MAFUNZO YA KUANDIKA MCHANGANUO WA BIASHARA YA UPENDO CAFE SIKU YA PILI 26/12/2022 | JIFUNZE UJASIRIAMALI

MAFUNZO YA KUANDIKA MCHANGANUO WA BIASHARA YA UPENDO CAFE SIKU YA PILI 26/12/2022

mkahawa mdogo wa upendo

SIKU YA PILI 26/12/2022, KUANDIKA MPANGO WA BIASHARA, UPENDO CAFE HATUA KWA HATUA

 

Habari za muda huu ndugu mdau wa masomo haya;

Katika mafunzo yetu leo tutakwenda kuona jinsi ya kuandika vipengele vitatu ambavyo ni kati ya vile vipengele 8 vinavyounda mchanganuo mzima wa biashara yetu kama tulivyoona jana. Navyo ni;

                1.      MUHTASARI,

                2.      MAELEZO YA BIASHARA na

                3.      MAELEZO YA SOKO

Baada sasa waanzilishi wa cafe huu kumaliza kazi ya kufanya  utafiti wa biashara yao kwa kina na kupata majibu ya maswali mbalimbali, kilichobakia ni wao kuketi chini na kuanza kuandika vipengele kimoja baada ya kingine hadi mwisho.

Hawafungwi na ni kipengele gani waanze nacho ila tu kurahisisha mambo mimi nimeonelea hapa tuanze na kipengele cha kwanza (muhtasari) na kuendelea jinsi mfululizo wa vipengele rasmi unavyoonyesha. Tungeliweza hata kuanza katikati au karibu na mwishoni kwa mfano kipengele cha Uongozi na wafanyakazi  ilimradi tu wakati wa kumaliza basi tukumbuke kuja kuvipanga jinsi mlolongo unavyotaka viwe.

Samahani kidogo kuna kitu nilisahau jana, baada ya Jalada la nje tulitakiwa kuona YALIYOMO ni nini kinakaa pale, sasa ngoja nizungumzie hapo kidogo ingawa tulitakiwa tufanye hivyo jana.

Ukurasa wa Yaliyomo ni muhimu na pale ndipo unatakiwa kuorodhesha yale mambo yote muhimu katika kila sura pamoja na namba za kurasa mambo hayo yanakopatikana kusudi wasomaji iwe rahisi kwao kujua ni vitu gani andiko lako limebeba na vipo wapi.

 

Sasa hebu tuanze rasmi mada zetu za leo;

1. MUHTASARI TENDAJI

Hii ndiyo sehemu/sura ya kwanza kabisa kwenye mchanganuo wako. Ingawa inaanza mwanzoni lakini ndiyo huandikwa mwishoni baada ya kumaliza kuandika sura nyingine zote. Hapa tutaelezea tu jinsi ya kuiandika lakini ya UPENDO Cafe tutaandika mwishoni.

Wakati wa kuandika Muhtasari wako unatakiwa kuchagua zile pointi muhimu tu za mchanganuo wako. Unaweza kuchukua ufupisho wa kila sura ambao tutakwenda kuona wakati wa kuandika sura zingine au hata ukachagua sentensi moja moja au chache kwenye kila sura na kuunda Muhtasari wako na hapo unakuwa umemaliza.

 

2.0 MAELEZO YA BIASHARA/KAMPUNI

 

Sura hii ni ya pili na huwa ina vipengele vyake vidogo kama tulivyokwishaona jana, ambavyo kila kimoja inabidi ushughulike nacho peke yake. Vipengele vyake hivyo vidogo ni hivi vifuatavyo;

2.0 MAELEZO YA KAMPUNI / BIASHARA

2.1 Maono

2.2 Dhamira kuu

2.3 Malengo

2.4 Siri za mafanikio

2.5 Umiliki wa Biashara

2.6 Kianzio(kwa biashara mpya au historia kwa kampuni

       iliyokwishaanza)

2.7 Eneo la biashara na vitu vilivyopo 

Kwanza Sura yeyote ile huanza na muhtasari wa sura nzima ambao pia huandikwa mwishoni baada ya kumaliza sura husika. Sasa baada tu ya neno MAELEZO YA KAMPUNI pale juu chini yake acha nafasi kwanza (kama nilivyofanya mimi) ya kuja kuandika muhtasari wa sura yako kisha endelea na Maono...........

 

2.1 Maono

Maono ni picha pana ya biashara yako unayotaka uione baada ya muda kupita, (You visualize) mara nyingi huwa ni muda mrefu. Biashara yako inaweza ikawa ni ndogo tu lakini maono yako ni lazima yawe makubwa (think Big but start small),  na kwenye biashara hii ya Upendo maono yao ni haya hapa;

Kuja kumiliki msururu wa Migahawa mikubwa nchini Tanzania.

 

2.2 Dhamira kuu

Dhamira kuu ni ile biashara unayoifanya. Kwa mfano kwa kuwa Upendo ni biashara ya chakula basi dhamira kuu ya waanzilishi wake ni lazima ionyeshe ni kitu gani wanakusudia kukifanya. Lakini pia katika kuelezea kile unachokusudia kukifanya unaweza kuongezea na ubunifu fulani katika kujitofautisha na biashara nyingine kama yakwako, kwa mfano ukasema wewe dhamira yako ni kutoa huduma za chakula mahali fulani lakini siyo chakula ilimradi tu ni chakula  bali ni chakula bora kisichokuwa na mafuta mengi. Dhamira kuu ya Upendo ni hii hapa;

 

“Kuuza vyakula na vinywaji baridi ikiwemo supu na chapati laini kwa madereva wa vyombo vya usafiri wa umma na abiria katika stendi ya Goba Njia nne Ubungo Dar es salaam”

 

2.3 Malengo.

Tuingie kwenye Malengo. Hizo namba mwanzoni nimeweka kuonyesha msisitizo kwamba namba ni sura ya 2 kipengele cha 3, ila unaweza kutumia staili nyingine yeyote ile.

