Uchambuzi Kwa kina Sura ya 11 ya kitabu cha FIKIRI & UTAJIRIKE (THINK & GROW RICH-SWAHILI EDITION) – Sehemu ya i
Sura hii kwa ujumla
wake inazungumzia matumizi mazuri ya mhemko wa ngono – jinsi binadamu
anavyoweza kuzitumia hisia za ngono au mapenzi ya kujamiiana ambazo ndiyo kichocheo cha akili kati ya vichocheo
vingine 10 kilichokuwa na nguvu zaidi na kilicho na uwezo wa kufanya maajabu
makubwa katika maisha ya binadamu kimafanikio. (kuna aina kuu nne(4) za mapenzi kwa mujibu wa kitabu hiki)
Fikra za ngono
zinaweza kumjenga au kumbomoa mtu kulingana na yeye mwenyewe atakavyoamua
kuzitumia.
Kwenye sura hii
tutakwenda kufahamu yafuatayo;
· Ni
kwanini watu wengi mafanikio yao makubwa huja pale wanapofikisha umri kuanzia
miaka 40 – 60?
· Sababu
kubwa ni kwanini kila mwanaume mwenye mafanikio makubwa au utajiri nyuma yake
kuna mkono wa mwanamke?
· Kwanini
wasanii wengi na wanamichezo waliofanikiwa hujiingiza kwenye ulevi wa dawa za
kulevya, pombe na bangi?
· Kwanini
wanamauzo wengi ni watu wenye ushawishi
mkubwa(kingono) kimapenzi?
· Tofauti
kubwa kati ya MAPENZI, UPENDO, NGONO, MAHABA na KUJAMIIANA
· Kwanini
wahalifu sugu wanaweza kurekebishwa kupitia ushawishi wa wapenzi wao?
· Kwanini
UPENDO ndiyo uzoefu mkubwa zaidi maishani?
· Aina
kuu 4 za Mapenzi(UPENDO) ni upi unaochoma zaidi moyoni?
· Kwanini
watu husema, “Mke anaweza kumjenga au kumbomoa mume”?
· Chanzo
kikuu cha Wanandoa kugombana.
· Kwanini
inasemekana wanaume wote wenye mafanikio
na utajiri mkubwa chanzo ni ushawishi wa wapenzi wao(wake)?
· Kwanini
Wanyama wanatuzidi binadamu kwa ustaarabu kwenye tabia za mapenzi mfano jogoo
hawezi kumbaka kifaranga lakini baba mzima anaweza kumbaka hata mwanaye wa
kumzaa?
Neno kubadili au kugeuza kwa lugha nyepesi ni uhamishaji wa kitu kimoja au aina ya
nguvu kwenda katika kitu cha aina nyingine. Vivyo hivyo na hisia za mapenzi au
ngono ndivyo zinavyoweza zikabadilishwa kutoka katika hali yake ile ya kawaida
tuliyoizoea mfano hali ya kujamiiana baina ya mwanaume na mwanamke kuwa katika
hisia nyingine tofauti kabisa kwa kutumia mbinu rahisi tu tutakazokwenda
kujifunza katika sura yetu hii ya 11 ya kitabu maarufu cha Fikiri na Utajirike(Think
& Grow Rich-swahili edition).
Mapenzi (Ngono),
ijapokuwa kitabu hiki kimeelezea faida na uzuri wake kama nitakavyoorodhesha
hapo chini hivi punde, lakini hisia hizi zimekuwa pia ni chanzo kikubwa cha
matatizo na uchungu mwingi kwa binadamu kutokana na sababu moja tu ya sisi binadamu
kutokuwa na uelewa wa kutosha au elimu sahihi kuhusiana na mhemko huu wa
kipekee kabisa.
Mhemko huu umekuawa
ni chanzo cha Wanafunzi wengi wa shule na vyuo kufeli mitihani yao au kukatisha
masomo, chanzo cha wanaume wengi na wanawake kujiua kwa kujinyonga, chanzo cha
watoto wengi wa mitaani na chanzo cha karibu kila aina ya madhila na majanga
yanayozikumba ndoa na familia nyingi Duniani kama Napoleon Hill mwenyewe
anavyouelezea utafiti wake wa miaka takriban 25 ndani ya sura ya 11 ya kitabu
hiki cha Kanuni 13 za mafanikio kuwahi kuandikwa popote pale pengine Duniani.
