KWANINI KUNDI LA KUSHAURIANA(MASTER MIND GROUP) NI MUHIMU KWA KILA ANAYETAFUTA MAFANIKIO? | JIFUNZE UJASIRIAMALI

KWANINI KUNDI LA KUSHAURIANA(MASTER MIND GROUP) NI MUHIMU KWA KILA ANAYETAFUTA MAFANIKIO?


USHIRIKIANO WENYE FAIDA
Mada niliyokuletea leo hii itaegemea katika maudhui yaliyopo kwenye kitabu cha THINK & GROW RICH (FIKIRI UTAJIRIKE) Kitabu hiki tunatoa tafsiri yake kila siku katika Group la Whatsapp na email la MICHANGANUO ONLINE na baadhi ya sura za kitabu hicho pia zipo kwenye blogu hii ya jifunzeujasiriamali.

Katika sura ya 10 ambayo tumeanza kupost sehemu ya kwanza jana katika group, Napoleon Hill mwandishi wa kitabu hicho maarufu duniani anazungumzia kitu kiitwacho, “MASTER MIND” au “MASTER MIND GROUP”. Maneno haya yanamaanisha ushirika wa watu 2 au zaidi waliounganisha nguvu, kwa maneno mengine unaweza ukaita ni “KUNDI LA KUSHAURIANA” au “KUNDI LA MASHAURIANO”


Kama kuna silaha kubwa na yenye nguvu zaidi iliyowahi kutumiwa na watu wengi waliofanikiwa duniani, wawe ni matajiri, wenye viwanda, wasanii mashuhuri, wanasiasa na wasomi, basi ni silaha hii ya ya Kundi la mashauriano(Master Mind Group)

Katika kundi la kushauriana, mtu anaweza kupata nguvu kubwa itokanayo na wenzake katika kundi na pia nguvu kutoka juu kwa NGUVU iliyo kuu zaidi ya zote au MUNGU, vyovyote vile utakavyoiita nguvu hii, katika kitabu hiki imetajwa kuwa ni NGUVU KUU(INFINITE INTELLIGENCE) ambayo kimsingi kama wewe unaamini, ni Mungu muumba wa nguvu nyingine zote Ulimwenguni.

UTAUNDAJE KUNDI LAKO LA KUSHAURIANA MASTER MIND GROUP?

1.  Chagua watu ambao tayari wana maono yanayofanana na ya kwako bila kujali kama wamekupita sana kiuwezo lakini hakikisha angalao mpo katika levo moja kiuwezo(mnafanana) au wanakuzidi iwe ni kiuchumi, kielimu nk.

2.  Ukweli ni kwamba watu hupenda kuwa katika ushirikiano lakini wanashindwa kupata watu sahihi wanaoendana nao kimaono. Lakini siku hizi Intaneti ikiwa imerahisisha sana mambo tofauti na enzi za nyuma kuunda group la kushauriana imekuwa jambo jepesi sana.

3.  Unaweza ukatumia mitandao ya kijamii kuunda kundi lako la mashauriano mfano facebook, whatsapp na mengineyo.

4.  Idadi ya watu katika kundi la kushauriana huanzia watu wawili na kuendelea.

5.  Makundi haya siyo sawa na vyama ambapo kunakuwa na uongozi na wanachama wengine kuwajibika kwa viongozi hapana, ndani ya kundi mnaishi kwa masikilizano(harmony), kusaidiana, kuiunuana kimawazo na kiushauri na hata wakati mwingine kwa hali na mali.

Sura hii ya 10 ina umuhimu mkubwa kwa yeyote anayesoma au aliywahi kusoma kitabu hiki. Ushirikiano unaotajwa hapa ni moja ya kigezo kikubwa mno katika kufanikiwa mtu yeyote yule. Hakuna mtu leo duniani anayeweza akasimama na kudai aliweza kufanikiwa katika nyanja yeyote ile mwenyewe pasipo kuwepo na msaada wa kundi lake la mashauriano(master mind group). Upana wa somo hili sina namna ninayoweza kukueleza hapa ukaupata wote zaidi ya wewe mwenyewe kuisoma sura hiyo kwa kituo.


Napoleo Hill anawataja baadhi ya watu mashuhuri na waliokuwa matajiri wakubwa wa Dunia nyakati hizo kama kina Henry Ford, Thomas Edison na Andrew Carnegie kuwa walikuwa na makundi yao ya kushauriana. Mfano Bwana Ford akiwa na elimu yake ya miezi 3 tu shuleni, aliweza kulitumia vyema kundi lake la kushauriana na  kujikuta ndani ya miaka 10 akiwa ni zaidi ya Profesa wa chuo kikuu kwa maarifa mengi aliyochota kutoka kwa wanachama wa kundi lake. Alikuwa mjanja kuchagua watu sahihi.

