RIPOTI YA USOMAJI THINK & GROW RICH AWAMU YA PILI (PAGE 9 – 18 / UKURASA.17 – 37) SURA YA 1 | JIFUNZE UJASIRIAMALI

RIPOTI YA USOMAJI THINK & GROW RICH AWAMU YA PILI (PAGE 9 – 18 / UKURASA.17 – 37) SURA YA 1

 

Ripoti awamu /session 1

RIPOTI YA USOMAJI KITABU THINK & GROW RICH-AWAMU/SESSION- 2 (SURA YA 1)

 

English version:

Chapter 1:  INTRODUCTION

THE MAN WHO “THOUGHT” HIS WAY INTO PARTNERSHIP WITH THOMAS A. EDISON

 

Nakala ya kiswahili:

SURA YA1: Utangulizi

MTU ALIYEFIKIRI NJIA YAKE KUWA MBIA NA THOMAS A. EDISON

Katika Sura hii ya kwanza Mwandishi anaanza kwa kueleza jinsi ilivyokuwa kweli kwamba ‘FIKRA au MAWAZO ni vitu halisi’ na ni vitu vyenye nguvu pale vinapochanganywa na nia thahiri, msimamo na shauku kubwa katika kuvigeuza kuwa utajiri ama vitu vingine vinavyoweza kushikika

Tutaona mfano wa kwanza kabisa atakaoanza nao kuthibitisha kauli hiyo ni habari ama hadithi ya mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Edwin C. Barners. Bwana huyu siku nyingi sana alikuwa akigubikwa na shauku kubwa ya kutaka kuwa mbia na mgunduzi maarufu wakati huo aliyejulikana kama Thomas Edison.

Akiwa na ndoto yake hii kubwa kumbuka hakuwa na chochote kile mfukoni wala hakuna mtu aliyekuwa anamjua achilia mbali connection yeyote ile ambayo labda ingeliweza kumfanya akutane na mgunduzi huyo. Kitu pekee alichokuwa nacho kichwani mwake ni hilo wazo na shauku kali ya kutaka kuitimiza ndoto hiyo

Sasa alifanyafanyaje mpaka ndoto yake ikaja kuwa kweli, tafadhali sana hebu tujumuike pamoja kusoma kurasa hizi 10 leo.

Alipoona hana jinsi mwishowe aliamua kusafiri kwa treni la mizigo mpaka mji aliokuwa akiishi Thomas Edison kuliko kukosa kabisa kwenda. Aliwasili katika maabara ya Bwana Edison na kutangaza kwamba alikuwa amefika pale kuingia ubia wa kibiashara na Mgunduzi 

Miaka kadhaa baadae Bwana Thomas Edison mwenyewe katika mkutano mmoja na Edwin C.Barnes akiwemo alikuja kukiri kwamba alimpatia fursa ile Barnes kutokana na dhamira yake ya dhati ya kukipata kile alichokuwa akikitaka na alitamka maneno yafuatayo;

Nilikuwa nimejifunza kutokana na uzoefu wa miaka mingi na watu kwamba, mtu anapotamani sana kitu kiasi cha kuweka rehani mustakabali wake mzima wa baadaye kwa ajili ya kukipata, bila shaka atakuwa na uhakika wa kufanikiwa kukipata”

Kitu kilichokuja kubadilisha maisha ya Edwin C. Barnes moja kwa moja na ndoto yake kutimia akatoboa baada ya kufanya kazi za chini kwa bosi wake huyu muda mrefu ni chombo kipya cha sauti alichokuwa amekigundua Edison wakati huo ambacho hata leo hii tunakiita Earphone ama Ediphone.

Tukio hili lilikuja kama fursa iliyokuwa imejificha katika sura ya jambo lisilowezekana kabisa kwani kila mtu wakiwemo watu wote wa mauzo kwenye kampuni ya Edison walikuwa wakisema kwamba chombo kile cha ajabu kisingeliweza kuuzika kirahisi sokoni

Lakini mwanaume Edwin C. Barnes akajisemea moyoni, “hapahapa sitakubali, hapa ndipo fursa yenyewe ilipo”. Yeye aliamini kabisa mashine ile ya ajabu ingeliwe kuuzika bila wasiwasi wowote sokoni na kazi ikaanza rasmi......

