Katika
siku ya pili ya semina yetu tarehe 26/03/2024 masomo yalianza rasmi saa 3 na
tulichanganua mambo matatu kama utakavyoona. Hapa katika Blogu hii ya
Jifunzeujasiriamali najitahidi kuweka dondoo tu za semina na siyo semina nzima
kama ilivyokuwa kwenye group maalumu. Unaweza kuona baadhi ya sentensi kuna deshi-deshi-dshi.............kuashiria
kwamba kuna maelezo hayajakamilika.
Kuna
mambo mengi unaweza usiyajue ikiwa hukushiriki moja kwa moja katika hiyo semina
ikiwa ni pamoja na kutokuwa na rejea, nikimaanisha Kitabu cha Michanganuo ya Biashara na Ujasiriamali pamoja
na Mchanganuo kamili wa biashara
yetu ya ufugaji wa kuku wa kuroiler.
Tulianza
kwa sauti (voice note) kama uonavyo hapo chini kisha maelezo ya kawaida kwa
ujumbe wa maandishi huku washiriki wenye maswali wakiruhusiwa kuuliza maswali
yao muda wowote wapendao.
VOICE NOTE-1:
Baada ya kufanya utafiti wako katika mambo mbalimbali kuhusiana na biashara ya ufugaji wa kuku wa kuroiler sasa hivi utakuwa na taarifa za kutosha kuweza kuandika mchanganuo wako bila wasiwasi.
Leo tunajifunza vipengele vitatu (3) vifuatavyo;
1.
MUHTASARI
2.
MAELEZO
YA BIASHARA/KAMPUNI
3.
MAELEZO
YA BIDHAA
Jana kama utakumbuka nilisema huko mbele kila kipengele
tutakifafanua kwa undani zaidi nikimaanisha tuta ainisha vipengele vyake
vidogovidogo vinavyounda kipengele kikubwa.
1.0 MUHTASARI:
Unaweza mahali pengine ukakuta wameita Muhtasari Tendaji,
majina yote mawili ni sawa tu.
Katika Muhtasari kitu cha kustaajabisha kidogo ni kwamba,
ndiyo kipengele cha kwanza cha mchanganuo wa biashara lakini huwa kinaandikwa
mwishoni kabisa baada ya mtu kumaliza kuandika vipengele vingine vyote na hii
hutokana na sababu kwamba Muhtasari unabeba zile sehemu muhimu zote katika
andiko lako zima. Unachagua zile sentensi zenye uzito katika kila kipengele.
Mathalani katika mchanganuo wetu huu bunifu wa biashara
ya kuku wa kroiler katika muhtasari ni lazima pamoja na pointi nyinginezo
usiache kipengele kinachihusiana na ubunifu tutakaouweka katika hii biashara
Ni lazima Muhtasari wako umshawishi msomaji kwani mabosi
wengine mfano kwenye mabenki na taasisi mbali mbali za fedha hawana muda wa
kusoma andiko lako zima.
Kazi
kubwa za Muhtasari ni zipi?
1.
Kutoa picha kwa ufupi ya andiko lako
zima kwa kuangazia maeneo yote muhimu.
2.
Kumpa msomaji wa mpango wako uelewa wa
jumla wa kile unachotaka kumueleza kabla hata hajasoma andiko lenyewe zima
3.
Kumpa yule msomaji asiyekuwa na muda mwingi
wa kusoma mchanganuo wako wote ufupisho utakaomsaidia kupata zile pointi
muhimu.
Urefu
wa Muhtasari tendaji haupaswi................
2.0 MAELEZO
YA BIASHARA/KAMPUNI
Maelezo kuhusu Biashara au kampuni kwa kiasi kikubwa
yanahusu taarifa za ndani ya biashara zaidi kuliko kutoka nje ya biashara. Hapa
chini naorodhesha vipengele vidogo nitakavyozingatia wakati nikiandika
kipengele hiki kikubwa, kwa ujumla tutatoa maelezo kulingana na vipengele hivi
vidogo. Siyo lazima kuandika juu ya kila kipengele kwani itategemea biashara
inahitaji kitu gani, kama kitu hakina umuhimu hupaswi kukiweka
2.1 Dhamira kuu (mission)
2.2 Vision (Maono)
2.3 Malengo (Objectives)
2.4 Siri za mafanikio 2.5
Umiliki
2.6 Jina
2.7 Usajili
2.8 Kianzio
2.9 Eneo na vifaa
vilivyopo.
