BIASHARA NZURI YA KUANZIA UNAPOTAKA KUWA TAJIRI NA KUFIKIA UHURU KAMILI KIFEDHA | JIFUNZE UJASIRIAMALI

BIASHARA NZURI YA KUANZIA UNAPOTAKA KUWA TAJIRI NA KUFIKIA UHURU KAMILI KIFEDHA

Wafanyabiashara nzuri zinazolipa

Kwa karne nyingi binadamu wamekuwa ni viumbe walio na kiu ya kutaka kujua ni kwa jinsi gani wanaweza kupata utajiri kwa haraka na kuufikia uhuru wa kifedha katika muda mfupi kwa kadiri inavyowezekana. Lakini zoezi hilo kila mara kwa watu wengi limeonekana kuwa ni gumu. 

SOMA: Kuwa bilionea naweza kutumia njia zipi?

Katika somo letu la leo tutakwenda kuona kwanza kabisa, hatua za kuchukua pale mtu anapotaka kuianza safari ya kuusaka uhuru kipesa halafu pia tutakwenda kuona ipi ni biashara nzuri ya kuanzia unapotaka kuwa tajiri na kufikia uhuru kamili kifedha.

Hatua za kufuata 

Hatua ya 1: 

Anzisha na kumiliki Biashara

Hakuna vyanzo vya utajiri endelevu na wa uhakika nje ya biashara. Dalili ya utajiri huanzia tu pale mtu anapochukua hatua ya kufungua biashara ama kufanya uwekezaji wenye faida wa namna yeyote ile iwe ni kwenye ardhi, nyumba, shamba, ufugaji nk.

SOMA: Biashara 7 nzuri za kufanya zitakazokuingizia pesa hata kama umelala.

Biashara zenye faida Tanzania unazoweza kuanza nazo zipo nyingi lakini unatakiwa uwe makini kidogo, kuna kitu muhimu sana cha kuzingatia kama makala hii inavyoenda kukujuza.

Hapa unatakiwa kufanya kazi kwa bidii sana kabla biashara haijatengemaa na kuweza kujiendesha yenyewe bila ya wewe kulazimika kuwepo pale. Biashara kujiendesha maana yake inatumia nyenzo mbalimbali kama vile wafanyakazi, fedha za watu wengine, mifumo mbalimbali ya kimasoko kama vile tovuti na mitandao ya kijamii.

Lengo hapa ni ili baadae uweze kumiliki rasilimali zilizo na uwezo wa kukuletea kiasi kikubwa cha fedha hata ikiwa hautafanya kazi moja kwa moja. Katika steji hii ya mwanzo elimu ya pesa ni muhimu sana hasa kuzijua siri mbalimbali za pesa,. Saikolojia ya pesa na jinsi ya kujiwekea akiba.

SOMA: Je wajua unaweza kumiliki kiwanja au nyumba bila kutoa senti 5 mfukoni? soma kitabu cha dola milioni 5 ujue

kujua siri ya pesa hapa simaanishi eti uende kwa wale jamaa wanaojitangaza kwenye mabango njiani kuwa wanatoa ujajiri bila masharti au dawa ya mafanikio wakati ukishafika kwao sharti la kwanza tu unaambiwa ukalete kondoo mweusi.

Njia sahihi ya kuzijua siri za pesa na utajiri ni kusoma vitabu, mitandao ya kijamii kama hivi unavyosoma hapa, kuhudhuria semina mbalimbali za makocha na waalimu wa ujasiriamali nk.    

Hatua ya 2:

Weka vitegauchumi 

Chukua mapato yatokanayo na biashara yako uliyoanzisha hapo juu na uwekeze katika vitegauchumi vyenye uwezo wa kuzalisha faida kwa mfano, uwekezaji katika ardhi na majengo, hisa katika makampuni mengine, biashara za kuazimisha vifaa na mitambo, miradi hii itakuletea mapato ya ziada kila mwezi.  

