TAARIFA MUHIMU KWA WADAU WOTE WA BLOGU YA JIFUNZEUJASIRIAMALI NA GROUP LA MICHANGANUO-ONLINE | JIFUNZE UJASIRIAMALI

TAARIFA MUHIMU KWA WADAU WOTE WA BLOGU YA JIFUNZEUJASIRIAMALI NA GROUP LA MICHANGANUO-ONLINE

Habari ndugu msomaji na mdau wa blogu hii,  natumaini hujambo na unaendelea na majukumu yako vyema.

Kwa upande wangu mimi ni mzima ila leo hii alfajiri nilikumbwa na mkasa wa kuibiwa vifaa vyangu muhimu ikiwemo simu pamoja na laptop. Vifaa hivi ndio huniwezesha kuandika na kuposti makala katika blogu , wasap na hata katika mitandao mingine ya kijamii.

Kusudio langu la kutoa taarifa hii ni ili kuwajulisha wadau hasa wale waliokuwa katika group la wasap kwamba wanaweza kuona post yeyote pengine inayoweza kutumwa na wezi hao kwa namba au account yangu katika kipindi hiki kuanzia siku ya Jumamosi alfajiri mpaka siku ya Jumatatu, watambue kuwa siyo mimi niliyetuma. Nasema hivyo kwani process za ‘kurenew’ line siku za weekend polisi huwa hamna huduma ya kutoa ‘loss report’ kwa hiyo nalazimika kusubiri hadi jumatatu asubuhi ili kuipata tena laini yangu  ya 0765553030.

Aidha pia nawaomba wadau wasitishe mijadala katika group la MICHANGANUO-ONLINE mpaka pale mambo yatakaporekebishwa. Kwa upande wa ile semina yetu ya tarehe 12 siku ya Jumanne inayohusu, JINSI YA KUANDAA HESABU ZA MPANGO WA BIASHARA nayo nawaomba pia tuisogeze mbele kidogo mpaka tarehe nyingine tutakayopanga baadae kidogo . Kwa waliokwishalipia tayari nawaomba wasiwe na wasiwasi kwani rekodi zao zitakuwa salama katika email.

Nakutakia majukumu mema,

Peter Augustino Tarimo

Self Help Books Tanzania.


0 Response to "TAARIFA MUHIMU KWA WADAU WOTE WA BLOGU YA JIFUNZEUJASIRIAMALI NA GROUP LA MICHANGANUO-ONLINE"

Post a Comment