Duka la rejareja la mama yangu linanifunga, nashindwa kujipangia malengo yangu binafsi | JIFUNZE UJASIRIAMALI

Duka la rejareja la mama yangu linanifunga, nashindwa kujipangia malengo yangu binafsi


Mama yangu akiwa dukani kwake akiuza
Wiki hii tumefululiza safu ya Ongea na mshauri na lengo langu ni kuhakikisha nayajibu maswali yote ya wadau niliyoyaweka kiporo ndani ya wiki hii. Msomaji mwingine jina lake kwa kifupi O.S aliuliza swali lake kama ifuatavyo; 

Kaka mi n mfanya biashara ya duka la vyakula Ila c biashara yngu n ya mama angu... Ndoto yngu Ni kuwa mfanya biashara Na kutengeneza utajiri kupitia biashara Ila tatizo nililokuwa nalo nashindwa jinsi ya kuweka Malengo yngu binafsi Na hii biashara nnayofanya... Naomba msaada wako kwenye hili kaka


Hellow Mr. O.S,

Mahali popote pale unaweza ukajiwekea malengo bila kujali ni biashara ya kwako, ya mtu baki au ya ndugu wa karibu kama mama yako. Nadhani tatizo kubwa hapo unahisi kwa vile biashara ni ya mama, basi huwezi ukajiwekea malengo, ni kama vile anakubana hivi nk. Lakini nikuambie haipaswi kuwa hivyo. 

SOMA: Biashara ya mitindo ya nguo za kiume na viatu inavyoweza kukutajirisha.

Wewe kaa na mama yako mwelezo malengo  yako ni yapi, kisha mpange mkiwa wawili unataka baadae ufanye nini nk. Weka muda maalumu utakaokaa katika biashara hiyo pamoja na malipo unayotaka biashara hiyo ikulipe. Ukweli kwamba biashara ni ya mama yako hauwezi kukufanya usidai malipo kama mtu baki ilimradi tu yaendane na uhalisia wa biashara yenyewe, ule ukaribu wako na mama usikubali ufanye kazi bila malipo, biashara na undugu ni vitu 2 tofauti kabisa. Hebu tengeneza mazingira kama vile unafanya biashara na mtu baki kabisa na siyo mama yako.

Na hii itasaidia biashara hiyo pia kukua kwani utakuwa na nidhamu huku ukijua unalipwa kama mtu mwingine yeyote yule baki. Ni kwa njia hiyo tu utaweza ukajiwekea malengo na si vinginevyo huku pia malengo ya mama yako katika hiyo biashara nayo yakitimia bila kuathiriwa kwa namna yeyote ile.

SOMA: Je,unajua biashara yenye faida kubwa na ya haraka mara mbili ya mtaji utakaowekeza?

Malengo yeyote yale yanahitaji pesa(fund) sasa utatimizaje malengo yako pasipo kuwa na fedha? Ukiisimamia vizuri hii biashara ya mama yako nayo ikakulipa vizuri hatimaye utaweza ukaja kutimiza malengo yako mengine ya kimaisha baadae kwa urahisi zaidi kwani utakuwa na fedha za kufanya hivyo.

Bila shaka yeyote ile mama yako ndiyo mtu wa kwanza kabisa katika maisha yako anayependa ufanikiwe, hivyo na wewe usikubali kumwangusha, akijua una malengo ya kufika mbali sidhani kama atapenda usiyatimize, lakini ni kwa njia ya kuiboresha biashara hiyo kwanza ndipo mambo mengine yataweza kunyooka na siyo vinginevyo.

Kijana akiwaza na kuwazua juu ya maisha yake ya baadae


Hata ikiwa kwa mfano duka hilo halitaleta fedha za kutosha kugharamia mipango yako mingine kama utakavyotaka, lakini angalau fanya kwa uaminifu na kwa kujituma kwanza, muda ndio utakaosema wenyewe kwani itafika mahali kama hakieleweki utamwambia mama "Mother, mimi naona bwana nikahangaike kwingine, tutafute utaratibu mwingine wa kusimamia hili duka" Hapo mama atakuelewa na atakupa baraka zake zote na hata kusapoti chochote kile utakachokwenda kukifanya mbele ya safari yako.

SOMA: Biashara ya urembo inalipa, ni ya pili kutoka haraka baada ya chakula, ni fursa kubwa!

Inawezekana wewe ndoto yako si kuuza duka la vyakula la rejareja, labda ndoto yako ni kufanya biashara ya duka la nguo za mitumba na spesheli au umejiwekea malengo ya kwenda kufanya biashara ya urembo, tena uimiliki mwenyewe. Au hata umepanga kujiendeleza zaidi kimasomo nk. Malengo haya yote utaweza kuyatimiza tu endapo utakuwa na subira na uvumilivu wa kutosha, kumbuka duniani hakuna biashara yenye faida ya haraka haraka bila kwanza kuweka misingi imara.

Asante, natumaini majibu haya yatasaidia. 
............................................................

Kwa vitabu vyako Bora kabisa kutoka self help books Tanzania tembelea, SMARTBOOKSTZ

Kupata masomo ya fedha na michanganuo kila siku Whatsapp, karibu ujiunge na group la Michanganuo -online, 0765553030 kwa kiingilio cha sh. 10,000/= mwaka mzima.

2 Responses to "Duka la rejareja la mama yangu linanifunga, nashindwa kujipangia malengo yangu binafsi"

  1. Mimi natamani sana kufanya biashara lakin sina mtaji nisaidieni wenye mitaji mikubwa hata Mimi natamani niwe mfanya biashara mkubwa,napenda sana lakin mtaji sina.Muwezeshe mwanamke kwa ukombozi wa jamii nzima

    ReplyDelete
  2. Mimi natamani sana kufanya biashara lakin sina mtaji nisaidieni wenye mitaji mikubwa hata Mimi natamani niwe mfanya biashara mkubwa,napenda sana lakin mtaji sina.Muwezeshe mwanamke kwa ukombozi wa jamii nzima

    ReplyDelete