Hatua ya 3:

Jenga msimamo:

Endelea kuwekeza gawio na faida itakayotokana na miradi tuliyoiona namba 2 hapo juu katika vitegauchumi zaidi ili kunufaika na ongezeko kubwa la mapato mara dufu, kwanza kutokana na biashara yako ya awali lakini pia kutokana na vitegauchumi vilivyotokana na faida ya biashara hiyo.

 SOMA: Biashara ndogo rahisi kwa wajasiriamali zinazoenda na wakati tulio nao

Baada ya muda fulani mapato ya ziada yaliyotokana na biashara yako ya awali pamoja na vitegauchumi ulivyoanzisha yatakuwa yameshazidi gharama zako za maisha (matumizi) na hivyo kuwa tayari umeshaufikia uhuru wako kifedha.

Badala ya biashara ya kawaida mwanzoni kwenye ile hatua ya 1, unaweza hata ukaanza na kazi ya ajira yenye uwezo wa kukupatia mapato kila mwezi. 

Baada ya kufikia uhuru kifedha sasa unaweza kuachana na biashara yako ya awali au ajira na kuamua kufanya chochote utakacho kama vile kusafiri, kwenda kutalii maeneo mbalimbali duniani yenye vivutio, kutumia muda wako mwingi na familia yako au hata ukaamua kutulia tu huku ukiendelea kuwekeza katika vitegauchumi.

SOMA: Biashara ya mtaji mdogo yenye faida kubwa zaidi tanzania ilivyoshangaza darasa la michanganuo ya biashara

Kujianzishia makampuni mengine kwa ubia na watu hata kutoka nje ya Bara la Afrika kama alivyokuwa akifanya Marehemu Mzee Reginald Abraham Mengi (Mungu amlaze pema peponi). Mzee Mengi alikuwa ameshaanza mazungumzo na makampuni toka nje kuja kuwekeza viwanda vya simu na magari hapa Tanzania. Lakini kumbuka wakati huo mapato yako ya ziada (namba 2) bado yanaendelea kuingia.

Katika safari yako yote hiyo ni lazima uwe ni mtu wa kutengeneza mtandao  na watu mbalimbali, kujifunza kupitia vitabu na vyombo vingine mbalimbali vya habari hasa kuhusiana na taaluma yako au sekta ya biashara ulizowekeza, wajasiriamali na wawekezaji ni sawa tu kama walivyokuwa wanasheria, madaktari na wahasibu, ni watu wa kujifunza kabla na ni lazima ubobee katika kile unachokifanya ikiwa utataka mafanikio na utajiri, na haiwezekani ukatumia njia ya mkato ndio maana watu wengi huona kama ni jambo gumu kupata utajiri. 

SOMA: Biashara yenye mtaji mdogo isiyojulikana na watu wengi bado-1

Habari njema ni kwamba, kwa makadirio ikiwa mtu anaweza akafuata hatua zote vizuri inaweza ikamchukua takribani miaka 5 hivi kutajirika na kuwa huru kabisa kifedha, na hiki ni kipindi kifupi kabisa.

Jinsi ya kuwa na uhuru wa kifedha

Kabla hatujaenda kuona aina za biashara za kuanza nazo unapotaka kuufikia utajiri na hatimaye uhuru kifedha hebu kwanza tuone nini maana ya uhuru wa kifedha hasa.  Uhuru wa kifedha ni hali ambayo mapato yako ya ziada kutoka kwenye vile vitegauchumi usivyohusika moja kwa moja katika mchakato wa uzalishaji yanapokuwa makubwa kuliko gharama zako zote za maisha (matumizi).  

 

SOMA: Mbinu za kufanikiwa kufikia malengo katika uwekezaji wowote utakaofanya.

Kwa mfano kama una biashara inayoingiza faida shilingi laki 5 kwa mwezi kama mapato ya ziada na matumizi yako kwa mwezi ni  shiligi laki 3, tayari wewe unakuwa umeshaufikia uhuru kifedha na unaweza hata ukaachana na kazi yako ya awali.  

