Michezo ya redioni, luninga na hata simulizi
mbalimbali za mazombi zilizokuwa zikisimuliwa
tokea enzi na enzi na Wahenga, nyingi zimekuwa zikitoa ujumbe unaohusisha utajiri
wa pesa na mambo mbalimbali mabaya kama vile kafara, wizi, unyanganyi,
chinjachinja, ushirikina na mambo mengine mengi ya kutisha, wakati umasikini wa
pesa umekuwa ukionyeshwa katika upande wa picha ya unyoofu kama vile kwenda
peponi baada ya kifo na mambo mengine yote ya kimaadili katika jamii.
Tatizo hili la kupandikiza akilini mwa watu
wengi picha hizi mbili huanzia tangia utotoni pale watu katika akili zao za
ndani(Subconscious mind) wanapoamini kwamba pesa siyo kitu kizuri bali ni
ibilisi, matokeo yake huja kurithisha imani hiyo kwa watoto wao na kuzidi
kujenga hali ya umasikini kizazi hata kizazi jambo linalosababisha pia baada ya
muda kupita iwe vigumu mno kuing’oa imani hii vichwani mwa watu.
SOMA: Elimu ya pesa a umuhimu wake 2019 njoo tuunganishe nguvu tuhamishe milima.
SOMA: Elimu ya pesa a umuhimu wake 2019 njoo tuunganishe nguvu tuhamishe milima.
Wakati wote hapa duniani, pesa zimekuwa na
umuhimu mkubwa na hasahasa katika zama hizi tulizokuwa nazo karibu kila kitu
muhimu maishani huwezi ukakipata ikiwa huna pesa. Pesa imekuwa kama alama ya
uwezo/nguvu na njia ya kutengeneza matabaka miongoni mwa binadamu. Pesa pia
inaweza ikafananishwa hata na madawa ya kulevya kwa baadhi ya watu kwa jinsi
ambavyo wamekuwa wakizifukuzia na kushindwa kuishi bila ya pesa.
Katika upande huu wa mgawanyo wa pesa kwa
watu usiokuwa sawa kuna makundi makubwa matatu (3), wapo wasiokuwa na
pesa(Masikini wa kutupa), wale wenye kuwa nazo(matajiri wa kutupa) na wale
waliokuwa katikati(hawana pesa nyingi lakini pia siyo masikini)
SOMA: Njia saba7 halali na nzuri za kupata mafanikio na utajiri wa haraka
SOMA: Njia saba7 halali na nzuri za kupata mafanikio na utajiri wa haraka
Inavyoonekana ni kwamba baadhi ya watu, pesa
zimekuwa zikiwakwepa kama pande 2 za
sumaku zinazofanana wakati kuna wengine wanapozisogelea tu pesa hivi, huwafuata
zenyewe mithili ya mbwa amuonapo chatu. Jambo hili limekuwa likiumiza vichwa
vya watu wengi sana na kuhoji haki ipo wapi juu ya mazingira haya ya pesa kutoa
matokeo tofauti hata pale makundi yote haya 3 yanapoonyesha juhudi sawa katika
kuzitafuta. Mpaka wengine wamediriki kusema kwamba pengine hali hii inachangiwa
na wao kutokuwa na bahati ya pesa.
Lakini ukweli ni kwamba siyo swala la bahati
hata kidogo, katika ulimwengu huu tunamoishi kila jambo hutokea sawasawa na vile mtu alivyolifikiria kabla. Kila mtu
anafahamu kwamba mawazo/fikra ni kitu halisi. Na hii pia hufanya kazi katika
mtazamo wa mtu kuhusiana na hali yake kifedha na ndiyo husababisha hasa
mgawanyo usiokuwa sawa kwenye umiliki wa pesa duniani.
SOMA: Ufahamu wa pesa ni lazima ujengwe kwa kutaka isipokuwa tu labda mtu azaliwe nao.
