KANUNI YA SIRI YA COCA COLA, BIRIKA LA AJABU NA WAZO LA DOLA MILIONI 1 | JIFUNZE UJASIRIAMALI

KANUNI YA SIRI YA COCA COLA, BIRIKA LA AJABU NA WAZO LA DOLA MILIONI 1

Ikiwa kama bidhaa ya lile birika la shaba ingeliweza kuzungumza, ingeliweza kusimulia hadithi ya kusisimua ya mapenzi, ya wanataaluma wanaume kwa wanawake ambao kila siku huburudishwa nayo.

Mwandishi ana uhakika wa angalao moja ya hadithi hizo, kwani alikuwa sehemu ya hadidhi hiyo, na yote yalianza siyo mbali kutoka eneo lilelile ambalo muuza dawa(karani wa duka la dawa) aliponunua birika la zamani. Ilikuwa ni hapa Mwandishi alipokutana na mke wake, na alikuwa ni mke wake aliyekuwa wa kwanza kumuelezea juu ya birika la ajabu. Ilikuwa ni bidhaa ya lile birika waliyokuwa wakinywa wakati alipomuomba kumkubalia “kwa shida na raha” 

Sasa, kwamba unafahamu kilichokuwemo ndani ya birika la ajabu ni kinywaji maarufu duniani, inapendeza kwamba mwandishi anakiri kuwa, mji wa nyumbani wa kinywaji hicho ulimpa mke, pia kwamba kinywaji chenyewe kilimpa msisimko wa mawazo bila sumu, na hivyo kutoa burudisho la akili lililomwezesha mwandishi kufanya kazi yake nzuri.

Yeyote awaye, popote pale unapoweza kuwa unaishi, kazi yeyote ile unayoweza kuwa unafanya, kumbuka tu wakati ujao, kila wakati utakapoona jina “Coca cola” kwamba ni miliki kubwa sana ya utajiri na ushawishi iliyotokana na wazo moja, na kwamba kiambata cha ajabu, karani wa dawa – Asa Candler – alichochanganya na kanuni ya siri kilikuwa ni……Ubunifu !

Simama na ufikirie kuhusiana na hilo kwa muda kidogo.

Kumbuka, pia kwamba hatua 13 kuelekea utajiri zilizoelezwa katika kitabu hiki zilikuwa ni chombo, kupitia hicho, ushawishi wa coca cola umeenezwa kwa kila jiji, mji, kijiji na katika njia panda za dunia . Wazo lolote unaloweza kubuni lililokuwa zuri na lenye kustahili kama coca cola, lina uwezekano wa kuiga(kukopi) rekodi kubwa ya kinywaji hiki cha dunia nzima. Ukweli mawazo ni vitu, na upeo wake wa kufanya kazi ni dunia yenyewe.

Ningefanya Kitu Gani Kama Ningepata Dolla Millioni Moja
Simulizi hii inathibitisha ukweli wa ule usemi wa zamani, Penye nia pana njia Nilisimuliwa na yule mpendwa mwalimu na mchungaji, Frank W. Gunsaulus, ambaye alianza kazi yake ya kuhubiri katika eneo la Stockyards la Kusini mwa Chicago.

Wakati Dr. Gunsaulus alipokuwa chuoni, aligundua mapungufu mengi katika mfumo wetu wa elimu, mapungufu ambayo aliamini angeliweza kuyarkebisha ikiwa kama angelikuwa Mkuu wa Chuo. Shauku yake kubwa kabisa ilikuwa ni kuwa kiongozi mkuu wa chuo cha elimu ambacho vijana wadogo wa kiume na wa kike wangeweza kufundishwa “kujifunza kwa vitendo”

Alifanya uamuzi wa kuanzisha chuo kipya ambacho angeweza kutekeleza wazo lake jipya pasipo kulemazwa na njia za jadi za utoaji elimu. Alihitaji Dolla Milioni moja ili kutekeleza mradi ! Ni wapi angelaza mikono yake kwa kiasi kikubwa hivyo cha pesa? Hilo lilikuwa ni swali lililotawala sehemu kubwa ya mawzo ya mhubiri huyu kijana aliyekuwa na malengo makubwa.

Lakini hakuweza kuonekana kupiga hatua yeyote.

