Jinsi ya kuyafikia malengo fulani muhimu kabisa
maishani, kila binadamu hapa Duniani huanza kuwaza kitu hiki mapema kabisa
tangu akiwa mtoto mdogo pale akili inapoanza kupata ufahamu. Lakini kwa bahati
mbaya sana siyo kila ndoto za mtu huja kutokea kuwa kweli kama alivyoota
utotoni. Kwanini….? Wengi watakujibu ni
kwasababu hawakuweza kupata njia au namna ya kutimiza ndoto hizo, hawakuwa na
fedha za mtaji, walikosa mbinu sahihi za kufanikiwa kibiashara, walikosa hiki, walikosa
kile na blaa blaa chungu nzima! Ilimradi tu hazikosekani sababu.
Lakini ikiwa ingewezekana kurudisha muda
nyuma na kuchunguza mazingira ya watu hawa kwa umakini, ungeweza kugundua kuwa
sababu wanazozitoa hazina mashiko yeyote na fursa zilikuwepo tele ila tatizo tu
ni kwamba hawakuweza kuziona. Kwanini hawakuweza kuziona…..?, tuendelee tutajua
hapahapa…..
SOMA: Je upo kwenye kazi au fani uliyotamani kuwa tangu ulipokuwa mtoto mdogo?
SOMA: Je upo kwenye kazi au fani uliyotamani kuwa tangu ulipokuwa mtoto mdogo?
Ujue, Duniani na Tanzanaia ikiwemo wapo watu
wengi tu tunaowachukulia kama ni watu wenye “BAHATI” kwasababu wameweza
kufanikisha kila lengo walilojiwekea maishani, wana biashara nzuri za ndoto zao
zinazowaingizia mamilioni ya pesa, wana kazi nzuri zinazowapa mshahara mzuri,
wanamiliki magari ya kifahari, wana majumba na vitu vizuri kibao. Lakini watu
hao siri ya utajiri wao ni nini? na hii BAHATI iliwaangukia vipi?, Ni kwa njia
ya kuweza kuziona fursa mapema na huo ndio ukawa mwanzo wa wao kufanikisha
mipango iliyotimiza ndoto zao hizo, hakuna uchawi hapo wala sijui kitu gani.
Kuna watu hudhani eti kwamba ili mtu
ahesabike kwamba ana bahati basi ni lazima awe ameshinda bahati na asibu au
apate jiwe kubwa katika mgodi wa madini wanakochimba mamia ya watu. Lakini hebu
nikuulize swali moja, zile shamrashamra unazozionaga pale wimbi la la michezo
ya kubahatisha inapoibuka(Bingo nk.) huwa zinakoishia ni wapi? Si watu baada ya
kucheza weee….na kuchoka hushitukia hapo
hamna bahati na kuamua kupotezea wenyewe huku wahusika wakija kuibuka tena upya
na shamrashamra zingine baada ya watu kusahau?
SOMA: Maisha ya mafanikio? Soma vitabu hivi vya biashara na ujasiriamali kwa kiswahili.
SOMA: Maisha ya mafanikio? Soma vitabu hivi vya biashara na ujasiriamali kwa kiswahili.
Kwahiyo utakubaliana na mimi kwamba bahati za
ukweli hupatikana tu katika vitu vile unavyoweza kuvitabiri ama kuvifikiria
mwenyewe kwenye akili yako pasi na shaka kwamba unaweza kuvipata. Wajasiriamali,
Mawakili, Madaktari, Wagunduzi, Wanamichezo, Wanamuziki, Waalimu, Waandishi, na
wengine wote walio na fani mbalimbali, wote hao unaweza ukasema ni watu
walioona fursa mbalimbali na kwa kutumia akili zao wanaweza wakazigeuza fursa
hizo kuwa BAHATI kubwa kwao maishani.
SOMA:Ukweli uliofichwa juu ya pesa: Watu hawatafuti kazi bali hutafuta pesa.
SOMA:Ukweli uliofichwa juu ya pesa: Watu hawatafuti kazi bali hutafuta pesa.
Fursa ni nyingi mno unazoweza kuzitaja na
kila binadamu ana nafasi sawa ya kuzipata isipokuwa tu huwa zenyewe hazijianiki
barabarani wala kujitangaza bali huja zikiwa zimejificha ndani ya koti la matatizo
na magumu mbalimbali ya kimaisha kusudi ili wale waoga wasiokuwa na subira
wazikimbie na kusema, fursa duniani hamna tena siku hizi zimekwisha. Kwa wale
wajanja waliokuwa na subira huu huwa ndio mwanzo wa kutoboa na kuwa mabilonea.