Aya ya kwanza inayoanza na namba “2.0 Maelezo ya
biashara/kampuni” huandiki chochote kwanza, panabaki wazi kwani ni muhtasari mdogo wa vipengele hivyo
vingine vidogo vidogo chini yake. Kumbuka
katika kila kipengele kikubwa ni vizuri kikawa na muhtasari wake mdogo ambao
baadae ndio unaokuja kuunganishwa na mihutasari kutoka vipengele vingine kuunda
Muhtasa Tendaji tulioona pale juu mwanzoni
“2.1
Dhamira kuu”
Dhamira
kuu ni ile biashara unayoifanya. Kwa mfano sisi hapa kwenye mpango huu wa
Kuroiler tumesema hivi;,
“CPPC Dhamira yetu kuu ni ................................................”
2.2
Maono
Maono ni picha ya biashara yako unayotaka uione baada ya
kipindi fulani kupita, mfano yakwetu hapa inasema hivi;
“Ku........................................................................................”
2.3 Malengo
Hapa tunataja vile vitu tunavyokusudia kuvitimiza baada
ya kutekeleza mpango wetu. Malengo mazuri ni lazima yawe halisi, yanayopimika,
yenye kutekelezeka na yaliyokuwa na muda maalumu wa utekelezaji. Hebu tuone
baadhi ya malengo ya CPPC hapa chini;
· Kuanza
na idadi ya kuku 300 chotara kwa ajili ya nyama na kisha kuja kuongeza kuku wa
mayai hapo baadae mtaji ukikua mwaka wa pili
·
Kuuza
.........................................................................
·
Kutoa
............................................................................
·
Kupata
...........................................................................
·
Kuhakikisha
....................................................................
2.4
Umiliki wa biashara
Hapa tunataja jina la biashara yetu ambalo ni CHOTARA
POULTRY PRODUCTION (CPPC), jina la mmiliki ambaye ni ..................................
Katika kipengele hiki kidogo, tutataja pia aina ya umiliki wa biashara ambapo
ni biashara ya mtu mmoja
2.5 Siri za mafanikio(Keys
to success)
Katika siri za mafanikio tutataja vile vitu ambavyo
biashara inatarajia kuvipa kipaumbele kusudi iweze kufanikiwa, vyaweza kuwa ni
kitu chochote kile na hapa sisi tumetaja vitu kama ...............................................................................
nk. vingine unaweza kusoma kweye mchanganuo wako.
2.6 Mchango katika jamii na
kwa uchumi wa Taifa
Hapa tumeelezea manufaa wanayoyapata watu mbalimbali
kutokana na biashara hii mfano ajira, kilimo kutokana na mbolea itakayopatikana
nk.
2.7
Eneo la Biashara
Unalitaja hapa mfano kwa upande wetu ni ...................................................
taja vitu muhimu kama ukubwa ni square meter ngapi za eneo, majirani
waliopakana, vitu muhimu kama shule, hospital ink vilivyo karibu na mradi vinavyoweza
kuchangia ukuaji au maendeleo ya biashara yako
2.7
Kianzio
Hii ni biashara mpya na hivyo tunatakiwa kuorodhesha kwenye
jedwali mahitaji yote tukianza na .......................... mfano .......................,
kisha ........................................ kama ............................................................................
Namba tutakazozitumia hapa zitatokana na utafiti ule tulioufanya pale mwanzoni
mfano ...............................................................
Baada ya kumaliza sasa tutarudi pale mwanzoni katika aya
tuliyoiacha wazi kwenye namba “2.0
Maelezo ya Biashara.” Ilipoanzia sura yetu hii. Tutachagua katika kila
kipengele kidogo tulichokwisha andika mstari mmojammoja au maneno muhimu na
kuyapanga katika hii aya kutengeneza muhtasari mdogo wa kipengele au sura
nzima.
Inaendelea..........................
3.0
MAELEZO YA BIDHAA / HUDUMA
Katika sura ama kipengele
hiki cha maelezo yanayohusu bidhaa au huduma, hapa unatakiwa utoe maelezo
yanayohusu kile kitu biashara yako inachouza.
Kwa biashara yetu hii ya
ufugaji wa kuku aina ya Kuroiler bidhaa zetu kubwa ni ..................................
Lakini pia unaweza kuuza hata ..................................................................
Kama ilivyo kwa vipengele
vingine vikubwa vinavyounda mpango mzima wa biashara, hiki nacho kina vipengele
vyake vidogovidogo kadhaa ambavyo ndivyo huunda sura nzima au kipengele kikubwa.
