapojitokeza ikiwa kama hauna akiba yeyote ile ya fedha kutokana na vyanzo vyako vya msingi vya mapato. Na ukisema utakwenda kukopa mahali fulani labda benki ili uwekeze, jambo hili litakuwa gumu sana kwako kwani wakopeshaji wengi huwa hawamkopeshi mtu asiyekuwa na mradi aliouanzisha tayari kwa pesa zake mwenyewe ukaonekana.

Na hata ikiwa utabahatika kuanzisha biashara kwa fedha za mkopo, biashara hiyo itakuweka roho juu kiasi cha wewe kuweza hata kupatwa magonjwa ya presha na moyo kwani hatari kidogo tu ya kupotea kwa mtaji huo haiwezi kukupa kabisa amani akilini mwako, na hivyo kusababisha muda wote wewe uwe ni mtu wa kuishi kwa wasiwasi na stress tu. Ukishakuwa na wasiwasi hutaweza tena kuwa na ubunifu katika biashara au mradi wako

Umuimu mwingine wa mtu kujijengea tabia ya kuweka akiba ni kujenga nidhamu hata katika nyanja nyinginezo za kimaisha. Nidhamu ya pesa ni kama vile mazoezi ya kuikomaza akili yako izowee mazingira magumu na utakaposhinda mtihani mgumu wa pesa basi na ujue umeshinda mitihani mingine mingi ya kimaisha kwani kujinyima na kuweka akiba unajitesa kimwili sawa tu na mtu anayekwenda gym kujifua kimazoezi. 

Kumbuka siri nyingine kubwa sana ukitaka kupata pesa au mafanikio yeyote yale maishani ni nidhamu ya kuhakikisha unatenda jambo lilelile kila siku kwa muendelezo bila kuacha hata siku moja, ikiwa huna nidhamu kwenye ulaji wako, utanenepa ovyo, halikadhalika ukikosa nidhamu kwenye ratiba za masomo yako shuleni kamwe hutaweza kufaulu mtihani wako wa mwisho iwe ni ule wa darasa la saba, kidato cha nne, kidato cha sita au hata wa chuo kikuu.

Kutamka tu unataka kuweka akiba ni rahisi sana kuliko utekelezaji wenyewe, changamoto kubwa hutokana na “ni wapi unakoweza ukapata fedha za ziada za kutumbukiza katika akiba yako mbali na matumizi yako ya kila siku.”  Wakati mwingine unaweza kuwaza utawekaje akiba wakati kuna mahitaji mengine tena ya muhimu tu unashindwa kuyatimiza na kulazimika kuyaacha.

Kisingizio kikubwa mara nyingi kimekuwa ni watu kushindwa kuweka akiba kwa sababu tu hawana vipato kabisa au vipato vyao ni vidogo mno kiasi kwamba hawawezi kutoa hapo asilimia fulani kwa ajili ya kuweka akiba. Lakini jambo hili halipaswi kabisa kuwa ni sababu ya wewe kushindwa kujiwekea akiba kwani mpaka dakika hii unapoishi bila shaka kuna aina fulani hivi ya kipato unachopata kinachokuwezesha kuishi vinginevyo ungelikuwa umekwisha kufa kwa njaa siku nyingi.

Tukiachana na ajira na biashara ambavyo ndivyo vyanzo vikubwa zaidi vya kipato cha mwanadamu kuna aina vyingine za vyanzo vya kipato kama vile, ruzuku, msaada, zawadi nk. Chochote kile unachokipata kilichokuwa na thamani kiuchumi ni aina fulani hivi ya kipato hata kama ni kidogo kiasi gani, hivyo unao wajibu wa kuhakikisha unaweka hapo akiba asilimia fulani na wala siyo kujiwekea visingizio lukuki.  

