NAOMBA UZOEFU KIDOGO KWA ANAYEFANYA BIASHARA YA DUKA LA REJAREJA (MAHITAJI YA NYUMBANI) | JIFUNZE UJASIRIAMALI

NAOMBA UZOEFU KIDOGO KWA ANAYEFANYA BIASHARA YA DUKA LA REJAREJA (MAHITAJI YA NYUMBANI)

Kitabu cha duka la rejareja

Wakati semina yetu ya Jinsi ya kuandaa mchanganuo wa Biashara ikiendelea siku tunajifunza somo la Tatu kuhusiana na Cover page au Jalada la nje, kichwa cha mchanganuo na Yaliyomo alitokea mdau mmoja na kutaka kufahamu zaidi juu ya Biashara ya duka la rejareja marufu kama duka la mangi au duka la mahitaji ya nyumbani wengine huliita duka la vyakula.

Hii ni kawaida katika group letu la MICHANGANUO-ONLINE MASTERMIND GROUP kwani tumejiwekea utaratibu kwamba mdau yeyote anapokuwa na jambo lake linalomsumbua asisite kuuliza kusudi members na wawezeshaji wengine tuweze kumuondolea dukuduku lake. Swali hili nililifananisha na hadi mbuzi kufia kwa muuza supu kwani muulizaji hakuwa anafahamu kama ndani ya Group kulikuwa na Mtunzi wa Kitabu cha Biashara ya duaka la rejareja ambaye ndiye mimi hapa.

Basi na mimi sikuchelewa mara moja nikampa majibu kama ifuatavyo;

Mr. Julius binafsi mimi ninao uzoefu na biashara hii ya duka la rejareja mtaani maarufu kama maduka ya vyakula ila kwa kweli siyo la jumla.

Ninachoweza kusema ni kwamba maduka haya ni moja ya biashara rahisi sana kuanzisha kwamtaji wowote ule uliokuwa nao kwani siyo lazima uanze na vitu vingi. Wapo wanaoanzia hata majumbani mwao kwa kuanza na mche mmoja wa sabuni na mafuta ya kula ya kupima na mwisho wa siku mtu huyohuyo unakuja kumkuta kakodi fremu mahali anamiliki duka la malaki kama si mamilioni ya pesa.

Tusiandikie mate na wino ungalipo, katika kitabu changu cha MAFANIKIO YA BIASHARA YA DUKA LA REJAREJA nilielezea “exactly” kwa picha jinsi nilivyoanzisha duka langu mwenyewe la rejareja pale Msimbazi Kariakoo nikiwa na mifuko miwili tu ya keki, soda kreti moja na pakiti 4 za biskuti tena nje barazani, siyo kwenye fremu. Baada ya mwaka sikuwa tena mwenzio, nikawa tayari nipo ndani ya kiduka changu cha rejareja na msaidizi juu!

Kitafute kitabu hiki ndani nimeweka mbinu nyingi huwezi kuzipata popote na gharama yake ni shilingi elfu 6 tu soft copy toleo jipya la mwaka 2023, ukihitaji nijulishe.

Baada ya wadau wengi kutoa oda zao kupata kitabu hiki niliwasihi tuwasiliane ili waweze kukipata kitabu hiki ambacho ni moja ya vitabu vyangu bora zaidi kuandika kutokana na uzoefu niliopitia mwenyewe na wala siyo tafiti za kwenye vitabu na google.

“Tuwasiliane Wakuu hiki kitabu is one of my masterpiece, nimekitunga kutokana na uzoefu wangu binafsi kwa asilimia zaidi ya 80%” Niliwaambia.

0 Response to "NAOMBA UZOEFU KIDOGO KWA ANAYEFANYA BIASHARA YA DUKA LA REJAREJA (MAHITAJI YA NYUMBANI)"

Post a Comment