DAWA YA MTEJA ANAYEKUPITA KILA SIKU NA KWENDA KUNUNUA KWA WASHINDANI WAKO HII HAPA | JIFUNZE UJASIRIAMALI

DAWA YA MTEJA ANAYEKUPITA KILA SIKU NA KWENDA KUNUNUA KWA WASHINDANI WAKO HII HAPA

Mteja

Mwajabu ni mama mwenye duka la vyakula la rejareja katika mtaa wa Kumekucha Sinza jijini Dr es salaam. Jirani na duka lake amezungukwa na washindani watatu wanaomiliki maduka kama lakwake na yaliyo na bidhaa mchanganyiko zinazofanana na zakwake pia jambo linalosababisha pawe na ushindani mkali na wateja kuchagua ni wapi pakununua mahitaji yao ya nyumbani kila siku kulingana na unafuu ama huduma wanazopewa na maduka haya manne.

Ingawa Mwajabu hujitahidi kwa kila hali kutimiza mahitaji yote ya wateja wake ikiwa ni pamoja na kutoa huduma bora zinazozidi matarajio yao lakini bado alishangaa kuona kuna mteja mmoja tena mwanamke mwenzake humpita kila siku na na kwenda kununua bidhaa katika moja ya duka la washindani wake. Baada ya kujaribu kuchunguza sana ni nini mteja huyu anachovutiwa nacho kwa mshindani wake ambacho yeye hana hakuweza kupata jibu dhahiri.............................

SOMA: Chuma ulete anavyowatesa wenye maduka na wafanyakazi wao dar

Nitamalizia baadae kidogo stori hii ya Mwajabu lakini hebu kidogo tujadili sababu zinazowafanya wateja kuchagua duka au mahali pa kujipatia mahitaji yao/kununua bidhaa ama huduma zao. Kitu cha kwanza kabisa mteja anataka kutatua shida inayomkabili katika mazingira rafiki na rahisi kwa kadiri inavyowezekana. Kwahiyo inawezekana kabisa pamoja na kuwa na suluhisho la shida ya mteja lakini kuna mazingira fulani hujaweza kuyatimiza ndiyo maana mteja anaamua kukupita na kwenda kununua kwa mshindani wako.

Kuna sababu nyingi wateja huangalia kwa mfano bei, huduma bora, ucheshi wa muuzaji, ubora wa bidhaa/huduma, bidhaa na huduma tofautitofauti (mteja Napata kila kitu chini ya mwavuli mmoja), ukaribu na anapoishi mteja, mpangilio mzuri wa bidhaa, uhusiano wa karibu na mteja, punguzo la bei(discount), nyongeza nk. Mteja inawezekana hukupita tu kwa sababu muuzaji duka la jirani ana mahusiano naye kimapenzi lakini wewe huwezi kulijua hilo kirahisi.

SOMA: Biashara ya duka inavyoweza kukutoa kimaisha ukiwa mjanja

Vigezo vyote hivi na vingine ambavyo sikuvitaja hapa vinaweza kuwa ndiyo sababu kubwa ya mteja fulani kukupita kila siku na kwenda kununua kwa mshindani wako.

Nikimalizia ile stori niliyoanza nayo ni hivi; Mwajabu baada ya kujiuliza kwa muda mrefu ni kwanini mteja yule huwa anampita kila siku ili hali na yeye ana kila kitu maduka mengine walichokuwa nacho aliamua tu kutulia tuli na wala hakuweka kinyongo kwa yule mteja akimshukuru Mwenyezi Mungu kwani hamnyimi wateja kabisa na anauza tu kila siku mauzo ya kuridhisha. Akipita, tena Mwajabu humsalimia bila hiyana huku akiendelea na hamsini zake.

