UAMINIFU NI MTAJI MKUBWA KATIKA BIASHARA KUSHINDA FEDHA. | JIFUNZE UJASIRIAMALI

UAMINIFU NI MTAJI MKUBWA KATIKA BIASHARA KUSHINDA FEDHA.

Makala hii imetokana na mazungumzo yangu na ndugu Aois Francis juu ya suala la uaminifu kwenye biashara, Alois alinieleza jinsi ambavyo watu huweza kufanya biashara na wakaingiza pesa pasipokuwa na senti tano au wakati mwingine wakiwa na mtaji mdogo sana.

Akitolea mfano kwa Wahindi alisema, wanautumia vizuri sana mtaji huu na huwa unawapa mafanikio makubwa wao wenyewe na hata wale wadau wengine wanaofanya nao biashara  kama vile wafanyabiashara kutoka mikoa mbalimbali wanapofika katika jiji la Dar es salaam, wengi hwa na mitaji midogo sana. Baada ya kununua bidhaa kutoka dukani kwa Mhindi mara nyingi na Mhindi akagundua mtaji wake haukidhi mahitaji, basi atadiriki kumpa mzigo “malikauli” ilimradi tu mauzo yake yanaongezeka. Lakini hafanyi hivyo kiholela, ni baada ya ‘kumsoma’ kwa kipindi kirefu na kujiridhisha kweli kuwa ni mfanyabiashara mwenye malengo ya ukweli.

Alois anasema siyo Wahindi tu wanaoweza kunufaika na mbinu hii, bali hata na mtu mwingine yeyote anaweza kuitumia .Unapokuwa mwaminifu katika biashara na mdau yeyote yuke iwe ni wateja , wanaokusambazia bidhaa au taasisi za kifedha,  unajijengea hazina ya kuja kupata usaidizi wa namna yeyote ile katika biashara yako iwe ni kukopeshwa, kupata wateja zaidi baada ya wale uliowaonyesha uaminifu kwenda kuwatonya na wenzao au wa namna nyingine yeyote ule. Kwa mtindo huo unakuwa umejijengea mtandao mzuri wa biashara yako.

Anasema, yeye binafsi uaminifu katika kazi na biashara umemsaidia kwa kiasi kikubwa sana katika maisha yake ya kila siku, ukizingatia kwamba yeye ana kazi yake ya msingi lakini wakati huo huo hutumia “Mifereji" mingine tofauti tofauti katika kujiongezea kipato cha maisha yake ili aweze kufikia malengo yake makuu aliyojiwekea katika maisha.

Bwana Alois Francis ukiacha ajira yake, yeye ni Mwezeshaji na Mhamasishaji katika vikundi vya ujasiriamali na jamii kwa ujumla, anayo taaluma ya masoko na uuzaji “Great Salesman” na anao uzoefu wa siku nyingi. Yeye pia ni Msambazaji mkuu wa vitabu, DVDs na bidhaa zote za kampuni ya “SELF HELP BOOKS PUBLISHERS LTD” mikoa yote ya Tanzania Bara na visiwani, isipokuwa Dar es salaam peke yake.

Ana ‘dili’ pia na nchi za kanda ya Afrika Mashariki na ya Kati. Ukihitaji  vitabu kwa bei ya jumla au reja reja huko mikoani, mpigie simu:  0713 462590 au  0753 262590  Ama waweza kuwasiliana na makao makuu Dar es salaam tukakuunganisha naye. Anapatikana zaidi Mkoa wa Iringa, Makambako lakini pia hutembea mikoa mbalimbali Tanzania katika mtandao wake wa kimasoko.


0 Response to "UAMINIFU NI MTAJI MKUBWA KATIKA BIASHARA KUSHINDA FEDHA."

Post a Comment