Katika safu hii ya maswali na majibu, hapa
nitakwenda kulijibu swali la mdau wetu mmoja alilouliza kupitia whatsap na
aliuliza kama ifuatavyo;
· Historia ya mahesabu ya biashara ya siku za nyuma na uorodheshe pia dhamana zote zitakazoweza ku “back up” mkopo wako endapo utakuja kushindwa kuurejesha.
· Msisitizo pia unatakiwa katika kipengele cha ‘Sehemu za biashara’(Business Ratios)
· Watapenda pia kuona umeambatanisha katika mpango wako, maombi ya mkopo na ripoti zilizopita za kodi.
SOMA: Jinsi ya kuchora na kutumia chati & grafu kwenye mchanganuo wa biashara
· Pia orodhesha wanahisa waliopo pamoja na timu imara ya wafanyakazi
· Wanataka pia kuona mfumo imara wa biashara unaoaminika pamoja na ushahidi wa uwezekano wa biashara kukua vizuri(Business growth)
· Wawekezaji pia ni wavivu sana kusoma mchanganuo mrefu, hivyo tengeneza vizuri Muhtasari wako uweke mambo yote muhimu kwa kifupi ili ukiwavuta basi wakwambie upeleke mchanganuo mzima.
Mimi
nna tatizo kubwa kwenye upande wa makadirio ya gharama; naambiwa kuna namna
mbalimbali za kuandaa kulingana na mahitaji, mf. Kama unahitaji mkopo au
unaandika kwa ajili ya kuwapa wafadhili wa biashara yako. Naomba ufafanuzi hapo
kaka.
SOMA: Break Even Point: Ni lini biashara yako itarudisha gharama zote ulizotumia?
SOMA: Break Even Point: Ni lini biashara yako itarudisha gharama zote ulizotumia?
MAJIBU:
Swali lako hili lina vitu 2 tofauti,
· namna
ya kukadiria gharama mbalimbali na la pili ni
· namna
ya kuandika mpango wa biashara kwa ajili ya hadhira(wadau) tofauti mfano kuomba
mkopo benki au kwa ajili ya kuwasilisha kwa wawekezaji(investors)
Nitajibu maswali yote mawili hivi;
1.Kwenye
mpango wa biashara huwa tunakadiria vitu viwili ambavyo ni,
Gharama mbalimbali na Mauzo(mapato). Kati ya hivyo2 gharama ndiyo rahisi zaidi
kukadiria kwani kimsingi wala haukadirii bali unachukua moja kwa moja gharama
halisi za vitu/bidhaa/huduma sokoni. Mauzo ndiyo unayoweza kusema kabisa kwamba
tunakadiria kwani mara nyingi tunakuwa hatujajua kwa uhakika kama tutapata
“exactly” wateja wangapi au tutauza kwa bei ipi. Hata hivyo ukadiriaji iwe ni
gharama au mapato, vyote haupaswi kukadiria upate namba iliyo sahihi kwa
asilimia mia moja kwenye mpango wa biashara, bali ni makisio tu.
SOMA: Sababu 4 kwanini kipengele cha fedha ni moyo wa mpango wa biashara(The heart of a business plan)
SOMA: Sababu 4 kwanini kipengele cha fedha ni moyo wa mpango wa biashara(The heart of a business plan)
2.Kujibu
hilo swali la pili, kwa kifupi ni hivi;
Mpango wa biashara bila kujali unaandika kwa
ajili ya kupeleka Benki, kwa wawekezaji au unataka tu kwa ajili ya uendeshaji
wa biashara yako, michanganuo yote huwa na sura zinazofanana(common
structure). Ni lazima mchanganuo wowote ule uwe na sehemu zote muhimu
kama vile muhtasari, Maelezo ya biashara, Soko, Mikakati, Sehemu ya
fedha(Financials) nk.
Lakini unapoandika mfano kwa ajili ya Benki
kuna vipengele(sura) ambazo utazipa kipaumbele(emphasis) zaidi kuliko
viperngele vingine na maelezo yake yatakuwa pia ni mengi.
KWA
AJILI YA BENKI.
· Kwa
kuwa benki huwa hawatoi mikopo kwa biashara mpya kiholela kutokana na sheria za
nchi kwamba ni lazima mkopaji awe kwanza na dhamna za uhakika, benki katika
mpango wako wa biashara watapenda zaidi
kuona msisitizo katika sura ya fedha umeonyesha vizuri kwanza rasilimali
unazozimiliki wewe pamoja na wamiliki wengine kama wapo.
· Historia ya mahesabu ya biashara ya siku za nyuma na uorodheshe pia dhamana zote zitakazoweza ku “back up” mkopo wako endapo utakuja kushindwa kuurejesha.
· Msisitizo pia unatakiwa katika kipengele cha ‘Sehemu za biashara’(Business Ratios)
· Watapenda pia kuona umeambatanisha katika mpango wako, maombi ya mkopo na ripoti zilizopita za kodi.
SOMA: Jinsi ya kuchora na kutumia chati & grafu kwenye mchanganuo wa biashara
KWA
AJILI YA WAWEKEZAJI
· Wanapenda
msisitizo kwenye sura inayozungumzia Mahitaji ya fedha, unahitaji kiasi gani na
kwa ajili ya nini
· Pia orodhesha wanahisa waliopo pamoja na timu imara ya wafanyakazi
· Wanataka pia kuona mfumo imara wa biashara unaoaminika pamoja na ushahidi wa uwezekano wa biashara kukua vizuri(Business growth)
· Wawekezaji pia ni wavivu sana kusoma mchanganuo mrefu, hivyo tengeneza vizuri Muhtasari wako uweke mambo yote muhimu kwa kifupi ili ukiwavuta basi wakwambie upeleke mchanganuo mzima.
KWA
AJILI TU YA KUENDESHEA BIASHARA YAKO.
· Unaandika
sura zote ukipenda lakini weka msisitizo tu katika zile sura au vipengele
ambavyo wewe mwenyewe umepanga kuwa vitakuwa ndiyo kipaumbele chako katika
kuifanikisha hiyo biashara.
· Kwa
mfano mwingine anaweza kuamua kwamba katika biashara yake suala la wafanyakazi
ndio siri yake kubwa ya ushindi, hivyo sura hiyo ya ‘management’ itabidi aweke
maelezo yakutosha. Ikiwa ni katika soko na mauzo basi sura ya mikakati na
masoko itabidi uweke kipaumbele na maelezo ya kutosha kuliko sura zinginezo.
0 Response to "NINA TATIZO KUBWA UPANDE WA MAKADIRIO YA GHARAMA NA KUJUA AINA YA MPANGO WA BIASHARA(SWALI)"
Post a Comment