Vipengele hivyo vidogo ni hivi hapa chini;
3.1 Maelezo ya bidhaa/huduma
3.2 Utofauti/upekee wa bidhaa/huduma na za washindani
3.3 Vyanzo vya malighafi/bidhaa
3.5 Teknolojia
3.6 Bidhaa / Huduma za baadae
Kwahiyo maelezo yetu kwenye kipengele
hiki yanajikita katika mada hizo ndogondogo hapo juu. Hata hivyo siyo sheria
wala lazima kuweka vipengele vyote kwenye Sura yako, unaweka tu kipengele
unachoona kinafaa kulingana na mazingira ya biashara yako yalivyo lakini
angalao kuna vipengele kwa mfano “Maelezo yenyewe ya bidhaa/huduma" ni
lazima yawepo.
Kama tunavyoona kwenye
mchanganuo wetu huu wa kuku wa Kuroiler kwa ajili ya nyama, maelezo ya bidhaa
yanahusu .......................................................lakini pia,
wateja na bei ya ............................................ Kwa upande wa bidhaa
ya................................tumetaja wateja wake ni kina nani, kiasi cha bidhaa
itakayozalishwa na bei yake
Unaweza pia badala ya
kuelezea kla kipengele kidogo ukaandika maelezo mafupi tu (Muhtasari) kuhusiana
na bidhaa zako kama aya mbili au tatu hivi. Lakini katika maelezo hayo
hakikisha yanagusa sifa muhimu za huduma au bidhaa zako pamoja na upekee wake.
Hapa
ndiyo mwisho wa semina yetu kwa siku ya leo, tukutane tena kesho.
Asanteni sana kwa kusoma
Peter Tarimo
Ikiwa unahitaji semina hii nzima bado hujachelewa jiunge
leo hii kwa kulipia kitabu na mchanganuo wako wa Kuroiler sh. elfu 10 tu
kupitia namba zetu 0712202244 au 0765553030 jina Peter Augustino Tarimo kisha
ujumbe watsap au sms usemao “NATAKA SEMINA YA KUROILER NA OFFA YA VITU 6”
Kisha mara moja nitakutumia Kitabu chako cha Michanganuo
ya Biashara na Ujasiriamali kilichosheheni kila kitu mjasiriamali anachohitaji
kufanya biashara ya kisasa lakini pia nitakutumia michanganuo mbalimbali kama
ifuatavyo;
1.
Mchanganuo wa kuku wa nyama( Tumaini
Broilers)-kiingereza
2.
Mchanganuo wa kuku wa nyama (Tumaini) -kiswahili
3.
Mchangauo wa kuku wa mayai (Mayai Bora
Project)-kiswahili
4.
Mchanganuo wa Matikiti maji (Kibada
watermelon)-kiswahili
5.
Mchanganuo wa Mgahawa wa chakula (Jane
Restaurant)-kiingereza
6.
Mchanganuo wa Mgahawa wa chakula (Jane
Restaurant) -kiswahili
Kila siku masaa mawili mpaka matatu kabla ya kuanza
semina kwenye group maalumu huwa nawahi kwa madhumuni ya kuwafundisha kwanza
wale waliochelewa kuanza, haijalishi mtu ulichelewa muda gani lakini nakunoa
ili uweze kufikia viwango walivyofikia wenzako.
Staili niitumiayo ni kama ile iliyotumika na Napoleon
Hill kwenye kitabu chake cha THINK & GROW RICH katika kundi lake la
kushauriana(Master-Mind) na washauri wa kufikirika katika Sura ya 14 (MLANGOFAHAMU WA 6). Ukiisoma sura
hii vizuri utaelewa ni nini ninachojaribu kukielezea hapa.
SOMA NA HIZI HAPA PIA:
1. Gharama za ujenzi wa banda la kuku 100 chotara au kienyeji ni
shilingi ngapi?
2. Nina mtaji wa shilingi milioni moja (1000,000), naomba ushauri
nitafanya biashara gani?
3. Nguvu ya ajabu aliyotumia huyu mtoto unaifahamu?
4. Chapati biashara ya mtaji mdogo inayohitaji ujuzi mkubwa
5. BIashara ndogo ya mtaji wa 80,000/= niuze nini kupata faida ya haraka?
0 Response to "SEMINA YA MCHANGANUO WA KUKU KUROILER SIKU YA PILI: (MUHTASARI, BIASHARA & BIDHAA)"
Post a Comment