JINSI NITAKAVYOONGEZA TIJA ZAIDI NA UFANISI 2022 (HOW AM I GOING TO BE MORE PRODUCTIVE); MAMBO 4 MUHIMU SANA | JIFUNZE UJASIRIAMALI

JINSI NITAKAVYOONGEZA TIJA ZAIDI NA UFANISI 2022 (HOW AM I GOING TO BE MORE PRODUCTIVE); MAMBO 4 MUHIMU SANA

Kimeandikwa na Napoleon Hill 1938 na Kutafsiriwa na Peter Tarimo 2021
Blog ya jifunzeujasiriamali  mwaka wetu mpya wa 2022 tayari umekwishaanza na kama ilivyokuwa ada huwa kila mwaka kipindi kama hiki hapa kwenye Blogu natoa Dira itakayoenda kutuongoza kwa mwaka mzima zikiwemo kaulimbiu na malengo ya mwaka.

Kaulimbiu yetu mpya ya mwaka huu ni; BADILISHA TABIA KUJENGA TIJA NA UFANISI ZAIDI. Kauli hii itakwenda sambamba na ile ya mwaka jana ya "MTEJA NI KILA KITU, WAJALI WATEJA WAKO” Kwani tija ni nini kwenye mafanikio kifedha? Tija maana yake ni faida. Na ufanisi ni nini? Ufanisi maana yake ni ubora katika utendaji(efficiency). Kwa ujumla tunakwenda kujifunza utamaduni wa jinsi ya kujenga tija na ufanisi katika biashara au kazi zetu.

SOMA: Ukitaka mafanikio ya haraka mwaka 2021achana na mambo mengi komaa na siri hizi mbili (2) tu

Kwangu binafsi na timu nzima ya Jifunzeujasiriamali mwaka 2021 unamalizika tukifurahia kutimiza moja kati ya malengo muhimu kabisa tuliyokuwa tumejiwekea. Kukamilisha rasmi kazi ya kukitafsiri kitabu cha Think & Grow Rich katika lugha ya Kiswahili. Ikiwa wewe ni mfuatiliaji wa makala zangu, kwa kipindi kirefu kidogo uliona sikuweza kuwa hewani kama ilivyopasa na sababu kubwa ilikuwa ni jukumu hilo la kumalizia kutafsiri Fikiri & Utajirike

Napoleon Hill aliweza kukamilisha kuandika kitabu hiki kwa miaka zaidi ya 20, mimi bila shaka kazi tu ya kutafsiri isingeliweza kuwa ngumu na ya muda mrefu kiasi hicho lakini pia nathubutu kusema kwamba haikuwa kazi nyepesi hata kidogo.

SOMA: 2021 amua hatma yako, tengeneza mwaka uliokuwa bora zaidi kushinda mingine yote 

Katika safari hiyo nimegundua kuna vitu vinne (4) ambavyo ikiwa kama nitakwenda kufanya mabadiliko kidogo basi nitaongeza mara dufu ufanisi na tija katika shughuli zangu nyingine za kujitafutia pesa. Nitakwenda kufanya mabadiliko makubwa katika mfumo wangu mzima wa utendaji kazi na mambo haya yote nitakwenda kuyashirikisha moja kwa moja kwa vitendo kwenye kundi langu, MASTERMIND GROUP la Michanganuo-online kila siku tutakapokuwa tukijifunza elimu ya kifedha.

SOMA: Elimu ya fedha na umuhimu wake, njoo tuunganishe nguvu tuhamishe milima!

Kupitia mchakato mzima wa kukitafsiri kitabu cha Think and Grow Rich nilikutana na changamoto nyingi sana na nikajifunza pia mambo mengi kuhusiana na namna ya kujenga tija na ufanisi katika kukamilisha malengo. Mengi nitayashirikisha kwenye makala zangu zijazo katika blogu ya jifunzeujasiriamali lakini pia katika MASTERMIND GROUP kila siku usiku tunapojadili michanganuo ya biashara za mtaji mdogo zenye faida ya haraka.

Lengo kuu la mkakati huu ni kubadilisha kabisa tabia za zamani na kujenga tabia mpya/mazoea ya kiufanisi na tija kwenye kazi zangu. Kwa mfano kazi nilizokuwa nachukua mpaka masaa 5 kuzikamilisha sasa hivi inakwenda kunichukua masaa 2 tu. Mkakati huu pia utanisaidia kujenga mazoea ya kufanya vitu kila siku pasipo kuahirisha-ahirisha ovyo pamoja na kujenga mifumo ya biashara zenye uwezo wa kuingiza pesa hata wakati nimelala usiku na familia yangu.

SOMA: Biashara 7 nzuri za kufanya zitakazokuingizia pesa hata kama umelala

Siyo kwamba naenda kujaribu mfumo huu hapana, mbinu hizi tayari nimekwisha zifanyia majaribio, nimethibitisha zinafanya kazi na zinanipa matokeo chanya.

