NJIA 7 ZA KUBANA MATUMIZI BILA KUHISI UNAJITESA KUBORESHA BAJETI YAKO | JIFUNZE UJASIRIAMALI

NJIA 7 ZA KUBANA MATUMIZI BILA KUHISI UNAJITESA KUBORESHA BAJETI YAKO

kubana matumizi kuboresha bajeti yako
Kama umewahi kuwa shuleni, chuoni au katika mkusanyiko wowote ule wa watu ambapo muda wa mapumziko kila mtu anajinunulia kitu anachokipenda kwa ajili ya kunywa na kula utaelewa ni nini ninachotaka kumaanisha hapa. Wengine watanunua chipsi kuku, mayai na juisi, wengine sambusa nyama na soda, wengnine supu ya mbuzi, ndizi, pilau, biriani nk. wakati wewe unajichukulia mihogo yako ya kuchemsha au ya kukaanga na maji ya bomba maarufu kama kandoro kwa wakazi wa jiji la Dar es salaam lengo likiwa ni kubana matumizi ili bajeti yako isiende vibaya.


Kubana matumizi siyo kitu kibaya hata kidogo ilimradi tu kile unachotumia kina kidhi mahitaji yako na kukufanya uendelee kuishi kama ni chakula unashiba sawasawa tu na yule aliyekula biriani na kama ni kiu pia inakatika sawasawa tu na yule aliyekunywa juisi au soda. Shida haipo kwenye kukidhi haja bali ipo kwenye hisia za mtu, ile hali ya kuhisi akilini kwamba unajitesa.  Isingelikuwa hivyo wala kusingelikuwa na shida yeyote ile kwenye kubana matumizi.

Kwa bahati mbaya sana linapokuja suala la matumizi ya pesa, suala la kubana matumizi siyo rahisirahisi kama mtu unavyoweza kufikiria, hakuna mtu hata mmoja anayefurahia kujinyima kitu wakati anakiona na anaona wenzake wanatumia wala hakuna mtu anayefurahia kula ugali wa mchicha na dagaa wakati jirani yake kila siku anakaanga samaki na maini. Kusema ule ukweli hali hiyo mbaya ya kihisia hatimaye huwafanya watu wengi badala ya kuendelea kubana matumizi ili waweze kufikia malengo waliyojiwekea kimaisha wanaamua kujiingiza kwenye matumizi mabaya zaidi kushinda hata ilivyokuwa mwanzoni.


Mtu anaamua kuvaa miwani ya mbao, kuvaa miwani ya mbao maana yake ni kujifanya kama vile tatizo halioni, ni sawa na mtu anayeamua kulewa pombe na kufanya mapenzi na mtu ambaye katika hali ya kawaida asingeliweza kabisa kufanya hivyo. Kwahiyo mtu anaamua kuingia kwenye matumizi makubwa na kuharibu kabisa bajeti yake bila kujali kitu kutokana na hisia zile za kujitesa anazozipata pindi anapokuwa akibana matumizi, hali ya kuhisi kutokuwa nacho, wengi huamua kujisemea, “niache niponde mali bwana kwani kufa kwaja

Kwa hiyo leo hii katika group la masomo ya kila siku, somo letu la fedha ambalo ni somo la 3 miongoni mwa masomo 30 ya mwezi huu wote wa 12 tutakwenda kujifunza njia 7 mtu unazoweza kuzitumia na kuishi maisha kulingana na kipato chako unachopata bila ya kuhisi kabisa kama unajitesa wala kubana matumizi kupita kiasi.

Ndugu msomaji, masomo haya si ya kukosa ikiwa wewe unapenda kujifunza masuala ya fedha na ujasiriamali. Tulianza tangu mwezi January na sasa tuna masomo yanayojaza vitabu 3 vikubwa ambavyo pamoja na vitu vingine kama semina, michanganuo ya biashara mbalimbali zinazolipa na vitabu vya jinsi ya kuandika mpango wa biashara kwa Kiswahili na kiingereza vyote hivi tumevikusanya na tunakutumia katika mfumo wa softcopy( PDF.)


Ili kujiunga unalipia ada ambayo ni shilingi elfu 10 na muda huohuo tunakutumia masomo pamoja na kukuunganisha na group. Ada hiyo ni ya kudumu kwa mwaka mzima wa 2019 hutalipia tena chochote.

Namba za malipo ni 0712202244 au 0765553030  jina Peter Augustino Tarimo.
WHATSAP ni 0765553030

Ukishalipia tuma ujumbe wa kawaida au wa wasap usemao, “NIUNGANISHE NA GROUP LA MICHANGANUO-ONLINE”

Ikiwa hutumii Whatsapp hamna shida, masomo yote tunakutumia kupitia E-mail yako.

Mwisho wa offa ya masomo haya ni tarehe 30 Desemba 2018. Baada ya hapo tunaanza programu nyingine na masomo yote ya 2018 hayatakuwepo tena. Wahi kwani nafasi katika group pia zimebakia chache.


Pamoja na vitu vingine 10, Hapa chini ni vitabu 3 vyenye masomo na semina za toka Januari mpaka Novemba;








0 Response to "NJIA 7 ZA KUBANA MATUMIZI BILA KUHISI UNAJITESA KUBORESHA BAJETI YAKO"

Post a Comment