Hata kwa mfano, tuchukulie maisha yako wewe ni ombaomba barabarani, kipato chako ni zile fedha unazoomba watu wanakupa, hivyo unao wajibu wa kumega hapo sehemu fulani ya hizo pesa za msaada na kuiweka kama akiba kabla hata hujafanya matumizi yako mengine yeyote. Fedha hizi zitakuja siyo tu kukuwezesha kuanzisha vitegauchumi vya kukuondoa kwenye kazi ya kuombaomba bali hata msaada mkubwa pale linapoweza kutokea janga la ghafla kama vile ugonjwa nk. 

Hatua Muhimu 5 za Uwekaji Akiba

1.   Elimu

Jielimishe kuhusiana na pesa na uwekezaji kupitia vyanzo mbalimbali mfano, vitabu, mitandao ya kijamii kama hii, applications mbalimbali za kwenye simu za mkononi, madarasa ya ujasiriamali na vyombo vinginevyo vya upashanaji habari

2.   Kujiwekea bajeti

Bajeti maana yake ni kupanga kabisa jinsi utakavyofanya matumizi ya fedha utakazoingiza kabla hata haujazitia mkononi. Hii itakusaidia kuhakikisha matumizi yako hayaendi kinyume na ulivyopanga. Unaweza kupanga bajeti yako kwa kutumia karatasi na kalamu ama kwa kutumia apps mbalimbali za simujanja zinazopatikana Playstore na Appstore

Bajeti pia tunaikuta kwenye Mpango wa biashara na hivi ni vitu viwili vinavyoshabihiana sana. Wataalamu husema mpango wako utakuwa na uzito zaidi pale unapouandika katika karatasi. Vivyohivyo na bajeti ndivyo ilivyo.

Kumbuka masuala haya ya Bajeti na Michanganuo ya biashara kwa ujumla wake huwa tunajifunza kwa undani kabisa katika Group letu la MICHANGANUO-ONLINE MASTERMIND. Bajeti kipato chako cha siku, wiki na hata mwezi kisha uhakikishe unaiheshimu kwa kuifuata kikamilifu.

3.   Kujilipa kwanza wewe mwenyewe

Katika kipato chochote kile utakachoingiza anza kwanza kumega utakachoweka kama akiba kabla haujafanya matumizi mengine yeyote yale hata yale muhimu na ya msingi kama chakula, kulipa deni, bili mbalimbali nk.

4.   Badilisha tabia ya matumizi yako ya fedha

Jifunze kuwa bahili wa pesa zako kwa kutokununua kitu chochote kile ambacho hukukiweka katika bajeti yako ya siku hiyo. Kubadilisha tabia kunaanzia na kubadilisha mtazamo wa akili yako, ishi kama vile huna hela hata pale unapokuwa umepata hela nyingi. Ukitaka kupata pesa nyingi acha kujionyesha una pesa, jishushe chini ya kiwango chako cha pesa unazoingiza.

5.   Wekeza kwenye miradi inayolipa

Tumia sehemu ya akiba yako kuwekeza kwenye vitegauchumi/miradi salama inayoweza kukuingizia kipato zaidi hapo baadae. Ukishawekeza weka malengo ya muda mrefu.

Jinsi ya kuweka akiba kila mwezi ukitumia vyanzo vya pesa usivyotarajia kabisa

Pamoja na kuona kwamba akiba unapaswa kutenga kiasi fulani cha mapato yako lakini kuna vyanzo vya mapato vilivojificha ambavyo ni tofauti na kipato chako ulichokizoea. Haya ni maeneo ambayo mtu unaweza usiyatilie maanani kabisa kwamba yanaweza kukusaidia kutimiza azma yako ya kuweka akiba pasipo kuathiri sana bajeti yako ya kawaida ya kila siku. Maeneo hayo nitazungumzia kwa pande zote mbili, kwa Wafanyabiashara na kwa Wafanyakazi;

1) Wafanyakazi:

    .................................................................................................