SOMA: Mbinu hizi 2 za uendeshaji duka la rejareja kwa mafanikio hazipo mahali pengine popote

Subira huvuta kheri, hatimaye siku moja yule mteja alifika dukani kwa Mwajabu na kumtaka amuuzie bidhaa mbalimbali, jumla ni kama vitu vya shilingi elfu ishirini (20,000/=) hivi! Mwajabu hakuamini macho yake, akamfungia mzigo wake wakaagana akaondoka. Tangu siku ile yule mteja aliendelea kuwa mteja mwaminifu wa Mwajabu ingawa pia siku moja moja aliendelea kumpita kama kawaida yake.

Hitimisho

Stori hii ya duka la rejareja la Mwajabu inatufunza somo muhimu la uvumilivu na kutokukata tamaa. Mwajabu hakukimbilia kunena, “Ona sisi wanawake tusivyopendana kabisa, ningekuwa mwanaume angeshakuja kununua kwangu siku nyingi tu, muone ananipita kila siku na kwenda kutafuta duka analouza mwanaume” bali alivuta subira kwani hakuijua bayana ni sababu ipi iliyokuwa ikimfanya asinunue kwake siku zote hizo

Hebu jaribu kufikiria wewe mwenyewe ni maduka mangapi umewahi kuyaacha na kwenda mbali maduka mengine kutafuta kitu ulichokuwa ukikihitaji kutokana na sababu mbalimbali? Lakini si kuna siku pia unaamua kuwaungisha maduka hayo uliyoyapita kwa kuwa wanakidhi haja ya kile unachoihitaji wakati huo? Basi na wateja wako ni hivyohivyo walivyo wala hawakupiti kwa bahati mbaya, wewe wavumilie tu wala usiwanenee mabaya au kuwatukana kwani ipo siku isiyokuwa na jina utashangaa kuwaona wakija kwenye biashara yako kununua.

SOMA: Biashara ya soda maji juisi na sigara: tumia siri hii kuongeza mauzo × 2

Na zaidi ya hapo kila siku tafiti na kuboresha huduma zako, weka bidhaa mpya, inawezekana kabisa ukarekebisha udhaifu ulio nao unaowafanya baadhi ya wateja wakupite na mwishowe wakarudi kwako.

Kwa elimu ya kina zaidi na mifumo itakayokuwezesha kusimamia biashara yako ya duka la rejareja au biashara yeyote nyingine ile ya rejareja hata kama ni Genge la matunda na mboga usiache kupata nakala ya kitabu chako cha MAFANIKIO YA BIASHARA YA DUKA LA REJAREJA

Kinapatikana kwa bei ya sh. elfu 6 tu kupitia namba zetu hizi; 0765553030 au 0712202244 lipia nikutumie muda huohuo katika simu au kompyuta yako  au unaweza ukakidownload mwenyewe kutoka katika duka hili la mtandaoni.

........................................................

Ndugu Msomaji wa makala hii, HERI YA MWAKA MPYA 2025-01-01

Tulishasema kwamba mwaka huu ni wa kujirudishia ukuu wako tena (MAKE YOURSELF GREAT AGAIN) kwa kutumia ubunifu, akili mnemba na kasi ya kutenda mambo tofauti na ilivyokuwa mwaka uliopita

Programu zetu pia kwa mwaka huu nilishaweka wazi tangu Octoba 2024 kwamba tutaendelea kutoa huduma kupitia blogu ya jifunzeujasiriamali bure kabisa lakini pia kwa anayehitaji kujifunza kwa kina ikiwa ni pamoja na kushiriki moja kwa moja madarasa yetu(Mastermind Groups) basi atachangia ada kidogo ya shilingi elfu 10  

Endelea kufuatilia kila siku makala katika blogu yako hii kujua ni kipi kinachojiri.

 

Peter Tarimo

Simu: 0712202244  / 0765553030

Watsap: 0765553030

 

 

0 Response to "DAWA YA MTEJA ANAYEKUPITA KILA SIKU NA KWENDA KUNUNUA KWA WASHINDANI WAKO HII HAPA"

Post a Comment