Kabla hatujaenda kuona ni jinsi gani mtu
unavyoweza kutambua ikiwa sasa umeshakuwa huru kifedha au la, hebu kwanza tuone
maana ya dhana hizi mbili zinazoshabihiana sana, ‘Kipato cha ziada.’ na ‘Uhuru
wa kifedha’.
Tunapozungumzia kipato cha ziada (Passive income) maana yake hasa ni
kipato mtu anachoingiza pasipo kufanya kazi au kufanya kazi kidogo sana. ni
kipato kile mtu anachoweza kuingiza hata ikiwa yeye menyewe hayupo pale katika eneo
la tukio, labda anaweza kuwa yupo kazini kwake au ana mishemishe zingine mahali.
Mara nyingi kipato cha ziada huhusishwa na uhuru wa kifedha ingawa siyo lazima
mtu unapoingiza kipato cha ziada basi pia uwe huru kifedha.
Kwa upande mwingine uhuru wa kifedha unaweza
kuwa na maana moja kati ya hizi zifuatazo kulingana na mazingira na kipato cha
mhusika.
1. Maana
ya kwanza mtu anajihesabu kuwa huru kifedha pale anapokuwa na kipato cha ziada
kinachomtosha kugharamia mahitaji yake yote ya msingi.
2. Maana
ya pili ni pale mtu anapokuwa na kipato cha ziada cha kumuwezesha kulipia
chochote kile akitakacho maishani ikiwa ni pamoja na vitu vyote visivyokuwa
muhimu kama anasa nk.
Mtu aliyekuwa huru kifedha pia yeye afanye
kazi asifanye kipato huingia kama kawaida, lakini ikumbukwe kwamba kuwa na
kipato cha ziada tu peke yake hakutoshi kukuhakikishia uhuru wa kifedha mpaka
pale utakapohakikisha kipato hicho kinatosha kugharamia mahitaji yako yako yote
ya msingi na kubaki, wakati huohuo ukiwa haulazimiki kufanya kazi yeyote labda
tu ufanye kwa mapenzi yako au kama hobi.
Unahitaji
kipato cha shilingi ngapi kuwa huru kifedha?
Unaweza ukajiuliza, upate kipato cha ziada
kiasi gani kusudi ujue sasa umeshakuwa huru kifedha?” hupaswi wala kuumiza
kichwa kwani jibu lake ni rahisi sana.
Tumesema awali kwamba, kuwa huru kifedha
kunaweza kutafsiriwa katika maana 2, ya kwanza ni pale mtu utakapoweza kuyamudu
mahitaji yako yote ya msingi pasipo kubabaika na ya pili ni pale utakapoweza
kuingiza kipato cha ziada kinachotosha kugharamia mahitaji yako yote ya msingi
na hata yale yasiyokuwa ya msingi mfano anasa huku ukiwa huna haja ya kuuza
muda wako ndipo uweze kulipia gharama hizo.
....................................
Ndugu msomaji wa masomo haya, Hili ndilo somo tulilojifunza leo siku ya tarehe 29/4/ 2020 katika group la MICHANGANUO-ONLINE.
Kila siku masomo kama haya yahusuyo fedha hufundishwa pamoja na masomo yahusuyo jinsi ya kuandaa michanganuo ya biashara bunifu zinazolipa.
Ili uweze kuyapata masomo hayo yote yaliyopita na yatakayotolewa kwa mwaka wote huu wa 2020 unatakiwa kujiunga na group hilo. Ada kwa mwaka mzima ni sh. elfu 10 tu na tunakutumia pia na offa ya vitabu na michanganuo mbalimbali mara baada ya kujiunga.
Malipo ni kupitia namba zetu, 0765553030 au 0712202244 jina Peter Augustino Tarimo kisha tuma ujumbe usemao, "NIUNGANISHE NA GROUP LA MICHANGANUO NA OFFA YA VITU 6"
0 Response to "UTAJUAJE KAMA UMEUFIKIA UHURU KAMILI WA KIFEDHA? KANUNI HII HAPA"
Post a Comment