Katika mfululizo wa semina za kuandaa mipango
ya biashara za viwanda bunifu vinne 2019 tulianza rasmi mwezi huu wa Agost
tarehe 15 na tutaendelea mpaka Novemba kila mwezi. Semina yetu hiyo ya kwanza
ilikuwa inahusu kiwanda cha kuyfatua tofali za block Kiluvya Mkoani Pwani, na
ratiba yake ilikuwa kama ifuatavyo;
SIKU
YA KWANZA
Tulijifunza namna utafiti wa biashara hii
ulivyofanyika hatua kwa hatua.
SIKU
YA PILI
Tukaanza kuandika hatua kwa hatua Sehemu zote
8 za mpango wa biashara hiyo
SIKU
YA TATU
Tulijifunza kwa kina na kuandika Kipengele
cha fedha(Makisio ya faida na hasara, Break even Point, Pay back Period,
Makisio ya mtiririko wa fedha, Mizania ya biashara na Sehemu/Ratios)
Semina hii ilikuwa nzuri na kila mtu
aliyeshiriki alinufaika kwani baada tu ya kumalizika watu wengi walianza
kuchukua hatua za maandalizi kwa ajili ya viwanda vyao vidogovidogo walivyokuwa
wakiota siku nyingi kuvianzisha lakini bila mafaniko. Hatua ya mwanzo kabisa ya
kuanzisha kiwanda ni kuandaa mpango utakaokuwezesha kujua unahitaji kitu gani
na kwa gharama zipi.
Lengo kuu la semina hizi ni kuchochea moyo wa
kuanzisha viwanda nchini, kuunga mkono juhudi za Taifa hili la Tanzania kufikia
uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025. Vilevile ni ili kusaidia wajasiriamali
wadogo kuweza kujifunza mbinu mbalimbali za uendeshaji wa biashara za
uzalishaji wa bidhaa badala tu ya kung’ang’ania biashara za uchuuzi wa bidhaa
zinazotoka nje ya nchi ambazo faida yake ni kidogo na haziwezi kuwatoa watu
wengi kwenye umasikini.
Ikiwa basi ulikosa semina hii na ulipenda
kushiriki, bado kuna fursa ya kuweza kuipata. Tumeweka muda wa wiki moja kwa
ambaye hakuweza kushiriki kuipata semina hiyo iliyowekwa katika mfumo wa PDF
kupitia email. Pia kwa kulipia semina hii moja kwa moja utashiriki semina
nyingie zote 3 zilizobakia.
Siyo lazima uwe Whatsapp ndipo ujiunge na
semina hizi, unaweza kujiunga hata kama unatumia Email peke yake kwani tunatuma
pia kila kitu kupitia Email.
CHA
KUFANYA, KAMA UNAHITAJI TU LAKINI !
Lipia shilingi elfu 10 kupitia namba zetu, 0765553030
au 0712202244 kisha tuma ujumbe wasap 0765553030 au sms ya kawaida usemao, “NITUMIE SEMINA YA KIWANDA CHA TOFALI”
Nitakutumia mara moja Mchanganuo mzima wa
biashara hiyo ya tofali pamoja na Semina yote kama tulivyojifunza.
Lakini pia nitakutumia offa ya masomo na
vitabu mbalimbali kama ifuatavyo; *(Offa hii maarufu ya vitu 13 bado kidogo sana itaisha muda wake)*
1. Kitabu
cha MICHANGANUO YA BIASHARA NA UJASIRIAMALI kwa lugha ya Kiswahili.
2. Kitabu
kipya cha masomo ya Mzunguko chanya wa fedha 2018 part 1
3. Kitabu
kipya cha Masomo ya fedha 2018 part 2
4. Kitabu
kipya 1 cha jinsi ya kuandika michanganuo ya biashara hatua kwa hatua.
5. Kitabu
mashuhuri zaidi duniani, HOW TO WRITTE A BUSINESS PLAN kwa lugha ya kiingereza,
ndio kinachotumika vyuo vikuu vingi duniani.
6. SEMINA:
Masomo 11 ya jinsi ya kuandika mpango wa biashara.
7. Kifurushi
maarufu cha michanganuo 3 ya ufugaji wa kuku(MKOMBOZI CHICKS PLAN 3PACKS)
8. Mchanganuo
wa biashara ya mgahawa(JANE RESTAURANT) kwa Kiswahili na kiigereza
9. Mchanganuo
wa biashara ya kilimo cha matikiti maji.