FUTI TATU TU KUTOKA DHAHABU ILIPO

Katika sura hii pia kuna hadithi nyingine ya  FUTI TATU TU KUTOKA DHAHABU ILIPO” ambapo mwandishi anaeleza kisa cha watu wengi kuwa masikini kwa sababu tu ya kukata tamaa hata pale ambapo kumbe ilikuwa imebakia kidogo tu watoboe.

Habari hii inamhusu mjomba wake Bwana mmoja aliyeitwa R. U. Darby aliyekumbwa na “Homa ya dhahabu” kipindi cha mfumuko wa machimbo ya dhahabu huko Marekani na akaenda Magharibi kuchimba ili aweze kutajirika.

Lakini kilichotokea ni kwamba baada ya kuchangisha pesa kutoka kwa ndugu jamaa na marafiki kwa ajili ya ufadhili wa mradi ule na wakaingia mgodini kuchimba hatimaye yeye na mjombake walikata tamaa na kuuza ule mgodi kwa Muokota makopo mmoja mjanja ambaye alikuja kutajirika muda mfupi tu baada ya wao kurudi nyumbani.

Kumbe kipindi wanakata tamaa ilikuwa imebakia kama futi tatu tu wakutane na mwamba wenye dhahabu ya kutosha!

SOMO LA SENTI 50 KATIKA KUWA NA MSIMAMO

Stori nyingine ni hii ambayo pia inamhusu huyuhuyu Bwana Darby na mjomba wake pamoja na mtoto mdogo mweusi wa mpangaji wao. Baada ya kurudi kutoka machimboni walikoanguka vibaya,  Darby na mjombake maisha yaliendelea na mjomba kwa bahati nzuri alikuwa akimiliki shamba kubwa ambalo ndani yake kulikuwa na wapangaji wakati huo wengi wakiwa ni Waafrika weusi maskini

Siku moja Darby na mjombake wakiwa kwenye kinu cha kusagia nafaka wanapiga kazi, ghafla akaja mtoto wa mpangaji mmoja na kumjulisha mjomba kuwa mama wa mtoto huyo alikuwa na shida na aliomba apatiwe senti 50 tu. Lakini mjomba alikataa katakata na kumtaka yule mtoto aondoke mara moja kurudi kwa mama yake.

Hata hivyo mtoto alionyesha ung’ang’anizi wa ajabu na katu hakukubali kuondoka pale mpaka mjomba akatishia kumchapa bakora. Mwishowe mjomba mwenyewe alichoka akaingiza mkono mfukoni na kuchomoa senti 50 akampatia yule mtoto akaenda zake.

Sasa ni nguvu gani hii ya ajabu iliyoyeyusha moyo wa yule mjomba hata akaahirisha kumchapa yule mtoto bakora na kumtimizia kile alichokitaka? nguvu hiyo utaenda kuijua ukisoma hiki kitabu mpaka mwisho.

Bwana Darby miaka mingi baadae alikuja akawa mfanyabiashara mkubwa sana wa kuuza bima na katika maisha yake ya biashara mafunzo haya mawili aliyoyapata moja akiwa na mjomba wake kwenye machimbo ya dhahabu na la pili akiwa na mjombake kwenye kinu cha kusaga nafaka ambapo mtoto mweusi wa mpangaji alimtia mjomba adabu yalimsaidia sana, yalimwezesha hatimaye apate naye mafanikio makubwa kwenye biashara hii ya kuuza bima licha ya mapigo hayo 2, na hadidhi hii alimsimulia Napoleo Hill katika eneo lilelile kilipokuwa kinu cha kusaga nafaka zamani.

Napoleon anaendelea kutuambia kuwa, maisha ni ya ajabu, na mara nyingi hayafikiriki! Vyote, kufanikiwa na kuanguka vina mizizi yake katika uzoefu wa vitu rahisi kama hadithi hizo mbili za Darby na mjombake zilizosimuliwa hapo juu.

Utajiri huanza na hali ya akili, pamoja na udhahiri wa lengo, huku kukiwa na kazi kidogo sana au hata kutokuwa na kazi ngumu kabisa. Wewe na mtu mwingine yeyote, mnapaswa muwe wenye kuvutiwa na kufahamu jinsi ya kuwa na hali ya akili inayovutia utajiri.

Mara unapozielewa vizuri kanuni za falsafa 13 zilizoandikwa humu kwenye hiki kitabu na kuzitia kwenye matendo hali yako kifedha itaanza kuimarika. Kila kitu utakachogusa kitaanza kugeuka chenyewe kuwa rasilimali kwa faida yako na neno HAIWEZEKANI kwako litakuwa halipo kabisa

Mafanikio huja kwa wale wenye kufikiria mafanikio.