Kila siku aliingia kitandani na lile wazo. Aliamka nalo asubuhi. Alitembea nalo kila mahali alipokwenda. Aliligeuza tena na tena katika akili yake mpaka likageuka kuwa shauku isiyotulizika. Dolla Millioni moja ni fedha nyingi. Alitambua ukweli huo lakini pia aligundua ukweli kwamba kikwazo pekee ni kile ambacho mtu hujiwekea katika akili yake mwenyewe

Alikuwa mwanafilosofia na pia mhubiri, Dr.Gunsaulus alitambua, kama wafanyavyo wale  wote wanaofanikiwa maishani kuwa, udhahiri wa lengo ndiyo kituo ambapo mtu ni lazima aanzie. Alitambua pia kwamba udhahiri wa lengo huchukua umbo, uhai na nguvu unaposaidiwa na Shauku kubwa kulibadilisha lengo hilo kuwa katika kitu kinacholingana nalo.

Alifahamu ukweli wote huu mkubwa, lakini bado hakujua ni wapi au ni jinsi gani angeweza kuweka mikono yake kwenye dola milioni moja. Utaratibu wa asili ingeliweza kuwa ni kukata tamaa na kuacha, akisema , ‘Ah sawa, wazo langu ni zuri lakini siwezi kufanya nalo chochote kwa sababu kamwe siwezi kupata dolla millioni moja zinazohitajika’. Hivyo ndivyo hasa ambavyo watu wengi wangeliweza kusema, lakini sivyo Dr. Gunsaulus alivyosema.

Alichosema yeye, na alichokifanya, ni muhimu kiasi kwamba sasa namtambulisha na kumuacha azungumze, mwenyewe.

‘Siku moja Jumamosi mchana nilikuwa chumbani kwangu nikifikiria njia na namna ya kupata fedha ili kutekeleza mipango yangu. Kwa karibu miaka niwili nilikuwa nikifikiria, lakini sikuwa nimefanya chochote zaidi ya kufikiria.

Muda ulikuwa umewadia wa kuchukua hatua

Niliamua mara moja kwamba ningeweza kupata dolla milioni moja zilizohitajika, ndani ya wiki moja. Ki vipi? Sikujali kuhusiana na hilo. Jambo kubwa na la muhimu lilikuwa ni uamuzi wa kuzipata fedha ndani ya muda uliopangwa. Dakika niliyofikiria uamuzi huo, hisia ya ajabu ya kujiamini ilinijia kwa namna ambayo kamwe sikuwahi kuhisi hapo kabla. Kitu ndani yangu kilionekana kusema, “Kwanini hukufikia uamuzi huo muda mrefu? Pesa zilikuwa zikikusubiri muda wote !”

‘Mambo yalianza kutokea kwa haraka. Niliita magazeti na kutangaza kuwa ningeweza kutoa mahubiri(hotuba) asubuhi ya siku iliyofuata yanayohusu, “Ningefanya nini kama ningepata Dola million moja”

‘Nilikwenda kuifanyia kazi hotuba ile mara moja. Ni lazima nikueleze, ukweli haikuwa kazi ngumu kwasababu nilikuwa nikiiandaa hotuba hiyo kwa karibu miaka miwili. Roho yake ilikuwa sehemu yangu !

‘muda kabla ya usiku wa manane nilikuwa nimemaliza kuandika hotuba. Niliingia kitandani na kulala na hisia za kujiamini kwani niliweza kuona mwenyewe kama tayari nilikuwa nazo dolla milioni moja.

‘Asubuhi iliyofuata niliamka mapema, nikaenda bafuni, nikasoma hotuba, kisha nikapiga magoti na kusali ili hotuba yangu iweze kusikika na mtu ambaye angeliweza kutoa pesa zilizohitajika.

‘Wakati nikiwa nasali, tena nilijiwa na zile hisia za kujiamini, kwamba pesa zingeliweza kupatikana haraka. Kwa taharuki niliondoka bila kuchukua hotuba yangu, na sikugundua kosa hilo mpaka nilipokuwa kwenye mimbari yangu na karibu kuanza kuhutubia.

‘Muda ulishakwenda mno kurudi tena kuchukua karatasi, baraka lioje, badala yake akili yangu ya ndani mwenyewe ilizalisha vitu nilivyohitaji. Niliposimama kuanza hotuba yangu, nilifumba macho yangu na kuzungumza kwa moyo wangu wote na roho kuhusu ndoto zangu. Sikuzungumza na wasikilizaji wangu tu, bali pia niliigiza kama nazungumza na Mungu. Nilieleza ningeliweza kufanya kitu gani na dola milioni moja ikiwa kiasi hicho kingewekwa mikononi mwangu. Nilielezea mpango niliokuwa nao akilini mwangu kwa kuanzisha taasisi kubwa ya kielimu ambapo vijana wadogo wangeliweza kujifunza kufanya vitu kwa vitendo, na wakati huohuo wakikuza akili zao.

