TABIA ZA KUFANIKIWA: JE, UNASHINDWA KUKAMILISHA JAMBO LAKO MUHIMU ULILOANZISHA? | JIFUNZE UJASIRIAMALI

TABIA ZA KUFANIKIWA: JE, UNASHINDWA KUKAMILISHA JAMBO LAKO MUHIMU ULILOANZISHA?

Kijana akikamilisha jambo lake muhimu

Katika maisha kuna wakati tunajikuta katika hali ambayo tunashindwa kutimiza mambo muhimu maishani, mambo tunayotamani kwa udi na uvumba kuyafanikisha lakini tunakosa hamasa ya kuyakamilisha. Unaweza kuwa kwa muda mrefu labda umekuwa na ndoto ya kukamilisha kuandika kitabu chako, umekuwa na ndoto ya kuanzisha biashara fulani, kujifunza kozi fulani nk. lakini jambo hilo limegeuka kuwa kama jinamizi kwako kwa kutokuweza kulikamilisha. Unakosa tabia za kufanikwa ama tabia za mafanikio ambazo ni nguzo muhimu mno katika kufanikiwa jambo lolote maishani

Sababu ni kwanini unashindwa kutimiza ndoto zako hizo inaweza kuwa ni woga wa kushindwa kumaliza, woga wa kuchukua muda mrefu kupita kiasi au sababu nyingine zozote zile unazoweza kuwa nazo. Hata pale unaposema ngoja sasa nianze, mara nyingi unajikuta ukiachia njiani kwa kukosa hamasa ya kuendelea mpaka ukamilishe jukumu lako hilo nyeti maishani. Sasa kuna dawa au mbinu ambazo zinaweza zikatumika mtu ukaweza kukamilisha majukumu yako muhimi kwa wakati na siyo kuchukua tena muda wako mwingi huku hautimizi kitu. 

SOMA: Kanuni: Unaijua thamani ya fedha kwa muda wako ni shilingi ngapi?

Nakupa mfano wangu binafsi katika group hili la whatsapp la Michanganuo-online, wakati nilipoanza nilikuwa na wasi wasi na kujiuliza maswali mengi mfano, ‘hivi nitaweza kweli kuandika vitu kila siku?’, ‘Hawa watu ninaowaita kujiunga na group, nitawaeleza nini nitakaposhindwa kutimiza ahadi ya kuweka masomo humu kila siku?” Lakini wakati najiuliza hayo, nikakumbuka mbinu moja iliyoniwezesha kutimiza majukumu yangu mengi muhimu, majukumu au miradi hiyo huwa ninapoikumbuka hunipa hamasa kubwa kila ninapokuwa na jambo la kukamilisha iwe ni kuandika makala, kitabu au hata jukumu lolote jingine la kibiashara au la kijamii. 

Hakuna kitu kikubwa kama kujipangia muda maalumu wa kukamilisha jukumu, “DEAD LINE”  Ninapokuwa naandika kila siku najipangia kwamba, kabla ya kufika muda fulani ni lazima niwe nimekamilisha makala husika. Kwa kuweka muda maalumu wa kukamilisha jukumu hilo najijengea nidhamu ambayo kila siku nalazimika kuitimiza, na hata ninapokiuka siku moja moja dhamira yangu hunishtaki na najisikia vibaya, si hivyo tu bado ninapokumbuka nyuma yangu kuna watu nimewaahidi kuwaletea makala kila siku dhamira inakuwa inazidi kunisuta na hivyo kujisukuma kukamilisha kile ninachoahidi kila siku.  

SOMA: Njia 10 za kuhamasika na kuendelea kubakia na hamasa hiyo kwa muda mrefu ujao

Mfano mwingine nakupa wa mwanafunzi, hivi unaweza kukumbuka ulivyokuwa unasoma kama tayari ulishamaliza au kama bado unasoma unakumbuka mwalimu anapokupangia homework na kukupa dead line? Hakupi deadline tu ila anakuahidi pia viboko endapo utakwenda kinyume na muda huo wa mwisho. Unaweza kukumbuka hapo ni nini kinachokusukuma mpaka kweli unahakikisha kazi ya mwalimu inamalizika katika ule muda aliokupangia? 

Katika mifano hiyo miwili niliyotoa, lengo langu nilitaka ufahamu hapo vitu viwili tu navyo ni hivi hapa;........................................... ...........................................................................................................................................................................................................................................................................................................................makala hii bado inaendele group la Michanganuo-online................................

 

Kupata mtiririko mzima wa somo hili pamoja na masomo mengine yote yaliyopita kwenye group tangu lianze jiunge na Group letu kwa kulipa ada ya mwaka shilingi elfu 10 tu. Utapata pia na OFFA yetu ya vitu 12 yenye mchanganyiko wa vitabu na Michanganuo kamili ya biashara zinazolipa Tanzania kwa kiswahili na kiingereza.

Kulipia tumia namba zetu hizi; 0712202244  au 0765553030 jina ni Peter Augustino Tarimo. Kisha baada ya malipo tuma ujumbe wasap au sms usemao, "NATAKA OFFA YA VITU 12 NA KUUNGWA MASTERMIND GROUP". Muda huohuo nitakutumia kila kitu na kukuunganisha kwa group. Ikiwa hupendi group unataka offa ti peke yake nijulishe ili nisikuunge.

Ikiwa pia hutumii watsap, tunaweza kukutumia offa zako kwa njia ya email.

VITU HIVYO 12 VYA OFFA NI HIVI VIFUATAVYO;-

                 1.      COURSE/SEMINA: (compiled complete course) ya Jinsi ya kuandika Mchanganuo wa biashara –(Ukishindwa kuandika mchanganuo wako mwenyewe utarudishiwa pesa zako) - kwa kiswahili

                 2.       KITABU: Michanganuo ya Biashara na Ujasiriamali chenye course zote muhimu za BIASHARA, jinsi ya kuandaa michanganuo ya biashara na sample za michanganuo mbalimbali 10 iliyokamilika kila kitu.kwa kiswahili

                 3.      KITABU: Mifereji 7 ya Pesa na Siri Matajiri wasiyopenda kuitoa -kiswahili

                 4.      KITABU: Siri za upishi wa chapati laini-UPENDO CAFE pamoja na Mchanganuo wake kamili.-kwa kiswahili

                 5.       KITABU: Njia rahisi ya kuandika mpango wa biashara-dakika 30 - kwa kiswahili

                 6.       KITABU: HOW TO WRITE A BUSINESS PLAN  ni maarufu sana duniani na ndio hutumika vyuo vikuu vingi.-kwa kiingereza

                 7.       MCHANGANUO: Kuku wa nyama -Tumaini Broilers - kwa kiswahili

                 8.      MCHANGANUO: Kuku wa nyama –kwa kiingereza

                 9.      MCHANGANUO: Ufyatuaji tofali za saruji- kwa kiswahili

              10.    MCHANGANUO: Mgahawa wa chakula-Jane Restaurant –kwa Kiswahili

              11.    MCHANGANUO: Mgahawa wa chakula-Jane Restaurant –kwa kiingereza

              12.    MCHANGANUO: Kiwanda cha usagishaji Dona (Usado milling) - kwa Kiswahili

              13.    Kuunganishwa Group la masomo ya kila siku ya fedha na michanganuo mwaka mzima ukitaka. (Mentorship group) (Ni hiyari yako lakini, usipotaka hatukuunganishi)

0 Response to "TABIA ZA KUFANIKIWA: JE, UNASHINDWA KUKAMILISHA JAMBO LAKO MUHIMU ULILOANZISHA?"

Post a Comment