UKWELI ULIOFICHWA JUU YA PESA: WATU HAWATAFUTI KAZI BALI HUTAFUTA PESA | JIFUNZE UJASIRIAMALI

UKWELI ULIOFICHWA JUU YA PESA: WATU HAWATAFUTI KAZI BALI HUTAFUTA PESA

MBUNI AKICHIMBIA KICHWA MCHANGANI

Kuna wanaodai kwamba hii ndio sababu kubwa inayozifanya serikali zote duniani ikiwemo hata ile ya Marekani kutoruhusu elimu ya kupata pesa ifundishwe mashuleni moja kwa moja. Watu tangia utotoni huaminishwa tu kwamba kitu muhimu zaidi maishani ni kazi. Pengine inawezekana sababu kubwa za kuficha ukweli huu ni hofu kuwa endapo watu wengi wataujua basi dunia itageuka balaa tupu kwani watu watatumia njia zozote zile zikiwemo hata njia haramu ilimradi tu wajipatie pesa, mimi sijui, hebu fuatilia somo hili mpaka tamati.

SOMA: Njia 7 halali na nzuri za kupata mafanikio na utajiri wa haraka.

Tukiacha ajira katika migahawa, hebu niambie unapofanya kazi mahali au au biashara katika jengo fulani, ukifika muda wa chakula cha mchana(lunch) unaweza ukamega kipande cha jengo, mashine au fenicha ukakitia mdomoni na kukitafuna mithili ya chakula? Bila shaka haiwezekani, badala yake utachukua pesa unazolipwa au faida ya biashara  na kwenda mgahawani kununulia chakula ili uweze kula. Hivyo hapo hukwenda kutafuta kazi bali pesa.


Lakini mamilioni ya watu kote Duniani wamekuwa wakifanya kosa hili kubwa la kufikiria kwamba wanatafuta kazi, kweli wengi huwa wanapata kazi lakini hatimaye kazi hizo baadae hugeuka kuwa kitu kisichowasisimua kabisa huku zikiwalipa mishahara midogo wasiyoweza kukidhi mahitaji yao yote ya kimaisha. Kinyume chake ni kwamba unapoamua kutafuta pesa badala ya kazi, unapata vyote viwili, pesa pamoja na kazi nzuri. Unajua ni kwanini?...

Idadi kubwa ya wafanyabiashara hujiingiza katika biashara pasipo kuwa na malengo ya kutengeneza pesa. Makampuni nayo huajiri watu na kujiwekea malengo ya mauzo bila ya kujishughulisha kulenga katika lengo kuu la kuingiza pesa.


Ukitaka kuthibitisha ukweli kwamba watu wanachotafuta ni pesa na wala siyo kazi, hebu fanya jaribio lifuatalo; Nenda katika kampuni yenye wafanyakazi wengi kisha wajulishe kila mmoja kwa siri pasipo bosi wao kujua kwamba kuna kampuni nyingine inayofanana na ile ya kwao inatafuta wafanyakazi kwa mshahara mara 2 ya ule wanaolipwa pale.

Kama atabaki mfanyakazi hata mmoja kwenye hiyo kampuni basi ujue kwamba labda huyo atakuwa alikuwa anamiliki hisa katika hiyo kampuni, kama siyo hivyo basi kampuni ni mali ya baba yake na yeye huenda ndiye wa kuja kuirithi. Kila mtu atatamani kwenda kulipwa mara 2 ya mshahara anaolipwa sasa na hilo halina ubishi.

Sasa ni nini kifanyike?

Ingawa si viongozi wa kiserikali wala jamii........inaendelea......


Ndugu msomaji wa somo hili, huu siyo mwisho wa hili somo, bado litaendelea katika group la Whatsapp la Michanganuo-online leo februari 25 usiku saa 3. Masomo mengine mengi kama haya ni kila siku, pia unapojiunga na group tunakupatia masomo na semina zote zilizopita tangu mwaka uliopita, ni masomo mengi utakayochagua ni yapi yanakufaa zaidi.

Kujiunga kiingilio ni shilingi elfu 10 mwaka mzima na namba zetu za malipo ni, 0712202244 au 0765553030 jina, Peter Augustino Tarimo. Baada ya malipo tuma ujumbe wa wasap au wa kawaida ukisema, “NIUNGE NA GROUP LA MASOMO” Muda huohuo nitakuunganisha na kukutumia kila kitu.

Ikiwa hutumii wasap usijali kwani vitu vyote pia tunatuma katika email yako na updates zote muhimu tutakuwa tukikuforwadia kila siku, iwe ni masomo mapya, michanganuo, vitabu au semina.

Vitabu vya ujasiriamali na biashara kwa kiswahili pia vinapatikana, Softcopy na Hardcopy kwa bei nzuri, kama unahitaji fungua ukurasa huu, SMART BOOKS TZ 

0 Response to "UKWELI ULIOFICHWA JUU YA PESA: WATU HAWATAFUTI KAZI BALI HUTAFUTA PESA"

Post a Comment