Mimi binafsi nimelifanya kundi la whatsapp la MICHANGANUO ONLINE kuwa kundi la kushauriana(Master mind group). Namna tunavyoendesha mambo yetu kwenye kundi hili ni sawa sawa kma nilivyoeleza hapo juu. Wote tuna maono yanayofanana ya kutaka kufanikiwa zaidi kimaisha.


Ngugu msomaji ikiwa bado hujajiunga katika kundi hili, nakukaribisha sana njoo ujiunge, kuna faida nyingi utakazozipata mbali na masomo na vitabu. Sasa hivi tupo zaidi ya watu 50, wote ni watu makini na kila mmoja wetu yupo kwenye tasnia yake lakini kile kinachotuunganisha pamoja ni ujasiriamali.

Haijalishi ikiwa upo katika tasnia ya habari, ufugaji, kilimo, uhandisi, sheria au nyingine yeyote, lakini spirit yetu kubwawote ni kufanikiwa, kuwa na maisha bora zaidi kiuchumi, kiafya, kiroho na kiakili pia. Binadamu lazima vitu vyote hivi vibalansi ndipo mtu useme umefanikiwa. Haitosi tu kuwa na hela nyingi wakati ukitetereka kiafya au kimahusiano na wale uwapendao.

Jana katika group letu tulikuwa na somo la fedha lililosema ‘KANUNI YA KUPATA FEDHA INAJULIKANA, UGUMU UPO WAPI?’ pia tulianza sehemu ya kwanza ya Sura ya 10 ya tafsiri ya kitabu cha Think & Grow Rich.

Leo hii tutakuwa na somo la michanganuo na litahusu; “MAUZO YANAYORUDISHA GHARAMA”(BREAK EVEN SALES). Hii inatokana na maombi ya baadhi ya wanakikundi waliotaka ufafanuzi zaidi wa kipengele hiki kwenye mpango wa biashara hasa kwa upande wa biashara ya bidhaa zisizoweza kuhesabika moja moja  kwa urahisi. Leo somo hili tutalitazama kwa namna ya kipekee kabisa.


Ada ya kujiunga na Group hili ni shilingi elfu 10 ambayo ni kwaajili ya kuchangia gharama za uendeshaji wa shughuli hizi, mimi naamini kabisa faida nitakazozipata nikiwa kama mwanachama wa group hili ni nyingi kushinda hata kama ningelichaji kiingilio cha shilingi laki moja.

Ikiwa na wewe ndugu msomaji utapenda kujiunga na Group hili, unaweza kutuma ada kupitia namba hizi hapa, 0712202244  au  0765553030 jina ni Peter Augustino Tarimo kisha tuma ujumbe kwa meseji au ukitumia whatsapp 0765553030

Ikiwa hutumii Whatsapp bado unaweza kujiunga na group na ukapata masomo kupitia email au blogu ya private ya masomo.

Baadhi ya masomo yaliyopita na vitu mbalimbali tunavyotuma kwa mtu anayejiunga mbali na masomo ya kila siku ni hivi hapa chini;

1.  Kitabu cha MICHANGANUO YA BIASHARA NA UJASIRIAMALI kwa lugha ya Kiswahili.

2.  Masomo 11 ya semina kamili ya jinsi ya kuandika mpango wa biashara.

3.  Kifurushi maarufu cha michanganuo 3 ya ufugaji wa kuku(MKOMBOZI CHICKS PLAN 3PACKS)

4.  Kitabu mashuhuri zaidi duniani, HOW TO WRITTE A BUSINESS PLAN kwa lugha ya kiingereza, ndio kinachotumika vyuo vikuu vingi duniani.

5.  Mfululizo wa Tafsiri ya kitabu mashuhuri cha THINK & GROW RICH kwa Kiswahili.

6.  Kuunganishwa na blogu ya kulipia ya michanganuo bure.

7.  Vielezo(Templates) za michanganuo ya biashara inayokuwezesha kuandika michanganuo kwa muda mfupi.

8.  Masomo yote yaliyopita katika group la whatsapp la MICHANGANUO NA MZUNGUKO WA FEDHA.

9.  Mfumo mpya wa usimamizi wa duka la rejareja(2 IN ONE STORE MANAGEMENTA SYSTEM) unaomwezesha mmiliki wa duka dogo la rejareja au la kati kuthibiti mapato yake pasipo msaidizi kudokoa hata senti 5

10.      Somo muhimu sana la mzunguko wa fedha.

11.      Ukurasa mmoja wa mchanganuo.

……………………………………………………..............................

Kwa vitabu mbalimbali vya biashara na ujasiriamali katika lugha ya Kiswahili unaweza kutembelea ukurasa huu hapa, SMART BOOK TANZANIA

0 Response to "KWANINI KUNDI LA KUSHAURIANA(MASTER MIND GROUP) NI MUHIMU KWA KILA ANAYETAFUTA MAFANIKIO?"

Post a Comment