SOMA: Ufahamu wa pesa ni lazima ujengwe kwa kutaka isipokuwa tu labda mtu azaliwe nao.
1.Watu wa kipato cha kati.
Nitaanza na kundi hili la katikati, watu wa kipato cha
wastani, watu hawa katika mawazo yao wanaamini vitu vifuatavyo;
· Pesa
huhitaji mwelekeo wa fikra uliokuwa wa
kadri
· Pesa
hazihitaji kutafutwa kwa sababu za wivu
au husuda kwamba kwaninin fulani
amezipata basi na mimi ni lazi nizipate ili nimuonyeshee, iwe isiwe.
· Pesa
hazipaswi kuwa ndio lengo kuu maishani
· Katika
akili ya ndani ya watu hawa huzichukulia pesa kwa mtazamo wa kadiri, huwa
hawafukuzani na pesa kupita kiasi wala
hawakai nazo mbali sana.
2.Masikini
wa kutupa.
· Mwelekeo
wao wa kifikra kuelekea pesa siyo wa kadiri bali ni hasi kupindukia.
· Kutokana
na kukosa pesa kwa muda mrefu na vikwazo
mbalimbali vya kimaisha wameamua kuzichukia pesa mno katika akili zao za ndani.
· Tunaweza
tukasema watu hawa wameshakubaliana na hali halisi ya kukosa pesa au kupata
pesa kidogo sana maisha yao yote na hata vizazi vyao na wala hawana tena haja
ya kuhangaika kuzitafuta.
· Mtazamo
wao kuelekea pesa ni wa kinyonge na usiokuwa shindani kabisa.
SOMA: Watu wenye mafanikio kipesa wameweza kuyashinda matatizo haya 5 ya kitabia yaliyojificha ndani yao.
3.Matajiri wa kutupa
3.Matajiri wa kutupa
· Hawa
wana mtazamo ulio kinyume kabisa na ule wa masikini wa kutupa
· Utajiri
wao wengi wameupata kupitia nguvu zao wenyewe pasipo kurithi wala kusaidiwa na
ndugu, jamaa na marafiki
· Katika
akili ya ndani kabisa ya watu wa aina hii, mtu hujiwekea lengo kubwa na muhimu
la kifedha maishani mwake
· Wakati
mwingine lengo hilo hulihusudu hata kushinda vile linavyostahili
· Kutengeneza
faida kwake inaweza kuwa ni wazo lenye thamani kubwa kwake na lengo kuu
maishani
· Mara
nyingi watu wa kundi hili wana mafanikio makubwa kifedha maishani kushinda
makundi mengine yote 2
· Wana
wivu balaa wa kimaendeleo, huwa hawakubali wanapoona fulani kafanikiwa mpaka na
wao wamefanikiwa.
Yote yaliyoelezwa hapo juu ni asili tu ya
mgawanyo wa pesa ulivyo kati ya hayo makundi 3 lakini bado hakuna mapendekezo
yeyote yale ni kwa njia gani basi watu walioko
katika makundi mawili ya mwanzo, lile la kati na la masikini wa kutupa
wanavyoweza wakajinasua kutoka katika makundi waliyopo na kuingia katika kundi
la tatu la Matajiri.
SOMA: Kwanini kufanikiwa kifedha si dhambi na kila mtu anastahili afanikiwe?
SOMA: Kwanini kufanikiwa kifedha si dhambi na kila mtu anastahili afanikiwe?
Na ukumbuke pia kujitoa katika makundi hayo
ni shughuli pevu, ni sawa tu na ku “Uninstall”
programu mbaya(virus) kwenye kompyuta ili uweze ku “Install” programu nzuri isiyokuwa na kirusi kwenye kompyuta hiyo. Wakati mwingine ‘Antivirus’ za hivihivi tu huwa
zinagoma na unalazimika kuweka Window upya. Sasa utatumia antivirus gani kuondoa fikra hasi
zilizopandikizwa katika akili za watu za ndani kabisa tokea vizazi na vizazi?
.....................................................................
