SABABU YA KUVUNJA RATIBA YETU YA USOMAJI WA KITABU CHA THINK & GROW RICH | JIFUNZE UJASIRIAMALI

SABABU YA KUVUNJA RATIBA YETU YA USOMAJI WA KITABU CHA THINK & GROW RICH

Kuvunja ratiba ya usomaji Think & grow Rich

Mwazo tuliweka ratiba ya usomaji iliyoelekeza kila siku kusoma kurasa 10 kwa nakala ya kitabu ya kiingereza lakini kurasa 21 kwenye nakala ya kitabu kwa Kiswahili, Hata hivyo kutokana na changamoto ya kuchelewa kumaliza kusoma kwa wengi wetu, tumeamua sasa hivu kuvunja uratatibu wa kurasa 10 kwa siku na badala yake sasa tutaendelea kusoma kurasa 10 mpaka karibu kila mmoja anapokuwa amemaliza ndipo tunaanza tena nyingine 10

Kwa mfano mpaka leo hii bado hatujaanza kurasa 10 za session ya tatu bado tupo session ya 2 mpaka wadau wote waweze kumaliza. Tumeamua hivi kutokana na ukweli kwamba lengo letu la kuanzisha utaratibu huu wa kusoma hiki kitabu cha Think and Grow Rich ni ili kila mdau aweze kunufaika vilivyo na maarifa ya kipekee yaliyomo ndani ya hiki kitabu ambapo anaweza kwenda kuyafanyia kazi maisha yake yakabadilika na kuwa mtu mkuu - anayethaminika katika jamii (To become Great).

Taratibu taratibu kila mtu akizoea na sote tukiwa na kasi inayolingana au kupishana kidogo kwenye usomaji basi tunaweza tukarejea kwenye ratiba yetu siku za mbele.

Leo tayari nimemaliza kuandaa ripoti yangu ya usomaji kurasa 10 za session ya pili (pg. 9 – 18 for English version) na (uk.17 – 37 kwa nakala ya Kiswahili). Na nitaipost hapa kwenye group jioni baada ya kila mmoja wetu kukamilisha session hiyo.

Hivyo naomba sana tujitahidi kutafuta muda wa kupitia hizo kurasa 10 no matter what.

Leo hii unaweza kuona ugumu lakini kesho na keshokutwa itakuwa vigumu zaidi, haujawahi kupatikana muda muafaka kwa ajili ya kusoma kitabuchochote kile nadhani mwenyewe ni shahidi na unakumbuka jinsi hata mashuleni tulivyokuwa tukihaha na kukikimbizana misimu ya mitihani, hivyo jisukume itawezekana tu!

Nategemea pia mirejesho kwa namna ya ripoti fupifupi au hata ikiwezekana unaandaakabisa ripoti yako ya Sura, sura ikiisha unashea hapa si mbaya.

Majedwali 2 hapo chini yanaonyesha tathmini ya ratiba yetu tuliyopanga mwanzo ‘A’ na ile inayojitokeza kwenye usomaji halisi ‘B’

A                                                     B

SESSION 1

29/07/2025

 

SESSION1

29/07/2025

 

 

 

 

 

 

 

 

SESSION 2

30/07/2025

SESSION 2

30/07/2025

 

 

 

31/07/2025

 

 

 

 

SESSION 3

31/07/2025

SESSION 3

01/08/2025

 

Soma kilichopita kwenye Usomaji huu

Soma kifuatacho kwenye Usomaji huu


0 Response to "SABABU YA KUVUNJA RATIBA YETU YA USOMAJI WA KITABU CHA THINK & GROW RICH"

Post a Comment