DUKA LINALOJIUZA LENYEWE BILA MHUDUMU/MUUZAJI | Jifunzeujasiriamali

DUKA LINALOJIUZA LENYEWE BILA MHUDUMU/MUUZAJI

Duka la kjadi linalojiuza lenyewe bila mhudumu

Baada ya kuchambua Mifumo yote Duniani ya usimamizi wa duka la rejareja Kianalojia & Kidijitali katika kitabu hiki cha Siri ya Mafanikio ya Biashara ya Duka la Rejareja New Tech Edition2026, hatimae niliona si busara kuacha mfumo huu wa asili / mfumo wa kijadi / kitamaduni ulioasisiwa hapahapa kwetu Tanzania 

Kuna wengine wanaweza kuuita “mfumo unaotumia nguvu za giza” lakini mimi nakataa kwani hamna ushahidi wa wazi. Ijapokuwa  wenyewe wahusika ukiwauliza wanakujibu ni Nguvu za Kimungu hutumika, utafiti nilioufanya kwa muda mrefu umebaini vinginevyo kabisa (No research, No right to speak) nimeeleza nilichogundua baada ya utafiti wa kina wa kisayansi

Habari hizi za kustaajabisha kuhusiana na Biashara hasa Maduka ya rejareja na Magenge yanayojiuza yenyewe pasipo kuwa na muuzaji/mhudumu “zimetrend” zaidi huko Kanda ya Nyanda za juu Kusini mikoa ya Iringa, Njombe na Makambako

Mmiliki wa duka au genge hufungua biashara yake asubuhi na mapema kama kawaida kisha akishapanga bidhaa na kufanya usafi huondoka kuelekea kwenye mihangaiko yake mingine huku nyuma akiacha duka /genge wazi na wateja wakifika hujihudumia wenyewe na hata pesa kuna bango dogo juu ya Birika kubwa lililoandikwa, “UKISHACHAGUA BIDHAA TIA HELA HUMU KWENYE BIRIKA”

Kuna maduka mengine mmiliki hajawahi kabisa kuweka mlango au grili, na inapofika jioni huweka tu pazia jepesi mlangoni mtu analoweza kuingia kwa urahisi na huondoka kwenda kulala nyumbani kwake pasipo mwizi yeyote kuja usiku kumuibia. Haya ni matukio ya kweli siyo hadidhi za kutunga

Je watu hawa hutumia nguvu gani kulinda stoku ya bidhaa zao na fedha kwenye haya maduka?, hawatumii daftari la mauzo, POS wala Accounting Software yeyote kama nilizoeleza kwenye kitabu hiki lakini maduka yao yana “operate” kama kawaida

Nimechambua na kueleza A-Z kilichojificha nyuma ya pazia la Mfumo huu wa ajabu wa kijadi wa usimamizi wa duka au genge katika Sura ya 6 ukurasa wa 233, Toleo jipya la Kiteknolojia la kitabu “SIRI YA MAFANIKIO YA BIASHARA YA DUKA LA REJAREJA NEW TECH EDITIO 2026”

Bei ya kitabu ni sh. 15,000/= lakini kuna OFFA ya Sh. 10,000/= kwa watu wachache wa mwanzo

Kukipata lipia 10,000/=  kwa namba 0761002125 jina Peter Augustino Tarimo, kisha nitumie ujumbe na nitakutumia link ya kitabu na Coupon yako ya punguzo muda huohuo ukipakue

Ikiwa hujaamua kununua sasa hivi, bado pia kuna zawadi ya kitabu kingine cha bure (HATUA 10 ZA KUANZISHA DUKA LA REJAREJA) unaweza kukipata ndani ya Group la Wafanyabiashara za Rejareja Tanzania (TRG) kwa link hii hapa chini, ukiingia tu hivi unakutana na kitabu

https://chat.whatsapp.com/HNuS5F506Hp5Kt6f0CLLVd?s=cl&p=a&mlu=3


0 Response to "DUKA LINALOJIUZA LENYEWE BILA MHUDUMU/MUUZAJI"

Post a Comment