KWANINI BIASHARA HUMPA MTU UHURU ZAIDI WA KIFEDHA KULIKO AJIRA? | JIFUNZE UJASIRIAMALI

KWANINI BIASHARA HUMPA MTU UHURU ZAIDI WA KIFEDHA KULIKO AJIRA?

Uhuru zaidi wa kifedha
Hakuna shaka kwamba kila binadamu angetamani siku moja aje kuufikia  uhuru kamili wa kifedha, kwahiyo ikiwa lengo lako kuu kwenye safari hii ya maisha ndio hilo basi hauna budi kubadili ‘meli’ uliyopanda sasa kutoka ile ya ajira kwenda ya biashara, hili halina ubishi, inawezekana usibadili sasa lakini ni lazima utafanya hivyo hapo baadae hata baada ya kustaafu.

  

Katika somo letu hili leo, hiki hasa ndio kitu tutakachoenda kujifunza. Biashara peke yake tu inaweza isiweze kukupa uhuru kamili wa kifedha lakini ni moja kati ya viungo muhimu sana vinavyosaidia kuharakisha kukufikisha huko.

 SOMA: Kwanini ni rahisi zaidi kutajirika ukiwa kwenye ajira kuliko kujiajiri binafsi?

Uwezekano wa mtu kuufikia uhuru wa kifedha akiwa katika ajira ni mdogo ingawa hatuwezi kabisa kuuondoa uwezekano huo. Si kama mwajiriwa hawezi kabisa kupata uhuru wa kifedha ila mchakato wake ni mrefu na mgumu kuliko vile ilivyo kwa mfanyabiashara. Wafanyabiashara mara nyingi sana utakuta hujiandaa kisaikolojia katika safari hii, kivipi? - tutajua zaidi kwenye aya zinazofuata.

 

Katika kazi za ajira, watu wengi huishi maisha ya wasiwasi kutokana na upungufu wa fedha. Na wala haijalishi ni mshahara mkubwa kiasi gani aupatao mtu, mara nyingi utamkuta akibeba akilini fikra za upungufu wa fedha. Na hili hutokea kwasababu waajiriwa wengi wanakuwa na tabia ya kufanya matumizi mengi zaidi kushinda wenzao wafanyabiashara. Wafanyibiashara wao mara nyingi hupenda kuwa waangalifu sana kwenye matumizi yao ya fedha.

SOMA: Fedha zako zinapotea kiajabu? Njia rahisi ya kutambua fedha zako zinakoishia kila siku hii hapa. 

 

Kwanini basi mfanyabiashara huwa mwangalifu sana kwenye matumizi ya pesa?

 

Mchakato wa biashara mpaka imetengeneza faida unahusisha mlolongo wa vitu vingi na hivyo kumfanya mfanyabiashara kuchukua pia hatua mapema za kujihadhari kusudi biashara isije kuanguka. Kumbuka kwenye biashara hakuna ulinzi(security) kama ilivyo kwenye ajira, hivyo mfanyabiashara anajua kabisa akiteleza kidogo tu imekula kwake.

 

 Ufuatao ni mchakato mzima wa biashara mpaka imezalisha faida kisha FEDHA ZA ZIADA pale mwishoni kabisa


Chati hiyo hapo juu inaonyesha jinsi biashara inavyotengeneza yenyewe fedha za ziada. Utaona ya kwamba biashara hupitia mchakato mrefu mpaka imeweza kutengeneza fedha za ziada ambazo ndizo zinazobeba jukumu kubwa katika zoezi la kufanikisha uhuru wa kifedha wa mfanyabiashara kama tutakavyoona baadae kidogo.

 SOMA: Njia 7 unazotumia kubana matumizi lakini kumbe zinakuzidishia umasikini

Wakati sasa mfanyabiashara akitekeleza shughuli mbalimbali za biashara yake ndipo anapojijengea tabia hii ya kuwa muangalifu kupita kiasi kwenye matumizi ya fedha kusudi ahakikishe mwishoni kunakuwa na fedha za ziada kwa ajili ya kuzirudisha tena kwenye biashara kama mtaji lakini pia kwa ajili ya kulipia gharama zake nyingine mbalimbali za kimaisha.

