JINSI YA KUNG’ARA KWA URAHISI KWENYE BIASHARA / KAZI (GET A CHANCE TO SHINE EASILY) | JIFUNZE UJASIRIAMALI

JINSI YA KUNG’ARA KWA URAHISI KWENYE BIASHARA / KAZI (GET A CHANCE TO SHINE EASILY)

Mwanamke aking'ara

Hivi mtu akikuuliza swali lifuatalo utamjibu vipi?

Ni stadi gani muhimu kuliko nyingine zote maishani inayochangia mtu kung’ara kwa urahisi kwenye biashara / kazi anayoifanya? (Get a chance to shine easily in business or a job) Nikimaanisha kwamba stadi inayomwezesha mtu aweze kufanikiwa kwa urahisi zaidi kwenye biashara au kazi yake.

Asilimia kubwa ya watu wanaohitimu vyuoni na mashuleni huja kushituka wawapo kazini au kwenye biashara pale wanapobaini vitu vingi walivyokuwa wakijifunza darasani kumbe havifanyi kazi kwenye ulimwengu halisi kama walivyokuwa wakifikiri.

Tafiti mbalimbali zimedhihirisha pasi na shaka kwamba, ni stadi za mahusianao na za kijamii zinazoongoza katika kusababisha mafanikio yatokee kwenye biashara au kazi na miongoni mwa stadi hizo niliwahi kuziandika kwenye makala yangu nyingine moja iitwayo, JINSI YAKUTENGENEZA MVUTO WA AJABU WA KUPENDWA HARAKA NA KILA MTU, WAPENZI, WATEJA,NDUGU NA HATA JAMAA. Katika makala hiyo nilizitaja stadi tano (5)

Lakini leo tena nimevutiwa na stadi nyingine ya maisha ya mtu kuwa ni mtu wa Kuaminika ama Kutegemewa na watu wengine. Kuwa mtu wa kutumainiwa na watu ni moja kati ya sifa/stadi muhimu mno na ambayo watu wengi huichukulia poa au kutokuipa umuhimu unaostahili .

Ni stadi ya kuaminika inayokosekana mpaka mwanamke au mwanaume anafunga safari kwenda kwa mganga wa kienyeji kusaka dawa ya kupendwa na mpenzi wake. Ni kutokuaminika kunakosababisha mfanyabiashara kwenda kutafuta dawa ya kupendwa na wateja. Ni ukosefu wa sifa ya kutegemewa kunakosababisha mwajiriwa kwenda kwa ‘wataalamu’ kutengeneza dawa ya kupendwa kazini.

SOMA: Jinsi ya kupata wateja wengi kwenye biashara yako kwa kufanya kile wajasiriamali wengi wanachosahau kukifanya

Hakuna dawa ya mvuto wa mapenzi duniani (kupendwa) zaidi ya wewe mwenyewe kujenga  upendo na kuaminika kwa wengine. Kwenya uchumba kisa cha watu kukaa hata miaka 5 wakichunguzana ni ili kila mmoja ajue tabia za mwenzake na hasa kama ni mwaminifu, ana upendo wa dhati au la.

Hali ni hivyohivyo ilivyo kwenye biashara, wateja hawawezi kamwe kununua bidhaa ama huduma zako ikiwa kama bado hawajakuamini, hawakupendi na wala hawajakuzoea.

SASA NI JINSI GANI UTANG’ARA KWA URAHISI KWENYE BIASHARA AU KAZI YAKO ILI UPATE MAFANIKIO HARAKA?

Ili ung’are kwenye biashara au kazini kwako inakubidi utengeneze stadi hii ya kuwa mtu wa kuaminika na kutegemewa. Unaweza ukasema, mbona kila mtu analiweza hili? Ni kweli siyo jambo gumu kwa kulitazama harakaharaka lakini linahitaji mtu kuwa na nidhamu ya hali ya juu sana katika kutekeleza kila unachoahidi kukifanya kwa watu wengine.

SOMA: The sky is very wide, every star can shine (Mbingu ni kubwa mno, kila nyota inaweza kung'ara)

Kwa mfano tuchukulie wewe ni fundi cherehani umemuahidi mteja siku ya ijumaa aje kuchukua nguo yake. Ijumaa ikifika kweli akija aikute nguo yake ikiwa tayari na siyo kuanza longolongo.

Unapojenga tabia ya kuwa mtu wa kuaminika na kutegemewa ndipo utakapoanza kupata wateja zaidi na zaidi, utapata fursa ya kung’ara (kushine) kuwazidi wengine wote wanaokuzunguka iwe ni kazini, kwenye biashara, shuleni au katika jamii nyingine yeyote unayoishi. Kwa njia hii unaweza kupata miradi ya kila aina itakayokuingizia maelfu ya pesa kama siyo mamilioni ya shilingi kwani kila mtu anakuamini na anatamani kufanya na wewe biashara au kazi.

SOMA: Uaminifu ni mtaji mkubwa katika biashara kushinda fedha

Hakikisha unatimiza kile unachoahidi kila mara bila ya kutoa sababu zozote zile na stadi nyinginezo zitafuata taratibu. Sidhani kama kipo chuo ama shule inayofundisha somo la kuwa mtu wa kuaminika na kutegemewa lakini jambo la msingi ni mtu kutambua ni kwa jinsi gani KUAMINIKA na watu ilivyokuwa muhimu na hivyo kulenga katika kujenga nidhamu ya kuikuza stadi hii itakayokuwezesha kung’ara na kufanikiwa popote pale ulipo iwe ni kazini, kwenye biashara, shuleni, chuoni ama mahali pengine popote kwenye jamii.

 

………………………………….

Mpenzi msomaji wa makala hii, unaweza pia kujipatia huduma zetu nyingine za malipo zifuatazo;

1. Course kamili ya jinsi ya kuandaa mchanganuo wa biashara yeyote pamoja na OFFA ya vitabu, michanganuo, Templates & kuungwa group la masomo ya fedha na michanganuo kwa mwaka mzima. Course hii ni Tsh. 10,000/= badala ya bei halisi ya sh. Elfu 90

2. Vitabu vyetu mbalimbali na Michanganuo kamili ya Biashara iliyokwisha andikwa tayari. Unaweza kuvicheki kwenye duka letu hapa, SMARTBOOKSTZ

3. Huduma ya kuandikiwa mchanganuo wa Biashara yako. Gharama hutegemea ukubwa wa mtaji wa biashara husika. Tumekwisha waandalia Makampuni na biashara za watu mmoja mmoja, unaweza kuona baadhi yao hapa>BAADHI YA KAZI ZETU  

0 Response to "JINSI YA KUNG’ARA KWA URAHISI KWENYE BIASHARA / KAZI (GET A CHANCE TO SHINE EASILY)"

Post a Comment