Na haya ndio mambo yenyewe manne (4) muhimu sana katika safari hiyo ya kutengeneza tija na ufanisi mkubwa zaidi kifedha

1. Kupunguza vidakizi (Distractions)

Wakati nikitimiza majukumu yale ya msingi nitaondoa au kuzima kabisa baadhi ya mitandao ya kijamii nisiyokuwa na umuhimu nayo. Hakuna sababu ya kufungua facebook, tweeter, watsap, tick tock, redio, TV, au mtandao mwingine wowote ule wa kijamii wakati nikitimiza kazi zangu muhimu, vitu hivi nitavitengea muda maalumu au kutoshughulika navyo kabisa labda tu kuwe na ulazima sana. Sitazima kabisa simu kwani nategemea kupokea email na simu muhimu za biashara. Aidha sitatumia muda mwingi kwenye simu, sms watsap meseji au email zenye viashiria vya kunipotezea muda(Spams) bali zile tu zenye mlengo wa matatizo ya kweli ya wateja au zilizo na fursa kifedha.

2. Kukamilisha kazi zangu haraka na mapema zaidi iwezekanavyo.

Nitaacha kabisa mazoea ya kufanya kazi pale inaponilazimu na kufanya kazi kuwa ni jambo la lazima kukamilika kwa muda ule niliojipangia kila siku na nitafanya hivyo mpaka iwe mazoea kwangu. Hii itanisaidia sana kukamilisha zile kazi muhimu katika masaa ambayo mwili unakuwa na nguvu na tija ya kiwango cha juu. Jioni baada ya masaa hayo ndipo nitafanya zile kazi zisizokuwa na umuhimu mkubwa au kupumzika kwa burudani. Nitajitahidi kuamka kila siku saa 11 alfajiri na kumalizia kazi zangu muhimu saa 8 alasiri kabla sijajiingiza kwenye kazi au majukumu ya ziada.

3. Kujifunza vitu vipya kila siku.

Hili ni jambo ambalo sitakoma kulifanya kila siku maisha yangu yote. Kwenye ratiba yangu kila siku ni lazima nihakikishe najifunza kitu kipya kuhusiana na kazi ninazozifanya pamoja na kufanya marudio kwa baadhi ya mambo niliyowahi kujifunza siku za nyuma vikiwemo vitabu maarufu nivipendavyo vikiwemo vya elimu ya kifedha

4. Kufanya mazoezi na kula kwa usahihi.

Kila asubuhi nitakapoamka hata kama sitakimbia mchakamchaka au kuruka kamba, nitajinyoosha viungo vya mwili wangu angalao kwa dakika 15 hivi. Halikadhalika na jioni pia nitatenga muda kama huo tena kwa mazoezi mepesimepesi. Nitajitahidi kula mlo kamili kila siku, kunywa maji salama ya kutosha na kulala usiku angalao masaa 5 -6 kwa afya nzuri ya akili yangu. Kabla ya kulala nitafanya tafakuri na mwisho kusali na kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa zawadi ya uhai.

……………mwisho……………

Ikiwa mpenzi msomaji wangu utapenda na wewe kushiriki nami katika mfumo huu mpya wa maisha nakukaribisha sana! Njoo kwenye MASTERMIND GROUP LETU mahali pekee mimi na wanamastermind wenzangu tutakapoonyesha kwa vitendo kila siku namna mfumo huu wa ufanisi na tija unavyofanya kazi.

Hapa nimeandika kwa kifupi sana lakini kuna mambo mengi ndani ya Group tutayafanya katika kujenga tija na ufanisi mkubwa kwenye biashara zetu na maisha kiujumla. Kuthibitisha kweli tunakwenda kujenga tabia mpya za kimafanikio nitakuwa kila siku kwenye blog ya jifunzeujasiriamali nikitoa taarifa kwa ufupi ya kile kinachoendelea ndani ya Mastermind group hilo.

Ikiwa nimefanikiwa kukitafsiri kitabu cha Fikiri na Utajirike chote, nina uhakika hakuna kitu kinachoshindikana chini ya jua ikiwa mtu utaamua na ‘kufocus’ kwenye jambo moja mpaka likamilike mfano malengo ya biashara ya kuingiza pesa kiasi fulani kwa muda utakaoamua wewe mwenyewe.

 

Makala hii imeandaliwa na;

PETER AUGUSTINO TARIMO

Mwalimu na Mhamasishaji wa Mafanikio

Simu/Watsap: 0765553030 au  0712202244

0 Response to "JINSI NITAKAVYOONGEZA TIJA ZAIDI NA UFANISI 2022 (HOW AM I GOING TO BE MORE PRODUCTIVE); MAMBO 4 MUHIMU SANA"

Post a Comment