JALADA
LA MBELE – COVER PAGE
Narejea nakala ya Kiswahili kidogo na nitarudi kwa nakala
ya kiingereza nikifika kwenye Dibaji ya mwandishi.
Jalada limenakshiwa pembezoni kwa picha za noti pesa ya
Kitanzania aina mbalimbali toka Uhuru mpaka sasa. Katikati lina rangi ya njano
na maandishi makubwa meusi mchanganyiko na ya rangi nyeupe na nyekundu kidogo
Kisha unafuata ukurasa uliobeba jina la kitabu kwa lugha
zote 2 na majina ya mwandishi na Mfasiri wa kitabu. Ukurasa unaofuata ni wa
Hakimiliki, ISBN namba pamoja na anuani ya mfasiri. Unafuata ukurasa wa Wakfu
kisha Yaliyomo na Shukrani unaoanza kwa namba za kirumi ‘i’
SHUKRANI
Kwenye shukrani mfasiri ametoa shukrani zake za dhati
kwanza kwa Mwenyezi Mungu muweza wa yote, kisha kwa Familia na Waandishi
wengine waliomhamasisha kwenye kazi za uandishi
DIBAJI
YA MWANDISHI
Katika Dibaji ya mwandishi mwenyewe Bwana Napoleon Hill
anaanza kwa kuelezea Siri ya kupata pesa iliyozungumziwa ndani ya hiki kitabu.
Anasema siri hiyo ndiyo iliyowawezesha watu 500 matajiri zaidi aliowahoji
kufikia pale walipokuwa
Anasimulia kwamba siri hiyo alijulishwa kwa mara ya
kwanza kabisa na mtu aliyekuwa tajiri zaidi Marekani wakati huo na
aliyejulikana kwa jina la Andrew
Carnegie wakati alipokwenda kufanya naye mahojiano (Kumbuka Hill alikuwa mwandishi habari)
Bwana Carnegie alimtaka Napoleon Hill aende kuifanyia
majaribio kanuni (siri) hiyo kwa watu wengine Wanaume kwa Wanawake katika kila
nyanja ili kuonyesha utimilifu wake
Katika Dibaji hii mwandishi anajaribu kuelezea kwa kifupi
jinsi kanuni ama siri iliyoko ndani ya kitabu ilivyobadilisha maisha ya watu
mbalimbali kama sura nyingine za kitabu hiki zitakavyokwenda kubainisha kuanzia
Sura ya kwanza mpaka ile ya 15 ambamo pia ndipo zinakopatikana kanuni 13 za
Mafanikio
Ametaja kwa mfano Sura ya 3 inayohusu IMANI, jinsi
Shirika moja la chuma cha pua huko Marekani lilivyoitumia siri hii chini ya
kijana mmoja aitwaye Charles M. Schwab. Siri hii pia ilitumiwa na watu wengine
wengi kwa mafanikio makubwa mfano kina Randolf na wengineo
Anasema Siri imetajwa mara nyingi sana lakini siyo moja
kwa moja. Ni kwa aliyekuwa tayari tu kuipokea na kuitafuta ndio anayeweza
kuipata. Ikiwa mtu upo tayari kuitumia, anasema utaigundua tu angalao mara moja
katika kila sura ya kitabu hiki.
Kitu cha kustaajabisha kuhusu siri hii ni kwamba wale
wamaoichuka na kuitumia hujikuta wenyewe wakipata mafanikio makubwa huku
wakitumia nguvu kidogo sana na kamwe huwa hawarudi tena kwenye maanguko.
Anasema mtu huhitaji Elimu kubwa ndipo uweze kunufaika na
siri hiyo kwani watu wengi walioitumia kwa mafanikio makubwa walikuwa na elimu kidogo sana mfano kina
Henry Ford na John Wanamaker
Hili mwishowe anawataja kwa majina baadhi tu ya watu
Matajiri aliowahoji kwenye safari yake hiyo ya miaka zaidi ya 20 na kusema
majina hayo machache yanawakilisha baadhi ya mamia ya watu wengine mashuhuri
Marekani walioweza kufanikiwa kwa kutumia kanuni ya Carnegie
Mwisho anamalizia kwa kusema; “Ikiwa upo tayari kwa siri hii
tayari unayo nusu ya siri yenyewe, Utaitambua nusu ya siri iliyobakia punde tu
itakapofika akilini mwako” Akimaanisha wakati ukisoma kitabu hiki
DIBAJI
YA MFASIRI
Katika nakala ya Kiswahili kuna hii Dibaji ya mfasiri
ambapo alielezea umuhimu wa lugha ya Kiswahili kama lugha inayojitosheleza
katika nyanja zote kuu za kimaisha akitolea mifano vitabu vilivyowahi
kutafsiriwa kwa lugha ya Kiswahili kama vile vitabu vitakatifu vya Biblia na
Qurani Tukufu.
