Forever free POS & CRM
ni mfumo
maalumu wa bure kwa asilimia 100%
kwa matumizi ya msingi ya biashara za rejareja.
Inafanya kazi vizuri sana kwenye simu za mkononi, tablets
(Android/iOS) na hata katika kivinjari cha kompyuta za kawaida za mezani.
Inakusaidia kurekodi mauzo, kusimamia bidhaa, na kuona ripoti za faida &
hasara
Ingawa mfumo huu unafanya kazi vizuri sana kwenye
biashara ya duka la rejareja maarufu kama “Maduka
ya Mangi” lakini pia unaweza kutumiwa na biashara nyingine zote za rejareja
mfano, Genge la matunda na mbogamboga, kioski, baba na mama lishe, migahawa,
saluni, uuzaji wa nguo, vifaa vya kielektroniki, hardware, maduka ya dawa,
mabucha, biashara ndogondogo za sokoni na hata biashara za kuuza bidhaa za
rejareja mtandaoni
Sifa na Faida kubwa za Mfumo huu kwa biashara za
Rejareja
·
Usimamizi wa Mauzo (POS):
Unabadilisha simu au tablet yako kuwa mashine ya kusajili mauzo, risiti, na
kupokea malipo mbalimbali
·
Uwezekano
wa kutumia kotekote, kwenye simu ya mkononi, tablet na kompyuta ya kawaida
ya mezani
·
Udhibiti kikamilifu wa bidhaa (Stoku):
Unafuatilia kiwango cha bidhaa zilizobaki dukani kwa muda halisi (real-time) na
unapokea taarifa bidhaa zikiwa zinakaribia kuisha (alert) ili uagize nyingine
·
Kudhibiti Wafanyakazi: Unaweza
kuona nani ameuza nini, kwa muda gani, muda wa kuingia na kutoka pamoja na ni kiasi
gani cha fedha kilichopo kwenye droo
·
Ripoti za Biashara: Unatoa
ripoti za kina kuhusu faida, bidhaa zinazouza zaidi, na mwenendo wa mauzo ya
kila siku au kila mwezi
·
Uwezo wa
kurekodi Matumizi (Expenses) ya kila siku kwa ajili ya kujua Faida
halisi inayopatikana au Hasara katika kipindi chochote utakacho mfano lisaa au
siku
·
Kutunza Kumbukumbu za Wateja:
Inarekodi namba zao za simu na madeni yao kwa urahisi
·
Huduma ya Wateja (Loyalty):
Inakuruhusu kusajili wateja na kuwapa pointi za zawadi ili kuwahimiza kurudi
tena
·
Ni wa bure daima: Tofauti na mifumo mingi ya nje
na ndani ya Tanzania ambayo hukupa kipindi kifupi tu cha majaribio labda siku
10 mpaka 40, ForeverFree POS & CRM hauna kabisa kipindi cha majaribio na ni
bure daima!
Hatua na Jinsi
ya kuanza kuutumia mfumo wa ForeverFree POS & CRM
(1) Pakua app/programu
ya ForeverFree POS & CRM
(2) Jisajili
kwa akaunti ya bure kwenye tovuti au moja kwa moja kupitia app yako
(3) Ingiza
orodha ya bidhaa zako (Inventory), bei zake, na picha za bidhaa
(4) Anza
kufanya mauzo na kufuatilia biashara yako kupitia simu au kompyuta/laptop yako
Mafunzo hatua kwa hatua ya
jinsi ya kutumia mfumo huu yameanza rasmi leo katika kundi la whatsapp & Telegram
la Tanzania Retailers Whatsapp Premium
Group (TRPG)
Ikiwa unahitaji kutumia
mfumo huu kwenye biashara yako pasipo kuwa na malipo yeyote ya mwezi wala ya
mwaka na kutimiza mahitaji yote ya msingi kwa biashara ndogo au ya kati,
unaweza kuwasiliana na mimi nikupe utaratibu wa kujiunga na mafunzo hayo rahisi
mara moja
Mafunzo yote utayakuta ndani
ya group kuanzia somo la kwanza mara tu uingiapo
Mafunzo hayachoshi, si
marefu na wala huhitaji kuwa mtaalamu wa IT ndipo uelewe, unaweza kuchukua siku
1 mpaka 2 tu kujua kuutumia mfumo kikamilifu
Mawasilinao tumia kiungo kifuatacho au unaweza kunitumia ujumbe wa “ForeverFree” kwa namba 0761002125
Jiunge na group la mafunzo hapa

0 Response to "MFUMO MPYA WA BURE WA KUSIMAMIA BIASHARA YA DUKA LA REJAREJA (Forever Free POS & CRM)"
Post a Comment