Mwanzoni kabisa mwa
sura yenyewe Napoleon Hill anasema kwamba, kwasababu ya ujinga juu ya mada hii,
mhemko wa ngono mara nyingi huhusishwa na hali ya kimwili / kimaumbile kutokana
na sababu zisizokuwa sahihi ambazo watu wengi wamekuwa wakikutana nazo wakati
wa kujifunza elimu ya ngono, vitu vya kimwili vimekuwa ndiyo viunavyotawala na
hii ndiyo sababu kubwa inayofanya elimu ya ngono kuwa na usirisiri fulani hivi.
Faida
kuu 3 za Mhemko wa Ngono
1. Muendelezo
wa binadamu kupitia njia ya kuzaana
2. Kudumisha
Afya
3. Kumbadilisha
mtu kutoka hali duni kabisa kwenda katika hali bora kabisa kiubunifu kupitia
mageuzi (Hii ndiyo watu wengi hawaijui na
ndiyo tutakayokwenda kujifunza zaidi katika Sura yetu hii ya 11
Hamu ya ngono ndiyo
hamu ya binadamu iliyo na nguvu kushinda hamu nyingine zote. Watu wanaposukumwa
na hamu hii hutengeneza umakini mkubwa katika kufikiri, ujasiri, utashi,
msimamo na uwezo wa kiubunifu ambao hawakuwahi kuwa nao wakati mwingine.
Mguso wa kimapenzi
una nguvu na msukumo kiasi kwamba watu bila kuzuiwa na chochote kile huhatarisha
maisha yao na hadhi zao wakiuendekeza.
(Hii imenikumbusha stori yangu mimi mwenyewe binafsi wakati nilipokuwa
nasoma sekondari katika miaka yangu ya 15 - 20 Siku nilipohatarisha maisha
yangu usiku mkubwa kisa tu ikiwa ni kumuonyesha ujasiri na umwamba msichana rafiki
yangu niliyekuwa nampenda. Nilikwenda kwao siku ya sikukuu, tukiwa na vijana wengine
tulipiga stori huku tukinywa mbege, mpaka kila mtu anaondoka mimi niliamua niwe
wa mwisho bila kujali hatari yeyote ambayo ingeliweza kwenda kunikuta usiku ule
njiani tena kwa kutembea umbali mrefu kijijini, yote hii ilikuwa shauri ya
hisia za mapenzi juu ya msichana yule ambapo katika hali tu ya kawaida
nisingelithubutu kufanya vile)
Mpenzi
Msomaji wangu, tukutane tena Sehemu ya Pili ya uchambuzi wa Sura hii ya 11 ya
kitabu cha FIKIRI & UTAJIRIKE.
Asante
sana!
Peter
A. Tarimo.
Njia
2 za Kukipata Kitabu kizima cha FIKIRI & UTAJIRIKE (Think & Grow
Rich-swahili
1. Nakalatete(softcopy) kwenye Smartphone yako, Ingia kwenye mtandao huu wa GETVALUE na utaweza kukipakua ndani ya muda mfupi.
2. Nakala
ngumu (Hardcopy), wasiliana na sisi kwa namba 0765553030 au 0712202244
tukuletee popote pale ulipo nchini.
SOMA NA HIZI HAPA;
1. Think and Groe Rich kwa ufupi: Mapitio ya vitabu vya mafanikio(Books Review)
3. Downlad/ pakua hapa kitabu Fikiri Utajirike (Think and Grow Rich) kwa kiswahili, surazote 15 bure
3. Offa ya Kitabu cha Think & Grow Rich Toleo la Kiswahili 2021
0 Response to "MAAJABU YA KUBADILI FIKRA ZA MAPENZI (NGONO) KUWA MAFANIKIO –SURA YA 11 (i)"
Post a Comment