MAONO YAKO NDIYO CHANZO CHA MABADILIKO YAKO (YOUR FANTASIES ARE THE SOURCE OF YOUR CHANGES) | JIFUNZE UJASIRIAMALI

MAONO YAKO NDIYO CHANZO CHA MABADILIKO YAKO (YOUR FANTASIES ARE THE SOURCE OF YOUR CHANGES)


KUTOA PESA KWA PUPA
Ndani yako kuna nguvu kubwa kuliko hata ulivyo wewe mwenyewe, serikali na hata mustakabali mzima wa maisha yako. Binadamu anayo kawaida ya kuota, kuwa na ndoto au maono(fantasize). Kuota au kuwa na maono ni uwezo wa kugundua mambo yajayo unaotutofautisha sisi binadamu na na wanyama wengine.

Faida kubwa kimageuzi binadamu aliyoipata kupitia katika mabadiliko ya historia yake ni maono(uwezo wa kubuni vitu kabla havijatokea kuwa vitu halisi) Mfano mmoja ni pale kabla mtu hajajenga nyumba yake hujaribu kwanza kujenga taswira ya jinsi nyumba hiyo itakavyoonekana na wakati mwingine hata kuchora na ramani kabisa katika karatasi ndipo sasa huja kuanza ujenzi mpaka nyumba imekamilika na kuwa kama vile alivyofikiria mwanzoni.


Mara nyingi njozi za mwanadamu huwa ni zile zenye kutabiri mambo mazuri na yaliyokuwa bora zaidi kuliko yale yaliyopita na yaliyopo ndio maana katika mabadiliko ambayo yamekuwa yakitokea Duniani, vitu huwa bora zaidi kadiri siku zinavyokwenda kuliko siku zilizopita. Kwahiyo binadamu yeyote yule kuwa na ndoto njema juu ya maisha yake siyo jambo baya bali ndiyo mwanzo wa mabadiliko yake katika nyanja mbalimbali za kimaisha.

Mfano mmoja mkubwa ni katika biashara zetu na ajira. Mtu unapaswa uwe na ndoto au maono ya biashara yako au ajira yako miaka zaidi ya mitano ijayo. Kama leo hii unafanya kazi kama mpokeaji wageni, ndoto zako siku moja iwe ni kuja kuwa meneja au mkurugenzi wa kampuni. Na ikiwa wewe leo hii unafanya biashara ya kuuza matikiti maji, maono yako siku moja yawe ni kuja kumiliki mgahawa mkubwa au biashara ya usafirishaji mizigo na abiria mikoani na nje ya nchi. Taswira yako ikuonyeshe kabisa ukiwa unamiliki  vitu hivyo sasa hivi kabla hujavimiliki kiukweli.


Katika uandishi wa mpango wa biashara (Business Plan) kuna kipengele kidogo pale mwanzoni baada ya Muhtasari tendaji cha maono, na hata mpango wenyewe wa biashara unaweza ukasema ni maono kwani unatabiri mambo ambayo bado hujayafanya kiuhalisia. Lakini kumbuka nimeanza kwa kusema kuwa chanzo cha mabadiliko yote ya binadamu ni maono.

Hatuwezi kutimiza jambo lolote lile bila kwanza ya kulifikiria akilini namna tutakavyolitekeleza. Kila mtu anayefanikiwa kwenye biashara yake aliweka mipango madhubuti. Kinachofanya tuone kama vile watu hawapangi ni kwamba wengi wanafanya mipango yao kichwani tu na siyo kuiandika katika maandishi kwenye karatasi. Kwa yule anayepanga kwa maandishi ana uwezekano mkubwa zaidi wa kufanikiwa kuliko anayepanga tu kichwani.


Kozi ya namna ya kuandaa mpango wa biashara tayari tunayo na tulishaitoa kwa wale waliojiunga tayari katika group la masomo la MICHANGANUO-ONLINE. Masomo hayo ni rahisi sana isipokuwa tu kuna kipengele kimoja cha FEDHA(Financial section) ambacho watu wengi hulalamika ni kigumu. Sasa tumeandaa semina kubwa itakayohusu eneo hili tu kwa undani kabisa ili kila mtu anayeliona eneo hili kuwa ni gumu aweze kulielewa barabara.  Mtu yeyote akishazifahamu tu kanuni zinazotumika, ugumu katika kuandaa mchanganuo wa biashara unabakia kuwa historia kwake.

Semina hii itafanyika mnamo tarehe 20/3/2019 ndani ya group la masomo la Michanganuo-online kupitia njia za wasap na email. Kiingilio ni shilingi elfu 10 kwa yule ambaye bado hajajiunga na group la MICHANGANUO-ONLINE. Mshiriki pamoja na semina yenyewe hupewa pia  masomo ya pesa, vitabu, semina na michanganuo yote tuliyokwishaijadili katika group hilo siku zilizopita tangu mwaka jana uanze katika mfumo wa softcopy.


Namna za malipo kwa yule ambaye bado hajajiunga ni; 0765553030 au 0712202244 Baada ya malipo tuma ujumbe wa sms au wasap usemao, “NIUNGANISHE NA GROUP LA SEMINA”

Ikiwa hupendi kujiunga na Magroup ya wasap unaweza kujiunga na masomo tukakutumia kupitia email yako(Barua pepe)

Ikiwa pia unaona ni vigumu kutoa kiingilio hiki sh. elfu 10 kwa mara moja ni vizuri kuanzia leo hii ukaanza mpango wa kuweka sh. Elfu moja moja kila siku kwa siku 7 kisha siku nyingine 7 ukaweka sh. 500 kila siku, baada ya wiki 2 utakuwa umetimiza kiasi chote sh. Elfu 10.

Unaweza ukajiunga mapema kabla ya siku ya semina ukaendelea kushiriki  masomo ya kila siku ya fedha pamoja na mijadala mingine mbalimbali ndani ya group kuhusiana na ujasiriamali, biashara na maisha kwa ujumla. Group lina watu makini sana wanaojitambua na walio na fani mbalimbali katika biashara na kazi.

Dondoo zaidi za semina hii, yaliyomo na ratiba kamili nitaendelea kukujuza siku hadi siku mpaka tarehe ya semina itakapofika. Hii si semina ya kukosa kwani haijawahi kuwepo semina nyingine ya namna hii inayochambua kipengele cha fedha katika mpango wa biashara kwa vitendo na si kwa maelezo matupu kama wafanyavyo wakufunzi wengi katika mitandao mbalimbali.

WASAP 0765553030
SIMU: 0712202244
Peter Augustino Tarimo

0 Response to "MAONO YAKO NDIYO CHANZO CHA MABADILIKO YAKO (YOUR FANTASIES ARE THE SOURCE OF YOUR CHANGES)"

Post a Comment