JINSI YA KUSIMAMIA HESABU KATIKA BIASHARA NDOGO UNAYOMWACHIA MFANYAKAZI | JIFUNZE UJASIRIAMALI

JINSI YA KUSIMAMIA HESABU KATIKA BIASHARA NDOGO UNAYOMWACHIA MFANYAKAZI

Katika biashara ndogondogo shida kubwa haipo katika uwekaji wa kumbukumbu za hesabu hapana, bali shida ipo kwenye kudhibiti upoteaji wa mali au pesa. Kama utafungua biashara ambayo hautaweza kusimamia kikamilifu mahesabu yake basi na ujue biashara hiyo haiwezi kufika mahali popote pale itafia njiani, ni bora ukaachana nayo au ukaifunga kabisa kwani haina maana yeyote kwako zaidi ya kukupotezea muda na rasilimali zako chache ulizokuwa nazo.

Kuweka kumbukumbu za biashara ni jambo rahisi iwe wewe ni mjasiriamali mdogo au mkubwa, unayekaa mwenyewe kwenye biashara au uliyemwajiri mfanyakazi akuuzie. Tatizo linakuja kwenye usimamiaji na ufuatiliaji wa hesabu hizo kila mara. Wajasiriamali wengi huona kama ni kazi ngumu kufuatilia hesabu kila siku na mwishowe huamua kuacha mambo yaende kiholela na hapo ndipo huja kulia na kusaga meno baadae.

SOMA: Biashara ndogo kwa wajasiriamali zinazoendana na wakati tulio nao sasa.

Ikiwa mjasiriamali anaendesha biashara peke yake bila msaidizi, ufuatiliaji wa hesabu hauwezi kuwa na changamoto nyingi lakini mara tu utakapoajiri msaidizi changamoto nazo huibuka. Njia za kawaida za uwekaji wa kumbukumbu za mahesabu ya biashara ni zilezile hazibadiliki. Unaweka kumbukumbu za matumizi yote na mapato ya kila siku kisha baada ya kipindi fulani tuseme labda siku, wiki au mwezi unakuja kufanya tathmini umepata faida kiasi gani. Unaweza pia ukafanya tathmini ya hesabu nyingine kama vile mtiririko wa fedha taslimu na mizania ya biashara.

Uwekaji wa kumbukumbu na hesabu za biashara umeelezewa kwa undani sana katika kitabu cha “MICHANGANUO YA BIASHARA NA UJASIRIAMALI” ambacho nadhani kila mtu hapa kwenye Group la Michanganuo-online anayo nakala yake. Somo hilo lipo katika ukurasa wa 351 mpaka uk. wa 375 ni somo refu kwenye hicho kitabu. Vile vile katika kitabu kingine cha “MAFANIKIO YA BIASHARA YA DUKA LA REJAREJA” katika ukurasa wa  50 – 73 kimeelezea vilevile kwa kirefu namna ya kuweka kumbukumbu na kukokotoa hesabu katika biashara ya rejareja hususani duka.

SOMA: Biashara ya duka inavyoweza kukutoa kimaisha ukiwa mjanja.

Lakini leo hii hasa si lengo langu kuyarudia masomo hayo kama yalivyoelezwa katika hivyo vitabu na hata mahali kwingineko, bali nia yangu hasa ilikuwa ni kujibu swali au ombi la msomaji ambaye pia ni mwanagroup mwenzetu humu(hajaniruhusu kutaja jina lake lakini) aliyeniomba niandike kidogo kuhusiana na suala zima la udhibiti wa hesabu kwenye biashara ndogo ya uuzaji wa maziwa, mdau huyu anacho kioski chake cha kuuzia maziwa mbali na shughuli zake za msingi na amemwajiri kijana, sasa inamuwia vigumu katika kudhibiti mapato kila siku inapofika jioni.

SOMA: Kama adui mkubwa wa fedha zako ni wewe mwenyewe, utumie njia gani ili ziweze kuwa salama?

Kama nilivyotangulia kusema awali kwamba, “Ikiwa kama huwezi kudhibiti hesabu za biashara yako, basi ni bora uifunge au kuachana nayo kabisa”-Peter Augustino. Hapa nitaeleza kanuni muhimu sana ambayo ndiyo itakayokuwa muarobaini katika kudhibiti mapato ya biashara yako. Nitaelezea kwanza mahsusi(specifically) kwa biashara ya huyu mwenzetu ya uuzaji maziwa na kisha nitaelezea kwa ujumla ili hata kama kuna mtu anataka ‘kuiapply’ kanuni hiyo katika biashara nyingine yeyote ndogo basi aweze kufanya hivyo.

Kwa kuwa biashara ya maziwa………………

…………………………………………………
Mpenzi msomaji katika blogu hii, makala hii nzima tutajifunza leo kwenye Group la watsap la MICHANGANUO-ONLINE, masomo kama haya huwa tunajifunza kila siku saa 3 mpaka saa 4 usiku. Katika group hilo pia tunakuwa na semina za mara kwa mara juu ya uandaaji wa mipango ya biashara mbalimbali zilizo na fursa kubwa ya kuleta faida.

Ili kujiunga na Group lipia kiingilio sh. Elfu 10 kupitia namba zetu 0712202244  au  0765553030 kisha tuma anuani yako ya email kwa sms ikifuatiwa na maneno, “NIUNGANISHE NA GROUP LA MICHANGANUO”
Unapojiunga pia unapata masomo yote yaliyopita, semina pamoja na vitu mbalimbali kama ifuatavyo;


0 Response to "JINSI YA KUSIMAMIA HESABU KATIKA BIASHARA NDOGO UNAYOMWACHIA MFANYAKAZI"

Post a Comment