SOMO LA 5: MAELEZO YA BIASHARA AU KAMPUNI | JIFUNZE UJASIRIAMALI

SOMO LA 5: MAELEZO YA BIASHARA AU KAMPUNI


2.0 MAELEZO YA BIASHARA/KAMPUNI
Katika sehemu hii kuna vitu muhimu vinavyohitaji kuelezewa baada ya Dhamira kuu, maono na malengo ambavyo ni;
·       Utambulisho kamili wa biashara(inaitwaje?)
·       Umiliki wa biashara na mfumo wake kisheria
·       Historia ya biashara /kampuni na mahesabu ya nyuma kama biashara ni ya zamani, lakini kama ni mpya basi utaelezea mahitaji na vyanzo vya mahitaji hayo.
·       Eneo la biashara na vifaa vilivyopo pale kama vile majengo, ardhi, samani nk.

Kabla hujaanza acha nafasi kidogo kwa ajili ya aya moja ya muhtasari wa sura nzima ambao utatakiwa kuuandika mwishoni. Kuna michanganuo mingine kwa mfano hata ile iliyopo katika kitabu cha MICHANGANUO, utakuta vitu hivi vinne, Dhamira kuu, Malengo, Siri za mafanikio na hata wakati mwingine Maono yanafuata baada tu ya Muhtasari, halafu katika sehemu hii ya Maelezo ya biashara/kampuni, inabakia tu na maelezo yanayohusu umiliki kisheria, historia ya biashara, mahitaji, vyanzo vya mahitaji pamoja na eneo biashara ilipo. Kuweka vitu hivyo baada ya dhamira kuu au katika sehemu hii ya biashara hakuna athari yeyote.

2.1 Dhamira kuu.
Weka dhamira yako kuu hapa, dhamira kuu ni ile biashara unayoifanya kwa mfano biashara ya mgahawa unaweza ukasema hivi, “dhamira yangu kuu ni kutoa huduma bora ya chakula na vinywaji baridi kwa wakazi wa mji au eneo fulani”


2.2  Maono
Hapa weka kauli inayoelezea biashara yako itakuwaje baada ya kipindi tuseme labda ni miaka mitatu, mitano au kipindi kingine chochote kile ulichopanga. Kwa mfano unaweza ukasema maono ya biashara yako ya mgahawa ni, “kuwa na mgahawa mkubwa zaidi jijini Dar es salaam”

2.3 Malengo.
Taja vitu unavyokusudia kuvipata kutokana na biashara baada ya kutekeleza mpango wako. Vitu hivyo vinaweza vikawa, mauzo, faida, idadi fulani ya wateja, idadi ya wafanyakazi, au kitu kingine chochote. Kwa mfano unaweza ukasema moja kati ya malengo yako ni “kuwa na wafanyakazi watano baada ya mwaka mmoja”, au “kufikisha mauzo ya shilingi milioni hamsini mwishoni mwa mwaka wa tatu” nk.

2.4  Siri za mafanikio
Taja vitu vya pekee vinavyoifanya biashara yako ifanikiwe. Kila biashara ina vitu vinavyoifanya ifanikie kwa mfano utakuta biashara ya maduka mengi ya rejareja hufanikiwa zaidi yanapowekwa eneo zuri lililokuwa na watu wa kutosha, hivyo utasikia watu wakisema siri ya mafanikio ya duka ni eneo. Siri za mafanikio zaweza kuwa pia ni ubora, huduma nzuri kwa wateja, mtaji wa kutosha au kitu kingine chochote kinachoifanya biashara yako ishamiri zaidi ya vingine na unaweza ukataja zaidi ya kimoja.


2.5 Umiliki wa biashara
Katika kipengele hiki kidogo, taja jina la biashara na mmiliki wake au wamiliki kama ni zaidi ya mmoja ukielezea na aina ya usajili kisheria wa biashara hiyo kama ni ya mtu binafsi, ubia au kampuni.

XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX 

Soma somo zima, kwa njia 3, PDF, Sauti MP3 na kupitia njia ya e-mail. Unachotakiwa kufanya ili kupata masomo haya yote ni kulipia Semina shilingi 10,000/= tu, tuma na email yako au kama umejiunga kupitia blogu ya jifunzeujasiriamali kupata vitabu bila malipo basi huna haja ya kutuma tena anuani yako ya email. Kwa maelezo zaidi tuwasiliane kwa namba 0712 202244  au  0765 553030



 somo la 4                                                                                 
                                             
                   

0 Response to "SOMO LA 5: MAELEZO YA BIASHARA AU KAMPUNI"

Post a Comment