.....................................................................
Tuungane kwenye somo hili zima katika
group la masomo ya kila siku yahusuyo pesa watsap, la Michanganuo online.
Utapata na masomo mengine mengi ya fedha yaliyofundishwa siku zilizopita na ambayo
huwezi ukayapata mahali kwingine kokote kule.
Kujiunga na group au masomo haya kwa
njia za wasap au Email lipia kiingilio sh. Elfu 10 kisha tuma ujumbe usemao, “NIUNGANISHE
NA MASOMO YA FEDHA YA KILA SIKU”
Nitakutumia masomo, semina na vitabu
kisha kukuunganisha na group kwa ajili ya masomo ya kila siku yajayo.
Semina ya hivi karibuni kabisa utakayopata pamoja na mchanganuo kamili wa biashara ni ile ya BIASHARA YA KIWANDA KIDOGO CHA TOFALI ZA SARUJI(KILUVYA QUALITY BRICKS) Vitu vingine ni hivi vifuatavyo na offa yake ni ya muda mfupi sana karibu itamalizika;
Semina ya hivi karibuni kabisa utakayopata pamoja na mchanganuo kamili wa biashara ni ile ya BIASHARA YA KIWANDA KIDOGO CHA TOFALI ZA SARUJI(KILUVYA QUALITY BRICKS) Vitu vingine ni hivi vifuatavyo na offa yake ni ya muda mfupi sana karibu itamalizika;
1. Kitabu
cha MICHANGANUO YA BIASHARA NA UJASIRIAMALI kwa lugha ya Kiswahili.
2. Kitabu
kipya cha masomo ya Mzunguko chanya wa fedha 2018 part 1
3. Kitabu
kipya cha Masomo ya fedha 2018 part 2
4. Kitabu
kipya 1 cha jinsi ya kuandika michanganuo ya biashara hatua kwa hatua.
5. Kitabu
mashuhuri zaidi duniani, HOW TO WRITTE A BUSINESS PLAN kwa lugha ya kiingereza,
ndio kinachotumika vyuo vikuu vingi duniani.
6. SEMINA:
Masomo 11 ya jinsi ya kuandika mpango wa biashara.
7. Kifurushi
maarufu cha michanganuo 3 ya ufugaji wa kuku(MKOMBOZI CHICKS PLAN 3PACKS)
8. Mchanganuo
wa biashara ya mgahawa(JANE RESTAURANT) kwa Kiswahili na kiigereza
9. Mchanganuo
wa biashara ya kilimo cha matikiti maji.
10.
Vielezo(Templates) za michanganuo ya biashara
inayokuwezesha kuandika michanganuo kwa muda mfupi.
11.
Mfumo mpya wa usimamizi wa duka la rejareja(2
IN ONE STORE MANAGEMENT SYSTEM) unaomwezesha mmiliki wa duka dogo la rejareja
au la kati kuthibiti mapato yake pasipo msaidizi kudokoa hata senti 5
12.
Mchanganuo na semina ya jinsi ya kuandika
mpango wa biashara ya mgahawa(JANE FAST FOOD & JANE RESTAURANT)
13.
Somo muhimu sana la mzunguko wa fedha.
14.
Ukurasa mmoja wa mchanganuo.
Ili kuweza kujinyakulia OFFA hizi zote pamoja na kuendelea kupata masomo kamili ya kila siku yenye maudhui ya pesa lipia kiingilio chako shilingi 10,000/=(ELFU KUMI) kisha tuma ujumbe wa watsap au meseji ya kawaida kupitia namba 0765553030 usemao, "NITUMIE MASOMO YA FEDHA NA OFFA ZAKE"
*Ikiwa hutumii watsap, hamna shida EMAIL
inatosha, nitakutumia kila kitu kwa email.*
0 Response to "WATU NA PESA: YAPO MAKUNDI MATATU(3) DUNIANI, JE WAJUA WEWE UPO KUNDI GANI?"
Post a Comment