‘Nilipomaliza na kuketi chini, mwanaume mmoja taratibu alisimama kwenye kiti chake, mistari mitatu kutoka mstari wa mbele na kuja kuelekea ilipo mimbari(jukwaa). Nilishangaa alikuwa anakuja kufanya kitu gani. Alikuja mimbarini akanyoosha mkono wake, na kusema, “Mheshimiwa, nimependa hotuba yako. Ninaamini unaweza kufanya kila kitu ulichosema unaweza kufanya kama ungekuwa na dola milioni moja. Kuthibitisha hilo nakuamini pamoja na hotuba yako, kama utakuja kwenye ofisi yangu kesho asubuhi nitakupa dolla million moja. Jina langu ni Philip D. Armour”

Kijana Gunsaulus alikwenda ofisini kwa bwana Armour na kupewa Dola Millioni moja. Kwa kutumia fedha zile alianzisha Taasisi ya teknolojia ya Armour. Hizo ni fedha nyingi kushinda fedha wengi wa wahubiri walizowahi kuona katika maisha yao yote, bado msukumo wa mawazo nyuma ya pesa hizo ulianza katika akili ya mhubiri kijana katika nukta ya dakika.

Dolla Milioni moja zilizohitajika zilipatikana kama matunda ya wazo . Nyuma ya wazo kulikuwa na Shauku ambayo kijana Gunsaulus alikuwa ameilea katika akili yake kwa takribani miaka miwili.

Chunguza ukweli huu muhimu:
ALIZIPATA FEDHA NDANI YA MASAA 36 BAADA YA KUFIKIA UAMUZI NDANI YA AKILI YAKE MWENYEWE WA KUZIPATA NA KUAMUA JUU YA MPANGO KAMILI(DHAHIRI) WA KUZIPATA ! 

Kulikuwa hakuna kitu kipya au cha ajabu juu ya mawazo yasiyokuwa na uhakika ya kijana Gunsaulus kuhusiana na dola millioni moja na kuziwekea matumaini hafifu. Wengi kabla yake, na wengi tangu wakati wake, wamekuwa na mawazo yanayofanana na yakwake. Lakini kulikuwa na kitu fulani cha kipekee na tofauti kuhusiana na uamuzi alioufikia katika jumamosi ile ya kukumbukwa, wakati alipoyatupa nyuma mawazo yasiyokuwa na uhakika na kutamka waziwazi, “Nitazipata pesa ndani ya wiki moja !”

Mungu inaonekana hujitupa mwenyewe upande wa watu wanaofahamu kwa uhakika kile kitu wanachokitaka, ikiwa wana nia thabiti ya kukipata kitu hicho !

Zaidi ya hapo kanuni ambayo Dr. Gunsaulus aliitumia kupata dola milioni moja bado inaishi !  Inapatikana kwako ! Sheria hii ya wote inafanya kazi leo kama ilivyokuwa wakati kijana mhubiri alipoitumia kwa mafanikio. Kitabu hiki kinaelezea hatua kwa hatua, vipengele 13 vya sheria hii kubwa na kupendekeza jinsi zinavyoweza kuwekwa katika matumizi.

Ona kwamba Asa Candler na Dr. Frank Gunsaulus walikuwa na tabia moja inayofanana . Wote waliujua ukweli unaoshangaza kwamba, MAWAZO YANAWEZA YAKAGEUZWA KUWA PESA KUPITIA NGUVU YA LENGO LILILOKUWA DHAHIRI, PAMOJA NA MIPANGO KAMILI(DHAHIRI)

Kama wewe ni mmoja kati ya wale wanaoamini kwamba kufanya kazi kwa bidii na uaminifu tu peke yake vitaleta utajiri, achana na wazo hilo ! Siyo kweli ! Utajiri unapokuja kwa kiasi kikubwa kamwe siyo matokeo ya kazi ngumu! Utajiri huja, kama utakuja, kutokana na matakwa yaliyokuwa thahiri, chini ya matumizi ya kanuni zilizokuwa wazi, na siyo kwa kubahatisha au bahati njema.