Malengo unataja vile vitu unavyokusudia kuvipata baada ya kutekeleza mpango wako katika kipindi fulani, navyo vinaweza kuwa ni mauzo, faida, idadi ya wateja, idadi ya wafanyakazi, au  kitu kingine chochote kile. Malengo mazuri ni lazima yawe halisi, yanayopimika, yenye kutekelezeka na yaliyokuwa na muda maalumu wa utekelezaji.

Bibi Gladys na Mariam wameyataja malengo yao kwa Upendo Cafe kuwa ni haya yafuatayo;

                          1.      Kukanda kilo 5 za unga wa ngano kwa ajili ya chapati na vitafunwa vingine kama maandazi kila siku

                          2.      Kununua kilo 5 za nyama ya ngombe kila siku kwa ajili ya supu, mishikaki na mchuzi wa vyakula

                          3.      Kupata faida kila siku ya shilingi elfu 78

                          4.      Kufikisha mauzo ya shilingi milioni 100 kwa mwaka

                          5.      Kufungua tawi la kwanza ifikapo mwaka wa 3

Kama ulivyoona hapo, hivyo vipimo kama, kilo 5, kwa siku, mwaka, na mwaka wa 3 ni muhimu sana kwani ndio vitu vinavyoonyesha malengo yao yanapimika, kutekelezeka na yana muda maalumu.

 

2.4 Siri za mafanikio

Hiki ni kipengele kingine kidogo ndani ya kipengele kikubwa cha Maelezo ya Biashara/Kampuni.

*(Kumbuka vipengele hivi vidogo na hata vikubwa siyo lazima kwenye mchanganuo wako uviweke vyote kama vilivyo hapana, itategemea kama kina umuhimu wa kukiweka. Kuna aina au biashara nyingine kipengele fulani hakina umuhimu (irrelevant))

Siri za mafanikio maana yake utaorodhesha yale mambo muhimu kwako utakayoyapa kipaumbele katika biashara yako kusudi uweze kufanikiwa.

 

 

Upendo Cafe siri zao za mafanikio ni hizi hapa chini;

·      Uwezo wetu wa kuchagua Eneo zuri lililo na iadi kubwa ya watu

·      Kupunguza gharama mbalimbali kwa kadiri iwezekanavyo, zile za moja kwa moja na zile za kudumu

·      Kujijengea uwezo mkubwa wa kutambulika sokoni kupitia matangazo na ujenzi wa jina zuri katika jamii inayotuzunguka.

 

2.5 Umiliki wa Biashara

Hapa taja jina kamili la biashara na mmiliki au wamiliki wake ukielezea aina ya usajili kisheria kama ni ya mtu binafsi, ubia au kampuni.  Eleza kama ni  wamiliki zaidi ya mmoja, kila mmoja anamiliki hisa kiasi gani. Taja na sababu za kuchagua aina ya umiliki uliochagua. Hebu tuone Upendo waliandika nini;

 

Biashara itakuwa chini ya umiliki wa ubia kati ya kina mama wawili, Bibi Gladius Msaki na Bibi Mariam Salim, wote wawili wakiwa na umiliki wa asilimia 50 kila mmoja. Sababu za kuchagua aina hii ya umiliki kisheria ni urahisi wake katika maswala mbalimbali kama ya ulipaji wa kodi na upatikanaji wa mtaji.

 

2.6 Kianzio

Kwa kuwa ni biashara mpya inayoanza tutachora jedwali la mahitaji yote kisha jingine la vyanzo vya mahitaji hayo kama ifuatavyo; Mahitaji yetu ni gharama  zote zitakazotumika pamoja na rasilimali zote zitakazohitajika

 Mahitaji:

Gharama za Awali

Tsh

Ukarabati chumba cha biashara

150,000

Usajili na vibali

50,000

Matangazo

50,000

Mengineyo

50,000

Jumla

300,000

 

Rasilimali za kudumu (Vifaa na mashine)........

.........................................................

Masomo haya yanatolewa ndani ya group la MICHANGANUO-ONLINE kila siku na hii ni sehemu ndogo tu ya somo la leo. Ili kupata masomo kamili pamoja na masomo yote mengine ya siku za nyuma jiunge na group hilo kwa kulipia ada kidogo ya mwaka shilingi 10,000/=. Unaweza kutumia moja kati ya namba zetu hizi, 0712202244 au 0765553030 jina Peter Augustino Tarimo.

Wahi leo kabla zawadi yetu ya mwisho mwaka huu ya vitu 22+ haijamalizika rasmi leo usiku huu saa 6.

Kusoma dondoo za somo letu la fedha la jana usiku bonyeza maneno haya>> NJIA 9 ZA KUVUTA PESA, BAHATI & MAFANIKIO 2023

0 Response to "MAFUNZO YA KUANDIKA MCHANGANUO WA BIASHARA YA UPENDO CAFE SIKU YA PILI 26/12/2022"

Post a Comment