JINSI YA KUJIUNGA NA MASOMO YA SEMINA YA KUANDIKA MICHANGANUO YA BIASHARA | JIFUNZE UJASIRIAMALI

JINSI YA KUJIUNGA NA MASOMO YA SEMINA YA KUANDIKA MICHANGANUO YA BIASHARA

Kujiunga na semina za michanganuo ya biashara
Ndani ya darasa letu la WHATSAP na CHANNEL YA TELEGRAM la MICHANGANUO-ONLINE -MASTERMIND-GROUP tunajifunza kila siku masomo yenye maudhui ya pesa pamoja na Semina za mara kwa mara kuhusiana na uandishi wa Michanganuo ya Biashara za Kitanzania zilizo na fursa kubwa ya kuzalisha faida.

Kujiunga na Darasa hili, mwanachama hulipia kiingilio cha mwaka mzima (niezi 12) shilingi elfu 10 tu na tunampatia baadhi ya vitabu na Michanganuo ya biashara kwa ajili ya rejea wakati wa kujifunza.  

Darasa hili limeanzishwa mahsusi kwa lengo la kuhakikisha wale wote wanaonunua kitabu cha MICHANGANUO YA BIASHARA NA UJASIRIAMALI kwa lengo la kusoma michanganuo mbalimbali ya biashara pamoja na kujifunza namna ya kuandika michanganuo ya biashara zao wanapata fursa ya kuwa karibu zaidi na wakufunzi wa somo hili ikiwa ni pamoja na kuuliza maswali yanayowatatiza na mwisho kuhakikisha wanaandaa mipango ya biashara wanayoitaka wao wenyewe wakipewa usaidizi kila wanapokutana na ugumu wowote ule.

Katika maisha ya biashara na pesa ipo siku unaweza kujikuta unauhitaji mpango wa biashara. Hata kama hutahitajika kuandika mwenyewe lakini kuna wakati unaweza ukatakiwa labda na benki au taasisi yeyote ile ya fedha uwasilishe mpango wa biashara yako.  Sasa utakapokwenda kwa mtaalamu akuandikie unatakiwa angalao uwe na uelewa wa msingi juu ya mpango wa biashara ndipo mtaalamu aweze kukuandikia mchanganuo mzuri baada ya kukuhoji maswali kuihusu biashara yako.

Si hivyo tu kuna sehemu nyingine huwa wanahitaji upeleke mpango/mchanganuo wa biashara yako na kuuwasilisha mwenyewe kwa mdomo wako. Hivyo ni muhimu sana mtu yeyote uliyekuwa na ndoto za kuja kuwa mfanyabiashara na mjasiriamali mkubwa kujifunza walao hata kwa kusoma tu jinsi ya kuandaa mpango wa biashara na namna mipango yenyewe halisi inavyokuwa.


Lakini faida kubwa zaidi pengine kushinda zote za mtu kufahamu michanganuo ya biashara ni ile ya kuendesha biashara yako vizuri kwa ufanisi, unapofahamu namna ya kupanga biashara yako unazidisha uwezekano wa mafanikio katika biashara hiyo. Faida haipo kwenye mchanganuo wenyewe kama kurasa na maandishi hapana, bali ipo kwenye mchakato mzima wa kufikiria kwani MPANGO WA BIASHARA ni kila kitu kinachohusiana na biashara kuanzia wazo lenyewe la biashara mpaka unapofikia hatua ya kupata faida.

Kwa hiyo kile kitendo tu cha kukaa na kuifikiria biashara yako, mwanzo mwisho namna utakavyoiendesha ni mchanganuo tosha wa biashara hata pasipo kuchukua kalamu na karatasi. Ndiyo maana nasisitiza kuwa unaweza kujifunza michanganuo ya biashara hata kama hupendi kuiandika na hilo linatosha wewe kuendesha biashara yako vizuri kimkakati.

Ukiwa mwanachama wa Group hili unapata fursa ya kuuliza swali lolote lile  kuhusiana na Michanganuo na Ujasiriamali kwa ujumla lakini pia  kupewa usaidizi kwenye kuandaa mpango wa biashara utakayo. 

Namba za kulipia ada sh. elfu 10 ni  0765553030  au 0712202244 jina ni Peter Augustino Tarimo. Na baada ya ,alipo Tuma ujumbe ukisema; 

"NIUNGANISHE NA MASTERMIND-GROUP LA MICHANGANUO-ONLINE"


*TUNATOA PIA HUDUMA YA KUANDIKA MICHANGANUO YA BIASHARA ZA AINA ZOTE KWA GHARAMA RAFIKI*



8 Responses to "JINSI YA KUJIUNGA NA MASOMO YA SEMINA YA KUANDIKA MICHANGANUO YA BIASHARA"

  1. ninashukuru kwa msaada wa mawazo mazuri kwani inatufungua kuwa na maono ya mbali kutoka ki biashara

    ReplyDelete
    Replies
    1. Tunashukuru pia kwa mrejesho wako mzuri na tunaahidi kuendelea kuwaletea mambo mazuri zaidi siku za usoni

      Delete
  2. Inachukua Muda gani mpaka kuunganishwa

    ReplyDelete
  3. Nimependa somo kwanza nifanye mpango wa kujiunga

    ReplyDelete
    Replies
    1. Unakaribishwa sana Mdau wetu, njoo tujifunze ujasiriamali na mambo ya fedha.

      Delete