10.
Vielezo(Templates) za michanganuo ya biashara
inayokuwezesha kuandika michanganuo kwa muda mfupi.
11.
Mfumo mpya wa usimamizi wa duka la rejareja(2
IN ONE STORE MANAGEMENT SYSTEM) unaomwezesha mmiliki wa duka dogo la rejareja
au la kati kuthibiti mapato yake pasipo msaidizi kudokoa hata senti 5
12.
Somo muhimu sana la mzunguko wa fedha.
13.
Ukurasa mmoja wa mchanganuo.
HAPA CHINI NIMEWEKA MUHTASARI WA MPANGO WA
BIASHARA HIYO YA TOFALI (KILUVYA QUALITY BRICKS)
1.0 MUHTASARI
Kiluvya Quality
Bricks ni kampuni itakayozalisha na kuuza tofali za saruji pamoja na vifaa
vingine mbalimbali vya ujenzi vilivyo na ubora wa hali ya juu kwa bei rafiki
kwa mteja. Malengo yake makubwa ni pamoja na kufikisha wastani wa mauzo ya shilingi
milioni 12 kwa mwezi, kuongeza idadi ya mashine 2 mwaka wa 3 pamoja na kutoa
ajira ya kudumu kwa watu watatu. Wamiliki wa biashara ni Bwana Ahmed Yusuph na Grayson Moris ambao kila mmoja atatoa
kiasi cha shilingi milioni 6.5 kama kianzio.
Eneo la biashara lipo
katka mtaa wa Kiluvya madukani wilayani Kisarawe Mkoa wa Pwani. Tutaanza na
uzalishaji wa tofali na hali ya kifedha ikiimarika tutazalisha bidhaa
nyinginezo kama vile, paving blocks, makalavati, nguzo na mifuniko ya majitaka.
Soko letu tumeligawa katika makundi 2, Watu binafsi na Taasisi lakini
kipaumbele chetu kikubwa ni katika kundi la watu binafsi kutokana na kufikika
kwa urahisi na kwa gharama kidogo. Mahitaji makubwa ya tofali na vifaa vya
ujenzi katika eneo la Kiluvya yanatokana na wakaazi wengi wa jiji la Dar es
salaa kuhamia maeneo ya pembezoni hasa mkoa wa Pwani kwa ajili ya kuanzisha
makazi. Sababu nyingine ni ujenzi wa barabara ya Morogoro.
Ingawaje sekta ya
ujenzi imeonyesha kushuka kidogo mwaka huu toka asilimia 15.6 mwaka jana mpaka
asilimia 13.2 lakini bado sekta hiyo imeendelea kuongoza katika kuchangia pato
kuu la Taifa. Washindani wetu wakubwa waliopo ndani ya umbali wa kilometa 10
wapo wawiili ambao ni Kiluvya Traders na Bambam blocks & Bricks. Lakini washindani
hao wana udhaifu katika bei, ubora, usimamizi, teknolojia na kiwango cha
uzalishaji kwa siku.
Ili kuweza kutimiza
mahitaji yote washindani wetu waliyoshindwa kuwatimizia wateja tutatumia
mikakati mbalimbali ikiwemo, eneo letu la kimkakati, bei wateja wanayoimudu,
kukuza jina letu sokoni pamoja na kujenga ukaribu na mafundi wajenzi.
Uendeshaji wa shughuli za kila siku utasimamiwa na mwanzilishi mwenza Grayson
Moris Jumatatu mpaka Jumamosi. Gharama ya kuzalisha tofali moja ni sh. 738 na
kwa siku zinatarajiwa kuzalishwa tofali 400.
Viongozi wa kampuni
watakuwa ni waanzilishi wenyewe lakini pia watashiriki moja kwa moja katika
majukumu mengine ya kila siku. Wafanyakazi wa kudumu watakuwa 3 huku wengine
wakiwa ni vibarua watakaolipwa kwa siku. Kiluvya Quality inakisia faida kwa
mwaka kuwa ni shilingi milioni 20.6, Mauzo ya kurudisha gharama shilingi
milioni 3 au tofali 3085 kwa
mwezi na muda mradi utakaporudisha fedha zote za kuanzia ni miezi 7.
…………………………..
Peter
A. Tarimo
Mwandishi
na mhamasishaji.
0 Response to "JE, ULIKOSA SEMINA YETU YA KWANZA YA VIWANDA MWEZI AGOSTI?"
Post a Comment