BIASHARA KWA MKOPO NI NZURI KWA BIASHARA ZILE KUBWA TU NA SIYO KWA BIASHARA NDOGONDOGO, KWANINI? | JIFUNZE UJASIRIAMALI

BIASHARA KWA MKOPO NI NZURI KWA BIASHARA ZILE KUBWA TU NA SIYO KWA BIASHARA NDOGONDOGO, KWANINI?

Biashara ndogondogo ya kukopesha madela mtaani

Katika somo hili juu ya mauzo ya biashara kwa mkopo nitaegemea zaidi kwenye biashara ndogondogo.


Uhai wa biashara yeyote ile unategemea mzunguko chanya wa fedha nikiwa namaanisha fedha zinazoingia ziwe nyingi kuliko fedha zinazotoka nje ya biashara. Ingawa biashara inaweza kuwa na faida nzuri tu lakini mzunguko hasi wa fedha taslimu unaweza ukaifanya kuwa ni biashara isiyofaa kabisa wala kuwezekana kufanyika.

Moja ya makosa makubwa baadhi ya wajasiriamali wadogo wanayoyafanya ni kuuza bidhaa zao kwa mkopo bila kuzingatia vigezo muhimu kwa umakini. Kuna ambao hata huthubutu kuanzisha “BIASHARA ZA KUKOPESHA MITAANI”. Hapa mtu anakwenda Manzese, Tandika au Kariakoo, ananunua viatu, nguo au bidhaa zozote zile za jumla kwa fedha taslimu halafu akifika mtaani anaanza kupita nyumba hadi nyumba akiwahimiza wateja wakope  na kisha kuja kulipa baadae.

SOMA: Ajabu la nane(8) la dunia, nguvu ya kushangaza inayoweza kumtajirisha mtu bila ya kutoa jasho

Mtindo huu siyo mbaya ila tu ubaya huja pale biashara yenyewe inapokuwa ndogo, na bila ya mtaji wa kutosha. Hata ikiwa wateja wako wote watakuja kukulipa lakini je, watakulipa wote kwa wakati muafaka? Wateja kutokulipa kwa wakati kunaleta athari kubwa na mbaya sana katika mzunguko wako wa fedha kwenye biashara ndogo. Kwa kawaida imezoeleka sehemu nyingi duniani kuuza kwa mkopo kunafanywa na biashara kubwakubwa tu au makampuni na siyo biashara ndogondogo.

Wakopaji nao ni binadamu, anakuja vizuri na kukuambia nataka  mkopo wa  haraka wa bidhaa fulani, lakini cha ajabu inapofika siku aliyoahidi kulipa deni anakuja na hadidhi kibao, mara ...oo.. amefiwa, amesafiri, anaumwa, amelazwa au  anauguliwa na mtu wa karibu kama mtoto nk. Utampeleka polisi? 

Anaweza akaahidi kulipa mwezi unaofuata, vipi kuhusu mzunguko wa biashara yako wa pesa? Kwa hizo siku 30 za ziada utapata wapi fedha taslimu za kuziba pengo na wakati huo mtaji wenyewe pengine ni wa kukopa? Mzunguko wako wa fedha tayari kwa mwezi huo utakuwa hasi, hautakuwa na fedha taslimu za kwenda kufuatilia mzigo mwingine na matokeo yake hata fedha kidogo ulizolipwa na baadhi ya wateja unaamua kuzifanyia majukumu mengine.


Hii ndiyo sababu kubwa ni kwanini biashara nyingi ndogo za kukopesha vitu mitaani hazipigi hatua ya maana. Kuna gharama pia za kufuatilia madeni, muda nk. ukija kujumlisha vyote unakuta biashara ya namna hiyo haina tija zaidi ya kuumiza kichwa.

Sisemi katika biashara ndogo mtu hauwezi ukakopesha kabisa hapana, ila kama utaamua kukopesha na ni jambo lisiloepukika kwa asilimia 100, basi uhakikishe yule unayemkopesha unafahamu historia yake vizuri, unapajua na anakoishi, tena isitoshe weka idadi maalumu ya wateja utakaoruhusu wakope ikiwa utalazimika kukopesha.

Kwa mfano unaweza ukajiwekea malengo hivi, mzigo wako hebu tuchukulie labda ni mzigo wa madela ya kina mama pisi 100, kati ya hayo madela 100 amua ukisha kopesha hapo madela 15 au 20 tu basi, hayo mengine yanayobakia 85 au 80, piga ua hata aje nani hautamruhusu akope. Hii itasaidia sana kuwa na uhakika wa fedha taslimu ya madela yako 80.