Kwa ujumla, wazo ni msukumo wa mawazo unaohimiza kitendo kwa kuvutia ubunifu. Wawakilishi wote wakubwa wa mauzo hufahamu kwamba mawazo yanaweza kuuzwa mahali ambapo bidhaa haiwezi. Wawakilishi wa mauzo wa kawaida hawaelewi hili – hii ndiyo sababu wao ni wa “kawaida”

Mchapishaji wa vitabu  alifanya ugunduzi wemye thamani kubwa kwa wachapishaji kwa ujumla. Alijifunza kwamba watu wengi hununua majina ya vitabu na wala siyo yaliyokuwemo kwenye vitabu. Kwa kubadilisha tu jina la kitabu kimoja kilichokuwa hakinunuliwi haraka, mauzo yake kwenye kile kitabu yalipanda juu zaidi ya nakala milioni moja. Ndani ya kitabu hakukubadilishwa kwa namna yeyote ile. Aliondoa tu jalada lililokuwa na jina ambalo halikuwa likiuza, na kuweka jalada jingine jipya lenye jina lililokuwa na thamani ya “mauzo ya filamu”

Hivyo, rahisi kama inavyoweza kuonekana, ilikuwa ni wazo! Ulikuwa ubunifu!  Hakuna bei moja maalumu ya mawazo. Waanzilishi wa mawazo huweka bei zao wenyewe, na ikiwa ni wajanja, hulipwa kiwango hicho.

Tasnia ya picha zinazotembea(filamu) ilitengeneza kundi zima la mamilionea . Wengi wao walikuwa wanaume ambao hawakuweza kubuni mawazo – lakini walikuwa na ubunifu wa kutambua mawazo walipoyaona.

Andrew Carnegie alifahamu kidogo sana juu ya namna ya kutengeneza chuma cha pua(steel) – nina maneno yake mwenyewe Carnegie kwa hili – lakini alitekeleza kwa vitendo matumizi ya kanuni mbili kati ya kanuni zilizoelezwa kwenye kitabu hiki na kuifanya biashara ya chuma cha pua kumpa utajiri.

Habari za karibu kila utajiri mkubwa huanzia siku ambayo muanzilishi wa mawazo na muuzaji wa mawazo wanapokutana na kufanya kazi kwa masikilizano. Carnegie yeye mwenyewe alizungukwa na wataalamu walioweza kufanya vitu vyote ambavyo hakuweza kuvifanya , watu walioanzisha mawazo na watu walioyaweka mawazo katika vitendo na kuwafanya wao wenyewe na wengine kuwa matajiri wakubwa.

Mamilioni ya watu huishi wakitumaini mazingira yanayofaa(bahati). Pengine mazingirayanayofaa yanaweza yakampa mtu fursa, lakini mpango salama zaidi siyo wa kutegemea bahati. Ilikuwa ni bahati  iliyonipa fursa kubwa zaidi ya maisha yangu – lakini miaka 25 ya juhudi thabiti ilihitajika kwenye fursa ile kabla haijageuka kuwa rasilimali.

Mazingira yalijumuisha bahati yangu nzuri ya kukutana na kupata ushirikiano wa Andrew Carnegie. Alipanda ndani ya akili yangu wazo la kuziunganisha kanuni za kutimiza malengo kuwa filosofia ya mafanikio. Maelfu ya watu wamenufaika na ugunduzi uliofanyika katika miaka 25 ya utafiti, na utajiri mkubwa umelimbikizwa kupitia matumizi ya filosofia hii. Mwanzo ulikuwa rahisi. Ilikuwa ni wazo ambalo mtu yeyote angeliweza kulibuni.

Mazingira mazuri yalikuja kupitia Carnegie lakini vipi kuhusiana na kukata shauri, uthahiri wa lengo, shauku ya kulifikia lengo na juhudi zisizokoma kwa miaka 25?  Haikuwa Shauku ya kawaida iliyoweza kuhimili hali ya kuvunja matumaini, kukatisha tamaa, anguko la muda, kukosolewa, na tuhuma zisizoisha, juu ya “kupoteza muda”. Ilikuwa ni Shauku kuu, isiyotulizika !


Mwanzoni wakati Bwana Carnegie alipopanda wazo katika akili yangu, lilibembelezwa, kutunzwa, na kushawishika kubakia hai. Taratibu, wazo liligeuka kuwa kubwa chini ya nguvu zake lenyewe, na lilinibembeleza, kunilea na kuniendesha. Mawazo yako hivyo. Kwanza unatoa uhai, kitendo na ulinzi kwa mawazo, na halafu yanapata nguvu yao yenyewe na kusukumiza kando upinzani wote


Mpenzi msomaji na huo ndio mwisho wa sehemu yetu hii ya 6, usikose sehemu ya 7, "MIPANGO MATHUBUTI"



0 Response to "KANUNI YA SIRI YA COCA COLA, BIRIKA LA AJABU NA WAZO LA DOLA MILIONI 1"

Post a Comment