KUPATA MAFANIKIO MAKUBWA KIFEDHA UNAHITAJI MIFEREJI MINGAPI YA KIPATO/PESA? | JIFUNZE UJASIRIAMALI

KUPATA MAFANIKIO MAKUBWA KIFEDHA UNAHITAJI MIFEREJI MINGAPI YA KIPATO/PESA?

mifereji ya kipato

Nimewahi kuandika mara nyingi sana juu ya Mifereji ya pesa au kipato mpaka nikaandika na kitabu nilichokiita, MIFEREJI 7 YA PESA NA SIRI MATAJIRI WASIYOPENDA KUITOA. Bila shaka yeyote ile mtu kuwa na mifereji ya kipato ndiyo njia inayotambulika duniani kote kuwa yenye tija zaidi ya kutengeneza utajiri haraka au kuwa milionea ba hatimaye bilionea (Uhuru kamili wa kifedha)

Kwani Mifereji ya pesa au Mifereji ya Kipato ni kitu gani? Ni njia za kujiingizia kipato cha ziada nje ya kile mtu unachokipata kutokana na shughuli yako ya msingi unayoifanya, kwa mfano ikiwa umeajiriwa basi ukianzisha mradi wako pembeni, huo ni mfereji wa kipato na ukiwa na biashara moja ukianzisha ya pili basi ile ya pili ni mfereji wa kipato. Kwa ujumla shuguli yako ya msingi nayo ni moja kati ya mifereji inayokutiririshia pesa.

Kulingana na tafiti mbalimbali zilizokwisha fanywa na wachumi au wakereketwa wa masuala ya pesa sehemu nyingi Duniani imegundulika kwamba Mamilionea wengi na watu matajiri sana kwa wastani wanamiliki idadi fulani ya mifereji ya kipato. Idadi (namba) hiyo kama vile ni ya kimuujiza vile unaweza kushangaa ni kwanini iwe hiyo na wala siyo nyingine.

Zipo sababu kadhaa ambazo nitazizungumzia hapa hapa kwenye hili somo na wala sitasubiri mpaka somo jingine ingawa kwa kweli kulistahili niwe na somo zima kuzijadili sababu hizo nyeti kikamilifu.

Nilipokuwa natafiti Mifereji hiyo ya kipato nikiwa kama mwanafikra yakinifu (Critical thinker) maswali machache nitakayoorodhesha hapo chini yalinijia katika fikra zangu;

               (1)     Ni idadi hiyo ya Mifereji ya kipato iliyo na uwezo wa kimaajabu wa kumfanya mtu aweze kuwa Milionea ama imetokea tu kwa Mamilionea wengi kujikuta utajiri wao ukianzia katika hiyo namba/idadi ya mifereji ya kipato?

               (2)     Hivi inawezekana idadi yote ya Mifereji hiyo ya kipato ikawa katika kundi moja (sekta moja) kwa mfano katika sekta ya ardhi na majengo, sekta ya usafirishaji nk. au inapaswa kuwa katika makundi/sekta tofauti?

               (3)     La tatu na la mwisho, Hivi kweli waajiriwa katika zile fani zinazolipa fedha nyingi sana (wanaopokea mishahara minono) kuna umuhimu wowote ule kwa wao kumiliki idadi hiyo ya mifereji ya kipato au ni bora tu wakaendelea na ajira zao hizo zinazowalipa mamilioni ya shilingi?

Kwa bahati mbaya sana katika utafiti wangu huo mtandaoni na nje ya mtandao sikufanikiwa kupata kwa urahisi majibu ya maswali hayo ingawa mwishoni kabisa nilikuja kufanikiwa kuyapata majibu yote kwa usahihi kabisa.

Hivyo basi hebu turudi kwenye swali letu la mwanzo kabisa na la msingi katika somo hili lisemalo; Ni mifereji mingapi ya Kipato kwa wastani mtu yeyote yule anapaswa kuimiliki kabla hajatoboa na kuwa tajiri?

...............................................................................................................................................................................................................................................................................................................

Mpenzi mfuatiliaji wa masomo haya ya fedha kila siku, Somo hili ni moja kati ya masomo tunayojifunza kwenye Mastermind group letu la MICHANGANUO-ONLINE na hapa tumeweka sehemu fupi tu ya somo lenyewe. Somo kamili ni leo usiku saa 3  tarehe 23/1/2023

Ili kupata somo zima lililokamilika pamoja na masomo mengine yaliyopita zaidi ya 80, jiunge na Darasa letu kwa kiingilio cha shilingi elfu 10 tu kwa mwaka mzima.

Ukiwahi kujiunga kabla ya OFFA yetu kumalizika (OFFA ISIYOWAHI KUTOKEA) utatumiwa papo hapo vitabu na michanganuo ifuatayo hapo chini mwishoni. Kifupi ni kwamba unapata E-book zangu zote kwa bei karibu na bure! Offa hii itadumu muda mfupi.

Namba za malipo ni; 0712202244 au 0765553030 jina Peter Augustino Tarimo. Baada ya malipo tuma ujumbe watsap au SMS usemao; “NATAKA OFFA ISIYOWAHI KUTOKEA”

...............................

VITU VYA OFFA ISIYOWAHI KUTOKEA NI HIVI VIFUATAVYO;-

KITABU: Michanganuo ya Biashara na Ujasiriamali

KITABU: Siri ya Mafanikio ya Biashara Duka la Rejareja

KITABU: Mifereji 7 ya Pesa na Siri Matajiri wasiyopenda kuitoa

KITABU: Siri za upishi wa chapati laini-UPENDO CAFE

KITABUNjia rahisi ya kuandika mpango wa biashara-dakika 30

MCHANGANUO: Kuku wa mayai

MCHANGANUO: Kuku wa nyama - kwa kiswahili

MCHANGANUO: Kuku wa nyama –kwa kiingereza

MCHANGANUO: Kuku wa kienyeji

MCHANGANUO: Ufyatuaji tofali za saruji

MCHANGANUO: Mgahawa wa chakula –kwa Kiswahili

MCHANGANUO: Mgahawa wa chakula –kwa kiingereza

MCHANGANUO: Kiwanda cha Dona (Usado milling)

SEMINA: Jinsi ya kuandika mchanganuo wa kiwanda cha unga

SEMINA: Kuandika mchanganuo wa kuku wa nyama

MCHANGANUO: Kuandika mchanganuo wa Cafe


SOMA PIA NA HIZI HAPA;

1. Njia za kuingiza kipato cha ziada nje ya kazi yako

2. Biashara 7 nzuri za kufanya zitakazokuingizia pesa hata kama umelala

3. Kwanini kila mwanamke anastahili kumiliki vyanzo vingi vya mapato?

4. Njia 7 halali na nzuri za kupata mafanikio & utajiri wa haraka

5. Ujanja matajiri wanaoutumia kupata pesa kutoka vyanzo vingi vya mapato




0 Response to "KUPATA MAFANIKIO MAKUBWA KIFEDHA UNAHITAJI MIFEREJI MINGAPI YA KIPATO/PESA?"

Post a Comment