Hebu fikiria kwa mfano madela yako uliyanunua mwezi wa pili mwanzoni na ulitegemea mwishoni mwa mwezi wa pili kabla hata ya kuanza kwa mfungo wa ramadhani utafuata tena mzingo mwingine kusudi uje kuwahi msimu wa sikukuu za Pasaka na Idi. Lakini mwishoni mwa mwezi wa pili unajikuta ulikopesha zaidi ya robotatu ya madela yote na wateja wote kila unayemfuata anakupa sababu lukuki huku akiahidi kulipa mwezi wa tatu mwishoni. Hebu fikiria hizi siku 30 hapo katikati biashara yako ndogo na pengine wewe mwenyewe utaishije?.

Hata kama madela yako yana faida kubwa kisi gani........................... somo hili linaendelea......



................................................................................................................................................................................................................................

Mpenzi msomaji wangu; 
Hili ni somo letu la leo tarehe 11/6/2023 katika Group letu la Watsap la MICHANGANUO ONLINE. I
kiwa hutumii wasap tunatuma pia kwa email. Masomo haya ni kila siku usiku saa 3 - mpaka saa 4. Kiingilio ni  sh. elfu 10 ambayo ni ada ya mwaka mzima

Masomo mengine yote yaliyokwisha pita tangu tuanze tunakutumia inbox


Mbali na masomo haya ya kila siku yenye maudhui ya pesa pia tunakutumia OFFA yetu kubwa ya vitu 12, inayojumuisha vitabu na michanganuo kamili ya biashara kama uonavyo hapo chini mwisho

Ili kujiunga na kupata kila kitu lipia kiingilio chako sh. elfu 10 kupitia namba zetu, 0765553030 au 0712202244 jina Peter Augustino Tarimo. Kisha tuma ujumbe unaosema, "NIUNGANISHE NA GROUP LA MICHANGANUO-ONLINE PAMOJA NA OFFA YA VITU 12"

VITU HIVYO 12 VYA OFFA NI HIVI VIFUATAVYO;-

                 1.      COURSE/SEMINA: (compiled complete course) ya Jinsi ya kuandika Mchanganuo wa biashara –(Ukishindwa kuandika mchanganuo wako mwenyewe utarudishiwa pesa zako) - kwa kiswahili

                 2.       KITABU: Michanganuo ya Biashara na Ujasiriamali chenye course zote muhimu za BIASHARA, jinsi ya kuandaa michanganuo ya biashara na sample za michanganuo mbalimbali 10 iliyokamilika kila kitu.kwa kiswahili

                 3.      KITABU: Mifereji 7 ya Pesa na Siri Matajiri wasiyopenda kuitoa -kiswahili

                 4.      KITABU: Siri za upishi wa chapati laini-UPENDO CAFE pamoja na Mchanganuo wake kamili.-kwa kiswahili

                 5.       KITABU: Njia rahisi ya kuandika mpango wa biashara-dakika 30 - kwa kiswahili

                 6.       KITABU: HOW TO WRITE A BUSINESS PLAN  ni maarufu sana duniani na ndio hutumika vyuo vikuu vingi.-kwa kiingereza

                 7.       MCHANGANUO: Kuku wa nyama -Tumaini Broilers - kwa kiswahili

                 8.      MCHANGANUO: Kuku wa nyama –kwa kiingereza

                 9.      MCHANGANUO: Ufyatuaji tofali za saruji- kwa kiswahili

              10.    MCHANGANUO: Mgahawa wa chakula-Jane Restaurant –kwa Kiswahili

              11.    MCHANGANUO: Mgahawa wa chakula-Jane Restaurant –kwa kiingereza

              12.    MCHANGANUO: Kiwanda cha usagishaji Dona (Usado milling) - kwa Kiswahili

              13.    Kuunganishwa Group la masomo ya kila siku ya fedha na michanganuo mwaka mzima ukitaka. (Mentorship group) (Ni hiyari yako lakini, usipotaka hatukuunganishi)



Kujipatia vitabu vyetu vingine au Michanganuo mbalimbali ya biashara tembelea duka letu la mtandaoni hapa la SMART BOOKS TZ

Kupata toleo jipya 2023 la kitabu cha MAFANIKIO YA BIASHARA YA DUKA LA REJAREJA bofya hayo maandishi.

Kufuatilia Semina hatua kwa hatua jinsi ya kuandika MCHANGANUO WA BIASHARA YA KIWANDA KIDOGO CHA USAGAJI UNGA WA DONA bonyeza hiyo link

0 Response to "BIASHARA KWA MKOPO NI NZURI KWA BIASHARA ZILE KUBWA TU NA SIYO KWA BIASHARA NDOGONDOGO, KWANINI?"

Post a Comment