SAIKOLOJIA YA UMASIKINI: SABABU 9 KWANINI HUPATI PESA NYINGI HATA UKIJITAHIDI VIPI? | JIFUNZE UJASIRIAMALI

SAIKOLOJIA YA UMASIKINI: SABABU 9 KWANINI HUPATI PESA NYINGI HATA UKIJITAHIDI VIPI?

Msichana akicheza kamari

Kuna vitabu vingi, makala na maandiko mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii yanayohusiana na mada ya pesa au hali za watu kifedha. Katika somo letu hili la leo tutakwenda kuona ni aina gani za fikra na tabia zinazompeleka mtu kwenye umasikini na wala siyo kumpeleka kwenye kumiliki utajiri ambako ndio kila mtu hapa duniani anatamani kuelekea.

Siku hizi kwa kila mtu siyo siri tena kwamba fedha ni sawa na kama ilivyo nishati ya umeme iendeshayo karibu kila kitu. Nguvu ya umeme inapokatika nadhani sote tunafahamu ni taharuki kiasi gani watu huwa tunaipata, hali kadhalika na pesa nayo ndiyo hivyo hivyo ilivyo. Watu wanapoikosa au kuwa nayo kidogo sana huibua taharuki sawa na ilivyokuwa kukatika kwa nguvu ya umeme.

Ikiwa mtu hana pesa kuna uwezekano mkubwa kwamba ni mawazo na vitendo vyake vinavyochangia yeye kukimbiwa na nguvu hii muhimu, PESA. Hebu sasa pasipo kupoteza muda wako mwingi, tukaone ni kwa jinsi gani vitendo na fikra za mtu(saikolojia) inavyoweza kumnyima hela hata akadhania labda ameshalogwa tayari.

1. Pesa siyo furaha, haiwezi kununua kila kitu bwana!

Wakati upande mmoja wa nafsi yako akilini ukiwa umejijengea mtazamo kwamba pesa haiwezi ikanunua furaha, upande mwingine wa pili wa nafsi unatamani ule vizuri na familia yako, ununue simu nzuri ya gharama, ujenge nyumba, ununue kiwanja, uende matembezini na wale uwapendao kustarehe nk. Hivyo unapokuwa na pande mbili zinazokinzana juu ya jambo moja, ni dhahiri kabisa jambo hilo umeshaliwekea vizingiti na kamwe hautaweza kufaulu au kusonga mbele, na hivi ndivyo tunavyokosa pesa pasipo wenyewe kujua.

2. Sihitaji Pesa!

Ni kauli nyingine ya kimasikini iliyo rahisi kutamka mdomoni lakini inayoweza kugeuka na kuwa chanzo kizuri cha mtu kutokupata pesa inavyotakiwa. Kuridhika na kile kidogo unachokipata huku akilini ukiwaza tu juu ya kupunguziwa bei na kuweka akiba ya kile kidogo unachokipata wakati mwingine siyo sahihi na ni hatari pia kwani kunaweza kupunguza au kukatisha kabisa mzunguko wako wa fedha taslimu.

Fikra hii inamfanya mtu aishie tu kulenga katika kumiliki fedha kidogo(uhaba/ukata) badala ya kulenga katika kumiliki fedha nyingi(Ukwasi/Utajiri) hali ambayo hatimaye humlazimisha kutawanya rasilimali chache alizokuwa nazo badala ya kulenga katika kuzikuza na kuzizalisha zaidi.

3. Kushindwa kutumia Pesa

Pesa kama zilivyo nguvu za aina nyingine huwa haina tabia ya kustahimili udumavu, pesa haipendi kukaa tu bure bila ya kufanya kazi yeyote, na hii ndiyo sababu utawasikia watu wengi wakisema wanapata pesa zaidi na kwa urahisi pale wanapoamua kutumia pesa lakini wanapozibanabana zinapotea hawazioni (*Angalizo: lakini siyo matumizi holela, hapa namaanisha matumizi yale ya busara tu na yenye kuleta faida siyo utapanyaji)

Tafiti zimebainisha pia kwamba majanga mbalimbali kama vile magonjwa, wezi na majanga mengine ya asili huwa na kawaida ya kuwanyemelea zaidi watu walio na tabia ya kubana sana pesa zao wakihofia zitaisha au kupotea ilihali walizipata kwa jasho.

Cha ajabu sasa inakuwa ni kinyume chake kwani pesa hizohizo wanazochelea kuzitumia hatimaye zinakuja kutoka kirahisi kupitia kukabiliana na majanga hayo au nguvu za asili ambazo wanakuwa hawana uwezo mwingine wa kuzizuia zaidi ya kutumia kile walichokuwa nacho.

Sasa unaweza kujiuliza ni kwanini tu wasingeamua mapema kufanya matumizi ya pesa zao kupitia njia nzuri ya kuzizalisha kama vile uwekezaji katika miradi na biashara mbalimbali kuliko kuziweka kabatini wakisubiria majanga?