Ni kanuni ya asili iliyojijenga yenyewe
kwamba, fursa hujitokeza pale ambapo haitegemewi kabisa kuibukia na usije ukategemea
kamwe kwamba kuna siku moja mtu atakuja na kukuonyesha fursa ilipo, ila
uwezekano wa fursa hauna mwisho na kila mtu anaweza kuziona endapo tu ataamua
mwenyewe. Ili kulithibitisha hili nisemalo nakuomba ufanye jaribio lifuatalo;
Tafuta
zawadi nzuri zipatazo 5 hivi tofautitofauti, kisha chagua yule mtu umpendaye,
yeyote tu yule na si lazima awe ni mpenzi wako, halafu zifiche zawadi hizo
ndani maeneo tofautitofauti akiwa hayupo. Sasa mwambie azitafute mpaka azipate
ila usimwambie kama zipo ngapi wala ni zawadi za aina gani, wewe mwambie tu
zipo zaidi ya moja. Atazitafuta na akifanikiwa kuzipata 2 au 3 tu utamuona
amesitisha zoezi la kutafuta kwa sababu, kwanza hajui ni zawadi ngapi
ulizoficha, wala zawadi hizo ni zipi. Lakini kama ungelikuwa umemtajia idadi na
aina ya zawadi zote bila shaka
asingesita kuzisaka mpaka ahakikishe amezipata zote 5.
Hapo zamani za kale Binadamu aliishi katika
Dunia isiyokuwa na mwanga wa umeme, magari, simu za mkononi, kompyuta,
Intaneti, Tv wala redio. Lakini muda ulivyozidi kwenda Wabunifu na Wagunduzi
mbalimbali waliweza kubuni vitu vyote hivyo na sasa kila mmoja wetu
anavifurahia. Na bado katika karne zijazo kutakuwa na vitu vya kustaajabisha
zaidi ya hivi tuonavyo leo. Haya yote ni maajabu ya jinsi fursa zilivyotapakaa
na namna watu mbailmbali wanavyoziona na kuzitendea kazi.
SOMA: Njia mpya za kufanya mambo: Dunia, Biashara, Ajira vinabadilika kwa kasi ya ajabu
SOMA: Njia mpya za kufanya mambo: Dunia, Biashara, Ajira vinabadilika kwa kasi ya ajabu
Leo hii unaweza kulalamika fursa hakuna lakini
cha kustaajabisha ni kwamba mtoto ambaye hata hajazaliwa atakuja kuzaliwa na
atakuwa bilionea miaka ijayo sisi tumeshakufa kitambo, sasa hizo fursa
unafikiria atazitoa wapi ilihali leo hii sisi tunalalamika fursa hamna?
HITIMISHO.
Dunia imejaa fursa tele kwa watu wa rika
zote, jinsia na makabila yote, kila mtu anaweza akatimiza malengo yake yote
aliyojiwekea maishani. Kinachotakiwa tu ni mtu kujifunza jinsi ya kuitumia
akili yake vizuri katika kupata mbinu za kufanikiwa kibiashara. Inaweza ikachukua muda mtu kujitayarisha kiakili lakini
mwishowe inalipa. Katika maandalizi hayo iaminishe akili yako kabisa kwamba
mafanikio ni kitu kinachowezekana na hiyo ndiyo siri kubwa ya mafanikio.
Jaribu kuwa mbunifu, kwenye kitabu changu
kiitwacho, MICHANGANUO YA BIASHARA NA UJASIRIAMALI, chenye kila kitu mjasiriamali
anachohitaji kufanya biashara ya kisasa, dhana ya UBUNIFU na UJASIRIAMALI
nilizielezea kwa undani sana kwamba ndiyo injini kuu ya wafanyabiashara kuibua
mambo mapya na bila ubunifu basi duniani hakuna maendeleo ya aina yeyote yale.
SOMA: Ujasiriamali: Ubunifu ndiyo msingi wake mkuu na injini ya uchumi katika soko huria.
SOMA: Ujasiriamali: Ubunifu ndiyo msingi wake mkuu na injini ya uchumi katika soko huria.
Mfano mdogo tu ni kwamba ikiwa wewe ni
mfanyabisahara mdogo, unaweza ukashughulika kwanza na eneo dogo ambalo bado
watu wengi hawajaanza kulifanyia kazi sana, simaanishi eneo tu kama sehemu ya
nchi hapana, bali namaanisha eneo hata kisoko, aina fulani ya bidhaa, kwa
kimombo wanaita a ‘niche’ fanya hayo huku ukiamini fursa zipo. Fursa
zenyewe hazitakaa hata siku moja zisubiri mahali mtu aje na kuzichukua tu
kirahisirahisi kama embe au machungwa mtini.
