USILAUMU KUKOSA PESA, BALI LAUMU NJIA ILIYOKUFIKISHA PALE ULIPO(Part I & ii) | JIFUNZE UJASIRIAMALI

USILAUMU KUKOSA PESA, BALI LAUMU NJIA ILIYOKUFIKISHA PALE ULIPO(Part I & ii)


Mwanamke akijilaumu kukosa pesa
Katika makala hizi za kubadilisha mitazamo yetu kuhusiana na pesa, leo tutakwenda kuzungumzia namna ambavyo mtu anapaswa kuwa muangalifu na matumizi na usimamizi wa fedha zake kusudi asijekujilaumu hapo baadae kwa kukosa fedha, kufilisika, baada ya kustaafu kazi, au hata baada ya kuachana na shughuli alizokuwa akizifanya awali ambazo zilizokuwa zikimtiririshia pesa na kumfanya kupata pesa kwa urahisi.

Tukichukua mfano wa mtu anayemiliki biashara, anapofanya maamuzi mabovu, hujikuta hatimaye mambo yakimuendea mrama na kupoteza pesa au hata kuifunga kabisa biashara yake badla ya kupata pesa haraka, maamuzi kama vile matumizi kuzidi mapato, kutokuwa muangalifu katika kuwasimamia wasaidizi/wafanyakazi na kuwaacha kujifanyia mambo wanavyotaka wao nk.


Katika mchakato wa kutafuta pesa, njiani pia unatakiwa kupata taarifa sahihi zitakazokuwezesha kufanya maamuzi yako vizuri. Hata kujiunga na magroup kama hili la MICHANGANUO-ONLINE na maeneo mengine pia kama haya hujafanya uamuzi mbaya, upo sahihi kwani ni njia mojawapo sahihi za kujipatia taarifa mbalimbali ambazo pengine zitaweza kukusaidia katika kufanya maamuzi yako kwa usahihi zaidi. Ni lazima kama mjasiriamali upende sana kusoma au kupata taarifa mbalimbali iwe ni katika mitandao au nje ya mitandao ya kijamii kusudi uweze kupata mitazamo tofauti kutoka kwa watu mbalimbali.

SOMA: Pesa tuonazo ni makaratasi tu, jifunze njia ya kupata pesa za ukweli(Halisi)

Kuna usemi usemao kwamba, “FEDHA SIYO KILA KITU” ni kweli hata mimi naaamini hivyo pia, lakini ni lazima hapa tuwe wakweli kwamba kukosa pesa au hata kutokuwa na fedha za kutosha  ndiyo chanzo cha matatizo mengi ya kila siku hapa duniani. Hebu fikiria tu wewe leo hii umeugua ugonjwa ambao ili uweze kupona ni sharti upelekwe nje ya nchi kutibiwa kwa gharama ya fedha nyingi. Hebu nieleze kweli wewe hujafa tu, ikiwa huna uwezo na hata ndugu zako hali zao ni ngumu hawana namna ya kupata pesa au uwezo wa kuchangishana ili kupata pesa ni mdogo?....


.............................................................................

Mpenzi msomaji wa blogu hii, sehemu hii ya kwanza ya makala hii nitakwenda kufundisha katika Group la WHATSAPP la MICHANGANUO-ONLINE leo hii tarehe 2/5/2020. Sehemu ya pili ya somo hili tutakwenda kujifunza siku ya kesho tarehe 4/mei 2020. 

Masomo katika group hili ni kila siku usiku saa 3 hadi saa 4 kwa kiingilio cha shilingi elfu 10 tu ada ambayo ikishalipwa hulipi tena mpaka mwaka unaisha.

Ukitaka kujiunga na GROUP hili, tuma ujumbe whatsapp 0765553030 au simu 0712202244 wa niunganishe na group la MICHANGANUO na unaweza kulipa kabisa kupitia moja ya namba hizo au baada ya kuwasiliana na sisi. Ikiwa hutumii Whatsap pia hakuna shaka unaweza kujiunga na tukakutumia masomo na vitabu kupitia email yako.

Mbali na kupata masomo mapya kila siku lakini pia unapojiunga tu tunakutumia papo hapo masomo na semina zote tulizokwishawahi kujifunz siku zilizopita. Tunakutumia vitabu maarufu 2 vya jinsi ya kuandika mpango wa biashara yeyote ile kwa kiswahili na kwa kiingereza pamoja na vitu mbalimbali vifuatavyo;

1.  Kitabu cha MICHANGANUO YA BIASHARA NA UJASIRIAMALI -kwa kiswahili

2.  Kitabu mashuhuri zaidi duniani, HOW TO WRITTE A BUSINESS PLAN kwa lugha ya kiingereza, ndio kinachotumika vyuo vikuu vingi duniani.-kwa kiingereza

3.  Semina ya siku 7 na mpango kamili wa biashara ya usagishaji unga wa dona(USADO Milling) )-kwa kiswahili

4.  Kifurushi maarufu cha michanganuo 3 ya ufugaji wa kuku(MKOMBOZI CHICKS PLAN 3PACKS)-kwa kiswahili

5.  Mchanganuo kamili wa kilimo cha Matikiti maji(KIBADA WATERMELON BUSINESS PLAN) -kwa kiswahili

6.  Mchanganuo wa biashara ya mgahawa(JANE RESTAURANT) -kwa Kiswahili & kiingereza

7.  Semina nzima na Mchanganuo wa biashara ya Usagishaji Unga wa Dona (JUSADO MILLING) -kwa Kiswahili 





0 Response to "USILAUMU KUKOSA PESA, BALI LAUMU NJIA ILIYOKUFIKISHA PALE ULIPO(Part I & ii) "

Post a Comment