4. Peponi (Mbinguni) Hakuna Pesa !

Mawazo ya masikini wengi ni kwamba, hata ukitafuta pesa vipi lakini mwisho wa siku utaziacha hapahapa Duniani, hutaenda nazo peponi. Dhana hii inakufanya usione umuhimu wa ‘kufight’ kufa na kupona na mwishowe ni umasikini hadi unaingia kaburini kweli kama mawazo yako hayo yanavyokudanganya. Midhali unaishi na kupumua, tafuta pesa uishi maisha mazuri hapa Duniani, achana na dhana hizo za kiboya zisizofaa

5. Haujipi thamani wewe mwenyewe kama mtu, mtaalamu au raia unayestahili malipo makubwa

Hili mara nyingi limekuwa chanzo cha watu wengi kuishia kupata vipato vidogo. Mpaka pale wewe mwenyewe utakapoamini kwamba ni wa gharama(aghali) ndipo na nguvu ya pesa nayo itakapokuamini. Ili watu nao waweze kukupa pesa zao kwa ajili ya huduma ama bidhaa unazowauzia, ni muhimu kujifunza jinsi ya kutenganisha mahusiano ya fedha na watu kutoka yale mahusiano binafsi ya kawaida.  

6. Kutokuiheshimu fedha !

Ikiwa utatamka kwa kinywa chako kwamba “pesa ni makaratasi tu”, “Pesa haina mwenyewe” sijui “ pesa ni takataka”nk. fedha nayo utashangaa inakukwepa kama ukoma. Pesa haitaki hata kubebwa kwenye fuko kuu kuu lililochakaa. Kuwachukia na kuwadharau wenye pesa huku ukiwaita majina mbalimbali kama vile, freemasons, wachuma pesa za majoka, chuma ulete, misukule nk.

Yote hayo yanathihirisha jinsi mtazamo wako kwenye fedha ulivyokuwa potofu na namna amabvyo huamini kabisa katika kufanya kazi na kutajirika kihalali. Kwa vyovyote vile ni lazima utaishia kufa masikini kwani hakuna namna utakayoweza kujituma upate pesa zaidi ya kudhani wenye pesa wote ni madhalimu waliopora, kuua na kuiba.

Kuna kisa kimoja nilichoshuhudia kipindi uchumi ulivyokuwa bora sana watu wakipata pesa nyingi, jamaa mmoja aliamua kufanya kufuru na kuona pesa haina maana kwa kuajiri vibarua wamuoshee gari yake kwa kinywaji aina ya bia, alinunua kreti za bia nyingi vijana wakazimimina kwenye pipa na kuanza kuosha pajero lake huku wengine waliokuwa waroho wakijinyea kinywaji hicho chini kwa chini kutoka pipani. Yule jamaa ninavyoandika hapa hana hata mia na anatamani hata kikombe cha mbege hakipati ....................................... ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………...............................................


Mpenzi msomaji, Saikolojia ya Umasikini ina mambo mengi watu wala hatuyadhanii hata kidogo kama ndiyo chanzo cha sisi kuwa masikini.

Somo hili halijamalizika na litaendelea leo hii tarehe 31/5/2023 usiku saa 3 ndani ya Mastermind group la Fedha & Michanganuo-online

ü Mtu yeyote yule anakaribishwa kujiunga kwa kutoa ada ya mwaka mzima sh. 10,000/= kupitia namba zetu 0712202244  au  0765553030 jina Peter Augustino Tarimo.

ü Baada ya malipo tuma ujumbe wa, “NATAKA OFFA YA VITU 12 NA KUUNGANISHWA GROUP LA MASOMO”. 

ü Masomo ya fedha ni kila siku, na unapojiunga unatumiwa masomo mengine yote yaliyopita tangu darasa lianze pamoja na OFFA yetu ya vitu 12 yenye Vitabu na Michanganuo ya biashara 

ü Tunakuwa pia na semina za mara kwa mara juu ya Michanganuo ya biashara zinazolipa Tanzania

 

Kupata Vitabu zaidi na Michanganuo ya biashara kwa bei nzuri, tembelea Duka letu la vitabu & Michanganuo hapa>> SMARTBOOKSTZ

 

Tunatoa pia huduma ya kuandika Michanganuo ya biashara / Business Plans kwa biashara yeyote ile iwe kubwa au ndogo kwa lugha ya kiingereza au Kiswahili- mteja unachagua.

Michanganuo yetu ni ya kipekee kulingana na mahitaji ya mteja na huwa tunatumia taarifa utakazotupatia wewe, tunafanya pia utafiti pale taarifa zako zinakuwa hazitoshelezi mahitaji ya mchanganuo husika. Ukihitaji Tuwasiliane zaidi kwa namba 0765553030 au 0712202244

Unaweza kucheki kwa kifupi  summary za baadhi ya kazi tulizowahi kuwafanyia wateja wetu hapa>>BAADHI YA KAZI ZETU


Somo hii limeandaliwa na:

Peter Augustino Tarimo

Mtaalamu wa Michanganuo ya biashara aina zote

Phone/Watsap: 0765553030 au 0712202244



SOMA NA HIZI HAPA;

1. Usilaumu kukosa pesa, bali laumu njia iliyokufikisha pale ulipo(Parti & ii)

2. Njia 6 za kuondoa woga na stress za fedha katika maisha yako

0 Response to "SAIKOLOJIA YA UMASIKINI: SABABU 9 KWANINI HUPATI PESA NYINGI HATA UKIJITAHIDI VIPI?"

Post a Comment