ü Ndugu msomaji wangu somo hili bado halijamalizika na somo kamili unaweza ukalipata tu kwa kujiunga na kundi letu la masomo na semina Watsap (MICHANGANUO-ONLINE-MASTERMIND GROUP)

ü Mwanachama anapata zawadi (OFFA) ya Vitabu na Michanganuo jumla ni vitu 12, mara tu amalizapo kulipia ada ya mwaka mzima ambayo ni sh. 10,000/= TU

ü Kwenye group tuna masomo ya fedha adimu na ya kipekee kabisa zaidi ya 100 na kila siku tunakuwa na somo jipya. Huwezi kuyapata mahali pengine popote.

ü Masomo haya yanatoa mwanga mkubwa katika ufahamu wa suala zima la pesa, jinsi inavyozunguka kwenye biashara na hata saikolojia za watu na imani zao juu ya fedha na jinsi zinavyoathiri hali yao ya kiuchumi.

ü Pia zipo semina za mara kwa mara za michanganuo/Business Plans bunifu kwa biashara zinazolipa Tanzania

ü Kujiunga lipia ada kupitia namba zetu, 0712202244  au  0765553030 jina Peter Augustino Tarimo kisha Ujumbe usemao, “NATAKA OFFA YA VITU 12, NIUNGE PIA NA GROUP” Ikiwa hupendi kuugwa katika magroup basi acha nebo “NIUNGE  NA GROUP” kwani wapo wanaohitaji vitabu na masomo peke yake.


VITU 12 VYA OFFA NI HIVI VIFUATAVYO;-

                 1.      COURSE/SEMINA: (compiled complete course) ya Jinsi ya kuandika Mchanganuo wa biashara –(Ukishindwa kuandika mchanganuo wako mwenyewe utarudishiwa pesa zako) - kwa kiswahili

                 2.       KITABU: Michanganuo ya Biashara na Ujasiriamali chenye course zote muhimu za BIASHARA, jinsi ya kuandaa michanganuo ya biashara na sample za michanganuo mbalimbali 10 iliyokamilika kila kitu.kwa kiswahili

                 3.      KITABU: Mifereji 7 ya Pesa na Siri Matajiri wasiyopenda kuitoa -kiswahili

                 4.      KITABU: Siri za upishi wa chapati laini-UPENDO CAFE pamoja na Mchanganuo wake kamili.-kwa kiswahili

                 5.       KITABU: Njia rahisi ya kuandika mpango wa biashara-dakika 30 - kwa kiswahili

                 6.       KITABU: HOW TO WRITE A BUSINESS PLAN  ni maarufu sana duniani na ndio hutumika vyuo vikuu vingi.-kwa kiingereza

                 7.       MCHANGANUO: Kuku wa nyama -Tumaini Broilers - kwa kiswahili

                 8.      MCHANGANUO: Kuku wa nyama –kwa kiingereza

                 9.      MCHANGANUO: Ufyatuaji tofali za saruji- kwa kiswahili

              10.    MCHANGANUO: Mgahawa wa chakula-Jane Restaurant –kwa Kiswahili

              11.    MCHANGANUO: Mgahawa wa chakula-Jane Restaurant –kwa kiingereza

              12.    MCHANGANUO: Kiwanda cha usagishaji Dona (Usado milling) - kwa Kiswahili

              13.    Kuunganishwa Group la masomo ya kila siku ya fedha na michanganuo mwaka mzima ukitaka. (Mentorship group) (Ni hiyari yako lakini, usipotaka hatukuunganishi)

 

Offa hii ni ya muda mfupi!

 

Imeandaliwa na Peter Tarimo

Simu/Whatsap: 0765553030 au 0712202244


SOMA PIA:

0 Response to "JINSI YA KUWEKA AKIBA KILA MWEZI UKITUMIA VYANZO VYA PESA USIYOTARAJIA KABISA KUIPATA"

Post a Comment