Aina ya biashara nzuri ya kuanzia unapotaka kuwa tajiri na kufikia uhuru kamili kifedha

Kumiliki biashara bila shaka kunatajwa kuwa ndiyo njia bora zaidi ya kuwa tajiri haraka au kuanza safari ya kuufikia utajiri na hatimaye uhuru kamili wa kifedha, lakini siyo biashara zote zenye uwezo huo, baadhi yake mtu unaweza kutajirika haraka na kwa gharama kidogo lakini nyingine huchukua muda mrefu na uwekezaji wa pesa nyingi.

Biashara hizo ni hizi zifuatazo;....................................................

...............................................................................................................................................................................................................................................................................................................

Mpenzi mdau wa masomo haya ya fedha hii ni sehemu ndogo tu ya somo letu hili. Masomo kamili unaweza ukayapata yote ndani ya MASTERMIND GROUP LA MICHANGANUO-ONLINE ambapo yanatolewa mfululizo kila siku.

Kujiunga na Kundi hilo lipia ada ya mwaka sh. 10,000/= tu kupitia namba 0712202244 au 0765553030 jina Peter Augustino Tarimo kisha SMS au ujumbe wasap usemao “NATAKA OFFA YA VITU 14 NA GROUP LA MASOMO”

Ukishalipia tunakutumia pia OFFA ya vitabu na Michanganuo ya biashara mbalimbali kwenye simu au kompyuta muda huohuo, jumla ni vitu 14, tazama orodha hapo chini.

Ndani ya group pia tunakuwa na semina za jinsi ya kuandika Michanganuo ya biashara bunifu zinazolipa haraka.

 

CHINI NI ORODHA YA VITU 14 VYA HIYO OFFA;

                           1.       KITABU: Michanganuo ya Biashara na Ujasiriamali chenye course zote muhimu za BIASHARA, jinsi ya kuandaa michanganuo ya biashara na sample za michanganuo mbalimbali 10 iliyokamilika kila kitu.kwa Kiswahili

                           2.       KITABU: Njia rahisi ya kuandika mpango wa biashara-dakika 30 tu - kwa kiswahili

                           3.      KITABU: Mifereji 7 ya Pesa na Siri Matajiri wasiyopenda kuitoa -kiswahili

                           4.       KITABU: HOW TO WRITE A BUSINESS PLAN  ni maarufu sana duniani, hutumika vyuo vikuu vingi.-kwa kiingereza

                           5.      KITABU: Siri za upishi wa chapati laini-UPENDO CAFE pamoja na Mchanganuo wake kamili.-kwa kiswahili

                           6.       COMPILLATION: Masomo 30 ya fedha usiyoweza kuyapata popote, mengine 70 utayapata kwenye group kila siku - kwa Kiswahili

                           7.      MCHANGANUO: Kiwanda cha usagishaji Dona (Usado milling) - kwa Kiswahili

                           8.      MCHANGANUO: Mgahawa wa chakula-Jane Restaurant –kwa kiingereza

                           9.      MCHANGANUO: Mgahawa wa chakula-Jane Restaurant –kwa Kiswahili

                        10.    MCHANGANUO: Ufyatuaji tofali za saruji- kwa kiswahili

                        11.    MCHANGANUO: Kuku wa nyama -Tumaini Broilerskwa kiingereza

                        12.    MCHANGANUO: Kuku wa nyama -Tumaini Broilerskwa kiswahili

                        13.    MCHANGANUO: Kiwanda cha mvinyo na juisi ya Rosella –Choya Investment – kwa kiswahili

                        14.    MCHANGANUO: Kilimo cha Tikiti maji:- Kibada Watermelon Fruits – kwa kiswahili

 

0 Response to "BIASHARA NZURI YA KUANZIA UNAPOTAKA KUWA TAJIRI NA KUFIKIA UHURU KAMILI KIFEDHA"

Post a Comment