Kuanguka huja kwa wale ambao pasipo kujali hujiruhusu wenyewe kufikiri kuanguka. Lengo la kitabu hiki ni kuwasaidia wale wote wanaotaka kujifunza stadi za kubadilisha mawazo yao kutoka kufikiria maanguko kuwa katika kufikiria mafanikio.

SIRI YA MAFANIKIO YA HENRY FORD

Mwandishi anaelezea habari nyingine kumhusu Mgunduzi wa magari Bwana Henry Ford ambaye nyakati fulani hivi akiwa amebuni injini ya gari lake aina ya V-8 Motors, alichagua kuunda injini yenye silinda zote 8 ndani ya bloku moja lakini mainjinia wake (wahandisi) walimkatalia katakata kuwa isingeliwezekana, hata hivyo Ford hakuwakubalia pia kirahisi akawataka ni lazima waunde ile injini piga ua! Na mwishowe kweli kama mazingaombwe iliwezekana, dhamira ya Ford ikawa imeshinda!

Henry Ford amefanikiwa kwa sababu anafahamu na kuzitumia kanuni za mafanikio. Moja kati ya hizo ni SHAUKU: mtu kufahamu kitu unachotaka

WEWE “NDIYE BOSI WA MAISHA YAKO, NAHODHA WA ROHO YAKO

Mwandishi amenukuu mistari ya shairi la Mshairi mmoja wa Kiingereza aitwaye W.C. Henley isemayo “Mimi ni kiongozi wa majaaliwa yangu, mimi ni nahodha wa roho yangu” Hapa alitaka kutuambia kwamba, sababu ya sisi kuwa bosi wa maisha yetu, nahodha wa roho zetu ni uwezo wa kudhibiti mawazo(fikra) zetu.

Napoleon anasema kwamba mshairi alitaka kutueleza juu ya nguvu ya ajabu ya Kiulimwengu iliyojazwa angani na ambayo  hujigeuza yenyewe kuwa katika mfumo wa mawazo tunayofikiri katika akili zetu, na hutuathiri kwa njia za kawaida katika kubadilisha mawazo yetu kwenda katika mfumo wa vitu vinavyoweza kushikika.

Nguvu hii haibagui kati ya mawazo yanayobomoa na yale yanayojenga, itageuza kuwa vitu vinavyoshikika mawazo ya umasikiki sawasawa tu na vile ambavyo ingegeuza mawazo ya utajiri kuwa vitu vinavyoshikika. Ubongo (akili) zetu hupata nguvu mithili ya sumaku kwa mawazo yanayotawala katika akili zetu kwa njia ambayo hakuna mtu anayefahamu. “Sumaku” hizi huvuta kwetu nguvu, watu, mazingira katika maisha yanayoendana na aina ya mawazo yanayotawala fikra zetu.

Kabla hatujaweza kujipatia utajiri kwa kiasi kikubwa ni lazima kwanza tuziambukize akili zetu na shauku kubwa ya utajiri mithili ya sumaku vile ifanyavyo, hii inamaanisha kwamba tuzishughulishe akili zetu kuwaza (kufikiri) maswala yahusuyo fedha mpaka hamu hiyo inatufikisha hatua ya mpango kamili wa kuzipata.

Kidogokidogo ukweli umejifunua wenyewe kwamba, kanuni 13 zilizoelezwa ndani ya kitabu hiki zinabeba siri za namna ya kuyathibiti maisha yetu kiuchumi.

Mpaka hapo mpenzi msomaji wangu tumemaliza kurasa zetu 10 na tunakaribia kabisa kufika tamati ya Sura nzima ya kwanza kwani sura hiyo haikuwa na mambo mengi sana ilikuwa tu ni Utangulizi na mwandishi, bado hakuwa ameanza kueleza kanuni zake 13 za mafanikio.

Kurasa 10 zitakazofuata au session ya 3, tutamalizia kidogo kurasa chache zilizobakia za sura ya kwanza na kuanza kusoma Sura ya pili yenye Kanuni ya kwanza kabisa ya mafanikio ambayo ni SHAUKU, kaa tayari.

Usikose pia Early morning Motivation ya kesho Alfajiri saa 11 juu ya alama. Tutakuwa na mistari ya hamasa kutoka katika kurasa 10 za session ya tatu (3)

 

Soma kilichopita kwenye Usomaji huu

Soma kifuatacho kwenye Usomaji huu

 

.....................................