………………………………………
HII NI KWA YULE TU
AMBAYE BADO HAJAJIUNGA NA GROUP YETU YA MASOMO YA FEDHA YA KILA
SIKU(MICHANGANUO-ONLINE)
Ikiwa
tayari umeshajiunga, tafadhali usipoteze muda wako kusoma kwani muda ni pesa.
Ni
wajibu wangu kukukumbusha kila mara kwani najua inawezekana hujui mambo mengine
mazuri yanayoendelea kila siku nyuma ya pazia mbali na makala hizi ninazoandika hapa.
Unapolipia
ada ya kujiunga na Group unapata vitu vifuatavyo;
A. MAMBO MAPYA NA YANAYOKUJA HIVI PUNDE(new
& Coming soon)
1. Masomo
ya fedha kila siku usiku saa 3 mpaka saa 4
2. Kuna
Kitabu kipya chenye masomo mazuri sana ya fedha kitatoka siku ya Jumanne tarehe
3 Septemba
3. Semina
ya mpango wa kuanzisha kiwanda kidogo cha usagishaji nafaka. Tofauti na
michanganuo mingine yote tuliyowahi kufanya huu utakuwa na ubunifu wa kipekee mno!
na mtu ataweza kuutumia ubunifu huo kuuza unga wa mahindi kama njugu.(A Unique
marketing strategy)
B. OFFA YA ZAMANI (VITU 14) NA
INAYOKARIBIA KUISHA MUDA MCHACHE UJAO, BADO KIDOGO SANA TUTAIONDOA !
1. Kitabu
cha MICHANGANUO YA BIASHARA NA UJASIRIAMALI kwa lugha ya Kiswahili.
2. Kitabu
kipya cha masomo ya Mzunguko chanya wa fedha 2018 part 1
3. Kitabu
kipya cha Masomo ya fedha 2018 part 2
4. Kitabu
kipya 1 cha jinsi ya kuandika michanganuo ya biashara hatua kwa hatua.
5. Kitabu
mashuhuri zaidi duniani, HOW TO WRITTE A BUSINESS PLAN kwa lugha ya kiingereza,
ndio kinachotumika vyuo vikuu vingi duniani.
6. SEMINA:
Masomo 11 ya jinsi ya kuandika mpango wa biashara.
7. Kifurushi
maarufu cha michanganuo 3 ya ufugaji wa kuku(MKOMBOZI CHICKS PLAN 3PACKS)
8. Mchanganuo
wa biashara ya mgahawa(JANE RESTAURANT) kwa Kiswahili na kiigereza
9. Mchanganuo
wa biashara ya kilimo cha matikiti maji.
10.
Vielezo(Templates) za michanganuo ya biashara
inayokuwezesha kuandika michanganuo kwa muda mfupi.
11.
Semina na mchanganuo wa Biashara: Kiwanda cha
tofali za saruji Kiluvya.
12.
Mfumo mpya wa usimamizi wa duka la rejareja(2
IN ONE STORE MANAGEMENT SYSTEM) unaomwezesha mmiliki wa duka dogo la rejareja
au la kati kuthibiti mapato yake pasipo msaidizi kudokoa hata senti 5
13.
Somo muhimu sana la mzunguko wa fedha.
14.
Ukurasa mmoja wa mchanganuo.
Nirudie tena, vitu vyoote hivi unavipata kwa
shilingi Elfu 10 tu! Unaweza ikiwa utawahi kabla offa hii maalumu haijafungwa.
Thamani ya masomo na vitabu unavyoona hapo juu ni zaidi ya shilingi elfu 90 kwa
bei ya kawaida. Nilitamani sana wewe msomaji wangu upate masomo haya yote kwani ni
dhamira yangu kuu wewe kutumia vizuri kila fursa iliyokuwepo katika kufanikisha
ndoto zako.
Namba za malipo ni, 0765553030 au 0712202244
jina, Peter Augustino Tarimo, na baada ya kulipia, nitumie ujumbe wasap au meseji
ya kawaida kwa namba 0765553030 isemayo; “NIUNGANISHE MASOMO YA KILA SIKU NA OFFA INAYOISHIA”
Asante na Karibu sana…
Peter A. Tarimo
0 Response to "FURSA ZA MAFANIKIO KAMWE HAZITAKAA ZIISHE LAKINI PIA HAZICHUMWI MTINI KAMA EMBE"
Post a Comment