KAZI/AJIRA

Hivyo ndio kusema kwamba mwajiriwa hawezi kabisa kusimamia fedha zake vizuri mpaka na yeye akaufikia uhuru wa kifedha? Hebu tena tuangalie chati hii ifuatayo;


Kama ilivyokuwa kwa biashara, ajira nayo inaweza ikatengeneza fedha za ziada. Lakini tofauti na biashara katika ajira kunakosa muunganiko, kunakuwa na pengo kati ya ajira yenyewe(kazi) na fedha. Uthibiti wa mwajiriwa kwenye kutengeneza fedha zake za ziada umewekewa mipaka, kivipi? Kuna vitu viwili (2) vifutavyo;............

................................................................................................................................................................................................................................

SOMA: Unategemea mshahara wa mwezi au kipato kimoja? Hizi hapa mbinu za kujinasua na kuishi maisha mazuri unayotamani

..............................................................................................................

Ndugu msomaji somo hili litaendelea katia Group la Michanganuo- online leo hii tarehe 06/06/2023 usiku saa 3. Ili kuweza kulisoma kwa ukamilifu na masomo mengine yaliyopita yenye maudhui ya fedha, jiunge na group hilo kwa kiingilio cha sh. elfu 10 tu mwaka mzima.

Utapata pia na OFFA yetu ya vitu 12 yenye vitabu na michanganuo mbalimbali ya biashara. 

Namba za kulipia ni 0712202244  au 0765553030 Jina Peter Augustino Tarimo.  Baada ya malipo tuma na ujumbe usemao, "NIUNGANISHE MASTERMIND GROUP NA OFFA YA VITU 12

Utaunganishwa muda huohuo na kutumiwa kila kitu. Ikiwa hutaki group ungependelea offa peke yake nijulishe nisikuunge. 




OFFA HIYO YA VITU 12 NI HII HAPA CHINI;


                 1.      COURSE/SEMINA: (compiled complete course) ya Jinsi ya kuandika Mchanganuo wa biashara –(Ukishindwa kuandika mchanganuo wako mwenyewe utarudishiwa pesa zako) - kwa kiswahili

                 2.       KITABUMichanganuo ya Biashara na Ujasiriamali chenye course zote muhimu za BIASHARA, jinsi ya kuandaa michanganuo ya biashara na sample za michanganuo mbalimbali 10 iliyokamilika kila kitu. – kwa kiswahili

                 3.      KITABU: Mifereji 7 ya Pesa na Siri Matajiri wasiyopenda kuitoa -kiswahili

                 4.      KITABU: Siri za upishi wa chapati laini-UPENDO CAFE pamoja na Mchanganuo wake kamili.-kwa kiswahili

                 5.       KITABUNjia rahisi ya kuandika mpango wa biashara-dakika 30 - kwa kiswahili

                 6.       KITABU: HOW TO WRITE A BUSINESS PLAN  ni maarufu sana duniani na ndio hutumika vyuo vikuu vingi.-kwa kiingereza

                 7.       MCHANGANUO: Kuku wa nyama -Tumaini Broilers - kwa kiswahili

                 8.      MCHANGANUO: Kuku wa nyama –kwa kiingereza

                 9.      MCHANGANUO: Ufyatuaji tofali za saruji- kwa kiswahili

              10.    MCHANGANUO: Mgahawa wa chakula-Jane Restaurant –kwa Kiswahili

              11.    MCHANGANUO: Mgahawa wa chakula-Jane Restaurant –kwa kiingereza

              12.    MCHANGANUO: Kiwanda cha usagishaji Dona (Usado millingkwa Kiswahili

              13.    Kuunganishwa Group la masomo ya kila siku ya fedha na michanganuo mwaka mzima ukitaka. (Mentorship group) (Ni hiyari yako lakini, usipotaka hatukuunganishi)

 

Somo hii limeandaliwa na:

Peter Augustino Tarimo

Mtaalamu wa Michanganuo ya biashara aina zote

Phone/Watsap: 0765553030 au 0712202244

0 Response to "KWANINI BIASHARA HUMPA MTU UHURU ZAIDI WA KIFEDHA KULIKO AJIRA?"

Post a Comment