Kabla
hatujaendelea na semina yetu kwanza nikuombe sana radhi ndugu msomaji wangu kama
ulikuwa ukifuatilia mfululizo wa somo hili toka siku ya kwanza kutokana na siku
ya jana kushindwa kuweka somo kama tulivyoahidi.
Kulikuwa
na kuharibika kwa transofa maeneo yetu hivyo kwa siku nzima ya jana hadi leo
hii jioni nikashindwa kuwasha pc(compyuta) kwa ajili ya kuhamishia masomo kwenye
simu. Kwa hiyo siku ya leo nalazimika kuweka masomo ya siku 2 na kesho
tutamalizia kama kawaida sehemu ya mwisho.
Katika
siku hii ya 5 tutaandika Sura mbili, sura ya
6.
Mpango wa Uendeshaji na Sura ya
7.
Utawala
Tuanze
na sura ya 6;
6.0
Mpango wa Uendeshaji
Kwenye sura hii ya Utekelezaji kwa kawaida huwa inahusiana hasa na jinsi
biashara inavyofanya kazi(itakavyoendesha mambo mbalimbali) kila siku. Hapa
chini ni vipengele vidogo mbalimbali unavyoweza kuvitumia katika sura hii;
1.
Hatua mradi ulipofikia
mpaka sasa hivi
2.
Mchakato mzima wa
uzalishaji utakavyokuwa
3.
Teknolojia/maelezo ya
kiufundi
4.
Vihatarishi vya mradi
5.
Eneo
6.
Vifaa na gharama
mbalimbali
7.
Malighafi na vyanzo
vyake
8.
Masuala ya kisheria
9.
Sera ya mikopo nk.
Kwa upande wangu mimi kwenye mchanganuo huu wa USADO Milling
kama unavyoona nimechagua tu baadhi ya vipengele hivyo vidogo kulingana na
mahitaji ya biashara hii na nilielezea vitu vifuatavyo;
Mradi
ulipofikia
Nimetaja vitendo
mbalimbali muhimu vinavyotakiwa kutekelezwa ili mradi uweze kuanza na kila kimoja
nikaeleza kimefikia wapi mpaka sasa hivi. Unaweza kucheki katika mchanganuo huo
vitendo hivyo.
Vihatarishi
vya mradi
Biashara inaweza
ikakumbana na hatari au vikwazo mbalimbali ambavyo biashara nyingine mpya
hukutana nazo katika uchumi wa soko lenye ushindani mkali. Na ikiwa basi hatari
hizo hazitaweza kubainishwa na kushughulikiwa mapema basi biashara inaweza
ikafa muda mfupi. Katika Mchanganuo huu nimeainisha hatari kubwa 4, USADO
Milling inazoweza kukumbana nazo na jinsi ya kuzishughulikia.
Mahitaji
ya Kisheria
Katika kipengele hiki nimetaja taasisi mbalimbali USADO Milling
inazowajibika moja kwa moja kujisajili au kulipia tozo mbalimbali zinazotakiwa
na sheria ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Maelezo
ya Kiufundi.
Hapa nimeelezea Mifumo mikubwa 4 ambayo mahindi hupitia kabla ya
kupata dona safi na salama. Pia mambo mengine ya kiufundi niliyoainisha hapa ni
pamoja na uwezo wa mota ya mashine ya kusaga ambao ni Horse Power 40 saizi ya
kinu namba 100, kiasi cha umeme Kilowatts 29 kwa saa pamoja na taarifa
nyinginezo kama vile chanzo cha mashine hizo ambacho ni taasisi ya SIDO tawi la
Vingunguti Dar es salaam.
Eneo.
Hapa nimeelezea jinsi eneo walilochagua USADO Milling la Mbezi
mwisho lilivyokuwa la kimkakati kutegemeana na soko wanalolilenga na mikakati
yao kwa ujumla. Mambo mengine ya kiufundi niliyoyaelezea katika Sura hii ni
pamoja na;
· Uoshaji wa mahindi
· Ufungashaji unga
· Usambazaji
· Malighafi
· Vifaa na mashine
· Mapato na gharama mbalimbali
Na hapa ndio mwisho wa Sura ya 6 ya Mpango wa biashara hii ya
USADO Milling, Karibu kwenye Sura ya 7, “Utawala na Nguvukazi”
7.0
Utawala na Nguvukazi.
Kama kawaida Sura inaanza na muhtasari mdogo unaoandikwa
mwishoni na nitaacha kwanza nafasi ya aya moja hivi. Halafu nitazingatia
vipengele vidogo vinavyounda sura hii ambavyo mara nyingi huwa ni hivi hapa
chini;
7.1
Mfumo wa uongozi
7.2
Timu ya uongozi na wafanyakazi
7.3
Mpango wa mishahara
Mimi nilianza na kipengele kifuatacho;
7.1
Muundo wa Utawala
Hapa nimeelezea kwa maneno tu na siyo kuchora chati ya utawala
kwa kuwa timu ya wafanyakazi wa USADO Milling bado ina watu wachache. Nimetaja
kila kiongozi, wadhifa wake kwenye kampuni, historia yake kitaaluma na kikazi
pamoja na uzoefu aliokuwa nao kulingana na majukumu atakayokuwa nayo kwenye
kampuni.
7.2
Pengo la Utawala:
Hapa nimeelezea mapungufu yaliyopo katika nafasi mbalimbali za
kiuongozi na kiutendaji. Ni nafasi gani zinahitajika kujazwa na ni lini nafasi
hizo zitajazwa. Pia nimeeleza njia mbadala zitakazotumika ili kujaza pengo
lililopo.
7.3
Mpango wa Mishahara
Katika kipengele hiki kidogo nimeanza na maelezo kisha nikachora
jedwali linaloonyesha kiasi cha mishahara ya wafanyakazi wote kwenye kampuni
kwa kila mwaka kwa miaka yote mitatu. Nilianza kwa kujumlisha mishahara ya
mfanyakazi mmoja mmoja kila mwezi kisha kwa mwaka. Namba hizi nitakuja kuzitumia
pia kwenye ripoti ya Faida na Hasara hapo baadae
Na hapa ndio mwisho wa Sura ya 7 ya Uongozi au Utawala. Sura
inayofuata ni Sura ya Fedha.
SEMINA SIKU-4 SEMINA SIKU-6
SEMINA SIKU-4 SEMINA SIKU-6
0 Response to "SEMINA SIKU YA 5: MCHANGANUO WA BIASHARA YA KUSAGA UNGA WA DONA-HATUA KWA HATU"
Post a Comment