HUDUMA ZETU MBALIMBALI ZA MALIPO, (MAFUNZO, VITABU & MICHANGANUO)

 

1. Kujiunga na programu yetu ya MAKE YOURSELF GREAT AGAIN ndani ya group la VIP

Hii ni programu ya mafunzo na mentorship mwaka mzima yenye course mbalimbali ikiwemo, Kujifunza kuandika business plan kwa undani, usomaji wa think & grow rich kwa kina, kujifunza ubunifu kwenye biashara, masoko na mauzo nje na ndani ya mtandao, siri za biashara ya rejareja pamoja na uwekezaji. 

Kujiunga ada ni sh. 20,000/= kwa ajili ya vitabu na michanganuo ya rejea lakini kwa sasa ukiwahi muda haujaisha unalipia shilingi 10,000/= tu

Au unanunua tu kitabu cha Think & Grow Rich (Fikiri & Utajirike) softcopy au Hardcopy na kuunganishwa moja kwa moja

Ikiwa utalipia vitabu na michanganuo unapewa papo hapo Vitabu  5 kikiwemo cha Michanganuo ya biashara na Ujasiriamali , halafu OFFA ya Michanganuo kamili ya Biashara 7 kama uonavyo hapo chini. Jumla ni vitu 12 unatumiwa.

Michanganuo 7 ya offa iliyoorodheshwa unaweza kubadilisha kabla hujatumiwa kwa kuchagua mwenyewe ile uitakayo  miongoni mwa Michanganuo 18 utakayoorodheshewa pale chini kabisa mwishoni ilimradi tu imefika 7. Wasiliana nasi kwa namba 0765553030 / 0761002126

2. Kuandikiwa Mchanganuo wa Biashara yako

Tunaandika Mpango kamili wa biashara yeyote ile kwa Kampuni na wafanyabiashara binafsi kwa gharama rafiki, njoo tuzungumze kupitia namba za simu au wasap 0765553030 / 0761002125 Michanganuo yetu tunaandaa kulingana na maono ya mteja kama yalivyo pamoja na mazingira ya soko linalomzunguka

3. Kitabu cha MAFANIKIO YA BIASHARA YA DUKA LA REJAREJA

Kitabu hiki kilichowasaidia wajasiriamali wengi wadogo na wale wa kati kinatatua changamoto mbalimballi za biashara za rejareja kubwa ikiwa ni usimamizi wa mapato yasipotee au kudokolewa kiholela na wasaidizi wako, ni uzoefu wa miaka 12 wa mwandishi mwenyewe kwenye hii biashara.

Kukipata unaweza kulipia Tsh. 10,000/ kupitia namba 0761002125 jina peter Augustino Tarimo, kisha nitakutumia kitabu chako kwenye simu au kompyuta mara moja. Au pia unaweza ukatembelea duka letu la mtandaoni kukinunua hapo kwa kiungo hiki>>MAFANIKIO YA BIASHARA DUKA LA REJAREJA

 

4. Kitabu cha THINK & GROW RICH –SWAHILI EDITION (FIKIRI & UTAJIRIKE)

Kitabu hiki kilichosomwa duniani na zaidi ya watu milioni 100 tunayo nakala ya Kiswahili kwa bei zifuatazo;

Nakala ngumu hardcopy ukiwa Dar es salaam ni Tsh. 25,000/=  – Tunakuletea mpaka pale ulipo, ukishapokea kitabu ndipo unalipa pesa

Ukiwa mikoa mingine Tanzania tunatuma kitabu kwa njia ya Mabasi kwa  gharama jumla Tsh. 35,000/= kitabu na usafiri

Nakala laini Softcopy; Ukiwa popote pale Duniani unaweza kukipata kwenye mtandao wa GETVALUE kupitia kiungo hicho kibofye kuingia ununue sasa hivi na kukidownload.

5. Vitabu zaidi &Michanganuo mbalimbali ya biashara

Kwa vitabu zaidi na Michanganuo mbalimbali ya biashara iliyo tayari tembelea duka letu hili  la mtandaoni uweze kuona na kujinunulia kwa urahisi kabisa>>SELF HELP TANZANIA ONLINE BOOSHOP


0 Response to "RIPOTI YA USOMAJI THINK & GROW RICH AWAMU YA PILI (PAGE 9 – 18 / UKURASA.17 – 37) SURA YA 1"

Post a Comment