Lakini pia vitabu vya Shakespear alivyotafsiri Baba wa
Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Mapepari wa Venis na Julias Kaizari
pamoja na hiki cha Think & Grow Rich. Alieleza pia sababu kubwa
iliyomsukuma kufanya kazi hii ya kukitafsiri hiki kitabu
......MWISHO
WA RIPOTI YANGU YA LEO...
Tukutane tena kwenye ripoti zijazo, nategemea washiriki wengine pia kuandaa ripoti zao
hasahasa ile ya Sura nzima, lakini hata mtu waweza kuandaa ya kurasa 10
tunazosoma kila siku. Andaa vyovyote vile jinsi ulivyoelewa na mafunzo
uliyoyapata
Peter A. Tarimo
0765553030 / 0761002125
Tukutane Kesho Alfajiri saa 11 kwenye Early Morning motivation, Dont Miss kwani
ikiwa kama kweli wewe ni mwanamafanikio unayetafuta kuujenga ukuu wako sidhani
kama saa 11 inakukuta umejifunika shuka.
Soma kilichopita kwenye usomaji huu hapa
Soma kifuatachi kwenye usomaji huu hapa
HUDUMA ZETU NYINGINE MBALIMBALI, VITABU
& MICHANGANUO YA BIASHARA
1.
KUANDIKA MICHANGANUO YA BIASHARA
Tunaandika mipango ya
biashara kwa ajili ya Wajasiriamali na Makampuni inayoendana na mazingira yao
halisi kwa gharama rafiki sana, tuwasiliane kwa namba 0765553030 au 0712202244.
Unaweza pia kuona baadhi ya kazi za wateja wetu hapa kwa ufupi tulizowahi
kufanya
2.
KUANDIKA WASIFU WA BIASHARA (COMPANY PROFILE)
Tunaandika company profile
zenye mvuto na za kipekee kulingana na maono ya mteja mwenyewe na gharama
huanzia Tsh. 50,000/=
3.
KITABU CHA FIKIRI & UTAJIRIKE (THINK & GROW RICH-SWAHILI EDITION)
Dar es salaa tunampelekea
mteja alipo kwa gharama ya Tsh. 25,000/= na mteja hufanya malipo akishapokea
kitabu. Mikoa mingine kwa mabasi ni sh. 35,000/=. Nakala laini (softcopy)
kinapatikana app ya GETVALUE popote pale ulipo, bonyeza link hiyo kununua.
4.
KITABU CHA MAFANIKIO BIASHARA YA DUKA LA REJAREJA & GENGE TOLEO LA 2025
Nakala ngumu ni Tsh. 20,000/= Dar tunamfikishia mteja
alipo, anapokea kitabu ndipo analipa na Mikoa mingine kwa mabasi ni Tsh.
30,000/= Nakala laini (softcopy) tunatuma kwenye simu au kompyuta ya mteja kwa
bei ya Tsh. 10,000/= Pia unaweza kununua mtandaoni kwenye duka letu kwa bofya
kiungo hiki>>>Siri ya mafanikio ya biashara
ya duka la rejareja 2025 & genge ndani yake
5.
VITABU ZAIDI & MICHANGANUO YA BIASHARA
Kupata vitabu vingine zaidi
pamoja na Michanganuo ya biashara mbalimbali iliyokwisha andaliwa tayari
tembelea Duka letu la mtandaoni kwa kiungo kifuatacho>>>; Augustinopeter bookshop
Watsap/Call/Sms: 0765553030 au 0761002125
Peter Augustino Tarimo
0 Response to "RIPOTI YA USOMAJI KITABU CHA THINK & GROW RICH KURASA ZA MWANZO NA DIBAJI YA MWANDISHI-SIKU YA KWANZA, 29/07/2025"
Post a Comment